Kwenye ndoa za kikristo uasherati pekee ndio uliruhusiwa kuvunja ndoa, kwanini wakristo huvunja ndoa kwa sababu zingine ambazo hazijaruhusiwa?

Kwenye ndoa za kikristo uasherati pekee ndio uliruhusiwa kuvunja ndoa, kwanini wakristo huvunja ndoa kwa sababu zingine ambazo hazijaruhusiwa?

Mbona nimeambukizwa ukimwi na mume wangu na nimesamehe...tuko happy tunachukuliana ARV?
Mioyo ipo tofauti mama angu, hilo kwako n la kawaida na unaendelea na maisha, lkn mwngn hy hali inaweza kumfanya kujiua.
 
Nadhani huelewi tofauti ya mambo. Wakristo hawafungwi na torati. Ndio maana huwezi mkuta mkristo anampiga mawe mchawi japo torati inaamuru hivyo.

Kwamba mafundisho ya Agano Jipya hayana sheria? kidding me?
Yesu aliposema mpende jirani yako kama nafsi yako yalikuwa ni maoni? Au alipowaambia wanafunzi Amri mpya nawapa, pendaneni yalikuwa ni maoni?

Aliposema enendeni ulimwenguni mkaihubiri injili nayo yalikuwa maoni?
Someone is confused here!


Acha kudanganya watu. Na haya ni maoni ama? Au na Biblia nayo haielewi dini?
"Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe." - 1 Wakorintho 7:10-11


Haya pingana na Yesu hapo...
"Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi" - Yohana 13:34-35

Hapo hakuna amri mpya Sheikhe!
Acha ubishi usio na maana.

Kwenye injili hakuna sheria mpya hata Moja.
Unaposoma Biblia jaribu kuelewa kuwa Sheria zipo Kwa Musa, huko kwingine ni maoni na mafundisho ya manabii na mitume.
Haihitaji akili kubwa kutambua Hilo.

Hiyo amri ya Upendo IPO kwenye Torati,

Kumbukumbu la Torati 6:5-7
Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyasema uishipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.

Mambo ya Walawi 19:18
Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.


Huyo Paulo mambo mengi aliyokuwa anayaeleza ni maoni yake binafsi Kwa Wamataifa.
Ukisoma Biblia jaribu kuelewa anayeandika yupo katika Mazingira gani, na alikuwa anawaandikia kina nani.

Usipojua hayo utajikuta badala ya kupata maarifa unakuwa mjinga zaidi.

Alafu kuna mambo bado huyaelewi kuhusu sheria hizo za kupiga mawe, ungeomba ueleweshwe.

Wayahudi Mwanzoni kabla ya kuwepo wafalme walikuwa wanaongozwa na Mungu mwenyewe, baadaye wakakataa kuongozwa na Mungu hivyo wakataka kuongozwa na wafalme wa kibinadamu Kama mataifa mengine.
Ndipo wakatokea Waamuzi kabla ya ujio WA Wafalme.

Mpaka hapo bado hujaelewa Kwa nini watu hawapigwi mawe?
Jibu ni Kwa sababu dunia haifuati sheria za Mungu Kwa 100% isipokuwa zinafuata upagani na ushetani.

Bado hujanielewa?

Sheria za Mungu ni zilezile hazibadiliki
 
Mbona zaka na fungu la kumi ni agano la kale ila makanisa ya zama hizi yanasisitiza waumini watoe.. hawasemi waache maana ni agano la kale
Nielewe ikiwa Jambo hilo limejakuwa addressed upya by Jesus Christ unatakiwa usimame kwenye maelezo ya Yesu!
Chukulia mfano Musa aliruhusu talaka ila Yesu alirekebisha.
Twende kwenye hoja yako: zaka na 10% , Je kuna popote ambapo Jesus ametoa corrective statement? If yes fuata alichoelekeza Yesu
 
Mioyo ipo tofauti mama angu, hilo kwako n la kawaida na unaendelea na maisha, lkn mwngn hy hali inaweza kumfanya kujiua.
Kwa ujinga gani nijiue?
Hao wasio na HIV mbona ndio spanner mkononi zaidi...ikubali hali, kubali tukio samehe move on!
 
Nielewe ikiwa Jambo hilo limejakuwa addressed upya by Jesus Christ unatakiwa usimame kwenye maelezo ya Yesu!
Chukulia mfano Musa aliruhusu talaka ila Yesu alirekebisha.
Twende kwenye hoja yako: zaka na 10% , Je kuna popote ambapo Jesus ametoa corrective statement? If yes fuata alichoelekeza Yesu
alirekebisha ??? Yesu alikuja kurekebisha sheria za kale ??
 
alirekebisha ??? Yesu alikuja kurekebisha sheria za kale ??
Ndio, Yesu alitutoa kwenye sheria, mafundisho yake hayakuwa ya kisheria bali ya kiroho.
Ndio maana kiroho tumekombolewa kwa damu ya Yesu, hatuitaji tena sadaka za kuteketezwa (Sheria) ili kufutia dhambi.
 
