Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Status
Not open for further replies.
Miezi michache iliyopita vyombo vya habari vilisheheni taarifa ya magaidi waliokuwa katika vijiji vya Handeni.

Taarifa zilifika Tanga kuwa kulikuwa na magaidi wanaishi katika mahandaki na operesheni maalum ilikuwa ikifanyika kuwateketeza.

Propaganda ikaenezwa kuwa walikuwa hawaitambui serikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Habari zilivuja Tanga mjini na vitongiji vyake kuwa kuna vijiji vimeteketezwa.

Kwa hakika kuna watu waliletwa Hospitali ya Bombo wakiwa na majeraha ya risasi.

Kwa watu waliofika Hospitali ya Bombo kwa kweli waliwaona vijana waliokuwa wamefungwa pingu wakiwa katika vitanda vyao huku wakilindwa na askari.

Taarifa zikafika vilevile kuwa kuna watoto wadogo wamefikishwa Tanga baada ya kukutwa porini.

Watoto hawa walikuwa wamehifadhiwa katika moja ya shule za hapo mjini.

Katika hali kama hiyo vilevile zikafika taarifa tofauti kwa Waislam wa Tanga kuwa hao walioletwa Hosptali ya Bombo na watoto waliookotwa porini ni Waislam wa vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande walioshambuliwa na askari pasi na sababu.

Juhudi za Umoja wa Taasisi za Kiislam Tanga (SHITA) chini ya Mayor Omari Guledi na Katibu wake Ahmed Mustafa kukutana na Mkuu wa Mkoa Chiku Galawa kupata ukweli zikagonga mwamba.

Hali ikawa tete baada ya Sheikh Rajab Ramadhani Chambuso mmoja katika masheikh vijana mjini Tanga kukamatwa na kuwekwa rumande kisha kuhamishwa Handeni ambako alifunguliwa kesi ya ''kushawishi mauaji.''

Ikavuma kuwa patakuwa na maandamano kushinikiza kuachiwa kwa Sheikh Chanmbuso.

Askari wa FFU walizingira misikiti kadhaa Ijumaa hiyo lakini hapakuwa na maadamano yoyote.

Alipopata dhamana na kuachiwa Sheikh Chambuso alikuja Tanga na habari za kutisha kuhusu dhulma iliyopita katika vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande.

Habari hizi alielezwa na mahabusi wendake katika hivyo vijiji vilivyoshambuliwa.

Sheikh Chambuso katika hotba aliyotoa katika moja ya misikiti maarufu Tanga aliwafahamisha Waislam kuhusu misikiti iliyovujwa na kuchomwa moto, Qur'an zillizochoiwa moto na nyumba za Waislam zilizoteketezwa kwa kisingizo cha ugaidi.

Wananchi jioneeni wenyewe yote hayo katika hizi picha.

PS: Weka cursor kwenye picha click utapata na maelezo ya picha.

Mhe. Rais aliyajua haya ndiyo maana akawawekea IGP muislamu,naamini angekuwa mkristo mngesema hujuma za wakristo.Je sasa muislamu mwenzenu anafanya vita dhidi ya uislamu? mm niwashauri waislamu msiwe wepesi kukimbilia kutaja udini katika matukio ya aina hii. mm siamini kuwa waliotendewa huo unyama ni waislamu peke yao kwani waislamu wana ndugu ambao sio waislamu na wengine hawana dini ambao wengine matukio haya yaliwakumba

mbona hauzungumzii vijiji viwili au vitatu vya Serengeti zilivyofutwa kwa nguvu ya polisi(nyamuma) na haya mnayolalamikia yalifanyika kule? je wakristo nao waamini kuwa ile ilikuwa hujuma dhidi ya ukristo iliyofanywa na waislamu? jibu ni hapana

tukumbuke ripoti ya kamati ya bunge ya juzi watu wametendewa unyama na uovu mkubwa ambao mwingine hata mkoloni asingeweza kuwatendea watu hawa lakini wametendewa. katika watu waliotendewa uovu walikuwemo watu wenye dini na wale wasio na dini. je hapa napo tuamini kuwa hayo yametokea kwasababu ya kutaka kuhujumu dini ya mtu, jibu sio kweli. tatizo naliona liko kwa watendaji wanaotumwa, inaonekana hawana uweledi wa taaluma yao hivyo wanafikiri wakifika wakachoma nyuma na kuwatendea watu uovu watakuwa wamewafurahisha mabosi zao na watapandishwa vyeo

mm niwashauri vijana wenzangu, kuwa udini sio mzuri kuuendekeza mwisho wa siku tutauana kwa madai ya kutetea dini zetu. hakuna vita mbaya duniani kama vita ya udini, mtu anaweza kufanya chochote ili kutetea dini yake

ushauri wangu ni kuwa nchi yetu imekumbwa na matukio mengi ya mauaji na utesaji wa watu na hakuna mtu ambaye hata leo amewajibishwa watu wakaona kweli hatua muhimu zimechukuliwa. la msingi kama nchi tujiulize ni wapi tulipokosea? kubwa zaidi hakuna uwajibikaji miongoni mwetu na viongozi wetu,kwani kuna makosa mengi yanafanyika ambayo watu walitakiwa washitakiwe hata kufungwa kabisa lakini hakuna hatua iliyochukuliwa hadi sasa.

