Kwenye msitu wangu kuna black mamba/ koboko natafuta njia za kumwangamiza bila kuleta madhara kwenye jamii

Kwenye msitu wangu kuna black mamba/ koboko natafuta njia za kumwangamiza bila kuleta madhara kwenye jamii

Nitatafuta nipost humu, nimewahi kuishi porini katikati ya mlima sikuwahi kuona nyoka sehemu ya makazi ya Watu, Lakini kwenye mlima kila siku Tulikuwa tunapishana nao.

Hadi wenyeji waliponiambia Siri ya miti iliyopandwa kuzunguka Eneo letu la kuishi
Yap! Tulio wengi pia tutajifunza hapo.
 
Kwa akili ya kawaida, hakuna namna utafanikiwa kuwadhibiti hao nyoka. Hilo shamba/pori ni makazi yao asili, na watakuwa wengi hadi mashamba ya jirani. Ni bora usihangaike maana kama lengo ni kufuga nyuki na siyo kilimo ambapo inabidi usafishe pori, hao nyoka huwezi kuwaondoa mkuu.
 
Jf salaam🙏

Ni muda sasa tangu aanze kuonekana huyu nyoka hatari koboko na inasemekana wapo wawili.

Taarifa zilianza kunifikia kutoka Kwa wazee wangu maana huo msitu ukweli sio wangu ni wa mzee ila kaniruhusu kufanya shughuli zozote za kujiingizia kipato.

Mara kadhaa amekuwa akionekana na muda wa usiku kupiga kelele flani Hivi.

Nakumbuka baada ya kupata mapumziko mafupi nilienda kijijni kwa wazee wetu. Nikafika na nikaenda mlimani(msituni) lengo nikufanya research kwa kina Ili niwekeze ufugaji wa nyuki (asali).

Nilimchukua dogo mmoja ambae Huwa anachunga mbuzi wangu tukaenda naye huku akinifotoa picha za kila aina na Kila Rangi.

Mwisho tukafika kwenye mti mzuri wenye kijani kibichi wenye matawi mazuri akanipigia picha za kutosha pale.

Baada ya hapo tukakaa chini ya mti huo kwenye jiwe huku nikipitia picha nilizopigwa na kufuta zile sikuzipenda

Tukiwa hapo tunapiga story ghafla tukasikia kelele za ndenge flani juu ya mti Mimi kelele zile nazijua huwa ni Alert ya hatari fulani wameiona wale ndege.

Kuinua macho juu sikuamini nilichokiona ni yeye koboko mtesa ametulia tulii Wala hatikisikii kama amekufa.

Dogo(muha) kumuona akapanic akaanza mbio nikamwambia simama hapohapo akasimama huku nami nikitoka eneo la tukio hadi kwa dogo.


Nyoka ni mkubwa na anaogopesha na kwa mazingira yale huwezi mshambulia kwa kutumia njia zetu hizi za asili(fimbo)

Maana ni mstuni vinginevyo anakuua ndani ya muda mfupi tu hakuna sehemu ya ku escape asikudhuru.

KUMBUKUMBU ZANGU

Miaka ya nyuma tukiwa wadogo nilishuhudia maiti za Watoto wenzetu watu na ng'ombe 7 zikiwa zimelala Chali (kufa).

Ni baada ya Hawa Watoto kuona huyo nyoka aina ya koboko na kumshambulia ndipo alipowageuka na kuwauma wote wawili na ng'ombe zao zote Saba na zilikufa hapohapo!

Nakumbuka kipindi hicho hicho nikiwa primary mtoto mwingine darasa letu Moja akiwa anaenda kuokota maembe kwenye mti wa mwembe akamuona koboko Kasimama wima naye pasina kujua alianza kumshambulia.

Hapo hapo alimgonga na kufa mama yake alisikia kelele za mwanae akilia Kwa uchungu Kwa sababu ilikuwa mbali na mwembe na mara zote walikuwa wanaenda Watoto kadhaa kuokota maembe pale. ile anatoka akamsaidie alimkuta tiyari kashafariki na nyoka amepanda juu ya mtu flani mfupi.

