Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Status
Not open for further replies.
Siku waislamu watakapopinga makundi kama boko haram, alshababu na wengineo mtaonekana dini yenu haina mafungamano na ugaidi.
Acheni kujilipua kwa jina la allah

Birds of the same feather fly together!
 
Magaidi lazima yapigwe kwa nguvu zote! Haijalishi ni waislamu au watu wa dini nyingine. Wapigwe tu tumechoka. Nasema wapigwee tu..!
 
Dunia kwa kweli inaumiza kichwa juu ya ugaidi
kuanzia wewe sisi tuupinge kwa nguvu zote ugaidi
ni kukosa akili kuua watu hata ambao hawana makosa
 
Magaidi lazima yapigwe kwa nguvu zote! Haijalishi ni waislamu au watu wa dini nyingine. Wapigwe tu tumechoka. Nasema wapigwee tu..!

Mafinyofinyo,
Kweli magaidi lazima wapigwe.

Lakini hao wana vijiji wa Madina na vijiji vya jirani hawakuwa magaidi.
Kama upo ushahidi wa ugaidi na uletwe uonekane.

Waliouliwa wamezikwa kimya kimya na waliobaki wamefunguliwa mashtaka
mahakama ya Handeni.

Katika mashtaka yao hakuna kosa la ugaidi.
Sheikh Chambuso anajulikana kama mwalimu wa madras Tanga.

Yeye shitaka lake ni kama nilivyoeleza awali.
Sheikh Chambuso kafunguliwa kesi ya ''kushawishi mauaji.''

Dhulma kama hizi zinasikitisha sana na hazitajenga taifa letu bali
kuleta chuki.

Kwa ajili hii tunapochangia mjadala kama huu ni muhimu sana kuwa
makini.
 
Mafinyofinyo,
Kweli magaidi lazima wapigwe.

Lakini hao wana vijiji wa Madina na vijiji vya jirani hawakuwa magaidi.
Kama upo ushahidi wa ugaidi na uletwe uonekane.

Waliouliwa wamezikwa kimya kimya na waliobaki wamefunguliwa mashtaka
mahakama ya Handeni.

Katika mashtaka yao hakuna kosa la ugaidi.
Sheikh Chambuso anajulikana kama mwalimu wa madras Tanga.

Yeye shitaka lake ni kama nilivyoeleza awali.
Sheikh Chambuso kafunguliwa kesi ya ''kushawishi mauaji.''

Dhulma kama hizi zinasikitisha sana na hazitajenga taifa letu bali
kuleta chuki.

Kwa ajili hii tunapochangia mjadala kama huu ni muhimu sana kuwa
makini.

Mkuu Mohamed Said hii elimu unayotoa hapa jukwaani kwa mtanzania mpenda amani lzm afahamu kuwa HAPO NDIPO KWENYE SIRI YA AMANI!

Hao wanaokalia hizo dhulma japo kuwa mbele ya macho ya maadui wa waislamu wanaoneka mashujaa, chuki wanazozidi kupandikiza moto utakao waka huko mbele. Sidhani kama kuna mtanzania atakuja nusurika.
Tumeyaona kwa wenzetu. Na wengi walianza kama hawa.

Tunaomba Mungu atunusuru na shari ya hawa wanyanyasaji walio laaniwa ktk nchi yetu.
Amin
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said, huu nao ni uchochezi.
Unasema kuwa ilibainika waliokamatwa ni waislamu, hii ndio hoja gani mzee?, hata kama wangekuwa ni wakristo, kama wamehusika na jinai wakamatwe tu.
Haiingii akilini kwamba wamekamatwa tu eti kwa kuwa ni waislamu!!, Tanzania ina waislamu wangapi?, mbona hawakamatwi?
Jibu lake ni kuwa hao waliokamatwa kuna sababu, tena ya kijinai.
 