naishauri ccm yenye serikali, iache mchezo kwenye maisha ya watu, kama ilivyoanza kuwashughulikia mawaziri mizigo na watendaji wasiofaa iongeze nguvu haya tunayoyaona yatatoweka kabisa. Lakini ccm ikijisahau wananchi wataendelea kuumia na matokeo yake wataifanya jamii iwachukie na kuwapenda wapinzani

nasema haya unayosema, si haki mtu kutendewa,tuwasiliane na watetezi wa haki za binadamu ili hatua zichukuliwe na wanaohusika wawajibishwe haraka iwezekanavyo. Naamini Mhe. Rais hatayafumbia macho, atachukua hatua ya haraka kama alivyofanya kwa mawaziri waliokiabisha chama, Serikali na Watanzania kwa ujumla. hakika hawa ndugu zangu wanastahili fidia kwa kadiri utu wao ulivyodhalilishwa

kingine tuombe taarifa ya uchunguzi ya kina sio kama ulivyoandika naona imekaa kiuchokozi sana, waandishi wapelelezi wafanye kazi yao kisha watuletee taarifa kwanini hatua hizo zilichukuliwa. unaweza kushangaa wale unaowatetea wao ndio wakawa wenye makosa? tuombe tume ifanyie kazi hili itueleze ukweli bila aibu, ndipo tutakuwa katika nafasi nzuri kuhitimisha mjadala huu
 
Naona mjadala umerudi mahala ulipopaswa sasa na sie wengine tusiopenda harsh language tunaweza kurudi jamvini .Shukrani kwako Ntuzu na huyu bwana anaitwa bin Rabah mmefanya kazi kubwa sana.Hapo juu ndugu yangu Ntuzu umenikumbusha swali langu mwanzoni kabisa nilimuuliza mzee Said naona anakula krismasi maana hajanijibu(natania tu),sasa sijui kama ndugu yetu bin Rabah na waislam wengineo humu mnaweza kutujibu mie na Ntuzu?Ntuzu ameuliza kama kuna harakati za kujitetea kwa kutumia nguvu zinazoruhusiwa na quran,bin Rabah ukamjibu vizuri tu kwamba zipo lakini kuna vigezo vya kuanzisha harakati hizo ili ziwe halali kwa mujibu wa quran,akauliza tena Ntuzu,akitaka umtajie hivyo vigezo,ndio na mie nakumbushia swali langu kwa mzee Said ambalo bin Rabah naomba uliongezee hapo kwenye swali la Ntuzu,nalo ni hili kwa kifupi,kuna fundisho lolote katika uislam linalomtaka muislam kuutangaza uislam wake kwa maneno na matendo ili upate kujulikana kwa usahihi kwa watu wote hata wale wasio waislam?kama lipo,je,waislam mnafanya nini ili kuhakikisha watu wanatofautisha uislam wa kweli na ule "wa kusingiziwa"?naongezea pia,tunawezaje kutofautisha harakati za haki za waislam na harakati za magaidi wanaotumia jina la uislam kufikia malengo yao mengine?hili ni tatizo kubwa sana ambalo linaukumba hata ukristo nyie wenyewe mnaona watu ni maaskofu wakubwa duniani lakini wanalawiti watoto,makanisa yanaruhusu ndoa za kishoga,hawa akina Cameron ni wakristo waanglikana wanakwenda kanisani na bado wanamwambia maskini wa kiafrika kwamba "hatukupi msaada hadi ukubali kuparamiana",na hii ni sera ya serikali zinazojinasibisha kuwa za kikristo,je biblia inaruhusu hayo?sasa mtu asiye mkristo tunamweleza nini ili atofautishe harakati za ukristo wa kweli na ule "wa kusingiziwa"?unaona hapo?si ndio hili tatizo hata kwa uislam pia isipokuwa tu huku ushoga kule ugaidi?tunazisafisha vipi dini zetu sisi wenyewe kwanza kabla ya wengine kutuambia la kufanya?sijui nimeeleweka?
Juve2012.
Kwanza kabisa nataka nikujulishe uislamu unapingana na UGAIDI usione hivi vikundi vinavyo jilipua kwa mwamvuli wa kutumia uislamu ukawahukumu waislamu wote.

Ukitaka kujadiliana siku zote mambo ya imani jadiliana kwa kupitia vitabu sahihi vya huyo unaejadiliana nae sio kukurupuka na kuingia kwenye mtandao na kucopy and paste kama wakristo wengi wanavyo fanya huku kwenye mitandao ya kijamii.

Utakuta mtu amechukua hadithi ya mtume Muhamad (S.A.W)na kuileta huku bila hata kujua wanachuoni/maulamaa wa kiislamu wanaizungumziaje hiyo hadithi ni sahihi au dhaifu.

Na katika uislamu kuna somo linaitwa "mustalawal hadithi" ni lazima ujue haya mambo ndio uweze kuelezea mambo ya hadithi na ujue pia kitu kinaitwa "ilmu rijal" ndio utajua mpokeaji wa hadithi hii ni mkweli au muongo na mengineyo.....