Ndoa ya Kikristo haina talaka kwa sababu yoyote ile. Kinachoruhusiwa ni kutengana na kutoishi pamoja. Ila bado ndoa ipo palepale!
Huwa hekima ya kichungaji inasema kama Yesu Kristo anatusamehe makosa na dhambi zote kwanini wewe usimsamehe mwenza wako? Huu hasa ndio msingi wa kanisa kusema ndoa ya kikristo haivunjiki.

Lakini maneno ya Bwana Yesu Kristo yapo clear, endapo mwenzi amevunja agano la ndoa kwa uzinzi (hapa niongezee kidogo; na ameendelea hivyo na hakusudii kubadilika) basi hapo unaruhusiwa kumuacha na ndoa inaisha.

Mathayo 5:32 SRUV
lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
 
Kuweka kumbukumbu sawa hapa.

Kwa mujibu wa imani ya kikristo ndoa haivunjiki mpaka kifo. Kwa sababu ya uasherati wanandoa wanaweza kuachana lakini ndoa yao itabakia pale pale (kwa maana kuwa hawaruhusiwi kuoa au kuolewa tena)

Mathayo 5:32 SRUV​

lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
 
Hapo hakuna amri mpya Sheikhe!
Acha ubishi usio na maana.
Umejibu jumla jumla kwa sababu unajua kuna mambo umedanganya
Kwenye injili hakuna sheria mpya hata Moja.
Unaposoma Biblia jaribu kuelewa kuwa Sheria zipo Kwa Musa, huko kwingine ni maoni na mafundisho ya manabii na mitume.
Haihitaji akili kubwa kutambua Hilo.
We endelea kutumia akili kubwa ama ndogo. Ila maandiko niliyoweka sio maoni. Labda kama neno maoni limebadilika maana. Ila kama unataka kung'ang'ania maoni maoni... sawa. Endeleea!
Hiyo amri ya Upendo IPO kwenye Torati,

Kumbukumbu la Torati 6:5-7
Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyasema uishipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.

Mambo ya Walawi 19:18
Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.
Aliyesema amri mpya nawapa ni mimi au Yesu? Bishana na aliyesema, sio mimi!
Kama hujaelewa kitu na ukawa mbishi hivi utabakia hivyo hivyo. Alichokisema Yesu yuko sahihi. Ile ni amri mpya aliwapa! Sasa bishana naye kama hutaki!

Huyo Paulo mambo mengi aliyokuwa anayaeleza ni maoni yake binafsi Kwa Wamataifa.
Ukisoma Biblia jaribu kuelewa anayeandika yupo katika Mazingira gani, na alikuwa anawaandikia kina nani.
Acha mbwembwe. Rudi kwenye amri alizozitoa Paulo. Tena anasema wazi sio amri zake ni za Bwana. Nimekuwekea kabisa ila unakaza shingo tu bila sababu.

Kama hupendi zichane toka kwenye Biblia yako, kama unayo, bakiza maoni!

Usipojua hayo utajikuta badala ya kupata maarifa unakuwa mjinga zaidi.
Wewe unajua kuliko Yesu, unajua kuliko Paulo. Unajua kuliko Mungu. Kwa mantiki yako unadhani ni mjinga kiasi gani?

Alafu kuna mambo bado huyaelewi kuhusu sheria hizo za kupiga mawe, ungeomba ueleweshwe.
Sidhani kama nahitaji kueleweshwa na mtu anyebishana na Biblia. Kama Yesu anasema amri mpya wewe unasema ya zamani, unadhani nahitaji kueleweshwa na wewe?

Wayahudi Mwanzoni kabla ya kuwepo wafalme walikuwa wanaongozwa na Mungu mwenyewe, baadaye wakakataa kuongozwa na Mungu hivyo wakataka kuongozwa na wafalme wa kibinadamu Kama mataifa mengine.
Ndipo wakatokea Waamuzi kabla ya ujio WA Wafalme.

Mpaka hapo bado hujaelewa Kwa nini watu hawapigwi mawe?
Kwa hiyo yule mwanamke waliyemleta kwa Yesu aliyekutwa amezini walitaka kumpigia magitaa au vinanda?
Na hapo Mungu alikuwa bado anawaongoza mwenyewe? Au una maana Herode na Kaisari alikuwa ni Mungu wa Waisraeli?

