Kwenye Ishu ya Uzanzibari na Utanganyika Lissu amekuwa upande wa haki siku zote

Kwenye Ishu ya Uzanzibari na Utanganyika Lissu amekuwa upande wa haki siku zote

Well said.
CCM wamezoea kuendesha mambo kienyeji sana. Kwa katiba hii anaweza tokea Mzanzibar mjeuri akaukwaa urais wa JMT akaiuza Dar yote na hakutakuwa na wa kumfanya kitu.

Tusiamini kuwa kila siku tutakuwa na rais wa JMT toka Zanzibar atakayekuwa na huruma na Tanganyika kama Samia au Mwinyi. Kwangu mimi Mwinyi na Samia (ambapo mmoja aliuza Loliondo na mwingine Bandari/Ngorongoro) nawaona wapole sana bado Samia anaweza kuuza hata Selous yote na hakuna kitu mtamfanya.

Turekebishe hii hali kabla mambo hayajawa mabaya zaidi
Well said
 
Lissu yuko sahihi.kila mwenye akili timsmu anamwelewa labda wanafiki na wabinafsi ndio wasiomwelewa.Huu muungano zinatumika nguvu nyingi sana kuulinda hiyo maana yake kuna madudu mengi ambayo hayako sawa,sasa badala wenye akili wayajadili mapema ili yakae vizuri wao wanataka kuyaficha ficha wakati hawatakuwepo milele kuyaficha.
 
Tatizo jingine ni kuwa Wazanzibari kwa kuwa sasa hivi mzanzibari mwenzao ndo anatawala Tanzania, wamekaa kimya, kelele za madai yao ya kutaka Zanzibar huru wameyapunguza ili wasimkwaze mwenzao kwenye kutawala ILA siku akiingia Mtanganyika Ikulu ndo utaanza kusikia kwa wingi kelele za Watanganyika wanatubana watuache tupumue!

Huu Muungano unahitaji marekebisho makubwa sana
 
Kuna watu wanajaribu kuchukulia kauli za Lissu kukerwa na aina hii ya muungano kuwa eti anajaribi kuleta mgawanyiko wa Utanganyika na Uzanzibari.

Kiukweli kabisa kama ukifuatilia miongoni mwa watu waliojaribu kuwatetea Wazanzibari dhidi ya muungano huu ni Tundu Lissu. Lissu amekuwa consistent kwa muda mrefu kuwa muungano huu unawaumiza Wazanzibari sana, na kwamba Zanzibar imepoteza mengi kutokana na muundo huu wa muungano. Amefanya hivyo katika mijadala na hata katika mikutano ya hadhara. Nakumbuka amewahi kufanya mkutano mkubwa sana kule Zanzibar akieleza ni kwa namna gani muungano huu unavyowaumiza Wazanzibari.

Leo Lissu ameanza kuzungumza pia namna muungano unavyowaumiza Watanganyika, kuna watu wanatoka huko mbiombio kutaka kumnyamazisha!. Yaani Lissu akitetea wazanzibari hiyo inakuwa sawa, lakini akitetea Watanganyika hiyo inakuwa nongwa!. Kwa nini?

Ukimsikiliza Lissu kwa makini hana Tatizo na Uzanzibari wa Samia kama mtu ila ana tatizo na muundo wa muungano unaomfanya Mtu ale "kotekote" with impunity huku maslahi ya upande mmoja ( Wa Zanzibar yakilindwa kwa katiba yao) huku maslahi ya Tanganyika yakiwa hayana mtetezi (Kikatiba).

Leo inakuwaje Rais kutoka upande mmoja wa muungano anakuwa na mamlaka kwa mambo ya upande wa pili wa muungano ambayo siyo ya muungano?. Utalii siyo Jambo la muungano, iweje Mzanzibari awe na power ya kuwaamulia Watanganyika mambo yao ya utalii lakini mtanganyika hana power hizo kwa Zanzibar?

Leo tuna katiba ya Zanzibar, inayopingana hata na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mambo kedekede na hayo mambo yako wazi na yanajulikana na yako documented lakini watu wazima wamekaa kimya wanajifanya hawayaoni. Leo akitokea mtu kama Lissu akashikia bango mapungufu haya ili yaondolewe inabidi apongezwe siyo kubezwa!.