Kwahiyo muislamu haruhusiwi kumuua mkristo hata kama anaishi nchi iliyo chini ya dola ya kiislamu, mkristo anahaki ya kuishi pale bila kubughudhiwa ilimradi atii sheria zilizoko pale na yeye atafanya ibada zake huko aliko bila ya kudhuriwa.

Kwahiyo haya yaliyotokea Kilindi mimi nilishangaa sana kwataarifa nilizo nazo nasikia ulikuwa ukionekana suruali yako ni fupi na unandevu nyingi unakamatwa unaonekana wewe ni GAIDI.

Napenda kuwafahamisha mtu kufuga ndevu au kukata suruwali sio GAIDI kwasababu haya ni mambo ya kiimani wala hayahusiani na UGAIDI na wakristo wengi wanapenda kuwashutumu watu wenye kukata suruali na kufuga ndevu na kuwaita AL QAIDA hicho kitendo sio kizuri na hakitupendezi sisi ni hayo tu.

Ahsanta.
 
Mhe. Rais aliyajua haya ndiyo maana akawawekea IGP muislamu,naamini angekuwa mkristo mngesema hujuma za wakristo.Je sasa muislamu mwenzenu anafanya vita dhidi ya uislamu? mm niwashauri waislamu msiwe wepesi kukimbilia kutaja udini katika matukio ya aina hii. mm siamini kuwa waliotendewa huo unyama ni waislamu peke yao kwani waislamu wana ndugu ambao sio waislamu na wengine hawana dini ambao wengine matukio haya yaliwakumba

mbona hauzungumzii vijiji viwili au vitatu vya Serengeti zilivyofutwa kwa nguvu ya polisi(nyamuma) na haya mnayolalamikia yalifanyika kule? je wakristo nao waamini kuwa ile ilikuwa hujuma dhidi ya ukristo iliyofanywa na waislamu? jibu ni hapana

tukumbuke ripoti ya kamati ya bunge ya juzi watu wametendewa unyama na uovu mkubwa ambao mwingine hata mkoloni asingeweza kuwatendea watu hawa lakini wametendewa. katika watu waliotendewa uovu walikuwemo watu wenye dini na wale wasio na dini. je hapa napo tuamini kuwa hayo yametokea kwasababu ya kutaka kuhujumu dini ya mtu, jibu sio kweli. tatizo naliona liko kwa watendaji wanaotumwa, inaonekana hawana uweledi wa taaluma yao hivyo wanafikiri wakifika wakachoma nyuma na kuwatendea watu uovu watakuwa wamewafurahisha mabosi zao na watapandishwa vyeo

mm niwashauri vijana wenzangu, kuwa udini sio mzuri kuuendekeza mwisho wa siku tutauana kwa madai ya kutetea dini zetu. hakuna vita mbaya duniani kama vita ya udini, mtu anaweza kufanya chochote ili kutetea dini yake

ushauri wangu ni kuwa nchi yetu imekumbwa na matukio mengi ya mauaji na utesaji wa watu na hakuna mtu ambaye hata leo amewajibishwa watu wakaona kweli hatua muhimu zimechukuliwa. la msingi kama nchi tujiulize ni wapi tulipokosea? kubwa zaidi hakuna uwajibikaji miongoni mwetu na viongozi wetu,kwani kuna makosa mengi yanafanyika ambayo watu walitakiwa washitakiwe hata kufungwa kabisa lakini hakuna hatua iliyochukuliwa hadi sasa.

naishauri ccm yenye serikali, iache mchezo kwenye maisha ya watu, kama ilivyoanza kuwashughulikia mawaziri mizigo na watendaji wasiofaa iongeze nguvu haya tunayoyaona yatatoweka kabisa. Lakini ccm ikijisahau wananchi wataendelea kuumia na matokeo yake wataifanya jamii iwachukie na kuwapenda wapinzani

nasema haya unayosema, si haki mtu kutendewa,tuwasiliane na watetezi wa haki za binadamu ili hatua zichukuliwe na wanaohusika wawajibishwe haraka iwezekanavyo. Naamini Mhe. Rais hatayafumbia macho, atachukua hatua ya haraka kama alivyofanya kwa mawaziri waliokiabisha chama, Serikali na Watanzania kwa ujumla. hakika hawa ndugu zangu wanastahili fidia kwa kadiri utu wao ulivyodhalilishwa

kingine tuombe taarifa ya uchunguzi ya kina sio kama ulivyoandika naona imekaa kiuchokozi sana, waandishi wapelelezi wafanye kazi yao kisha watuletee taarifa kwanini hatua hizo zilichukuliwa. unaweza kushangaa wale unaowatetea wao ndio wakawa wenye makosa? tuombe tume ifanyie kazi hili itueleze ukweli bila aibu, ndipo tutakuwa katika nafasi nzuri kuhitimisha mjadala huu
Haya unayoyasema usidhani waislamu wanakurupuka na hii yote inatokana na marekani kwasababu leo hii kila kinachotokea nchi za kiislamu utasikia kuna magaidi kila tukio baya ni waislamu ndio maana utaona waislamu nao wanalalamika.

