Kwenye maisha usiruhusu kila mtu akuzoee ni KOSA kubwa mno pia weka muda maalum wa watu kukupigia simu

Hicho ni kiburi tuu huna hela huna maisha na kwanza ndio umepanga et hupokei simu kwakua waanakulipa mshahara 1M

Acha ushamba maisha yako yanazungukwa na watu ukipatwa na jambo hao watu ndio wa kwanza kukusaidia na kukutolea michango pale inapobidi.. imagine umepatwa na magonjwa mazito hao watu watachanga kukusaidia...

Imagine jirani kaona mwizi dirishani kwako anakupigia kuna uwezekano wa kumkurpua maana wengine wanakua na spray wanakupulizia wanafanya kila kitu..

Mazoea ambayo mabaya ni yale mtu kuingilia maisha yako binafsi na sio kosa kusalimiwa hicho ni kiburi na ushamba ambao hauna3 faida yoyote

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
 
Aseeh!!
 
nyieeee,maisha hayako serious namna hiyo.
nyinyi ndio mnabandika ratiba za misosi kwenye kuta za jikoni[emoji1787][emoji1787][emoji1787].

mtu akikudharau unatoboka!!!si ni upuuzi wake unamsumbua??

mimi kanuni yangu katika maisha huwa sichagui wa kumzoea,sitarajii maajabu kwa binaadam maana nawajua wana visa,wajeuri,wana roho za kwanini,hivyo hata ninapokuzoea nimebeba matokeo yote.

kuna nyumba nilipanga na mama mmoja yeye alikuwa anaishi na watoto wake wa kiume 3,mkubwa ni mlevi mbwa,akija kalewa anaingia ndani kwangu full misele na kuyumba,anakomaa amabebe mtoto nakuwa naye makini tu,siku moja akakojoa ndani kwangu imagine,sijui alitarajia ningesemaje!!!nilikaa kimya tu maana ndio hawa viumbe waliomfanya Mungu akajificha,ni wakorofi sana.
 
BIG FACT
 
"....Kingine weka muda wa watu kukupigia simu ukiona unapigiwa simu mpaka usiku wa manane iyo ni dharau na wamekuchukulia cheap"

Umeandika kweli tupu.
Inategemea kama wewe ni mfanyabiashara simu ya kibiashara muda wote ruksa

Hayo ya kuweka muda maalumu ni ya nyie vibarua wa kuajiriwa na msio na cha maana kwenye maisha zaidi ya Kuchat kwenye simu
 
"....Kingine weka muda wa watu kukupigia simu ukiona unapigiwa simu mpaka usiku wa manane iyo ni dharau na wamekuchukulia cheap"

Umeandika kweli tupu.
Mnalishana ujinga mtupu
Mfano Raisi anakupigia usiku kuwa umepata uteuzi usiku wa manane atakuwa kakudharau?
Ziko post kizima simu kazi huna na huwezi panga upigiwe simu saa ngapi
 

Hii sms hata kwa maskini hohehahe, yaani mafukara?

Ndugu yangu, fukara hana jingine zaidi ya kujichanganya na walimwengu walau apate riziki yake.
 
Mkuu Hilo liko sawa na usipende kuweka Mambo yako na kazi unazofanya za kutafuta riziki hakuna mtu anayependa maendeleo yako Zaid ya mzazi Alie kuzaA
 
Kuna jamaa alikuwa hivyohivyo,sitaki mazoea sitaki mazoea.Saivi anasalimia Kilamtu nakila mtu ni msaada kwake..
Alipata ajali na gari yake tumiguu Hana anatembelea matako.Watu ni watu tu.
 
Perfect kabisa, lazima uweke limitation kwenye maisha yako bhana....Nimekuelewa...liwe somo kwa wengine.
 
Watu wengi tunaishi na wengine kinafki kwa kuhofia tukipata matatizo tutakosa msaada wa namna moja ama nyingine!.

Mtoa mada anazungumzia limit, limit kila mtu ana za kwake,

Mathalani mimi namuwekea kila mtu limit kulingana na mazingira nnayofahamiana nae, i.e mfanyakazi mwenzangu mi na yy ni kazikazi, jirani ni jirani tu hakuna zaidi ya hapo, boss wangu kazini ni kazini tu, ndugu ni ndugu tu na hatakiwi kuinglia kazi zangu, walevi wenzangu ni pombe na eneo la kukutana ni bar tu nje ya hapo ni kuwe na sababu ya msingi sana..

Kuhusu simu hizi kiukweli zimetuondolea ustaarabu, na hua hatuwazii upande wa pili. Mtu akikupigia simu usipopokea anageuza kesi hajui ulikua unafanya nini, au mtu anashindwa kujiongeza kua kuanzia saa 4 usiku mtu amechoka na mihangaiko yake hivyo simu zisizo za msingi za usiku ni usumbufu!.
Hizi simu kwangu mimi binafsi hua naona mtu anipigie mara moja tuu, simu iite mpaka ikate, isipopokelewa nikiiona missedcall ntapiga, kama ni urgent sana basi missed call na angalau meseji moja inayoelezea emergency yenyewe kwa kina na kwa ufupi.
 
Maake apo kwanza nikupigie simu🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…