Katiba ya Zanzibar inasema Kutakuwa na "Mzanzibari" na imeorodhosha mzanzibari ni nani. Sasa Tujiulize Mzanzibari akishika madaraka ya Muungano kisha maslahi ya Zanzibar yakagongana na Maslahi ya Tanganyika katika mambo yasiyo ya Muungano yeye atatetea maslahi ya wapi?

Na katiba ya Zanzibar ikaenda mbele kusema kuwa Zanzibar ni nchi miongoni mwa nchi mbili ZINAZOUNDA jamhuri ya muungano wa Tanzania, Pigia msitari neno ZINAZOUNDA siyo ZILIZOUNDA, Sasa hiyo nchi nyingine inayounda muungano na Zanzibar iko wapi na kiongozi wake ni nani na watu wake ni akina nani?.

Hoja ya Lissu siyo Uzanzibari wa Samia. Hoja ya Lissu ni muundo mbovu wa Muungano. Uraisi wa Samia ni mfano tu kuonyesha muundo huo ulivyo na tatizo.

Ni mpaka tukae chini tusolve hili tatizo, la sivyo huko tuendako ni shida tu. Ndiyo maana leo Kuna Wazanzibari wanataka Watanganyika waende Zanzibar na Passport. Na mimi sioni shida Wazanzibar wakija Tanganyika kwa passport.
Narudia tena kusema. Huu muungano Nyerere alifanya kosa kubwa sana la kihistoria. Ilitakiwa iwe nchi moja tu. Naamin muda si mrefu hili kosa litafutwa kama alivyofanya India pale cashmir. Hicho kinchi kinatakiwa kuwa mkoa basi.
 
Kuna watu wanajaribu kuchukulia kauli za Lissu kukerwa na aina hii ya muungano kuwa eti anajaribi kuleta mgawanyiko wa Utanganyika na Uzanzibari.

Kiukweli kabisa kama ukifuatilia miongoni mwa watu waliojaribu kuwatetea Wazanzibari dhidi ya muungano huu ni Tundu Lissu. Lissu amekuwa consistent kwa muda mrefu kuwa muungano huu unawaumiza Wazanzibari sana, na kwamba Zanzibar imepoteza mengi kutokana na muundo huu wa muungano. Amefanya hivyo katika mijadala na hata katika mikutano ya hadhara. Nakumbuka amewahi kufanya mkutano mkubwa sana kule Zanzibar akieleza ni kwa namna gani muungano huu unavyowaumiza Wazanzibari.

Leo Lissu ameanza kuzungumza pia namna muungano unavyowaumiza Watanganyika, kuna watu wanatoka huko mbiombio kutaka kumnyamazisha!. Yaani Lissu akitetea wazanzibari hiyo inakuwa sawa, lakini akitetea Watanganyika hiyo inakuwa nongwa!. Kwa nini?

Ukimsikiliza Lissu kwa makini hana Tatizo na Uzanzibari wa Samia kama mtu ila ana tatizo na muundo wa muungano unaomfanya Mtu ale "kotekote" with impunity huku maslahi ya upande mmoja ( Wa Zanzibar yakilindwa kwa katiba yao) huku maslahi ya Tanganyika yakiwa hayana mtetezi (Kikatiba).

Leo inakuwaje Rais kutoka upande mmoja wa muungano anakuwa na mamlaka kwa mambo ya upande wa pili wa muungano ambayo siyo ya muungano?. Utalii siyo Jambo la muungano, iweje Mzanzibari awe na power ya kuwaamulia Watanganyika mambo yao ya utalii lakini mtanganyika hana power hizo kwa Zanzibar?

Leo tuna katiba ya Zanzibar, inayopingana hata na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mambo kedekede na hayo mambo yako wazi na yanajulikana na yako documented lakini watu wazima wamekaa kimya wanajifanya hawayaoni. Leo akitokea mtu kama Lissu akashikia bango mapungufu haya ili yaondolewe inabidi apongezwe siyo kubezwa!.

