Kweli wanaume wengine kazi ipo ......

Kweli wanaume wengine kazi ipo ......

Unajua kiukweli na kibinadam hebu angalien ingekuwa hayo kayafanya mwanamke ingekuwaje jaman?
N huo udhaifu wa miaka saba ni wa aina gani huo?
Je angekufa huko ingekuwaje?au angenikuta mataizo aliyonisababishia yameniua je angerudi wapi?
Achen bwana,ninawacwac km ulishawahi kupenda tena kwa moyo wako wote alafu ukaumizwa na ukaujua uchungu wake wakati hapo hakuna ndoa,watoto wala mimba!
Alafu hapo mlishapitia magumu mengi labda ndio mmefanikiwa alafu ndio akakimbia!
Kwahilo kwangu ni ngumu sana na hapo tutadanganyana tu hata tukirudiana kamwe sitaweza kumpenda tena,
Labda tuishi kinafiki na binafsi huwa siwezi maisha ya maigizo ni bora niishi kwa shida peke yangu na si kuigiza!


hapa kinachokuja kuumiza zaidi ni majeraha ya tatizo ndo yatakayohukumu zaidi
 
sio vizuri kila kitu kumsingizia shetani. lakini kwenye sheria ya mapenzi wanasema bora aunganishae kuliko atenganishae. sitaki kujua kilicho mfanya aondoke na kilicho mrudisha. Hadi amerudi ina maana kajifunza. so kusamehewa na halali yake. Mimi kama figganigga nishaona mengi bora amsamehe ila wakapime UKIMWI kabla ya kufanya lolote.
dawa za kienyeji saa nyingine zinafanya kazi sema zikichuja ndo inakuwa kama hivyo. Mia
 
Dina, ulipata wasaa upi wa kumsamehe wakati hakuwepo?? maisha bila yeye hayakuwa rahisi kama mtoa mada alivyoeleza, mke alipitia machungu mengi! kuendelea na utaratibu wako wa maisha kana kwamba yeye bado hayupo ni kwamba bado hujasamehe hapo!

Madabwada, kwani kutoa msamaha lazima nitamke mbele yake kuwa sasa nimekusamehe unaweza kwenda? Na ndio maisha hayakuwa rahisi ndio maana najiuliza kuwa yeye ataleta urahisi gani sasa kama sio kuniongezea wingu jeusi moyoni? Angekuwepo wakati tunahangaika na mboga zetu ningesema that's my men, kwa shida na raha. Siamini kama nitakuwa nalipa kisasi kama Husniyo alivyosema kwenye mchango wake coz sioni kama kumkatalia kurudi naweza kufananisha na kuondoka kwake. Na je una maana ila msamaha utimie ni kwa kumkubalia arudi kwenye maisha yetu? Kama ndivyo, basi aende bila msamaha.
 
hapa kinachokuja kuumiza zaidi ni majeraha ya tatizo ndo yatakayohukumu zaidi

swali langu ni je pata picha mama yoyoo kakukimbia miaka 7 na amereje anataka umsamehe mrudiane! Utamsamehe? Vp utaishi nae? (uzungumze ya moyoni mwako) na hapo alikukimbia ulipokuwa umefulia but now alaa mambo super..nipe jawabu
 
hapa kinachokuja kuumiza zaidi ni majeraha ya tatizo ndo yatakayohukumu zaidi
Bora umelielewa hilo,
Tatizo ni yeye kutaka kusamehewa,labda angefuta vile nilivyomwambia aondoke na akaondoka,
Akanipa muda mpaka pale nitakapoona au ikitokea moyo wangu ukarudi labda sijui yani hata sijui itokee nn jaman,
Itafutwe namna ya kuweza japo tuwe tunaonea tu na kuwasiliana taratibu na akaweza kunishawishi kuponesha majeraha labda inaweza tokea tukaweza kujadili swala la kuwa pamoja tena,ila nahis inahitaji mda tena labda miaka 7!
 