Pamoja na kwamba mimi ni muislam naona uzi huu haupo kihalisia. Hakuna haja ya kuhalalisha ufedhuli kwa kupitia mgongo wa Uislam. Chiku namfahamu asingelikubali kama mwislam angalikuwa anaonewa. Jamani ndugu zangu tuache kutumia dini kwa manufaa yetu binafsi. Wakristu hawatuonei ila sie ni inferiority complex zinazotuangusha. Karibu Njinjo

Nanjilinji,
Hujanionyesha hicho kisichokuwa na uhalisi.

Wala hujanieleza ufedhuli wa hawa ndugu zetu wa Madina na Dibungo.
Sawa Chiku unamjua lakini haupo peke yako wanaomjua Bi. Chiku.

Nao pia wana yao juu yake.
Sijaona suala la complex katika hili.

Nakueleza kuwa katika hili yapo mengi na In Sha Allah tutayaweka hapa
dunia ishuhudie.

Tujaalie kuwa palikuwapo na ufedhuli na kuna complex.

Sheria gani inaruhusu mafedhuli kuuliwa na misikiti yao na nyumba kuchomwa
moto?

Labda uwe huamini kuwa haya hayakutokea.
 
Mleta mada MS ni gaidi..

Tedo,
Nimekuwekea kama attach. paper yangu niliyowasilisha Chuo Kikuu Cha
Ibadan kuhusu ugaidi.

CONFERENCE ON ISLAM TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT




Isome kisha rudi tujadili ''ugaidi'' wa MS.
 

Attachments

Mohamed Said, huu nao ni uchochezi.
Unasema kuwa ilibainika waliokamatwa ni waislamu, hii ndio hoja gani mzee?, hata kama wangekuwa ni wakristo, kama wamehusika na jinai wakamatwe tu.
Haiingii akilini kwamba wamekamatwa tu eti kwa kuwa ni waislamu!!, Tanzania ina waislamu wangapi?, mbona hawakamatwi?
Jibu lake ni kuwa hao waliokamatwa kuna sababu, tena ya kijinai.

Mjuni Lwambo,
Yaelekea huijui sheria ya ugaidi Tanzania na athari zake kwa Waislam mara tu
ilipopitishwa.

Prof. Hamza Njozi katika kitabu chake kilichopigwa marufuku ''Mwembechai
Killings...'' alieleza hatari ya sheria hii.

Mara tu baada ya kupitishwa sheria ya ugaidi waliokamatwa bila ya makosa
yoyote walikuwa akina Abry wa Iringa kwa kujenga shule na akina Hudhaifa
wa Tanga kwa kujenga misikiti na shule.

Hawa walikamatwa kwa Uislam wao.
Hoja yako ya Waislam wengi mbona hawakamatwi wala sina haja ya kuizungumza.

Sifa kubwa ya Madina na Dibungo ni utulivu na amani na hapakuwa na ''crime.''
Fanya utafiti utajua.

Yapo mengi.
 
Kuna kakikundi kadogo ka kiislam kanakopanda mbegu ya waislam kuonewa, mfumo kristu Tanzania na wanafanikiwa kupata waamini wengi. Lakini kuna waislam wengi wanaoijua historia ya dini yao wanamsimamo wao. Imefikia point hata jambazi akiuwawa km amevaa kanzu au barakashia wengi watadai kauwawa sababu ni mwislamu. Gazeti la Jamhuri wali report habari hii vizuri sana baada ya uchunguzi uliohusisha mkuu wa mkoa na RPC wa Tanga. Thread km hizi zina incite vurugu tu na ndo malengo ya hao wanaovaa push Pedo. This is a naked fact mtukane mfanyeje!

Ngoshombasha,
Nilizungumza na Mhariri wa Jamhuri baada ya kusoma ile makala na nikamwemeleza
kuwa walichoandika ni uongo mtupu na nikawaomba niwapatie ukweli.

Hawapokei simu zangu.