Yanayoendelea Afrika ya kati unayasikia lakini pale huambiwi ni ugaidi unaendelea na miskiti inachomwa moto wao hilo hata haliwasumbui inasikitisha sana halafu wanajeshi wa Ufaransa kutuliza ghasia!
 
Samahani Mkuu Bilal bin Rabah;

Ebu Naomba Tujaribu kuzichambua Taarifa ya Mleta mada ndugu Mohamed Said na ndugu Bopwe aliyo ileta ya gazeti la Nipashe kisheria!

Sio km nakupinga Mkuu hoja zako ila nachopenda tuangalie haya mambo Kwa pande zote! Ili tuweze kuiona Dhuluma dhidi ya Imani yako Mkuu!

Narudia tena samahani km ntakua nimekukwaza!

Thx!
 
Samahani Mkuu Bilal bin Rabah;

Ebu Naomba Tujaribu kuzichambua Taarifa ya Mleta mada ndugu Mohamed Said na ndugu Bopwe aliyo ileta ya gazeti la Nipashe kisheria!

Sio km nakupinga Mkuu hoja zako ila nachopenda tuangalie haya mambo Kwa pande zote! Ili tuweze kuiona Dhuluma dhidi ya Imani yako Mkuu!

Narudia tena samahani km ntakua nimekukwaza!

Thx!
Ntuzu.
Hebu jibu kwanza hayo maswali matano aliyouliza Bopwe kwenye hiyo taarifa kwenye gazetila nipashe halafu tuendelee na "mnakasha"
 
Ntuzu.
Hebu jibu kwanza hayo maswali matano aliyouliza Bopwe kwenye hiyo taarifa kwenye gazetila nipashe halafu tuendelee na "mnakasha"


Mkuu! Kwanza Nakushukuru Kwa hoja zako!

Nimeyapitia hayo maswali ya Mkuu Bopwe! Nimeona kuyajibu Mimi km Mimi ni magumu! Ila ninachweza Kusema km tungepata wataalamu Wa sheria wangetusaidia juu ya hili na kuweza ata kuyajibu hayo maswali ya ndugu Bopwa!

Ila ninachoweza Kusema ndugu Bopwe ameuliza maswali ya mwisho kabisa juu ya kadhia Hiyo na Kwa swala hili km hili lilivyo alikua anapaswa kuanzia mwanzo Yani kwenyechanzo mpk huko Kwa namna gani Polisi walitekeleza Hiyo Oparesheni Yao! Na ni vema kuangalia pande zote mbili!

Thx
 
Samahani mkuu usemalo ni UONGOOO!...

"The only real wisdom is knowing you know nothing" Socrates

In 628 CE, a delegation from St. Catherine's Monastery came to Prophet Muhammad and requested his protection.

In 628 CE, a delegation from St. Catherine's Monastery came to Prophet Muhammed and requested his protection.
He responded by granting them a charter of rights, which I reproduce below in its entirety. St. Catherine's Monastery is located at the foot of Mt. Sinai and is the world's oldest monastery.

It possesses a huge collection of Christian manuscripts, second only to the Vatican, and is a world heritage site. It also boasts the oldest collection of Christian icons. It is a treasure house of Christian history that has remained safe for 1400 years under Muslim protection.

The Promise to St. Catherine:

"This is a message from Muhammad ibn Abdullah, as a covenant to those who adopt Christianity, near and far, we are with them.

Verily I, the servants, the helpers, and my followers defend them, because Christians are my citizens; and by God! I hold out against anything that displeases them.

No compulsion is to be on them. Neither are their judges to be removed from their jobs nor their monks from their monasteries. No one is to destroy a house of their religion, to damage it, or to carry anything from it to the Muslims' houses.

Should anyone take any of these, he would spoil God's covenant and disobey His Prophet. Verily, they are my allies and have my secure charter against all that they hate.

No one is to force them to travel or to oblige them to fight. The Muslims are to fight for them. If a female Christian is married to a Muslim, it is not to take place without her approval. She is not to be prevented from visiting her church to pray. Their churches are to be respected. They are neither to be prevented from repairing them nor the sacredness of their covenants.

No one of the nation (Muslims) is to disobey the covenant till the Last Day (end of the world).
"
That is islaam that the world has lived with for centuries until the arrival of Osama bin laden and the likes. Arab and palestinian resistence to occupation has always taken a secular ideology until islamic fundamentalists took the stage and refused to put a difference between western imperialism and christianity and hence starting a hate campaign against christians. So what I am making reference to is the present time.
 
what do you mean by credible?.

