Lazaro Nyalandu ataongea na Watanzania kesho kuelezea udhaifu wa Upinzani kupitia kipindi cha Clouds 360

Lazaro Nyalandu ataongea na Watanzania kesho kuelezea udhaifu wa Upinzani kupitia kipindi cha Clouds 360

Ndiyo maana naamini kuwa kati ya wanasiasa wenye hekima, Lowasa ni miongoni.

Aliondoka CCM, hakupoteza muda wake kuisimanga CCM. Alitoka CHADEMA, hakupoteza muda kuisema.

MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU, ATAMDHARAU MWANASIASA YEYOTE ANAYEJIFANYA KUANZA KUELEZA MADHAIFU YA CHAA CHAKE CHA MWANZO BAADA YA KUONDOKA AU KUONDOLEWA.
Lowasa Hakuisimanga ccm kivipi, we hukumbuki kipindi alipoingia chadema alisema ccm si baba yake wala mama yake?
 
Ni oora agekaa kimya kulinda heshima yake, lakini kubwabwaja ni ishara ya kuonyesha ni jinsi gai usaliti wake unamtesa! Msaliti i msaliti tu hata angejisafisha na kuchafua wengie kwa kiasi gani!
Ngoja aanike ukanjanja wa happo ufipani mpaka tujue nani aliyechonga vilevikaratasi na kuvisambaza eti kula
 
Ni kweli, hivyo ndio inavyotakiwa iwe, ila watanzania 80%+ ya wapiga kura hawachagui kwa kuangalia sera, bali ushabiki, rushwa, vitisho na mazoea. Ukisema mtu anasema amechaguliwa kwa sera zake, basi ujue ni porojo kama porojo nyingine. Mfano ule uchaguzi wa kihayawani uliopita, unaweza kusema ilikuwa ni kwa ajili ya sera? Na kwa bahati Precidence aliyetengeneza Magufuli ya kushinda uchaguzi kwa kuunajisi, itachukua muda kuondoka maana ccm imeshapoteza ushawishi kwa umma, na haiko tayari kuachia madaraka kidemokrasia.
Hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho.....kama wasitukabidhi tunachostahili tutakichukua kwa mikono yetu......
 
Kwa nini hayo madhaifu asingewaambia hao CHADEMA kabla ya kutoka huko ili kuwapa mbinu za kuwakabili wapinzani wao, mpaka asubir abadili Chama zen ayaanike hadharani?? Yatasaidia nini?

Asituchoshe!
Bwashee hata ukiwaambia hawasikii.Si unakumbuka Mzee Lowassa aliwaambia waache uanaharakati waingie kwenye siasa za hoja, agenda,sera,na kujiandaa kukamata dola,matokea yake aliambulua vitusi chungu nzima.
 
Maccm kumejaa wanafiki na waongo waliokubuhu Mkuu na bila Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi hawa wahuni wataendelea kuiyumbisha nchi yetu kwa miaka sana ijayo.
CCM linapokuja suala la wizi wanakua kitu kimoja, sijawahi kuona wezi wenye umoja kama hawa jamaa
 
MaCCM hawawezi mpa cheo mpaka wamdhalilishe. Pole yake Nyarandu.
Chadema ipo ameikuta na ameicha.
 
Amedai Chadema ni dhaifu sana!

20210501_204107.jpg
 
Hapo lazima atazungumzia swala la Ruzuku,

Hakuna jambo sensitive Chadema kama Uwenyekiti na Ruzuku,

Mengine yote zungumzia lakini sio hayo mawili.

Kaa nayo mbali kwa usalama wako.
 
Kabla ya kuongelea hayo atueleze kilichomtoa CCM na kuhamia Chadema.
Kilichomtoa ccm kwenda chadema alikisema alipokua anaenda chadema , wakati huu ni wakuongelea kilichomtoa chadema kwenda ccm.
 
Hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho.....kama wasitukabidhi tunachostahili tutakichukua kwa mikono yetu......