Hapa ndiyo kwanza tumeanza yapo mengi In Sha Allah tutayaweka hapa jamvini ili
ukweli ujulikane.

Hakuna mahandaki Dibungo wala Lwande.
Cha kuchekesha sana baadhi yao hakupata kusikia neno Al Shaba katika maisha yao.

Ilikuwa kichekesho katika mahojiano na makachero.

Mwalimu wa madras akiulizwa anafundisha nini anajibu ''babu majah'' au anajibu ''riadh
salihin'' au anasema ''taafidh Qur'an...''

Iliwachukua muda makachero kuwapitikia kuwa walikuwa wamepiga namba siyo.
Hawa ndugu zetu hawakupata kuona bunduki ila kwenye picha.

Silaha ya karibu waiojuayo ni panga analokwendanalo shamba.

Tuna mengi ya kujifunza.
 
Mleta mada MS ni gaidi..

Tuelezee wanajamvi hapa nini maana ya gaidi,
ili tujue kama unajua unacho changia isije ikawa umekaririshwa kuwa ukiona majina/IDs fulani wewe pinga tu haina haya ya kusoma yaliyomo ndanimwe,

Hujakomaa wewe wala hujui ukichangiacho,

Jaribu kuwa kimya wakati mwingine, yaani jifanyize kwamba simu yako imeisha chaji,
 
Mzee Mohammed Said na waislam wote nawapeni pole.Pole yangu naitoa iwapo tu tukio hilo ni la kweli lakini hata kama si la kweli bado nitaendelea kuwapa pole waislam kwa kuubeba huu mzigo wa "ugaidi" iwe wanataka au hawataki.Hii ni perception inajengwa duniani kote na watu waislam na wasio waislam kutokana na matendo ya watu fulani wanaojiita waislam na watu fulani wanaojiita anti terrorist experts(U.S n.k).Sijafahamu kama nyinyi waislam mnaujua ukubwa wa tatizo hili lakini mie naliona kubwa sana.Unapogusia jambo linalohusu mamilioni ya watu duniani si jambo dogo hilo na hatupaswi kuliongea kwa maskhara kama wafanyavyo baadhi ya watu hapa.Huwa nakuwa mwangalifu na mambo ya uislam kwa kuwa najua katika kizazi chetu hiki,hata kama ni kwa lazima bila kupenda,kuna uhusiano wa karibu kati ya uislam,ukristo na uyahudi.Wakati sie wenye dini hizi tukipambana kwa doctrines,wapo watu ambao wao ndani ya mioyo yao hawapendi dini hizi zote.Naamini ni kutokana na historia ya dini hizi huko nyuma kutumika kama tool ya kumkomboa mwanadamu toka kwenye mikono ya watawala waovu na hata kuangusha tawala kubwa sana duniani ndio maana hivi leo dini hizi zimewekewa "jicho" ndani yake na nje pia,kwa kudhibiti leadership system yake na hata ikibidi doctrines na tafsiri zake ili ziendane na matakwa ya kitumwa ya wakuu wa dunia hii ambao hujitukuza zaidi ya Mwenyezi Mungu na hapa ndipo ugomvi wetu wanadini na hawa watu unapoanzia.Hivyo kwa mwanadini yeyote kati ya hizi tatu,atakuwa alerted na matatizo ya mojawapo ya dini hizi kwa sababu ya huyu common enemy tuliye naye.Ipo silaha moja kubwa ya kupambana na kashfa na kusingiziwa.Silaha hii ni "kuwajibika kujisafisha" kwa kukaa kwenye kile unachoamini na kukitekeleza kwa uwazi ili watu waone uhalisia wako tofauti na vile unavyozungumzwa.Katika biblia takatifu,kitabu cha imani yangu, kuna fungu linasema hivi,"Having your behaviour seemly among the gentiles,that wherein they speak against you as evil-doers,they may by your good works,which they behold,glorify God in the day of visitation."(1peter 2:12).Katika biblia ya kiswahili inasema hapo,"Muwe na mwenendo mzuri kati ya mataifa,ili,iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya,wayatazamapo matendo yenu mazuri,wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa."Je,katika uislam lipo suala kama hili la muumini kuwajibika kwa maneno na matendo kuonyesha ukweli na uhalisia wa dini yake ili jamii inayozunguka hata kwa wale wasio waislam,wafanye right judgment na kujengewa mtazamo sahihi juu ya uislam?kama jibu ni ndio,swali langu kuu linakuja kwako mzee wangu,nyinyi kama waislam,mnalichukuliaje tatizo la ugaidi na mnafanya juhudi gani kujisafisha na kuutenganisha uislam na shutuma hizi ambazo ulimwengu unaaminishwa hasa tukizingatia kuwa wapo watu wanaojiita waislam na wanatumia jina la uislam kufanya ugaidi(na watu huona damu ya ndugu zao ikimwagika kwa jina la uislam) situation ambayo inaleta legitimacy ya watu kuuhusisha uislam na ugaidi?na katika hili mzee wangu ukumbuke kuwa ni rahisi mbaya wako kutafuta "wajinga" ndani ya nyumba yako ili akumalize na kusema nyumba ile wote wajinga,unafanyaje hapo mzee wangu?kwa ujumla nauliza waislam mkiwa kama watu wenye responsibility ya kwanza kuilinda,kuitetea na kuitangaza dini yenu,mnafanya juhudi gani kuutenganisha uislam na huu "uzushi" wa ugaidi?
 