Katiba ya Zanzibar inasema Kutakuwa na "Mzanzibari" na imeorodhosha mzanzibari ni nani. Sasa Tujiulize Mzanzibari akishika madaraka ya Muungano kisha maslahi ya Zanzibar yakagongana na Maslahi ya Tanganyika katika mambo yasiyo ya Muungano yeye atatetea maslahi ya wapi?

Na katiba ya Zanzibar ikaenda mbele kusema kuwa Zanzibar ni nchi miongoni mwa nchi mbili ZINAZOUNDA jamhuri ya muungano wa Tanzania, Pigia msitari neno ZINAZOUNDA siyo ZILIZOUNDA, Sasa hiyo nchi nyingine inayounda muungano na Zanzibar iko wapi na kiongozi wake ni nani na watu wake ni akina nani?.

Hoja ya Lissu siyo Uzanzibari wa Samia. Hoja ya Lissu ni muundo mbovu wa Muungano. Uraisi wa Samia ni mfano tu kuonyesha muundo huo ulivyo na tatizo.

Ni mpaka tukae chini tusolve hili tatizo, la sivyo huko tuendako ni shida tu. Ndiyo maana leo Kuna Wazanzibari wanataka Watanganyika waende Zanzibar na Passport. Na mimi sioni shida Wazanzibar wakija Tanganyika kwa passport.
Lissu ni mtu ya Mungu sana
 
Mkuu Lisu ni mmoja ya mtu makini sana, kosa la lisu sio kuwatetea watanganyika, wala kulalamika juu ya mambo wanayohisi yanawaumiza kwenye muungano, Tatizo la lisu ni kunasibisha matatizo ya Samia na uzanzibari wake. Hiyo ni moja njia ya kutengeneza chuki za kibaguzi kwenye jamii, Lisu anajua nini anafanya anachofanya lisu ni kutembea na upepo unavyovuma Lakini Lisu anaelewa vizuri sana ni nani anaeumia kwenye huu Muungano, Infact karibuni tu aliwahi kuzungumza kuhusu hizo ishu za nafasi za ubunge na ukuu wa wilaya ni moja kama rushwa wanayotoa Tanganyika ili waendelee kuwatuliza wana CCM wa Zanzibar waendelee kutawala zanzibar.

Mimi ni mshabiki mzuri wa Lisu, ila tuseme ukweli kuwa safari hii ameteleza kidogo,. Ila kwa upande wa pili anachokifanya Lisu wazanzibari wanakifurahia sana mana ndipo wanapopataka kinuke ili kieleweke. tafauti na watangyika wengi wanavyohisi humu mitandaoni wao wanahisi kama vile wanawakomalia.
 
Tatizo jingine ni kuwa Wazanzibari kwa kuwa sasa hivi mzanzibari mwenzao ndo anatawala Tanzania, wamekaa kimya, kelele za madai yao ya kutaka Zanzibar huru wameyapunguza ili wasimkwaze mwenzao kwenye kutawala ILA siku akiingia Mtanganyika Ikulu ndo utaanza kusikia kwa wingi kelele za Watanganyika wanatubana watuache tupumue!

Huu Muungano unahitaji marekebisho makubwa sana

Hapana mkuu hilo sio kweli, Kinachowafanya wazanzibar kuwa kimya nikuwa wana hope kuwa Samia anaweza akafanya kitu Zanzibar, inavyosemekana kumekuwa na vikao vya siri vya hapa na pale baina ya Samia na ACT, na amekuwa akimbana bana Mwinyi kwenye mapambao yake na ACT. Kama unakumbuka majuzi tu ACT walitangaza kuwa wanajitoa Serikali ya umoja wa kitaifa, Samia aliwaita wakaelewana na ndio mana wametulia.

Wanahope kuwa anaweza kutatua matatizo ya tume ya Uchaguzi zanzibar. na ndio mana unawaona wametulia.
 
Narudia tena kusema. Huu muungano Nyerere alifanya kosa kubwa sana la kihistoria. Ilitakiwa iwe nchi moja tu. Naamin muda si mrefu hili kosa litafutwa kama alivyofanya India pale cashmir. Hicho kinchi kinatakiwa kuwa mkoa basi.

