Kwenu wanafunzi wa form 4 na wazazi, Form 5 na 6 ilishapitwa na wakati.Ni vizuri kuanza chuo mapema baada ya form 4 na hupanua zaidi goli la ajira

Kwenu wanafunzi wa form 4 na wazazi, Form 5 na 6 ilishapitwa na wakati.Ni vizuri kuanza chuo mapema baada ya form 4 na hupanua zaidi goli la ajira

kikubwa kujua ENGLISH, COMMUNICATION SKILLS NA NEGOTIATION SKILLS baaassiiiii
 
Una smartphone jaribu na wewe kuwa smart kidogo.

Ingia google sechi haya maneno >> high school diploma jobs in us

Utaziona kazi wanazohitajika wenye elimu husika

mifano: https://www.indeed.com/q-high-school-diploma-jobs.html?vjk=d61c27ec482e727c
M NATAKA KUJUA UKO KWNY HIGH SCHOOL DIPLOMA WANASOMA MASOMO GANI? KUHUSU KAZ N KWASABABU WAO WANACHANGANYA NA FANI NYINGNE MASOMO YAO KAMA HUU MTAALA MPYA WA ELMU NA PESA KWAO SIO TATZO, LAKN UJUE HAKUNA UNESI, UFAMASIA WALA SHERIA WANAFUNDISHWA UKO N YALEYALE WANAOSOMA ADVANCE UKU NAWAO WANASOMA PAMOJA NA FANI NA UFUND MBALMBAL
 
Form six ni ya muhimu sana,ukitoka form 4 kwenda chuo unaitwa una elimu ya kuunga unga na ukitaka kwenda chuo kikuu kuna baadhi ya vyuo vikubwa vinakukataa
Kuna chuo kikubwq kuliko UDSM? Kama UD unakubalika nani mwingine akupinge?

Halafu futa kauli ya kusema elimu ya kuunga unga. Ukitoka Diploma tayari unakuwa uanelewa nini unasomea. Nzuri zaidi unaingiza pesa huku unasoma.
 
Hasa kwa wale wenye malengo ya kuja kuajiriwa kwasababu ukweli mchungu wa mfumo wetu wa elimu yetu inaandaa zaidi wahitimu kuajiriwa serikalini, wachache sana wamevunja mwiko huu kwa kutumia elimu zao kujiajiri kwa hiari

Ni kwanini form 6 ilitokea kuwa maarufu zaidi ?

Hapo zamani nchi ilikuwa na uchumi mdogo sana wa kuendesha vyuo na watu wachache sana walioelimika kufundisha vyuoni (wenye elimu walitumika zaidi mambo mengine ya serikali), Kuendesha chuo ni gharama kubwa sana kuanzia kulipa walimu mishahara ya milioni 3, umeme na majenereta, hostel za kisasa, vifaa vya taaluma, majengo ya gharama, kujaza vitabu maktaba, n.k. kukabiliana na hili serikali iliona mbadala ni shule za A Level kwasababu ni gharama rahisi zaidi kulipa mishahara ya walimu, hakuna haja ya umeme na majenereta, mabweni ya bei rahisi, majengo bei rahisi, n.k.


Vyuo vilikuwa ni vichache sana vinavyopokea wanafunzi wa Form 4 na ni wale wanaosomeshwa na serikali, ilikuwa ni jambo la kushangaza sana mwanafunzi wa form 4 kwenda chuoni, Ni takribani asilimia 1 tu walichaguliwa vyuoni, wote waliobaki walipelekwa form 6. kwa wanafunzi wengi sana walipitia njia hii, form 6 ilipata umaarufu mkubwa sana hadi leo hii kuna shule za gharama kubwa.

Zama zimebadilika, Mambo yamebadilika, wahi fasta chuoni !!

Siku hizi kuna vyuo vingi, Wanafunzi wanaweza kuanza kujifunza taaluma zao mapema, kwa bahati mbaya kuna lile zimwi la kuipa umaarufu mkubwa form 6 bado linaandama baadhi ya wanafunzi wengi sana, Unaweza kukuta mwanafunzi kwao wana uwezo wa kumsomesha chuoni lakini bado atangangania form 6, anaacha kwenda chuoni kusomea taaluma.

Chuoni unaenda kusomea taaluma form 6 unasomea masomo sio taaluma, Chuoni utasoma certificate mwaka moja, Diploma miaka miwili, Degree miaka mitatu hadi mitano, Wale wa form 6 taaluma yao wengi ni degree pekee.

Ni jambo la hekima zaidi kuanza mapema kusomea kazi, hayo utaweza kuyatimiza kwa kuanza kusoma chuoni mapema mara tu baada ya kumaliza form 4 kwasababu form 6 hakuna taaluma yoyote inayosomewa, form 6 ni kombi za masomo.

Kwa maandalizi ya mapema kwenye selection za form 4 vipe vyuo kipaumbele zaidi, ukikosa selection tuma maombi binafsi chuoni

Nenda form 6 kama
  • Kwenu hakuna pesa ya kukusomesha chuoni, Form 6 za serikali ada elf 70
  • Una malengo ya kusomea degree yako nje ya nchi, vyuo vizuri vipo Marekani na Ulaya, ada na gharama za kuishi kwa mwaka ni takribani milioni 40+, vyuo kama havard milioni 100 kwa mwaka
  • unataka kuwa mwalimu wa form 6, ni njia itayokupa uzoefu zaidi ikiwa utakuja kuwa mwalimu wa form 6.

Ni kwamba ukienda chuo mapema una advantage kwasababu una sifa za kufanya kazi za certificate na diploma, Degree hawaruhusiwi kwasababu hawana vyeti husika vya taaluma, hivyo wewe una uwanja mpana zaidi na unaweza kuingia kazini kwa diploma baada ya muda kukawa na uhitaji wa watu wenye degree huwa wanaanzia kuangalia watu wa ndani hio ni advantage.

Halafu pia CV ya mtu aliewahi kuanza chuo ni nzito kwasababu inaonyesha kasomea taaluma miaka mingi zaidi, kafanya mazoezi ya kazi ya vitendo mengi zaidi, ana vyeti vingi zaidi vya taaluma, n.k. Unaweza kuta mhitimu mwenye cheti kimoja cha taaluma cha degree yupo anaiweza kazi zaidi lakini cv inamuangusha, kuna mameneja / mabosi wanavutiwa zaidi na cv iliyoshiba.

Uwanja mpana wa Ajira kwa mifano halisi

A.

inatokea mhitimu wa form 6 na diploma wote hawana ada / mkopo wa kwenda degree, Mwenye Diploma ana taaluma na kigezo cha kuajiriwa, Form 6 ndio imetoka hio !! hata kama mshahara utakuwa mdogo lakini Diploma at least ana uhakika wa kuajiriwa kwa taaluma, Ni kweli diploma analipwa kidogo kuzidi degree lakini si haba, Sehemu ambayo Degree analipwa milioni 1 diploma anaweza kulipwa laki 7, better for something than nothing.

B.

Kuna kazi mbili:

Pepsi - Diploma mshahara laki 7
Coca - Degree mshahara milioni 1

Form 6 mwenye degree pamoja na mwenzake form 4 mwenye Diploma na degree wanaenda Coca kuomba nafasi ya degree, kwa bahati mbaya wote wanaikosa kazi ya degree, Lakini yule form 4 mwenye Diploma na degree anaweza kuomba na kuipata kazi ya Pepso mshahara laki 7, form 6 mwenye Degree anarudi mtaani, akianza kumwambia mwenzake kwamba kazi aliyopata ina mshahara mdogo wakati yeye yupo kitaa tutamwelewa ?
Nilisha sema hapa kuwa form 5 na 6 ni saikolojiki effect ya kuvunja moyo wanafunzi wasisome kwa bidii form 4 ...mfumo wa kenya ni bora mara 100 wa watanzania elimu ya msingi iwe hadi form 2 hapo tunaongeza mwaka mmoja primary yaani miaka 8 ya primary mtoto atoke na elimu ya form 2 kisha secondary miaka 4 kisha chuo
 
Form 5 na 6 ya bongo ni ya kikoloni ya miaka haina taaluma yoyote ile, haina kazi yoyote.

Kenya walifuta hizo 5 na 6, ukimaliza form 4 tayari ni high school na wameelimika zaidi, mbali mno.
Ndio maana nasema kuna haja ya kureview mfumo mzima maana umezalisha kondoo wa kutosha sasa tuunde mfumo mpya tuzalishe binadamu wenye impact, ubunifu na uwezo wa kutawala na kuboresha mazingira yao! Sio wanaamini hamna maisha bila uchawa na usanii! Kila nyanja inataka watu wa kuiboresha na kuendeleza sio kutazama shortcuts km kufuta elimu fulani! Nimesema sana elimu ya kimagharibi haijasaidia Tanzania na kuona huhitaji pesa nyingi kufanya reseaech ni kutazama tu sample ya wasomi chawa na wanasayansi wetu wakubwa wanavyosubiri uteuzi na hawana impact kwnye global body of knowledge na jinsi wqnavyoishi kwa kusifia wanasiasa!