Unawajua hao akina bush na bandar bush au hujawahi kusikia mambo yao?.
Juzikati hapa huyo prince bandar ambae ndo chief wa saud intelligence amekwenda sochi Russia na akajaribu kumtisha putin kwamba aachane na mambo ya kuisaidia syria ama sivyo magaidi wa kichechniya ambao wako controlled na wao watalipua michezo ya olimpiki ya sochi.hii kitu iko reported na Mainstream media na si concipiracy.
Huyu bush junior wakati akitaka kugombea urais ,babake yaani Bush mkubwa alimwambia,''The man to talk to if you want to succeed is Bandar,talk to him''.
Kuna connection kubwa sana kati ya hawa watu na mambo ya kigaidi mengi yanayofanyika ni kiini macho tu kwa ajili ya kufikia agenda fulani.
mkuu kinachoandikwa kwenye mainstream media kinakuwa na chembe ya ukweli kuliko conspiracies ambazo hazibebi mainstream thinking na mara zote zimejaa pessimistic views.
pia ujue hata habari inapoandikwa mwandishi naye anayo mapenzi binafsi anaweza kuwa biased. majuzi obama aliruhusu gaidi mmoja maarufu sana na kiongozi kutoka taliban aachiwe huru kwa lengo la kwenda kuwashawishi wenzake waachane na uasi dhidi ya marekani na hii ikiwa na lengo kuwa ni mkakati mpya wa marekani kufikiria kuacha matumizi ya nguvu kupambana na ugaidi kwakuwa ni muda mrefu hayajaonyesha mafanikio.pia kuna swala la kufunga gereza la guantanamo, lakini wapo watakoamini kuwa marekani inashirikiana na magaidi. marekani ndio ilipeleka azimia UN kuhusu vita dhidi ya ugaidi iweje leo tuamini kupitia habari za vichochoroni kuwa marekani ndio wanaopika kilakitu.
 
Si kweli kwamba ati waislamu tunatetea kila jambo hata ovu walifanyalo waislamu kisa tu ni wa imani yetu. Kinachowafanya nyinyi muone tunatetea ni kwakuwa sisi tunahoji sababu za waislamu kuingia katika vita au kuua hovyo wasiokuwa waislamu. Ndio haya tuyasemayo na aliyoyaleta mzee MS yaani propaganda. Waislamu wanaingia katika matendo ya ulipuaji na kuuwa hata watoto, wakinamama na wazee na hata wale ambao hawajahusika katika uovu waliofanyiwa waislamu kwakuwa imewabidi kufanya hivyo. Tizama uovu wanaofanyiwa watoto,wanawake na waislamu wote kwa ujumla pale Somalia na majeshi ya kigeni na yale yaliopo nchini mule ambao ni vibaraka wa Amerika na washirika wake. Hivi mtoto miaka mitano anayeshuhudia mzazi wake akiuliwa kikatili unadhani atakuwa na mentality gani? Je baadae nae akienda kuua ndugu za yule aliyemuua mzazi wake tukambandika jina la ugaidi ni sawa? Je mimi nikihoji au kuwa upande wake ndio nionekane mimi natetea uislamu?
Wengi tunaamini ukiwaua watu wasiokua na hatia yoyote ni ugaidi na kama ni muamini wa dini yoyote ni dhambi kwa mwenyezi mungu
 
Sio kweli kwamba kule kilindi Tanga kulikua au kuna al shabab. Ukitaka kujua anza kutafuta nini ilikua sababu ya operation ile hatamu.
Chanzo cha vurugu ni ugomvi wa mgambo na wakulima na wafanya biashara wa hiliki.mgambo walikua wanalazimisha kwa kutumia nguvu ulipaji wa kodi haramu kwa mazao.na inaonekana ni mazoea yao kutumia mwanya wa kuvaa magwanda yao na kuwaonea raia wasi na hatia. Wananchi kwa pamoja walikataa uonevu ule hali iliyopelekea mapambano na kusababisha kifo cha mgambo mmoja na wananchi kadhaa kujeruhiwa.
Tukio lile likafika polisi nao badala ya kufanya uchunguzi wa tukio walikwenda ki operation na ilawa ni hali ya mapambano baina yao na raia watu wengi wakajeruhiwa na akiwamo polisi.
Polisi wakaongezewa nguvu na ndipo walipo fanya collective punishment. Na raia wakajificha kwenye misikiti lakini hio haikua dawa kijiji kizima kilikua katika kushambuliwa wanawake wakakimbia mapolisi wakaacha watoto wao. Wanaume wengi wakakimbilia maporini.
Kutokana na uhalifu ulofanyika kuwa mkubwa ndio kama kawaida afande masawe akatangaza kuwa ilikuwa operation ya kupigana na alshabab.
Yote kujaribu ku cover up uhalifu waliowafanyia raia.
Wakati yeye akitangaza anapambana na alshabab mkuu wa mkoa bibi chiku anasema hakuna gaidi ni wavunja sheria tu.
Hivyo tukirudi kwenye suala la mada kuu jibu ni kuwa vita ya ugaidi inatumiwa kama mwanya wa kuubamiza uislam. Waloathirika ni waislam .misikiti yao ilivamia na maimam ndio walokamatwa.
Kutoka vurugu za kuuza hiliki mpaka ikageuzwa kuwa ugaidi...

pengine ni kwa maslahi ya taifa katika kuzuia machafuko ya kidini nchini yanayojitokeza nchini, labda chiku akajaribu kubadilisha kauli kwa kutumia lugha za kisiasa, ama hawakuwa wametaarifiana, japo sina hakika kwamba wananchi wanatakiwa waamini kauli ya nani kati ya mkuu wa mkoa na mkuu wa polisi. ushauri wangu hapa ni kuwa huyu shekh na wenzake warudi wakamuulize tena bi chiku aseme alichokisema mwanzo na ahojiwe kuwa mbona kauli yake inatofautiana na ya mkuu wa polisi?
pia nilishaeleza chiku sio afisa upelelezi ni mwanasiasa tu sitegemei atoe habari za kiuchunguzi. Ni daktari tu na mtoto mdogo wanao uwezo wa kutoa ushahidi utakaoaminika kwa wananchi kwani unakidhi vigezo vya kiupelelezi zaidi na sheria za kimahakama. na ikumbukwe kwenye lile tukio walikuwepo watoto waliodaiwa kuwakana wazazi wao kuwa sio waislamu halisi.
mwisho nilitoa maelezo nilihitimisha kuwa vyovyote vile hata kama jeshi la polisi lina makosa kiasi gani bado halina lengo la kupambana na uislamu.
 