swali langu ni je pata picha mama yoyoo kakukimbia miaka 7 na amereje anataka umsamehe mrudiane! Utamsamehe? Vp utaishi nae? (uzungumze ya moyoni mwako) na hapo alikukimbia ulipokuwa umefulia but now alaa mambo super..nipe jawabu

kabla ya kutengana ni lazima kuna suala ambalo limepelekea kufikia hatua hiyo na inategemea nani mkosaji maana unaweza ukakosa wewe lakini hatua akachukua mwenzako ... kwa maana hiyo narudi kule kule kidonda / jeraha la wakati wa kuachana ndilo litakalokuongoza kwani hata kama ingekuwa miaka 10 bado kuna mambo wewe binafsi unaweza kuyaangalia na umuhimu na ulazima wa mtu huyo kuwa nae ..
lakini kumbuka nawe unakuwa si malaika hivyo utajikuta umeanzisha mahusiano na hilo nalo litachangia katika maamuzi yako
 
kutendwa sio sababu ya kutopenda tena, kwanini umulike ulipoangukia na usimulike ulipojikwaa?? bado tunarudi pale pale, hatuchagui wenzi wetu kutokana na upendo wa kweli but merely from other minor factors, uzuri, kazi nzuri, fedha, etc ... sasa hapo wakati wa misukosuko ya ndoa kwanini msiangukie pua?? hakuna miujiza hapo ... its purely a wrong selection from the scratch!
Sasa kwa mwanaume wa aina hiyo c ndio wrong selection yenyewe!
Kwa upande wangu kwa ujaji huo sitaweza kuwa naye,labda aondoke zake mpaka hapo itakapotokea moyo wangu ukafikiri vinginevyo jambo ambalo litakuwa gumu coz bado nitakuwa na majeraha.
 
Bora umelielewa hilo,
Tatizo ni yeye kutaka kusamehewa,labda angefuta vile nilivyomwambia aondoke na akaondoka,
Akanipa muda mpaka pale nitakapoona au ikitokea moyo wangu ukarudi labda sijui yani hata sijui itokee nn jaman,
Itafutwe namna ya kuweza japo tuwe tunaonea tu na kuwasiliana taratibu na akaweza kunishawishi kuponesha majeraha labda inaweza tokea tukaweza kujadili swala la kuwa pamoja tena,ila nahis inahitaji mda tena labda miaka 7!

C heri pia umeelewa maana kama ulikuwa na jeraha kubwa la kuachana unaweza kujikuta unachukua shoka na unamaliza ghadabu zako zote
 
Madabwada, kwani kutoa msamaha lazima nitamke mbele yake kuwa sasa nimekusamehe unaweza kwenda? Na ndio maisha hayakuwa rahisi ndio maana najiuliza kuwa yeye ataleta urahisi gani sasa kama sio kuniongezea wingu jeusi moyoni? Angekuwepo wakati tunahangaika na mboga zetu ningesema that's my men, kwa shida na raha. Siamini kama nitakuwa nalipa kisasi kama Husniyo alivyosema kwenye mchango wake coz sioni kama kumkatalia kurudi naweza kufananisha na kuondoka kwake. Na je una maana ila msamaha utimie ni kwa kumkubalia arudi kwenye maisha yetu? Kama ndivyo, basi aende bila msamaha.

hapo ndipo haswa, my dia ... ndio maana nasema kusamehe sio jambo rahisi, its a sacrifice, lkn ni rahisi tu kama upendo "usiochakachuliwa" upo!
 
hapa kinachokuja kuumiza zaidi ni majeraha ya tatizo ndo yatakayohukumu zaidi

BPM, healing is gradual process, ni kama kuuguza kidonda chochote kile mwili, maumivu hupungua kadri muda unavyokwenda, hatimaye hupona. Utabakia na kovu, lakini maumivu hayatokuwapo tena!!
 
Sasa kwa mwanaume wa aina hiyo c ndio wrong selection yenyewe!
Kwa upande wangu kwa ujaji huo sitaweza kuwa naye,labda aondoke zake mpaka hapo itakapotokea moyo wangu ukafikiri vinginevyo jambo ambalo litakuwa gumu coz bado nitakuwa na majeraha.

lakini acha kuwa so rude mpaka naogopa dah..Easy cantalisia jamani..chonde chonde
 
Sasa kwa mwanaume wa aina hiyo c ndio wrong selection yenyewe!
Kwa upande wangu kwa ujaji huo sitaweza kuwa naye,labda aondoke zake mpaka hapo itakapotokea moyo wangu ukafikiri vinginevyo jambo ambalo litakuwa gumu coz bado nitakuwa na majeraha.

the good news is, utakuwa na majeraha but with time utapona. na kwa hakika, nadhani furaha ya kupona kidonda huwa unaijua, hhuitaji nikuelezee hilo ... only sky will be the limit!!
 