Mods futa huu uzi umeletwa na Gaidi MS..

Watu hawakurupuki hapa, na kama wewe umefanikiwa kujua kuwa mleta uzi ni gaidi,

Kwanini usiwasaidie Usalama wa Taifa kuwapa ushirikiano juu ya ugaidi wake?

Wewe pia una kesi ya kujibu kwa kitendo hicho,

Hao mods wanajitambua sana huwezi wafundisha kazi,

Toa mchango juu ya uzi, kama kichwani huna cha kuchangia, bora yako ni kuketi kimya,

Jaribu kupitisha macho tu kisha ukapitiliza,

Ntafurahi endapo busara zako zitabaki pale kwenye huo ushauri hapo juu, na huku katika habari mwendelezo uwaachie wenye uwezo na muono wa mbali/jicho la tatu,

Ahsanta kwa kujielewa kwako.
 
Ngoshombasha,
Nilizungumza na Mhariri wa Jamhuri baada ya kusoma ile makala na nikamwemeleza
kuwa walichoandika ni uongo mtupu na nikawaomba niwapatie ukweli.

Hawapokei simu zangu.

Hapa ndiyo kwanza tumeanza yapo mengi In Sha Allah tutayaweka hapa jamvini ili
ukweli ujulikane.

Hakuna mahandaki Dibungo wala Lwande.
Cha kuchekesha sana baadhi yao hakupata kusikia neno Al Shaba katika maisha yao.

Ilikuwa kichekesho katika mahojiano na makachero.

Mwalimu wa madras akiulizwa anafundisha nini anajibu ''babu majah'' au anajibu ''riadh
salihin'' au anasema ''taafidh Qur'an...''

Iliwachukua muda makachero kuwapitikia kuwa walikuwa wamepiga namba siyo.
Hawa ndugu zetu hawakupata kuona bunduki ila kwenye picha.

Silaha ya karibu waiojuayo ni panga analokwendanalo shamba.

Tuna mengi ya kujifunza.

We nadhani ndo mpokea hela za hao magaidi kutoka kwa alshabab na boko haram.
Naona unatetea ulaji wako.
 
Dini zote zinazohubiri kwamba kuna moto baada ya kufa zinahubiri ugaidi.

Kina hii ya wavaa suti inaruhusu kuuza na kununua binadamu mwenzio kama mtumwa
6:5 Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom