Kwenye hili sitaki nifeli, naombeni ushauri wenu waungwana

Kwenye hili sitaki nifeli, naombeni ushauri wenu waungwana

Mkuu Mimi naweza kukushauri kulingana na uzoefu wangu kwenye biashara ya steshenari,waweza pata hadi sh 200,000 kwa siku ikiwa utapata eneo zuri

Mfano Mimi hununua ream kwa Shiling 9000 na hiyo ream ina karatasi 500 na kopi huwa natolea sh 100 ,printing sh 500 typing na printing sh 1000 per page, kwa hiyo kama eneo ni zuri kwa biashara, ream tatu kiwango cha chini zaweza isha kwa siku Moja ambapo utakuwa umeingiza takribani 150,000 kwa kila ream.

Ukija kwenye karatasi za kusafishia picha,box Moja huwa na karatasi 100 ,ambapo Mimi huwa nasafishia kwa sh 300 ikiwa mteja atakuja na picha zake, ila nikimpiga Mimi nafanya sh 700,ambapo kama uko eneo zuri kwa siku waweza maliza box 5 kwa kiwango cha chini ambapo utakuwa umepata sh 50,000 kwa kila box hadi kuisha

Hapa ni kwa uchache sana,maana utaweka vitu Vingi tu humo bandani,maana Mimi pia Nina freezer huwa nagandisha ice creams, so faida hii unaipata bila shida mkuu

Try it,nadhani hata Mimi wakati nataka kufungua hii biashara nilileta Uzi humu,japo hili wazi la steshenari sikulitoa humu,maana nilipewa na kaka yangu ambaye hata hajasoma ila faida yake naiona,ninampango wa kuchukua mkopo nipanue hii ofisi iwe kubwa zaidi,maana hata ukiniamsha usiku ukaniuliza biashara yenye faida maradufu hapa Tanzania ni ipi nitakujibu steshenari.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app

Hili nalo wazo
 
Njoo mtera tufanye biashara ya samaki wa kubanikwa,soko lipo songea ni uhakika,tukianza na 500k siyo mbaya. Bei ya samaki bwawani 30-35/= na bei ya kuuzia Songea ni 100-200/=

Nipo tayari kusimamia hiyo biashara,karibu sana

Mtoa mada hii idea nilishawahi kuisikia kwa dogo mmoja hivi hivi nadhani inaweza kuwa nzuri sana.

Mtafute huyu
 
Nimemaliza chuo muda (2016) kidogo, nimesota sana kupata ajira, nimesota sana mpaka nilifikia kukata tamaa ya maisha, Mungu mkubwa mwaka jana mwezi wa 5 nikaja kupata kazi kwenye mradi mmoja hivi, kutokana na mapito ya kukosa kazi na kuangaika mtaani, nilijichanga mnooo mnoo nilijichanga kupita maelezo na sikutaka kupoteza hata sent tano kijinga.

Mwishoni nimefikisha kiasi cha sh Milion 10 cash.

Sina uzoefu na biashara kiukweli kabisa

Nina kiwanja kipo Dar (kama asset yangu nilikinunua nikiwa chuo kwa bumu), natamani sana nijenge (napenda sana sana nyumba)

Naombeni ushauri wenu; ni biashara gani nikifanya kwa siku naweza kulaza sh elfu 50 kama faida kupitia hiyo pesa milion 10 (naombeni ushauri wenu uwe mzuri mkuu maana hii ela ikipotea pasipo kupiga atua naweza kufa kwa pressure maana nimeipata kwa tabu mnoo)

Maeneo ya kimakazi ni mawili Dar es Salaam pamoja na Mwanza.

Karibuni kwa ushauri.
mkuu hongera km umejichanga na kusave toka mwezi may last year hadi sasa ni mwaka mmoja na una 10mil basi hiyo kazi yk inalipa..

kifupi hiyo hela igawe mara mbili nusu ya hela fanya biashara na nusu kaanze ujenzi kwenye kiwanja chako.
biashara zipo nyingi inategemea na wewe unapendelea ipi na namna ipi ya usimamizi, mm nitakushauri mbili tu..
moja km unataka biashara uifanye ww mwenyewe iwe chini yk 24 hrs basi hapo fanya online business tu km online financial markets e.g forex, indexes na kadhalika ila biashara hii zinakuhitaji uwe mwingi wa maarifa na mfuatiliaji wa mambo ulimwenguni hivyo km upo bize sana achana nayo ..

badala yake,
kwa mtajiwa 5mil fungua biashara ya mpesa,tigopesa,airtelmoney crdb wakala na nmb tafuta sehemu iliyochangamka hata km wapo watoa huduma km hizi usiogope angalia udhaifu wao then wewe boresha zaidi hii biashara ni nzuri na kwa mtaji huo utapata faida nzuri tatizo ni moja tu utapeli na kumpata msimamizi mwaminifu basi utapiga hatua kubwa tu.

mwisho, km utahitaji usimamizi wa biaashara yoyote kati ya hizi au tofauti na hizi nipo teyari mkuu tuyajenge.
 
Back
Top Bottom