BPM, healing is gradual process, ni kama kuuguza kidonda chochote kile mwili, maumivu hupungua kadri muda unavyokwenda, hatimaye hupona. Utabakia na kovu, lakini maumivu hayatokuwapo tena!!

unaweza kuuguza kidonda lakini kila ukikiangalia na jinsi ulivyokipata unawez akuumiza zaidi
 
unaweza kuuguza kidonda lakini kila ukikiangalia na jinsi ulivyokipata unawez akuumiza zaidi

hahahhaaaaa ... ni kweli, lakini with time utasahau tu. Furaha ni siku utakapo pona kabisa!
 
hahahhaaaaa ... ni kweli, lakini with time utasahau tu. Furaha ni siku utakapo pona kabisa!


hakuna time limit maana hata ukisema kidonda kimepona bado kovu litakuwepo na unaweza kujikuta jambo dogo tayari umeshachukua hatua kwa haraka kitu ambacho si kizuri kuishi kwa tahadhari au kwa kudhania jambo
 
kabla ya kutengana ni lazima kuna suala ambalo limepelekea kufikia hatua hiyo na inategemea nani mkosaji maana unaweza ukakosa wewe lakini hatua akachukua mwenzako ... kwa maana hiyo narudi kule kule kidonda / jeraha la wakati wa kuachana ndilo litakalokuongoza kwani hata kama ingekuwa miaka 10 bado kuna mambo wewe binafsi unaweza kuyaangalia na umuhimu na ulazima wa mtu huyo kuwa nae ..
lakini kumbuka nawe unakuwa si malaika hivyo utajikuta umeanzisha mahusiano na hilo nalo litachangia katika maamuzi yako

Lakini ujue si wanaume tunapenda hawa wenzetu watusamehe lakini sie huwa wagumu kweli na matusi juu
ANGALIZO: ukimtelekeza mwanamke mwenye kipato chake ukirudi umeisha jela nje nje umkute kwenye silent mode labda
 
Lakini ujue si wanaume tunapenda hawa wenzetu watusamehe lakini sie huwa wagumu kweli na matusi juu
ANGALIZO: ukimtelekeza mwanamke mwenye kipato chake ukirudi umeisha jela nje nje umkute kwenye silent mode labda

wakati wa kuachana kuna mambo ambayo huongoza katika hatua harisi nayo ni kiburi, dharau majivuni etc sasa nini unatarajia ukirudi???
 
C heri pia umeelewa maana kama ulikuwa na jeraha kubwa la kuachana unaweza kujikuta unachukua shoka na unamaliza ghadabu zako zote

Hiyo kitu ni ngumu sn,tena ashukuru amemkuta angekuta kaolewa je angemwombaje huo msamaha!alafu wanaume mnateteana ingekuwa ni kinyume chake dah cjui huu uzi ungekuwa page ya ngapi!mie hapo ni kumfukuza tu akaendelee na maisha yake tu ujio wake utanitonesha maumivu upya!
 
Hiyo kitu ni ngumu sn,tena ashukuru amemkuta angekuta kaolewa je angemwombaje huo msamaha!alafu wanaume mnateteana ingekuwa ni kinyume chake dah cjui huu uzi ungekuwa page ya ngapi!mie hapo ni kumfukuza tu akaendelee na maisha yake tu ujio wake utanitonesha maumivu upya!

C unaweza ukawa umeoa au kuolewa baada ya kukimbiana lakini hukumu ya ukaribu au walau uwepo wa mtu unategemea na huyo uliyenaye maana naye atakupa msukumo kisaikolojia
 
Baba X aliondoka nyumbani kwake miaka 7 iliyopita na kuambatana na nyumba ndogo yake,na kumwacha mkewe akiwa mjamzito miezi tisa na watoto wakubwa wawili, ,bila hata huruma,na hakuwa na mawasiliano yoyote kujua wife na wanawe wanaendeleaje,
,mama wa watu alijifungua mtoto wake salama maisha yakiwa magumu na kuwalea wanae kwa taabu akifanya biashara ya kuuza mboga mboga , mungu si athumani kasomesha mwanae mkubwa sasa yuko form five ,mwingine form two,Na yule alokuwa tumboni sasa yuko la kwanza ,
Juzi mama wa watu akiwa anaandaa chakula mara mmewe huyo after seven years aliyowatelekeza..
Mama kwanza alidhani kaona mzuka na kuanguka chini huku fahamu zikimpotea ,,
Baada ya kuzinduka anakuta jamaa analia huku anaomba kusamehewa.....
eti shetani ndo alimpotosha ,anatubu dhambi zake na sasa anaomba wasameheane waanze upya..:hatari:

Kama wewe ndo mwanamama ulokumbwa na dhahama hili ungefanya maamuzi gani???:A S-coffee:

mh! Hapo kumshauri nashindwa
 
Back
Top Bottom