Uchaguzi 2020 Lazaro Mambosasa ametoa tamko kwa wanaopanga kupinga matokeo ya Urais

Uchaguzi 2020 Lazaro Mambosasa ametoa tamko kwa wanaopanga kupinga matokeo ya Urais

Nikweli mkuu, ndio maana wameanza matamko kutisha watu, lkn watambue hii miaka mitano inayokuja nimiaka tofauti kabisa na mitano iliyopita.
Miaka itabaki kuwa miaka na hakuna kitakachobadilika, pigeni kelele mkimaliza maisha yaendelee..!
 
Hii nchi siyo mali yake wananchi wana haki ya kuandamana kwa mujibu wa katiba ya tanzania na wanahaki ya kukataa matokeo maana kama sheria inakataza kwenda mahakamani basi wananchi ndiyo wenye mamlaka ya kukataa matokeo na yeye kazi yake ni kuwalinda hao wananchi kukataa ni halali yao kama ilivyo kwa wanaunga mkono huo uchafuzi

Tunafuatilia Mienendo yenu. Madhara ya kuandamana yatakuwa makubwa kuliko madhara ya kutulia nyumbani.

Uchaguzi umeisha, Rais JPM aungwe mkono , siasa zimeshaisha. Mtatolewa kafara na hakuna Human Rights yoyote itakayoingilia mzozo, acheni hayo mambo.

Miongoni mwa hao mnaopanga nao kuandamana wapo watu wetu hivyo itakuwa ni rahisi sana kuwatia nguvuni kama wale vijana wa IT waliokuwa wanajaribu kuvuruga mifumo ya matokeo mwaka 2015 some of them were our members. So watch out !

Only to advise!
 
Huo wizi hauwezi kuachwa hivihivi hakuna atakayekubali wizi wa mchana na ushahidi upo hakuna kulala yeye atoe matamko tu lakini sisi wananchi ndiyo wenye mamlaka hatujatoa mamlaka kwa wizi wa hivo tangu tanzania izaliwe haijawahi kushuhudia wizi wa hivo ni aibu lazima tukatae wizi na hao wote walioshitiki kwenye wizi tutahakikisha wanatajana hadi aliyewatuma Nyerere alishasema tukiogopa tutatawaliwa na madikiteta basi tuone mwisho wake kama hizo silaha zitashinda nguvu ya umma. Kama wanafikiri wamekata internet VPN iko kila mahali

Tutakuita uje kuthibitisha wizi, ukishindwa kuthibitisha, utaijibu Jamuhuri kwa uchochezi
 
Leo nikiwa kwenye mataa hapa esso chuga,wamama wawili wako na rav 4 iliyochafuliwa na mabango ya ccm,walipita wanapuliza vuvuzela kushangilia ushindi wa chama cha mafisi hakuna hata RAIA mmoja aliekuwa anawasuport, watu wana hasira na ccm,kama nyie wamama mko huku jf basi njooni aibu iliyowapata mkane kama so kweli.
 
Tunafuatilia Mienendo yenu. Madhara ya kuandamana yatakuwa makubwa kuliko madhara ya kutulia nyumbani.

Uchaguzi umeisha, Rais JPM aungwe mkono , siasa zimeshaisha. Mtatolewa kafara na hakuna Human Rights yoyote itakayoingilia mzozo, acheni hayo mambo.

Miongoni mwa hao mnaopanga nao kuandamana wapo watu wetu hivyo itakuwa ni rahisi sana kuwatia nguvuni kama wale vijana wa IT waliokuwa wanajaribu kuvuruga mifumo ya matokeo mwaka 2015 some of them were our members. So watch out !

Only to advise!
Mkiua wananchi nchi nzima mtamuongoza nani? Msilazimishe hisia za watu.
 
Mambo sasa kumbuka.. ukivua hayo magwanda unakua Raia.

Pia una ndugu ambao sio polisi..
Ni vyema kuchunga kauli kama hizi ambazo hazihitajiki muda huu.
"Tumepata taarifa kwamba kuna vikundi vya watu wachache, wameamua kuanza na vikao vya siri wakihamasishana kwamba wasikubaliane na matokeo ambayo kimsingi ni maamuzi ya Wananchi wenyewe, yoyote anayelianzisha asijutie yale atakayokuatana nayo, Dar es Salaam siyo shamba la bibi, hatutowaacha waende zaidi ya mita kumi" Lazaro Mambosasa - Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Tanzania.



 
Huyu ni mpuuzi, maoni ya wananchi yamebakwa na kulawitiwa mchana kweupe hilo haoni.
Hizi kura za Rais zilizo pigwa kabla ya 28 jimbo la kawe.
IMG_20201030_195255.jpeg
 
Tundu alisema yeye kazi yake kashamaliza kazi yake sasa ni zamu ya wananchi kuandamana. Akaongeza pia ameshawasliana na bobu ili awasilishe malalamiko yenye ushahidi ICC

Haya maneno ya Tundu yanafikirisha sana.
Kwanini Tundu hakusema sisi wananchi pamoja na mimi Tundu mwenyewe tumeazimia kuandamana?
Kama kiongozi hakuweka mipango kuhusu hayo maandamano kwamba yanafanyikaje?
Nani anatakiwa kuorganise hayo maandamano?
Yanaanza lini? wapi? na yatafanyika kwa muda gani?
Kwanini Tundu anatamani sana tuingie kwenye vurugu?
Kwanini anatumia nguvu nyingi sana kutaka ICC?