Binaadamu mwenye kutumia akili huwa haangali nini wengi wanafanya!
Bali huangalia UKWELI WA MAMBO!

Matukio mangapi ambayo mataifa yana azimisha kila mwaka ambayo yanapewa majina mazuri lkn UHALISIA WAKE SIO KABISA HUO!

Na unaposema " better find which source is more credible to you"!!

Vipi mtu mwenye busara aamue yeye mwenyewe kuchagua credible sources azitakazo yeye?? Na asijali zile zinazokubalika kimataifa??

Wewe vipi unaweza ku crisis Source yyt wakati hujatuonyesha sababu za kuzifanya hizo source not credible enough? ?

Au ni zile chuki zako za kigalatia zimekufunga macho mpaka sources zozote zenye Uhusiano wwt na Muslim zinakuwa hazifa?

Akili za namna hii huwa zina tabia ya kumuathiri mwenyenazo tu! Na si mwingine.

mkuu labda nifafanue, ni kawaida source zinazoaminika duniani mbali na kuaminika huko pia zina weza kutofautiana kimtazamo. mfano CNN,BBC, SKY NEWS zinaweza kutofautiana kwa mtazamo na Aljazeera, CCTV. though they all credible sources.
lakini kutumia conspiracies kama source ya kupata habari mfano wakina david icke, huu utakuwa ni upuuzi. watu makini wanaheshimu mainstream thinking na sio skepticism from minor. mwenzako amenielewa hapa. mtu makini anaweza kutambua credible sources, na anajua hizi sources zinatabia ya tofautiana pia hata katika habari ya aina moja.
 
TANGA: Mji wenye tamaduni nyingi za Kiislamu


MJI wa Tanga ni moja kati ya miji iliopo katika ukanda wa Pwani wa Afrika ya Mashariki wenye Waislamu wengi. Inakadiriwa kuwa karibu asilimia 80 ya wenyeji wa mji huo ni Waislamu jambo lililofanya mji huo kuwa na tamaduni nyingi za Kiislamu. Kwa miaka mingi mji wa Tanga umekuwa moja ya miji ya Afrika ya Mashariki ambao umekuwa ukiheshimiwa miongoni mwa Waislamu wa Afrika Mashariki.
WENYEJI wa mji huo ni Wadigo na Wasegeju ambapo ukichukuliwa kimkoa una mchanganyiko wa Wazigua, Wabondei na Wasambaa. Katika sehemu zote za mji huo ambazo utatembea utakuta madrasa ndogo ndogo za watoto zisizo na idadi, Misikiti na pia kuna vyuo vikuu vitatu vinavyotoa elimu ya dini ya Kiislamu. Vyuo hivyo ni TAMTA, ZAHRAU na MAA-WA.
Chuo cha TAMTA ambacho ni cha kwanza na cha muda mrefu zaidi kilichopo eneo la Gatundu kiliasisiwa na Sheikh maarufu Afrika Mashariki, marehemu Sheikh Mohammed bin Ayoub, aliyefariki mwaka juzi na kuacha uongozi kwa mwanafunzi wake mkuu Sheikh Mohammed Bakar.
Chuo hiki huchukua wanafunzi mbalimbali kutoka nje ya mkoa na nje ya nchi na kina matawi yake katika wilaya za mkoa huo na nje ya mkoa. Wanazuoni wengi wenye madrasa kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini walipata elimu zao kutoka chuo hiki.
Aidha, Chuo cha ZAHRAU ambacho kiliasisiwa na marehemu Sheikh Selemani kilichopo eneo la Madina, pia huchukua wanafunzi kutoka nje ya mkoa na kina matawi yake kadhaa hapa nchini. Hivi sasa kinaongozwa na Sheikh Mohammed Selemani ambaye ni mtoto wa kwanza wa Sheikh Selemani.
Chuo cha MAA-WAL kipo eneo la Mwakizaro na kimejenga shule ya sekondari katika eneo la Ngamiani. Chuo hiki kilianzishwa na marehemu Sheikh Shabani na hivi sasa kinaongozwa na Sheikh Mohammed Hariri.
Miongoni mwa Misikiti mikubwa ya Ijumaa iliopo katika mji huo ni Msikiti wa Riyadha uliopo katika eneo la Ngamiani ambao ndio mkubwa kuliko yote uliojengwa tangu enzi za wakoloni ambapo katika miaka ya karibuni uliongezwa tena.
Pia kuna taasisi ya Kiislamu ya Answar Sunna ambayo imeendeleza zaidi maendeleo ya Uislamu ya mji huo kwa kuanzisha shule ya chekechea ya Kiislamu na shule ya msingi ambayo pia hutoa mafunzo ya kidini na kufundisha Kiarabu. Shule hii ipo eneo la Msambweni.
Taasisi hii pia imejenga kituo cha watoto yatima kilichopo eneo la Makorora na ina mpango wa kujenga shule ya sekondari katika eneo la Pongwe.
Kwa vile asilimia kubwa ya wenyeji wa mji huo ni Waislamu, Uislamu unaonekana kuwa na nguvu kuliko dini nyingine na hivyo mji mzima kutawaliwa na mazingira ya Kiislamu.
Tukiacha Misikiti inayoonekana katika mitaa mbalimbali pamoja na madrasa za watoto, mavazi rasmi ya wazee wa mji huo ni kanzu, kofia na bakora. Kwa upande wa wanawake, mabaibui hutumika kama vazi maalum la kutokea. Mavazi ya hijabu na kujitanda khanga mbili ni ya ada sana kwa wasichana waliofikia umri wa kuolewa.