Unasikitisha sana, Halafu nawewe pia unawezakuta unalalamikia wakoloni walituonea wakati mindset yako haina tofauti na walivyokuwa wao.
 
Unasikitisha sana, Halafu nawewe pia unawezakuta unalalamikia wakoloni walituonea wakati mindset yako haina tofauti na walivyokuwa wao.
Kwan wakolon walikuwa na shida gan ambayo leo haipo. Tufafanulie
 
Kuna watu wanajaribu kuchukulia kauli za Lissu kukerwa na aina hii ya muungano kuwa eti anajaribi kuleta mgawanyiko wa Utanganyika na Uzanzibari.

Kiukweli kabisa kama ukifuatilia miongoni mwa watu waliojaribu kuwatetea Wazanzibari dhidi ya muungano huu ni Tundu Lissu. Lissu amekuwa consistent kwa muda mrefu kuwa muungano huu unawaumiza Wazanzibari sana, na kwamba Zanzibar imepoteza mengi kutokana na muundo huu wa muungano. Amefanya hivyo katika mijadala na hata katika mikutano ya hadhara. Nakumbuka amewahi kufanya mkutano mkubwa sana kule Zanzibar akieleza ni kwa namna gani muungano huu unavyowaumiza Wazanzibari.

Leo Lissu ameanza kuzungumza pia namna muungano unavyowaumiza Watanganyika, kuna watu wanatoka huko mbiombio kutaka kumnyamazisha!. Yaani Lissu akitetea wazanzibari hiyo inakuwa sawa, lakini akitetea Watanganyika hiyo inakuwa nongwa!. Kwa nini?

Ukimsikiliza Lissu kwa makini hana Tatizo na Uzanzibari wa Samia kama mtu ila ana tatizo na muundo wa muungano unaomfanya Mtu ale "kotekote" with impunity huku maslahi ya upande mmoja ( Wa Zanzibar yakilindwa kwa katiba yao) huku maslahi ya Tanganyika yakiwa hayana mtetezi (Kikatiba).

Leo inakuwaje Rais kutoka upande mmoja wa muungano anakuwa na mamlaka kwa mambo ya upande wa pili wa muungano ambayo siyo ya muungano?. Utalii siyo Jambo la muungano, iweje Mzanzibari awe na power ya kuwaamulia Watanganyika mambo yao ya utalii lakini mtanganyika hana power hizo kwa Zanzibar?

Leo tuna katiba ya Zanzibar, inayopingana hata na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mambo kedekede na hayo mambo yako wazi na yanajulikana na yako documented lakini watu wazima wamekaa kimya wanajifanya hawayaoni. Leo akitokea mtu kama Lissu akashikia bango mapungufu haya ili yaondolewe inabidi apongezwe siyo kubezwa!.

Katiba ya Zanzibar inasema Kutakuwa na "Mzanzibari" na imeorodhosha mzanzibari ni nani. Sasa Tujiulize Mzanzibari akishika madaraka ya Muungano kisha maslahi ya Zanzibar yakagongana na Maslahi ya Tanganyika katika mambo yasiyo ya Muungano yeye atatetea maslahi ya wapi?

Na katiba ya Zanzibar ikaenda mbele kusema kuwa Zanzibar ni nchi miongoni mwa nchi mbili ZINAZOUNDA jamhuri ya muungano wa Tanzania, Pigia msitari neno ZINAZOUNDA siyo ZILIZOUNDA, Sasa hiyo nchi nyingine inayounda muungano na Zanzibar iko wapi na kiongozi wake ni nani na watu wake ni akina nani?.

Hoja ya Lissu siyo Uzanzibari wa Samia. Hoja ya Lissu ni muundo mbovu wa Muungano. Uraisi wa Samia ni mfano tu kuonyesha muundo huo ulivyo na tatizo.

Ni mpaka tukae chini tusolve hili tatizo, la sivyo huko tuendako ni shida tu. Ndiyo maana leo Kuna Wazanzibari wanataka Watanganyika waende Zanzibar na Passport. Na mimi sioni shida Wazanzibar wakija Tanganyika kwa passport.
Shida ni moja wachumia tumbo ukigusa maslahi Yao tu unaonekana mbaya
 
Back
Top Bottom