Sio kwa uoga huu boss. Kumbuka hapa kwetu bado watu wanaogopa njaa, utasikia mtu anasema mimi nijitokeze kisha nikipata tatizo nani atalisha familia yangu?
 
CCM linapokuja suala la wizi wanakua kitu kimoja, sijawahi kuona wezi wenye umoja kama hawa jamaa

Hofu yao kubwa ni kwamba wakichukua chama kingine, nusu ya waliokamata vyeo wataishia jela kwa jinsi walivyolipiga hili shamba la bibi. Pata picha Jenista Mhagama, Ndugai nk wako kwenye karandinga na manguo ya pink wanaenda kufanya usafi kwa Mkuu wa mkoa.
 
Aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya kati na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho mh Nyalandu kesho 3/5/2021 asubuhi atazungumza na taifa kupitia kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na runinga ya Clouds.

Wananchi wote mnaombwa kufuatilia ili muyselewe madhaifu ya upinzani na hasa Chadema na kwanini CCM itaendelea kutawala kwa miaka 50 ijayo.

Maswali na hoja zenu zitajibiwa na mwanasiasa huyu nguli na aliyetegemewa sana na Chadema.

Kazi Iendelee!
Angetulia tu Nyalandu,anajidhalilisha.
 
Ila CCM bhana, yale matusi yote kuwa yeye ni rojorojo kama wa Mombasa leo mnamsifia?
 
Amedai Chadema ni dhaifu sana!
Sawa wekeni uchaguzi wa haki msitumie dola muone udhaifu wao

Bahati nzuri hilo mnalifahamu ... yaani CCM mpo kama vile Mbwa anvyobweka akiwa kwao akitoka uraiani huko peke ake anaficha mkia tumboni unaufyata afu anajificha Nyuma ya dola chezea CDM chini ya kudume Mbowe [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Afu saivi wananchi tushawajua kwahiyo hamtupi taabu wangapi wameondoka CDM bado inadunda tu imara kama chuma
 
Nyarandu kamanda mtiifu wa CDM kaiacha Chadema,ama kweli,,siasa' si hasa",,,!
Umasahau kuwa kilichomuoandoa CCM ni wale Twiga, na sasa anaona anaweza kupata pumzi tena? Huyu jamaa alikimbia Iowa bila hata kumaliza shule kwa vile alikuwa na kesi ya FBI lakini akapata connection ya kuwa karibu na mama Anna Mkapa ambaye alimhifadhi kufuta kesi ile. Jamaa anajua sana kutumia opportunities!
 
Aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya kati na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho mh Nyalandu kesho 3/5/2021 asubuhi atazungumza na taifa kupitia kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na runinga ya Clouds.

Wananchi wote mnaombwa kufuatilia ili muyselewe madhaifu ya upinzani na hasa Chadema na kwanini CCM itaendelea kutawala kwa miaka 50 ijayo.

Maswali na hoja zenu zitajibiwa na mwanasiasa huyu nguli na aliyetegemewa sana na Chadema.

Kazi Iendelee!
Sema mi naona kama ni utoto unapoamua kuondoka kwenye mahusiano au kuvunja mahusiano/ndoa halafu unaenda kuzungumza mabaya ya yule uliekua nae kwenye mahusiano, kwa kifupi that is childish, unapoamua kuachana na mtu, achana na yote move, fungua kurasa mpya kwa sababu hata wewe una kasoro nyingi

Nyalandu angeonekana matured kama aneamua kukaa kimya, ameondoka chadema sioni kama ni busara kuzungumza siri au udhaifu wa chama badala yake angejikita kupambania chama chake kipya au labda na sisi tuamini kwamba alikua chadema kwa kazi maalumu na sasa anataka kuichafua

Upinzani wasipobadilika basi wana safari ndefu sana, hawa mamluki wanaotoka ccm hawapaswi hata kupokelewa chadema, sijui kwa nini chadema huwa wanajitoa akili kuwaamini hawa watu tena wanawapa na uongozi kabisa
 
Back
Top Bottom