Miongoni mwa mambo yanayodhihirisha kutopea kwa tamaduni za Kiislamu katika mji huo ni salamu wanayopeana watu wanapokutana bila kujali ni wa dini gani. Salamu kubwa inayotumika katika mji huo ni Salaam Alaikum. Hata Wakristo wachache wa mji huo wameizoea salaam hii na kupeana hata wenyewe kwa wenyewe. Ni jambo la kawaida pia kumsikia mtu akishukuru kwa tamshi la Alhamdulillahi au akitumia neno IshaAllah hata kama si Muislamu.
Katika mji huo kunakuwa na mabadiliko makubwa katika miezi ya kawaida na mwezi wa Ramadhani. Pamoja na kuwepo na watu wa dini nyingine lakini anaweza kuhisi kuwa kila mtu anafunga katika mwezi huo kwa sababu unaheshimiwa na hata wasiokuwa Waislamu.
Huduma za chakula wakati wa mchana zinakuwa adimu. Unaweza kuzunguka mji mzima bila kukuta mgahawa ulio wazi na pale unapobahatika kukuta sehemu inayouza chakula utakuta pazia kwenye mlango ili kuficha waliomo ndani. Biashara ndogondogo kwenye mitaa kama vile kahawa, tangawizi, maji baridi na nyinginezo huachwa na kuonekana wakati wa magharibi.
Katika kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani kunakuwa na makundimakundi ya kina baba na kina mama kwenye maduka kutafuta nguo mpya za watoto wao kwa ajili ya sikukuu ya Idd el Fitr inayoadhimishwa kila baada ya mfungo wa Ramadhani.
Ni katika kipindi hiki ambapo wenye maduka ya nguo katika mji huo huneemeka na kufanya biashara zao kwa uhakika zaidi. Kuna maduka ambayo hufufuka katika kipindi hiki tu na baada ya sikukuu kupita hufa na kusubiri mfungo mwingine.
Tanga ni mji unaongoza Tanzania kwa ustahamilivu wa kidini.hakujawahi kuwa na misuguano kati ya wakristo na waislam. Nimeishi Tanga kwa miaka mitatu.zile Big November Crusade kila mwaka zilikuwapo Tanga, wala haijawahi kutokea rabsha yoyote ingawa waislam ni wengi na mikutano ile ikifanywa katika maeneo yao.kwa tanga msuguano kati ya Zaharau na Tamta ni mkubwa sana kwenye mambo ya Maulid na mengineo , ni msuguano wa kitaalam zaidi kila mmoja akishandana na mwenzie kuhusu lipi sahihi na lipi si sawa katika iman.
Ushabiki huu wa TAMTA NA ZAHARAU umeenea maeneo yote ya mkoa wa Tanga ikiwamo Kilindi.
Iliripotiwa hivi kwenye sherehe za Tamta mwaka jana:
ZAHARAU DAY SIKU MOJA NA TAMTA
Sherehe za mwaka huu za taasisi kongwe nchini katika hali nadra sana zimeanza na kumalizika kwa siku moja.mahudhurio nayo yalionekana kugawanyika kisawa sawa.muda wote sherehe za siku tatu waumini walionekana wakikatiza kutoka barabara itokayo TAMTA kuja Zaharau.Kwa vile sherehe za Tamta zilimaliza mapema saa sita usiku makundi ya watu walikatiza kuelekea Zaharau kuendelea kusikiliza mawaidha.
Hawa ndio watu wa TANGA.


Jee TAMTA NA ZAHARAU KUNA MSUGUANO GANI ?
Msuguano huu sio wa kupigana bali kama wa simba na yanga naweza kuuita.Lakini mahusiano kati ya waislam na wakristo yapo shwari kabisa hakuna msuguano hata wa kimawazo kama huu wa ndugu zao Tamta na zahrau.

Lakini Leo wanapangwa viongozi kuwatumikia wananchi lakini wanakuja na fitna za kutaka kuwagombanisha kwa kuja na agenda za watu wengine.
sheikh Mohamed said atanirekebisha maana yeye mjuzi zaidi wa huko Tanga

Crabat,
Umeyaweka sawa kabisa.