Tundu ameanza kuwajua watanzania kidogo, ila bado anataka kuwatumia kwa maslahi yake binafsi ili aendelee kuichafua nchi.
Wananchi hawawezi kuandamana kwa kushurtishwa, wala kwa kumsaidia Tundu kutimiza malengo yake binafsi.
Wananchi huandamana pale wanapokua wameonewa na Hilo huwa hawaambiwi, hawakatiziki wala hawazuililiki

Watanzania tumeamua kwenda na John Pombe Magufuli!!!!!
Tundu, Maalim na magenge yao waheshimu maamuzi yetu
 
Mambo sasa angetulia kwanza.Tatizo kubwa la polis wetu kukurupuka..
 
Tundu alisema yeye kazi yake kashamaliza kazi yake sasa ni zamu ya wananchi kuandamana. Akaongeza pia ameshawasliana na bobu ili awasilishe malalamiko yenye ushahidi ICC

Haya maneno ya Tundu yanafikirisha sana.
Kwanini Tundu hakusema sisi wananchi wa Tanzania tunaandama?
Kama kiongozi hakuweka mipango kuhusu hayo maandamano kwamba yanafanyikaje?
Nani anatakiwa kuorganise hayo maandamano?
Yanaanza lini? wapi? na yatafanyika kwa muda gani?

Tundu ameanza kuwajua watanzania kidogo, ila bado anataka kuwatumia kwa maslahi yake binafsi ili aendelee kuichafua nchi.
Wananchi hawawezi kuandamana kwa kushurtishwa, wala kwa kumsaidia Tundu kutimiza malengo yake binafsi.
Wananchi huandamana pale wanapokua wameonewa na Hilo huwa hawaambiwi, hawakatiziki wala hawazuililiki

Watanzania tumeamua kwenda na John Pombe Magufuli Tundu, Maalim na magenge yao waheshimu maamuzi yetu

Dada haya maji marefu si saizi yako kabisa.

Wewe endelea kuburudika na VPN ya beberu tu.

Huyu mwizi tutapambana naye sisi. Tukimaliza hutahitaji VPN tena.
 
Hasa polisi wa JMT
Kama uzalendo kwa nchi na heshima kwa wakuu wa nchi,hawa jamaa nimewavulia kofia maana niliamini kwa jinsi wanavyosuswa na hao wakubwa wanaowasaidia kuwaweka madarakani na jinsi walivyo na maisha duni wasingelijitoa kuwapigania kipindi ichi cha uchaguzi ila jambo la kushangaza polisi wamejitoa sana kuhakikisha 'sisiemu' inashika nchi.
Polisi mnafeli wapi hao sisiemu wanawatumia kipindi kama ichi mwisho wa siku wakipata wanawaacha kwenye mataa,mnataabika mnaishi maisha magumu na kuaibika mtaani.
#PolisikaziYaAjabu!
 
Dada haya maji marefu si saizi yako kabisa.

Wewe endelea kuburudika na VPN ya beberu tu.

Huyu mwizi tutapambana naye sisi. Tukimaliza hutahitaji VPN tena.

Sawa kaka nyie pambaneni, ingieni mabarabarani, andamaneni bila kikomo ila chondechonde msitulazimishe na sisi wengine kuingia kwenye hizo fujo
 
Kama uzalendo kwa nchi na heshima kwa wakuu wa nchi,hawa jamaa nimewavulia kofia maana niliamini kwa jinsi wanavyosuswa na hao wakubwa wanaowasaidia kuwaweka madarakani na jinsi walivyo na maisha duni wasingelijitoa kuwapigania kipindi ichi cha uchaguzi ila jambo la kushangaza polisi wamejitoa sana kuhakikisha 'sisiemu' inashika nchi.
Polisi mnafeli wapi hao sisiemu wanawatumia kipindi kama ichi mwisho wa siku wakipata wanawaacha kwenye mataa,mnataabika mnaishi maisha magumu na kuaibika mtaani.
#PolisikaziYaAjabu!
Mjomba alipoona maji yanazidi unga polisi na wanajeshi waliongezewa mishahara ili wamlinde.
 
Mkiua wananchi nchi nzima mtamuongoza nani? Msilazimishe hisia za watu.

Maelekezo yapo straight kabisa. Uchaguzi umeshaisha. Tumetoa maoni yetu kipindi cha kampani ili kufanya maboresho. Kampeni zimeisha. Uchaguzi umeisha. Wananchi wamemchagua JPM , ni jukumu la kila raia kutoa ushirikiano kwa JPM kama Rais wetu.

Kwa yeyote Mtanzania anaejaribu maandamano kwa mitandao au kwa vikundi anakwenda kinyume na sheria za nchi, Jamhuri haitosita kutumia nguvu kwa maslaha mapana ya Taifa.

Vijana msirubunike, don’t trust anyone, hao mnaopanga nao wapo watu wetu, utashangaa familia yako haikuoni tena, acheni hayo mambo. Fanya kazi kwa bidii, soma kwa bidii, wapende wazazi wako , itoshe kusema hivo

Kama mnataka maandamano, hakikisha Mbowe, Lema, Tundu, yule Muha Wote wanakaa Front page nyie mkiwa nyuma ili Jamhuri ianze na hao walio mbele.

Tarehe 5 au Jumatatu tuta muapisha Rais. Tunaomba maisha yaendelee na amani itawale. Tumesikia shida zenu na tutatatua baadhi ya changamoto at the earliest.
 
Back
Top Bottom