Niache Nteseke
JF-Expert Member
- Apr 29, 2020
- 2,162
- 2,616
Heshima kwenu wakuu.
Naomba kuwasilisha tangazo lilitolewa na Wizara ya Afya Tanzania kuhusiana na hizi ajira 1650 zilizotangazwa wiki iliyopita, kuna thread nikiiweka inayosema kuwa Tangazo la kazi lililotolewa na Wizara ya Afya lina Mapungufu.
Mapungufu yaliyopo kwenye tangazo walilolitoa kwa waombaji wa hizo nafasi waliandika kuwa kuna nafasi za madereva (4).
Lakini kwenye maelezo ya vigezo husika kwa kada walizozitoa naona hawakuweka maelekezo kwa nafasi za kada ya udereva, ndio nikaweka hiyo thread hapo juu kuuliza kuhusu hilo suala lakini mpaka dakika hii naandika hii nyingine hakuna jibu lolote kutoka Wizara ya Afya Tanzania na bahati nzuri wapo huu Jamiiforums.
Nikasema niingie kwenye website ya Wizara kuangalia hizo nafasi kuona labda zimesahaulika kwenye tangazo, lakini nilipoangalia kwenye website ya Wizara katika kufanya usajili katika tovuti yao pia hawajaweka nafasi za madereva pia.
Swali ni kwamba, mpaka hili tangazo limeruhusiwa kutoka ina maana wahusika hawakuliona hili tatizo/pungufu...?
Lakini pia, wanaweza kuwa hawajaliona sawa labda kwa kujisahau ila pia baada ya kukumbushwa walipaswa kutoa maelezo juu ya huu mkanganyiko lakini mpaka dakika hii hakuna majibu yoyote kutoka Wizara ya Afya Tanzania.
Natumai Jamiiforums inasomwa na wengi wakiwemo viongozi wa serikali na pia kuna mambo mengine yaliletwa hapa jamvini dhidi ya serikali na mengi yalipatiwa ufumbuzi, hivyo basi ni Matumaini yangu hata hili pia litaweza kupatiwa ufumbuzi na watu wa Wizara kwa kuwa nao pia tupo nao humu Jamiiforums.
Natanguliza shukran zangu za dhati kwenu. Ahsante.
NAWASILISHA.
Naomba kuwasilisha tangazo lilitolewa na Wizara ya Afya Tanzania kuhusiana na hizi ajira 1650 zilizotangazwa wiki iliyopita, kuna thread nikiiweka inayosema kuwa Tangazo la kazi lililotolewa na Wizara ya Afya lina Mapungufu.
Mapungufu yaliyopo kwenye tangazo walilolitoa kwa waombaji wa hizo nafasi waliandika kuwa kuna nafasi za madereva (4).
Lakini kwenye maelezo ya vigezo husika kwa kada walizozitoa naona hawakuweka maelekezo kwa nafasi za kada ya udereva, ndio nikaweka hiyo thread hapo juu kuuliza kuhusu hilo suala lakini mpaka dakika hii naandika hii nyingine hakuna jibu lolote kutoka Wizara ya Afya Tanzania na bahati nzuri wapo huu Jamiiforums.
Nikasema niingie kwenye website ya Wizara kuangalia hizo nafasi kuona labda zimesahaulika kwenye tangazo, lakini nilipoangalia kwenye website ya Wizara katika kufanya usajili katika tovuti yao pia hawajaweka nafasi za madereva pia.
Swali ni kwamba, mpaka hili tangazo limeruhusiwa kutoka ina maana wahusika hawakuliona hili tatizo/pungufu...?
Lakini pia, wanaweza kuwa hawajaliona sawa labda kwa kujisahau ila pia baada ya kukumbushwa walipaswa kutoa maelezo juu ya huu mkanganyiko lakini mpaka dakika hii hakuna majibu yoyote kutoka Wizara ya Afya Tanzania.
Natumai Jamiiforums inasomwa na wengi wakiwemo viongozi wa serikali na pia kuna mambo mengine yaliletwa hapa jamvini dhidi ya serikali na mengi yalipatiwa ufumbuzi, hivyo basi ni Matumaini yangu hata hili pia litaweza kupatiwa ufumbuzi na watu wa Wizara kwa kuwa nao pia tupo nao humu Jamiiforums.
Natanguliza shukran zangu za dhati kwenu. Ahsante.
NAWASILISHA.