Kwenye ndoa za kikristo uasherati pekee ndio uliruhusiwa kuvunja ndoa, kwanini wakristo huvunja ndoa kwa sababu zingine ambazo hazijaruhusiwa?


Hayo ni maoni ya Yesu ambayo yupo sahihi.

Kama waliunganishwa Kwa sheria basi jua wanaweza kuachanishwa na sheria.
Sheria ndio inamfanya mwanamke na Mwanaume kuwa Mume na Mke, sijui wapi huelewi.
Na sheria huyohuyo ndio inaweza kuwatenganisha wakawa Watalaka.

Mtu haruhusiwi kutenganisha alichounganisha Mungu Kwa sheria. Ila sheria za Mungu zikikiukwa wanandoa wanaachanishwa Kwa zilezile sheria zilizowaunganisha.

Sijui kama unaelewa kuhusu mambo ya sheria hata za kibinadamu.
 
Naona magugu yanazidi kuwa makubwa kuliko ngano.
 
Kwa ujinga gani nijiue?
Hao wasio na HIV mbona ndio spanner mkononi zaidi...ikubali hali, kubali tukio samehe move on!
Sasa tujiulize hao wanaoachana/kujiua n kwann wamekosa moyo kama wako, tuko tofauti.
 
Naona we niachane na comments zako hapa! Mtu anasema nawaagiza, na tena anasema sio mimi ni Bwana, bado unaokomaa tu. Basi endelea kukomaa hivyo hivyo!

Ndio maana nikakuambia yeye anatuagiza kama Nani?

Kamwambie aliyekufundisha Biblia arudie tena kwani hukuelewa ili usijepotosha watu huku.

Sheria ndio inaweza Kuruhusu na kukataza na sio Maoni ya watu.

Sheria pekee kwenye Biblia zilishuka Kwa Mkono wa Musa zinaitwa TORATI
Sasa wewe wapi hauelewi?
Unashindwa kutofautisha Kati ya sheria za nchi na Sera za nchi?
 
Sasa yamekuwa magugu peke yake.

Robert, pata nafasi ujifunze ukristo kupitia mafundisho sahihi. Huo ni ushauri wangu kwako.
 
1 Wakorintho 7:10-11, Mathayo 19 kwa uchache!

Hizo sio sheria, jaribu kuelewa.

Ni Sawa uende mahakamani alafu upeleke vitabu vya physics au chemistry, au vitabu vya Afya. Hivyo vinaweza kutumika Kama vielelezo lakini visiwe SHERIA.

Kwa kukusaidia msikilize Yesu ili ukiulizwa na mtu mambo ya sheria za Biblia usijeleta mambo ya Zaburi au mathayo au ufunuo,

Marko 10:17
Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?

Marko 10:18
Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.

Marko 10:19
Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako.

Unafikiri Kwa nini Yesu hakumnukuu Isaya, au Yona, au Hagai au Daudi, ni Kwa sababu kwenye maandiko unanukuu Aya kulingana na mtu anapouliza, Aya za sheria atamnukuu Musa, kama alivyofanya usizini, usione, usije n.k.

Aya za unabii atamnukuu Isaya, kina Daniel n.k. ndio maana kuna wakati alikuwa akisoma Chuo cha Nabii Isaya kuelezea mambo ya kinabii.

Sasa Wakristo wengi Kwa ujinga wa kutokujua neno la Mungu ndio maana wanashindwa kuelewa mambo madogo Kama hayo.

Ukishaambiwa ishu ya sheria lazima uende kwenye Torati.
Ukishaambiwa ishu ya Neema lazima uguse Injili
Sasa wapi pagumu,
 
"Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe" - Mathayo 19:6

Swali: Mungu huwa anashuka saa ngapi kuwatenganisha watu hawa
Hili ni swali zuri sana. Utengano unatokea pale ambapo mmoja katika ndoa anaamua kuwa na mwingine bila kuwa na dhamira ya kujirekebisha.

Umelihusisha hili andiko na tamaduni za wayahudi ukimaanisha halifanyi kazi kwa kanisa?

Andiko limezungumzia mke na kwa context ya kanisa tunafahamu mke ni yule ambaye mmeshaunganishwa katika uwepo wa Mungu.
 
Uliiacha ngano siku nyingi sana na sasa hivi hata magugu nayo unayaacha unaelekea babeli.🤣
 
1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng’ambo ya Yordani.
2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
-----------
Hapa tunaona swali la mtego. Na swali liko wazi, ni halali kumwacha mke kwa kila sababu?

4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
-----------
Majibu ya Yesu kwa hili swali yako wazi kabisa. Mungu aliumba mume na mke (kwa hiyo ushoga na usagaji hauwezi kuwa ndoa). Tena akasema wakiisha kuoana sio wawili bali mwili mmoja. Na anamalizia na kusema alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Yesu anaweka nukta, kamaliza kujibu swali lao kwa ukamilifu.