Ndipo alipo piga yowe kuomba msaada na walifanikiwa kumuua.

Inavyosemekana na Mimi naweza kuwa shahidi wa hili ni kwamba....

Nyoka aina ya black mamba ni wapole kupita kiasi pale anapokuwa katika Hali yake ya kawaida.

Pia anasikia kuliko kawaida anaupeo mkubwa wa kuhisi hatari na hata harufu na hivyo kujiweka tiyari Kwa ajiri ya mapambano.

Akiona mazingira aliyopo sio salama kwakwe kufanya shambulio hujiondokea kabla hujamfikia Wala kumuona.

Lakini pale ukimuona wewe jua kakusubiri na amejiandaa Kwa muda mrefu sana amegojea tu ulianzishe upate unachostahili.

Kwa matukio hayo mawili ambayo siyo ya kusimuliwa na hili langu Mimi mwenyew Tena mwezi 2 tu mwka huu nakubaliana na hili kuwa Hawa nyoka ni wapole na ni hatari.

Tukio la wale watoto wawili na ng'ombe wao. Sisi ndo tulikuwa wa kwanza kumuona yule nyoka na ilikuwa Hivi.....

Siku Moja tunaenda machungani katikati ya njia kulikuwa na mti flan Hivi kama kichaka (ipo miti Ina randa na kutengeneza kichaka kizito)

Tulipitisha mifugo yetu yote salama na sisi wenyewe tukapita salama mtu wa4 ndo akatumbia oneni yule nyoka tukarudi kumtazama asee alikuwa mrefu sana na ametulia kama hajui kinachoendelea...

Tulichokifanya ni kwenda kuwambia wakubwa wetu karibu na eneo lenyewe. Na walipokuja wakamuona na kumtambua walitumbia ondoeni ng'ombe na mifugo yenu hapa tukafanya hivo.

Nao walipoona tumeondoka waliondoka pia bila kumfanya chochote.

Bahati mbaya sana Kwa wenzetu siku chache mbele wao walipo muona tu ujasiri uliwaingia na kuanza kumshambulia huo ndo ulikuwa mwisho wao na ng'ombe wao pia.

Yowe lilipigwa nyoka huyo akauliwa.

Nimekuja kuomba ama kufundishwa njia/mtego Ili nimuue bila kuathiri watu wa maeneo hayo.

Msitu huu nimepanga kufugia nyuki Kwa wingi lakni kinacho niogopesha ni uwepo wa black mamba kwenye eneo hili.

Eneo ni zuri sana Kwa nyuki kwani maji yapo si zaidi ya mita250 na nyuki ni wengi sana hasa kwenye mapango ya miti,mawe na wengine hujitengenezea asali juu ya mti tu.

Najua humu Kuna watu wa maliasili na wataalamu wa maswala haya naombeni namna ya kumuondoa huyu mdudu na nimeambiwa wapo wawili.

Wapo walio waona Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti na usiku hupiga kelele zao Kwa kupokezana wasi wasi wangu zaidi watazaliana na kuongezeka zaidi.

Ahsanteen sana.

View attachment 2945391
Maadamu unelileta humu sisi tutakushauri

Ushauri wangu ni huu. Wasiliana na maafisa wanyamapori waje kuchukua nyara yao
 
Kwa akili ya kawaida, hakuna namna utafanikiwa kuwadhibiti hao nyoka. Hilo shamba/pori ni makazi yao asili, na watakuwa wengi hadi mashamba ya jirani. Ni bora usihangaike maana kama lengo ni kufuga nyuki na siyo kilimo ambapo inabidi usafishe pori, hao nyoka huwezi kuwaondoa mkuu.
Aaah! Usimkatishe tamaa aisee. Hakuna lisilo wezekana chini ya hili jua. Kama amedhamiria ; lazima itapatikana njia tuu. Kikubwa hapo ni yy kuwa mstahimilivu kwani huenda ikamchukua muda (lakini ni muda mfupi sana) kupata ufumbuzi tatizo hilo.
 
