Kwenye suala la misitu Tanzania ndiyo tulitakiwa tuwasaidie UAE, sio wao watusaidie sisi

Kwenye suala la misitu Tanzania ndiyo tulitakiwa tuwasaidie UAE, sio wao watusaidie sisi

Baada ya Bandari kupewe Dp World na mjadala kuwa mzito sana kiasi cha kuacha mashaka pande zote.

Serikali mwaka huu ilisaini MoU na waarabu(UAE) kushirikiana nao kwenye misitu.

Juzi raisi aliinyooshea kidole TFS kuwa haifanyi vizuri, haileti tija. Je ushirikiano huu ni mwanzo wa mwisho wa TFS? Watashirikiana vipi kwenye mambo ya misitu? Kauli ya raisi ya karibuni ilikua inalenga hayo?

Mwisho kabisa tumekubali hatuwezi chochote ndio maana mwarabu aliye jangwani anakuja kukufanyia kazi za misitu?

View attachment 2663243
Kama naona kwa mbaaali Bendera ikipepea nusu mlingoti tena!
 
Ndugai tusamehe tuliokushambulia. Uliona mbali.
MIMI UVCCM
 
Hakuna la maana zaidi miti yetu na misitu yetu kuvunwa na waarabu.

Maana yake hii itakua their second mainland nakuhakikishia.
Nilipoona TFS wanasemwa juzi, nikajua tayari kimenuka. Kweli katika taasisi zote TFS ndio wabaya?
 
Ushirikiano kwenye misitu una shida gani? Hujui sasaivi nchi zinaingiza mapato kupitia uuzwaji wa hewa ya Carbon?

Kenya tu juzi kasaini mkataba na Saudi Arabia kuwauzia hewa ya Ukaa. Sasa sijui shida kwenu iko wapi?

Ndo mana kuna mdau anasemaga humu akili za kijamaa ni za kijinga sana.

Mmejaa ushamba tu. Mambo hamjui alafu mnakuwa judgemental!!
Wewe hakuna asiyejuaa kuwa huna ubongo
 
Ushirikiano kwenye misitu una shida gani? Hujui sasaivi nchi zinaingiza mapato kupitia uuzwaji wa hewa ya Carbon?

Kenya tu juzi kasaini mkataba na Saudi Arabia kuwauzia hewa ya Ukaa. Sasa sijui shida kwenu iko wapi?

Ndo mana kuna mdau anasemaga humu akili za kijamaa ni za kijinga sana.

Mmejaa ushamba tu. Mambo hamjui alafu mnakuwa judgemental!!
Ujamaa una husiana nini na mambo ya Carbon!!!
 
Mama...Mama sio shida.
Watunga sheria ndio shida, wanajiangalia wao.
Sheria ili ikamilike lazima raisi anasaini. Pia Kama uoikua hujui kabla ya muswa wa sheria kwenda bungeni huanzia kwanza kwenye baraza ambalo raisi ni mwenyekiti
 
Kama naona kwa mbaaali Bendera ikipepea nusu mlingoti tena!
Haya ni mambo nisiyoyapenda, sikubaliani na mambo mengi ya serikali lakini hiki unachosema hapana, sio uungwana
 
Mwezi February mwaka huu, Serikali ya Tanzania ilisaini hati ya makubaliano (MOU) na Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa ajili ya kutusaidia kuendeleza misitu yote nchini, inayosimamiwa na Wakala wa misitu (TFS). Yani waarabu wanaoishi Jangwani wanatusaidia kuendeleza misitu. Kwanini wasipande misitu kule kwao waondokane na Jangwa?

Nadhani kwenye suala la misitu sisi ndio tulitakiwa tuwasaidie waarabu sio wao watusaidie sisi. Sisi tuna misitu ya asili na misitu ya kupanda. Tuna mapori ya akiba na mapori tengefu. Tuna misitu ya mvua (Rain forest) misitu ya minene (tropical thick forest), na misitu hafifu (broadleaf forest). Yani kwa kifupi kuhusu misitu, mapori na masuala ya miti na utunzaji wake, hakuna wa kutuambia kitu. Tupo vizuri.

Waarabu wao ndio wanatakiwa waje wajifunze hapa kwetu kuhusu misitu. Na sisi ndio tunapaswa tuwasaidie ili waweze kuwa na misitu kule kwao au hata mapori ya akiba. Lakini eti wao ndio wanatusaidia sisi kuendeleza misitu? Yani watu wasio na msitu hata mmoja wana kipi cha kutusaidia sisi ambao tuna misitu na mapori kila wilaya? Hii ndio mara ya kwanza nasikia Mzaramo anataka kumfundisha Mmasai kuhusu ufugaji wa ngombe. Apaaa ndenga.!!
View attachment 2663245
Source: VPO | News
Kulikoni waarabu awamu hii, kuna nini majameni tuamke tunauzwa hivyo!
 
Baada ya Bandari kupewe Dp World na mjadala kuwa mzito sana kiasi cha kuacha mashaka pande zote.

Serikali mwaka huu ilisaini MoU na waarabu(UAE) kushirikiana nao kwenye misitu.

Juzi raisi aliinyooshea kidole TFS kuwa haifanyi vizuri, haileti tija. Je ushirikiano huu ni mwanzo wa mwisho wa TFS? Watashirikiana vipi kwenye mambo ya misitu? Kauli ya raisi ya karibuni ilikua inalenga hayo?

Mwisho kabisa tumekubali hatuwezi chochote ndio maana mwarabu aliye jangwani anakuja kukufanyia kazi za misitu?

View attachment 2663243
Hii ndiyo ile Dr. Slaa alisema ipo mikataba mingine ilisainiwa kipindi hicho sambamba na wa bandari. Maza anaupiga mwingi kweli
 
Mungu atawaondoa kwenye kiti wote wanaopanga kuiangamiza Tanganyika

Tanganyika haitauzwa kwa waarabu
 
Taratibu, wameanza na Ngorongoro, loliondo. Ile mikataba 17 Rais aliyoisani akiwa kwenye UAE ilihusu nini?
 
Sheria ili ikamilike lazima raisi anasaini. Pia Kama uoikua hujui kabla ya muswa wa sheria kwenda bungeni huanzia kwanza kwenye baraza ambalo raisi ni mwenyekiti
Unaonaje Bunge likikataa...
Mfano: Bunge lingekuwa na uwakilishi wa 50/50 na upande wa pili, wakaikatalia Serikali.
 
Hivi huu ni wa ngapi kati ya ile 37?
 
Hii ndiyo ile Dr. Slaa alisema ipo mikataba mingine ilisainiwa kipindi hicho sambamba na wa bandari. Maza anaupiga mwingi kweli
ujinga kipaji
Waarabu wanakuja sana siku hizi kusaini mikataba ya kununua hewa ya carbon
Kenya mwenyewe kawauzia Saudi juzi. Nyie endeleeni na ushamba wenu tu
Screenshot_20230620-160542_Chrome.jpg
 
Back
Top Bottom