7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
-----------
Kwa sababu lengo ilikuwa kumtega, wanataka kumgombanisha na Musa ili watu wamwone mzushi. Maana watu walijua Musa ni nabii, na walikuwa wakimfuata Yesu kama mtu aliyetumwa na Mungu. Kwa hiyo kimsingi wanamhoji, kama wewe unatoka kwa Mungu na unasema hakuna talaka, basi mbona Musa, amabaye kila mtu anajua ni nabii akaturuamuru kutoa talaka? Huoni kama unapingana na Musa? Kumbuka lengo ni kumtega na sio kwamba hawajaelewa jibu!

8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
------------
Anawajibu kuwa design ya Mungu ya ndoa ni maisha. Musa aliwapa ruhusa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Yesu essentially anawashtaki hawa watu kwa Musa. Kwa wanaojua Biblia wanajua wana wa Israeli wana historia ya shingo ngumu. Walimtia presha Haruni mpaka akatengeneza mungu ndama wakati Musa kachelewa kurudi wakijua amekufa. Walifanya Musa akakosea mara kadhaa na mara ya mwisho ikamkosti kutoiingia Kanaani. Yesu kimsingi anawaambia "Wakaidi ninyi, mlisababisha Musa kuwapa hii amri kwa sababu mlikuwa jeuri, ila mpango wa Mungu sio huo".
Hawakubisha kwenye hili, Na ndipo unakuja mstari ambao kwa maoni yangu umetumika vibaya kuhalalisha iliyo haramu!
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
-------------
Biblia iko wazi kwanza kinachoongelewa hapa ni Uasherati ndio sababu ya kutenganishwa na sio uzinzi. Lakini pili itabidi uamini Yesu anajichanganya hapa maana keshasema mstari wa 4-6 kuwa ndoa ni maisha. Mungu hajichanganyi wala hajipingi. Wengine hukimbilia kusema maandiko ya asili ya Kiyunani yanasema blah blah. Wakasome Biography za Translators wa KJV halafu wajipime kama wanadhani wanajua Neno sahihi lilikuwa Uzinzi na sio uasherati. Kimsingi hapa at best hapako clear na at worst hapahusiani na wanandoa waliooana.
Kupotezea maandiko ambayo yako wazi na kujificha kwenye kichaka cha neno moja ni hatari sana kwa Mkristo!
10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
--------------
Huu ni mstari ambao huwa hatuutafakari. Kama mke au mume akifumaniwa anapewa talaka inaishia hapo kwa nini wanafunzi wake wakasema hivi? Huu mstari unaleta maana tu kama Yesu alimaanisha hata ukifumania ni wako huyo. Vinginevyo mtu anisaidie kwa nini waseme hivi na ninaweza kuacha na kuopoa mwingine?
Kwa hiyo kwangu, maandiko haya na ukiongezea na 1 Wakorintho 7 ni definitive kwamba hakuna talaka katika Ukristo. Na Yeyote anayetoa talaka anakuwa anachukua nafasi ya Mungu ya kujaribu kutenganisha. Hii ni kufuru na ninaamini haitakiwi kufanyika!
 
Sasa yamekuwa magugu peke yake.

Robert, pata nafasi ujifunze ukristo kupitia mafundisho sahihi. Huo ni ushauri wangu kwako.

Ukristo wa wengi humu ni upagani.
Ukristo wowote unaopinga sheria za Mungu/Torati ni upagani, ushetani.

Ukristo ni Neema ya Mungu Kwa Wanadamu dhidi ya dhambi iliyotokana na kushindwa kutii sheria za Mungu.
Bila sheria hakuna Ukristo
Kwani sheria ndio huleta dhambi, na na dhambi ilishindwa na Kristo msalabani Kwa kutupa Neema.
Ila neema haiondoi sheria Bali ni Kama second chance Kwa Wadhambi
 
Kwasababu dini ya kweli ni moja tu ilokuja na muongozo wake kutoka kwa Muumba

Izo nyengine ni dini za watu ambazo zina mapungufu mengi mnoo

Atakaenipinga aje na facts
 
Hili ni swali zuri sana. Utengano unatokea pale ambapo mmoja katika ndoa anaamua kuwa na mwingine bila kuwa na dhamira ya kujirekebisha
Biblia imesema alichkiungamanisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. Maana yake ili talaka itokee Mungu ni lazima ndiye atenganishe na sio mtu. Huyo mwingine unayemuongelea ni mtu au Mungu? kama ni mtu bado andiko linasimama!