Kwa akili ya kawaida, hakuna namna utafanikiwa kuwadhibiti hao nyoka. Hilo shamba/pori ni makazi yao asili, na watakuwa wengi hadi mashamba ya jirani. Ni bora usihangaike maana kama lengo ni kufuga nyuki na siyo kilimo ambapo inabidi usafishe pori, hao nyoka huwezi kuwaondoa mkuu.
Wakiongezeka na hatari inaongezeka kabisa
 
Aaah! Usimkatishe tamaa aisee. Hakuna lisilo wezekana chini ya hili jua. Kama amedhamiria ; lazima itapatikana njia tuu. Kikubwa hapo ni yy kuwa mstahimilivu kwani huenda ikamchukua muda (lakini ni muda mfupi sana) kupata ufumbuzi tatizo hilo.
Upo sawa mkuu yaani anamanisha Hadi 2050 nakuendelea mstu uwe wa kuhifadhi manyoka tu ! Hapana kwakweli
 
Hakuna shida mkuu, nyoka kwake ni porini na huko ndo maskani yake na ukitaka kum-disturb ndo utaangamia. Yaani mpaka umefika hapo kwenye msitu wako umewapita nyoka kibao sema Kwa kuwa hujawashitukia unaamini huko kwenye mashamba mengine hakuna nyoka.

Nyoka Kwa binadamu ni mwoga na akimwona binadamu huwa akiwa kwenye position nzuri huwa anatoka nduki hasa akiwa chini kwenye nyasi ila akiwa juu ya mti huwa hana option ya kufanya na mara nyingi huwa anapiga kimya (unamuona katulia tu na ulimi wake) na huwa ana assume hujamuona. Na hapo sasa bahati mbaya za kugongwa na nyoka hutokea ukipita karibu yake ana assume kama unamfuata lakini napo hakugongi tu mpaka uwe karibu sana kiasi kwamba anahisi una jambo unataka kujifanya

Wewe endelea na shughuli zako yaani hapo akiona Kila siku mpo hapo atatafuta sehemu nyingine ya kujistiri
Ahsantee Kwa ushauri ila yataka moyo sana mkuu
 
Ni msitu wa ukoo kama umenisoma vizuri katka maelezo yangu nimekiri sio wangu ni WA mzee ndo mmriki wake katika siku za Hivi karibuni nimedhamiria kuanzisha mradi wa ufugaji nyuki mle maana Kwa upande wa mzee Hana shida na yeye kama mzazi wangu ndo atakuwa mnufaika mkubwa
 
Ushauri umetulia huu
Watu wengi wamependekeza Hivo kuwa niruhusu wachoma mkaa ila Kwa sharti la kuwaambia waache baadhi ya miti pakiwa peupe hawezi kaa.

Kabla sijafanya hiyo njia nikawaza nililete humu lengo nikuwa mazingira yataharibika iwapo nitaruhisu wachomaa mkaa najua Fujo za wasukuma katika kukata miti Huwa wanaichimba Hadi visiki
 
Atawapata kivipi au anawa-introduce kwenye msitu wake kwa njia gani na atawazuiaje ili wabaki hapo msituni wasije nao wakahama then ikawa ni back to square one.?
Uzuri wa wale wanapenda maeneo ya vichaka , mangroose anaweza kuwakamata na kuwapeleka ila inahitaji gharama wangu wa vijijini wanajua kuwatega , ila 🦡 ni ngumu kumkamata.

Kwa nature ya eneo aliloelezea wanayapenda sana hawa wadudu sidhani kama wanaweza kuhama labda wafukuzwe
 
Huyu kiumbe ni hatari sana hasa anapokuwa na hasira ana mbio na uwezo wa kuruka , japo huwa sio mkubwa kivile wengine humpamba kwa uhatari wake.

Kwanini usiwaruhusu wanakijiji wamuue au nao hawataki kusikia
Shida anaoneka mstuni tu yaani porini laiti angelionekana maeneo ya wazi angekuwa kama uawa muda sana
 
Back
Top Bottom