LATRA yawataka wenye mabasi ya abiria kuanza kutumia tiketi za mtandao, watakaoshindwa kufanya hivyo kufutiwa leseni

Kwa hiyo unaililia Tanzania kwa sababu gani? Mbona huo ni utaratibu mzuri?
 
Tena tumechelewa ije sasa
TRA na wizara ya fedha wanazingua,ilitakiwa wapungeze Kodi kidogo % alafu malipo yeyote ya zaidi 20k tulipe kielekrotoniki,ili Mambo ya kutotoa risiti yafe kibudu.
 
Tahadhari yangu imelenga migomo ya wenye mabasi
Watakuwa wehu,yaaani hii itawasadia wao/wenye mabasi kunufaika San kwa kudhibiti nauli na mapato.... Hivi unajua juzi tu Xmas abiria walikuwa wanakatiwa tiketi da-mwza Hadi 65k Ila mwenye gar/basi anafungiwa hesabu ya 30/35.

Sawa Ni tulipe kwa kielekrotoniki [emoji3581], japo waanze na Safari za mbali au zile nauli Ni 15k+
 
Sasa mtu wa buchosa ndani ndani akitaka ticket na kwenye mambo ya kutumia mtandao yuko chini inakuwaje hapo

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
Atafundishwa polepole atajua, Mimi napenda tunavyosogea kidigital hata elimu ya watu wazima irudi, Kila mtu atajua kusoma ni kupata elimu ya kuelimika na siyo kupoteza muda na kwenda kupata joto madawati.
 
Unapomuongezea gharama mfanyabiashara, mfanyabiashara lazima aongeze bei au gharama kwa mteja ili asipate hasara. Kwa hiyo hapa tegemea bei za tiketi za mabasi kupanda juu. Sasa wanaopanda mabasi ni watu wa kipato gani? Watapunguza safari? Kama ni wafanyabiashara nao lazima na wao waongeze bei za bidhaa zao ili wasipate hasara. Mfano kama mtu analeta maindi kwa mabasi ya abiria lazima ayaongeze bei.
 
Kama kweli wanataka Mapato na Kuimarisha Udhibiti kwanini Tamko lao limetoka leo wakati Sikukuu zote Muhimu Kikalenda zimeshamalizika?
 
Wangeanza na pilot project kwanza kwa hawa abiria wa kilimanjaro wa hii december kwa kuanza kutoa matangazo kuanzia october sasa wao wanakurupuka ghafla huku mitaani kuna watu wenye akili mingi sana
 

Heeee jamani nyie [emoji28][emoji28]
 
Hahahaaa hii techology unayo ipigia kelele huwa na double standard maana kwenye mambo ya msingi sana na yenye tija huwa siwaoni mkisema twende na technology mf. Kupiga kura, kabadili katiba iendane na usasa nk huko hakuna technology.
 
Maskini serikali ya makanikia imeishiwa kiki , siku hizi kiki zinatafutwa mpaka viongozi kuchapa watu viboko , Sasa mara Latra , Mara Siro kaitisha mkutano na waandishi wa habari usio na kichwa wala miguu , mtakaa sana kiki zimekuwa adimu wapinzani hawapo .
 
Hahahaaa hii techology unayo ipigia kelele huwa na double standard maana kwenye mambo ya msingi sana na yenye tija huwa siwaoni mkisema twende na technology mf. Kupiga kura, kabadili katiba iendane na usasa nk huko hakuna technology.
akikujibu nistue
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…