Tuna maprofesa chungu nzima wasio na filosofia unajiuliza kwa nn wamepoteza miaka yao shule then wanaamini mambo yao hayaendi bila uchawi! Yani hawaamini kwenye elimu waliyosomea na kufundisha miaka na miaka, unajiuliza sasa prof wa namna hii nimpe mtoto wangu atamfundisha nini, matokeo yake ni vijana waliojaa mtaani hata kuandika cv au application letter za kuomba kazi tu hawajui.

Wakati nchi zilizoendelea mtu anayesomea Masters anategemewa kuanzisha ajira, wa Tz anamaliza anakuja JF kuomba connection za kina mwashamba, unajiuliza thesis yake ilikuwa ya nini na anashindwaje kufanya projects kutokana na thesis yake, so kafanya research study kaiandika ili apate cheti kama form 4 then what?. Tunaishi kinyumenyume, wanaotakiwa kuanzisha ajira wao pia wanataka ajira! Maajabu haya yapo Tanzania tu. Hata nchi zingine za weusi hazipo hivi

By the way projects kubwa za social na sciences kwa walioendelea zilianzia vyuoni, na school dropouts waliofanya makubwa walitengeneza projects zao wangali wanasoma, hawakudrop ndio wakaanze kufanya mambo, ndoto zao zilianzia high schools na vyuoni.
 
Nilisha sema hapa kuwa form 5 na 6 ni saikolojiki effect ya kuvunja moyo wanafunzi wasisome kwa bidii form 4 ...mfumo wa kenya ni bora mara 100 wa watanzania elimu ya msingi iwe hadi form 2 hapo tunaongeza mwaka mmoja primary yaani miaka 8 ya primary mtoto atoke na elimu ya form 2 kisha secondary miaka 4 kisha chuo

Hata wakifuta form 5-6 bila kuboresha contents za tunachofundisha tutabaki hivihivi tutapunguza umri wa vijana kugraduate tu na hakutakuwa na impact yoyote!
 
Kuna chuo kikubwq kuliko UDSM? Kama UD unakubalika nani mwingine akupinge?

Halafu futa kauli ya kusema elimu ya kuunga unga. Ukitoka Diploma tayari unakuwa uanelewa nini unasomea. Nzuri zaidi unaingiza pesa huku unasoma.
Hao hao udsm wabaguzi kishenzi siku hz
 
Hata wakifuta form 5-6 bila kuboresha contents za tunachofundisha tutabaki hivihivi tutapunguza umri wa vijana kugraduate tu na hakutakuwa na impact yoyote!
Ndiyo maana nasema elimu ya msingi iboreshwe iwe miaka 8 mtoto atoke na elimu ya form 2 yaani ndani ya elimu ya msingi kuwe
Primary 6 years + 2yr secondary form 2=8yrs wanafunzi wa primary wakimaliza na elimu ya kidato cha pili wanaweza kuajilika au kwenda vyuo vya ujuzi mbalimbali ...yaani darasa la 7 liwe form one na darasa la 8 liwe form 2
 
Inategemea na fani unayo somea.

lkn fani nyingi, kazi za diploma mshahara wake ni mdogo, hakuna exposure, growth na carrier development ni ndogo mno. Plus huwa wabakujaga kuona umuhimu wa degree wakikaa kazini miaka 5, ndo unakuta mtu anakuja kujiendeleza akiwa na familia kazi kusumbua lecturers wamuongezee maksi.

Chapa degree yako bhana, hata usipo pata kazi, exposure ya shule itakusaidia kunyooosha mambo yako.

Mwenye masikio na asikie
Kwani ukiipiga diploma then ukaunga degree?
 
Kwanza unakosea sana kushauri watu ujinga. Kijana au binti ambaye hajaenda form six akakimbilia chuo cha kati hawezi hata kuandika sentensi moja ya kiingereza ni weupe sana vichwani. Amini nakwaambia kaa nao utaona yaani hana tofauti na la saba. Halafu kwa mfumo wa elimu yetu yaani uwe na basic ya form 4 tu unakua kama ulifeli tu hivyo acha ujinga wa kupotosha watu humu. Kama na wewe uliruka form six basi na weae ni kilaza tu
Kwamba ukiweza kuandika sentesi kwa kiingreza ndio msomi?
 
Back
Top Bottom