Jibu ni Kwa sababu dunia haifuati sheria za Mungu Kwa 100% isipokuwa zinafuata upagani na ushetani.
Sheria zote msingi wake ni Mungu. Kamwulize hakimu kwa nini ni kosa linalostahili kifo kuua mtu?

Bado hujanielewa?

Sheria za Mungu ni zilezile hazibadiliki
Sheria za Mungu ni zile zile kweli, ila hakuwapa wanadamu zote kwa pamoja. Na zina application tofauti kwa context tofauti.

Uko chaka sana kwenye mtazamo wako. Ukiacha kudhania unajua Biblia kuliko waandishi wa Biblia utasogea mahali!
 
Ndoa ya Kikristo inatalaka kulingana na sheria.
Tofautisha maoni na sheria.

Dini zinaongozwa Kwa sheria na sio Maoni.

Sheria zipo kwenye Torati tuu huko kwengine ni mafundisho na maoni ya mitume na manabii.
Mfano Mtume Paulo Kwa sehemu kubwa alikuwa anatoa maoni yake zaidi ambayo watu wengi hasa Wakristo wasioelewa Dini wanafikiri maoni yake ndio SHERIA.

Hata Yesu katika Injili hakuleta Sheria yoyote mpya isipokuwa alikuwa anatimiliza sheria.

Kwenye Dini sheria zipo za Talaka.
Asipoelewa nitag nimfumue kichwa
 
Ndoa ya Kikristo inatalaka kulingana na sheria.
Tofautisha maoni na sheria.

Dini zinaongozwa Kwa sheria na sio Maoni.

Sheria zipo kwenye Torati tuu huko kwengine ni mafundisho na maoni ya mitume na manabii.
Mfano Mtume Paulo Kwa sehemu kubwa alikuwa anatoa maoni yake zaidi ambayo watu wengi hasa Wakristo wasioelewa Dini wanafikiri maoni yake ndio SHERIA.

Hata Yesu katika Injili hakuleta Sheria yoyote mpya isipokuwa alikuwa anatimiliza sheria.

Kwenye Dini sheria zipo za Talaka.
Hapa umechanganya ngano na magugu.
 
Nadhani huelewi tofauti ya mambo. Wakristo hawafungwi na torati. Ndio maana huwezi mkuta mkristo anampiga mawe mchawi japo torati inaamuru hivyo.

Kwamba mafundisho ya Agano Jipya hayana sheria? kidding me?
Yesu aliposema mpende jirani yako kama nafsi yako yalikuwa ni maoni? Au alipowaambia wanafunzi Amri mpya nawapa, pendaneni yalikuwa ni maoni?

Aliposema enendeni ulimwenguni mkaihubiri injili nayo yalikuwa maoni?
Someone is confused here!


Acha kudanganya watu. Na haya ni maoni ama? Au na Biblia nayo haielewi dini?
"Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe." - 1 Wakorintho 7:10-11


Haya pingana na Yesu hapo...
"Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi" - Yohana 13:34-35

Huyo Paulo kwenye Wakorintho Hana mamlaka ya kumuagiza yeyote kuhusu mambo yanayohusu Amri za Mungu.

Anasema watu wasiachane Kwa maoni yake na wala sio Kulingana na sheria za Mungu, kama zilivyoshuka Kwa Mkono wa Musa,

Kumbukumbu la Torati 24:1
Mtu akiisha kutwaa mke kwa kumwoa, asipopata kibali machoni mwake, kwa kuwa ameona neno ovu kwake, na amwandikie hati ya kumwacha, akamtilie mkononi mwake, na kumtoa katika nyumba yake.

Kumbukumbu la Torati 24:2
Naye akiisha kuondoka katika nyumba yake, ana ruhusa kwenda akawa mke wa mtu mwingine.

Kumbukumbu la Torati 24:3
Na huyo mumewe wa sasa akimchukia, na kumwandikia hati ya kumwacha, na kumpa mkononi mwake, na kumtoa katika nyumba yake; au akifa yeye mumewe wa sasa, aliyemtwaa kuwa mkewe;

Kumbukumbu la Torati 24:4
yule wa kwanza aliyemwacha asimtwae kuwa mkewe tena, akiisha kutiwa unajisi; kwa kuwa haya ni machukizo mbele za BWANA; kwa hiyo usiitie dhambini nchi, akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi.


Hizo ni sheria na sio Maoni ya mtu Kama yalivyomaoni ya Huyo Paulo ambaye Hana tofauti na kina Mwakasege

UKISOMA BIBLIA AU QURAN zingatia Nani anasema na Nani anaambiwa katika muktadha au Mazingira yapi
 
Hapa umechanganya ngano na magugu.

Tatizo Wakristo wanachanganya sheria za Dini na sheria za Kanisa😂😂

Sheria za Dini zipo kwenye Biblia, sheria za Kanisa baadhi hazipo katika Biblia.

Kisheria na Kidini talaka inaruhusiwa.
Ila taratibu na kanuni za Kanisa haziruhusu Talaka.

Kwenye Biblia sheria utazipata kwenye Torati asijeakakudanganya mtu.
Zaburi, injili, vitabu vya unabii au historia hazitoi sheria yoyote isipokuwa Mafunzo ya kupigilia msumari umuhimu wa sheria
 
Huwa hekima ya kichungaji inasema kama Yesu Kristo anatusamehe makosa na dhambi zote kwanini wewe usimsamehe mwenza wako? Huu hasa ndio msingi wa kanisa kusema ndoa ya kikristo haivunjiki.
Hii pia ni sababu nzuri ila siyo ultimate reason. Sababu kuu ambayo wote hapa mtatakiwa kuijibu ni hii:
"Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe" - Mathayo 19:6

Swali: Mungu huwa anashuka saa ngapi kuwatenganisha watu hawa?

Lakini maneno ya Bwana Yesu Kristo yapo clear, endapo mwenzi amevunja agano la ndoa kwa uzinzi (hapa niongezee kidogo; na ameendelea hivyo na hakusudii kubadilika) basi hapo unaruhusiwa kumuacha na ndoa inaisha.

Mathayo 5:32 SRUV
lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
Kwanza andiko ulilonukuu halisemi Uzinzi, bali uasherati. Uasherati ni kwa watu ambao hawajafunga ndoa. Na kwasababu kwa desturi za Wayahudi mwanamke akiposwa huyo ni mke wa aliyemposa, hata kabla ya ndoa, hili la kuachana kwa uasherati lina apply. Ndio maana Yusufu alitaka kumwacha Mariamu alipogundua ni mjamzito akijua amefanya uasherati. Malaika alimwita Mariamu mke wa Yusufu japo walikuwa hawajaoana bado.

Zaidi ya hayo, ukienda Mathayo 19, Yesu kalifafanua hilo kwa undani sana na hakuna talaka. Next comment nitaiweka Mathayo 19 na kuweka maoni yangu kwenye mistari. Utaona hakuna talaka kwa ndoa ya Kikristo kwa sababu yoyote ile!
 
Mbona zaka na fungu la kumi ni agano la kale ila makanisa ya zama hizi yanasisitiza waumini watoe.. hawasemi waache maana ni agano la kale
Zaka ipo agano jipya ila sasa hivi hauitoi kama sheria bali unaitoa katika imani kwamba Bwana Yesu Kristo anaipokea.. soma waebrania sura ya saba yote.
 
Nadhani huelewi tofauti ya mambo. Wakristo hawafungwi na torati. Ndio maana huwezi mkuta mkristo anampiga mawe mchawi japo torati inaamuru hivyo.

Kwamba mafundisho ya Agano Jipya hayana sheria? kidding me?
Yesu aliposema mpende jirani yako kama nafsi yako yalikuwa ni maoni? Au alipowaambia wanafunzi Amri mpya nawapa, pendaneni yalikuwa ni maoni?

Aliposema enendeni ulimwenguni mkaihubiri injili nayo yalikuwa maoni?
Someone is confused here!


Acha kudanganya watu. Na haya ni maoni ama? Au na Biblia nayo haielewi dini?
"Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe." - 1 Wakorintho 7:10-11


Haya pingana na Yesu hapo...
"Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi" - Yohana 13:34-35

Alafu unaposema Wakristo hawafungwi na Torati unazungumzia Wakristo wapi hao?

Maana kuna Wakristo Wapagani ambao ndio hao hawafuati amri za Mungu (hawamuamini Mungu)
Alafu kuna Wakristo wanaomuamini Mungu.

Ukishajiona Huna uwezo wa kumuoa Mama yako au Binti Yako basi jua unafungwa na torati maana yenyewe ndio inakataza mtu kufanya hayo.

Ni mtu Mpumbavu pekee au asiyeelewa anasema nini ambaye atasema hafungwi na torati ilhali Kwa zaidi ya 90% ya maisha yake yanadhibitiwa na sheria za torati.
 
Huyo Paulo kwenye Wakorintho Hana mamlaka ya kumuagiza yeyote kuhusu mambo yanayohusu Amri za Mungu.

Anasema watu wasiachane Kwa maoni yake na wala sio Kulingana na sheria za Mungu, kama zilivyoshuka Kwa Mkono wa Musa,
Naona we niachane na comments zako hapa! Mtu anasema nawaagiza, na tena anasema sio mimi ni Bwana, bado unaokomaa tu. Basi endelea kukomaa hivyo hivyo!
 
Back
Top Bottom