Umelihusisha hili andiko na tamaduni za wayahudi ukimaanisha halifanyi kazi kwa kanisa?
Namaanisha kuna vitu kuvielewa lazima muktadha wa tamaduni husika lilipoandikwa uwe considered.
Mfano kuelewa kwa nini Yesu anaitwa mwanakondoo wa Mungu lazima ujue utamaduni wa Kiyahudi ambao Mungu aliwaamuru kuuishi. Ukiamua kulitafsiri hilo andiko kiBongo bongo utachomoka na tangopori moja kali sana!

Andiko limezungumzia mke na kwa context ya kanisa tunafahamu mke ni yule ambaye mmeshaunganishwa katika uwepo wa Mungu.
Alikuwa anaongea na Wayahudi na sio Watanzania. Sasa ili uelewe hilo lazima uliangalie andiko kwa namna hiyo. Uelewa wa leo wa Mke ni tofauti sana na wakati Yesu anafundisha hili andiko. Usipolitambua hilo utapotea ndugu yangu.

Hizi ni kanuni za msingi za kutafsiri maandiko. Nakuwekea hapa link angalau uelewe ndoa ya Wayahudi ambao Yesu alikuwa anaongea nao ilikuwaje. Achana na zetu hizi unapotafsiri mstari kama huu

 
Umelielezea vizuri sana na hakika mtu ambaye yupo kwenye ndoa anapaswa kumsamehe mwenzi wake katika hali zote iwapo amekiri kosa, ameomba msamaha na amekusudia kubadilika.

Huo mstari wa kuachana hapo unatumika iwapo mtu ameamua kuacha ndoa yake na ameenda kupata talaka mahakamani na akaenda kuolewa na mwingine. Hapa sioni sababu kwanini huyu aliyekuwa mwaminifu awe katika kifungo.

Inanikumbusha lile andiko ambapo mtu ambaye yupo nje ya imani na akiamua kuondoka basi mtu wa Mungu anakuwa huru. Mtu akiamua deliberately kuacha ndoa yake na kuwa na mwingine huyo ameikana imani na kwasababu ameondoka basi yule mwaminifu anakuwa huru.
 
Ndio maana nikakuambia yeye anatuagiza kama Nani?
Paul, an apostle of Christ Jesus by the will of God Eph 1:1
Paul, an apostle of Jesus Christ by the will of God, according to the promise of life which is in Christ Jesus - 2Tim 1:1
Paul, a servant of Jesus Christ, called to be an apostle, separated unto the gospel of God Roma 1:1

Ana mamlaka kuliko "maoni" yako!
 
Vitu unavyoandika wewe humu ndani havihusiani na ukristo kwasababu hata maagizo ya Mungu kupitia Paulo unayakataa. Na mbaya zaidi hata maagizo ya Yesu unayaita ni maoni yake.

Sidhani kama unafahamu kuwa mkristo maana yake ni nini.
 
Ukristo wa wengi humu ni upagani.
Ukristo wowote unaopinga sheria za Mungu/Torati ni upagani, ushetani.
Basi Paulo ni mpagani namba moja. Nyuma yake mpagani naba mbili kwa post yako hii na mpagani mkuu ni Yesu aliyemtuma Paulo.

Waraka wa Wagalatia utakufaa sana, maana nawe umerogwa kama Wagalatia wa enzi zile!
 
Ndoa na sheria kipi kilianza?
 
Huo mstari wa kuachana hapo unatumika iwapo mtu ameamua kuacha ndoa yake na ameenda kupata talaka mahakamani na akaenda kuolewa na mwingine. Hapa sioni sababu kwanini huyu aliyekuwa mwaminifu awe katika kifungo.
Kanisani huwa vinafanyika vitu viwili. Moja inafungwa ndoa mbele za Mungu. Hii ni mpaka Mungu aitenganishe.
Baada ya hapo kuna mkataba wa kiserikali ili kuwatambua kama wanandoa.

Ndoa ni Mungu pekee ndiye anatenganisha. Mkataba wa serikali, ni serikali ndio inatenganisha!
Kwa hiyo Mahakama huwa haitangui ile ndoa iliyofungwa mbele ya Mungu bali mkataba wa ndoa mliosaini ili mtambulike na Jamhuri na kupata faida zote za wanandoa katika Jamhuri.

Hizi ni mamlaka mbili tofauti na zina jurisdiction tofauti na mahakama haikosei inapofanya mambo ambayo yapo katika jurisdiction yake!
 
Biblia imesema alichkiungamanisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. Maana yake ili talaka itokee Mungu ni lazima ndiye atenganishe na sio mtu. Huyo mwingine unayemuongelea ni mtu au Mungu? kama ni mtu bado andiko linasimama
Mtu akienda nje ya ndoa na akaamua kuishi na mwingine huyo ameiacha imani. Mstari unaohusika hapo ni huu:

1 Wakorintho 7:15 SRUV
Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…