Nakuuliza kuhusu uthibitisho, unajibu kuhusu imani.
Huelewi uthibitisho wala imani.
Kwanini unaona wewe tu ndiyo unayetakiwa kupewa uthibitisho kwa vitu usemavyo havipo kwa kutumia hisia zako bila kutoa ushahidi wenye kuthibitisha kwa kutokuwepo kwa hivyo usemavyo havipo?
Halafu pia neno imani ni neno ambalo mmejaribu sana kulitolea tafsiri potofu ili kuendana na hisia zenu lakini mmeshindwa, hivyo kuwa mpole unapolitumia hilo neno
Wapi nimesema ni mimi tu ndiye natakiwa kupewa uthibitisho?
Unaelewa uthibitisho ni nini na mipaka yake ni ipi?
Unasema neno imani tumelitolea tafsiri potofu bila ya kueleza ni kwa vipi tumetolea tafsiri potofu, wala kutuelezea tafsiri sahihi ni ipi.
Umeshindwa mara mbili.
Umeshindwa kuonesha kwamba tafsiri yetu ya imani ni potofu, lakini pia umeshindwa kutuonesha kwamba tafsiri yako ya imani ndiyo sahihi.
Toa huo uthibitisho wa hivyo unavyosema havipo na pia utoe tafsiri ya imani ili tujue tofauti ya uthibitisho na imani.
Sijapata kuona uthibitisho maishani wangu bali nimeona ushahidi tu
Inawezekana haya kinachodaiwa kitolewe na baadhi ya watu hakipo na hakijawahi kuwepo!
Sijapata kuona uthibitisho maishani wangu bali nimeona ushahidi tu
Inawezekana haya kinachodaiwa kitolewe na baadhi ya watu hakipo na hakijawahi kuwepo!
Uthibitisho upo mkuu....Maana uthibitisho ni zile njia za kimantiki zilizotumika na zilizopitiwa kuleta huo ushahidi unaosema umewahi kuuona mkuu. Nani wa kuuleta kati ya hao wanaolumbana mimi na wewe hatujui ngoja tuone hadi mwisho...
Unaandika kwa world view ya hakuna mungu unataka ujibiwe katika muelekeo wa world view yako.
Hufundishiki...
Wapi unatoa uongo huo?
Ukifuatilia arguments zangu, utaona naanza kuandika kwa worldview ya kukubali kwamba mungu yupo.
Ila katika worldview hiyo, kwa sababu habari ya kuwepo kwa mungu wenu ni ya uongo, kuna logical inconsistencies.
Upande mmoja tunaambiwa mungu ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, upande mwingine tunaona ulimwengu ambao watu wanapata tabu sana, Nepal huko watu maelfu wamefukiwa kwenye vifusi baada ya tetemeko la ardhi, wengine watoto wachanga wasio hatia.
Imekuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akaumba ulimwengu huu?
Alishindwa kuumba ulimwengu bora zaidi?
Au aliweza hakutaka tu?
Kama aloshindwa, basi hawezi yote.
Kama aliweza, ila hakutaka tu, basi hana upendo wote bali ni katili kuliko yeyote katika ulimwengu mzima.
Unatumia msingi gani?
Kile ambacho kinadaiwa kiwepo ambacho hakipo na hakijawahi kuwepo ni mungu wenu huyo.
Nimeshaonesha kwamba isea ya kuwepo kwake inajipinga yenyewe, na hivyo hawezekaniki kuwapo.
Tatizo linalokukabili ni kuonyesha namna ambayo inajipinga hutaki zaidi Sana ni upotofu wa fikra zako.
Hoja zako zinajizungusha kwenye mtazamo wako potofu kwamba:
Mungu mwenye uwezo,nguvu na upendo wote hawezi kuwepo kwa kuwa duniani kuna maovu ama mateso. Hilo ndilo waliona dai la kimantiki.
Unaulizwa weka hoja zenye mantiki kuonyesha uhusiano wa kuwepo kwa maovu na kutokuwepo kwa Mungu, unabwabwaja tu...
Wengine tunataka kufahamu namna ambavyo uwepo au kutokuwepo kwa Mungu kutokane na dunia kuwa ama kutokuwepo kwa maovu na mahangaiko mengine.
Mwenye upendo wote na uwezo wote anaweza kuachia anaowapenda wapatwe na mabaya?
Badala ya kujibu hoja na kuonyesha namna uhusiano wa uwepo wa Mungu unavyokinzana na uwepo wa maovu unauliza swali
Jibu hoja kwanza ndiyo uliza swali lako.
Maswali yako ni magumu kwa world view ya binadam robot ambaye hajapata kuwepo, kwa sisi wenye reasoning tunamajibu ya kuridhisha kwa kuangalia world view yetu.
Jibu hoja husika kwanza then upate darasa .
Tatizo ukijibiwa kwa Socratic method, hata jibu likiwekwa mbele ya macho yako hulioni.
Nimekuuliza uthibitisho unaelewa ni nini na unaishia wapi, mipaka yake ni ipi, hujajibu.
Unatumia msingi gani?
Kile ambacho kinadaiwa kiwepo ambacho hakipo na hakijawahi kuwepo ni mungu wenu huyo.
Nimeshaonesha kwamba isea ya kuwepo kwake inajipinga yenyewe, na hivyo hawezekaniki kuwapo.
Uthibitisho kuhusu nini na kwa msingi gani?
Mwenye upendo wote na uwezo wote anaweza kuachia anaowapenda wapatwe na mabaya?
Uthibitisho haupingiki hii inamaana kwamba utakachokitolea uthibitisho hakuna atakaeweza kukipinga popote,hiki sijapata kuona popote pale duniani na ndio maana tuna mahakama na mahakimu ili kutoa uamuzi kutokana na uashahidiUthibitisho upo mkuu....Maana uthibitisho ni zile njia za kimantiki zilizotumika na zilizopitiwa kuleta huo ushahidi unaosema umewahi kuuona mkuu. Nani wa kuuleta kati ya hao wanaolumbana mimi na wewe hatujui ngoja tuone hadi mwisho...