Hakika hiyo ndiyo Tanga waijuayo wengi.
 
Umekosa cha kukanusha hapo umeishia kutoa kejeli tu, huu ni ukweli usiopingika.
Uenezaji wa uislamu sio persuasion, ni kuforce.

Nimeipenda hii;
Waislamu wakiwa

1%, utawaona ni wapole sana, huku wakirecruit mionr groups, jail hadi street gangs,
Wakifika 5%, wanaanza kudai halal food, inawapa ajira ya kuandaa vyakula,
8%, wanaanza kudai wajitawale kwa sharia zao tu,
20%, hapa tegemea maandamano na vurugu,
40-50%, ubaguzi na chuki dhidi ya wasio waislamu,
80%, hapa ni genocide na non believer cleansing, uchomaji wa makanisa na mauaji ya mapadre na wachungaji ni jambo la kawaida katika asilimia hii mpaka ifikie 100%waislamu.
Lengo likiwa ni kusilimisha dunia nzima na kuweka sharia.

Haya ndio malengo halisi ya uislamu, ndio maana malalamiko wa waislamu hayawezi kukoma mpaka dunia nzima itakapo silimu.
We kiumbe wa ajabu sana!
Unatuwekea SOURCE FROM "CIA" Halafu unaweka swali mbele yake!!

We ulivyo msukule unategemea CIA wataongea mambo MAZUUURI KUHUSU WAISLAMU SIO??

Elimu za kata ni janga kuu!!
Akili za ku copy and paste huwezi kuzigeuza.
 
That is islaam that the world has lived with for centuries until the arrival of Osama bin laden and the likes. Arab and palestinian resistence to occupation has always taken a secular ideology until islamic fundamentalists took the stage and refused to put a difference between western imperialism and christianity and hence starting a hate campaign against christians. So what I am making reference to is the present time.
My Dear Kmbw hope u r OK; Hakuna ukweli kuwa tuna hate Christians !! NO NO and big NO !! The last wife of our prophet SAW was a Christian.... Muslim are respecting the CHRISTIANS and for year they live side by side. Mkuu acha kunukuu kama kasuku maneno ya WACHONGANISHAJII waisilamu wema na Waumini Islam wa kweli hujua Obligations za Dini zote zilizoteremka. Asilimia kubwa tumesoma as one nation na tunaiishi as One humankind. Heshima za kijamii zinadhihirisha uaadilifu wetu juu ya wakiristo na dini za mbinguni..... Tafadhali fungua kifua uone uzuri na amani ya wenzio... usijifunge na kubobea chuki zilizopikwa. Kwa miaka mingi nchini tunasafiria Mtumbwi au Meli moja "sasa kama kuna wabaya wanaanza kutoboa mgongo / kizingiti wa chombo chetu, Basi tutazamaa majini. Mungu apishe mbali... With love and prospects together. Good Luck and stay in peace.
 
My Dear Kmbw hope u r OK; Hakuna ukweli kuwa tuna hate Christians !! NO NO and big NO !! The last wife of our prophet SAW was a Christian.... Muslim are respecting the CHRISTIANS and for year they live side by side. Mkuu acha kunukuu kama kasuku maneno ya WACHONGANISHAJII waisilamu wema na Waumini Islam wa kweli hujua Obligations za Dini zote zilizoteremka. Asilimia kubwa tumesoma as one nation na tunaiishi as One humankind. Heshima za kijamii zinadhihirisha uaadilifu wetu juu ya wakiristo na dini za mbinguni..... Tafadhali fungua kifua uone uzuri na amani ya wenzio... usijifunge na kubobea chuki zilizopikwa. Kwa miaka mingi nchini tunasafiria Mtumbwi au Meli moja "sasa kama kuna wabaya wanaanza kutoboa mgongo / kizingiti wa chombo chetu, Basi tutazamaa majini. Mungu apishe mbali... With love and prospects together. Good Luck and stay in peace.
Its good to read such kind words. Thanks
 
Umekosa cha kukanusha hapo umeishia kutoa kejeli tu, huu ni ukweli usiopingika.
Uenezaji wa uislamu sio persuasion, ni kuforce.

Nimeipenda hii;
Waislamu wakiwa

1%, utawaona ni wapole sana, huku wakirecruit mionr groups, jail hadi street gangs,
Wakifika 5%, wanaanza kudai halal food, inawapa ajira ya kuandaa vyakula,
8%, wanaanza kudai wajitawale kwa sharia zao tu,
20%, hapa tegemea maandamano na vurugu,
40-50%, ubaguzi na chuki dhidi ya wasio waislamu,
80%, hapa ni genocide na non believer cleansing, uchomaji wa makanisa na mauaji ya mapadre na wachungaji ni jambo la kawaida katika asilimia hii mpaka ifikie 100%waislamu.
Lengo likiwa ni kusilimisha dunia nzima na kuweka sharia.

Haya ndio malengo halisi ya uislamu, ndio maana malalamiko wa waislamu hayawezi kukoma mpaka dunia nzima itakapo silimu.
hakika maneno ya msingi sana hayo
 
Jamani huu ni upumbavu. tutakao bahatika kuishi miaka 10 mbele mtakataa kama mliwahi kujadili huu upumbavu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom