Pamoja na kuwa hana sifa za Ustaa,Lakini kama Mwananchi Mwenyw exposure na MwanaJamii Mwenzetu ,Nimeona Gazeti la Mwananchi la leo Tarehe 19 Desemba,2015 Ukurasa wake wa 21 Upande wa kulia kabisa limetoka na habari "Dk Mwaka awachonganisha Mastaa Mitandaoni"
Nalilimukuu sasa "Mastaa Mbalimbali wamepigana vikumbo kwenye mtamdao wa Instagram na wengine kufikia kurushiana vijembe kisa mtabibu wa dawa za asili maarufu Dk Mwaka".
........
"Lemutuz Nation yeye alimpongeza daktari huyo aliyemuita ni Rafiki yake na kumuahidi hatamkimbia kipindi hiki cha matatizo kwani wananchi wengi leo wana kitendawili na maswali mengi na mtu pekee anayeweza kuyajibu ni yeye."
Hata hivyo muda mfupi baadae Mange Aliweka ujumbe ambao alidai kutumiwa na Le Mutuz ambao ulikuwa ukisema "Mange mimi ni Le Mutuz nakupigia please pokea i need to talk to you(Nahitaji kuzungumza na wewe),Mange bado nakupigia ,dada kadri unavyomshambulia Dk Mwaka ndivyo unavyozidi kunikosesha mkataba wangu,Mange naomba nisikilize japo mara moja ninatakiwa kusaini mkataba kuanzia kesho siwezi kwenda hata kumuona kwa haya Mashambulizi"
MY TAKE:
1:Hivi niliposema viongozi wetu ni taswira ya sisi wananchi tulivyo nilikosea? Le Mutuz ni member wa JF na kwa miaka mingi hapa tumekuwa tukijadili,tukikubaliana na kutokubaliana kuhusu mwenendo wa serikali ya Tanzania
Lakini leo anajadili kuhusu maslahi yake binafsi Vs Afya za Watanzania
Kwamba unamtetea mtu na kumlamba mtu miguu kwa maslahi yako kwa gharama ya afya za watanzania.Wakati huo huo unawashambulia na kuwatukanawana-JF wenye mtazamo tofauti na wewe.
2:Mara kadhaa hapa amekuwa mstari wa mbele kutukana watu asiokubaliana nao hapa jukwaa la Siasa kuhusu Social life yao lakini leo anaonekana kuwa mpiga magoti kubembeleza biashara inayowaumiza watanzania kwa Faida yake
Sasa kwa vile tunaamini mabadiliko huanza na sisi wenyewe,na kwa vile Le Mutuz ni member wa hapa kwa muda mrefu na amekuwa akijinasibu kama mzalendo mwenye exposure (Pamoja na kuwatukana watu hapa tangu 2006) ,Basi sasa aje asafishe credibility yake hapa hapa kwenye jukwaa la kisiasa
Kwa vile umri ni namba tu na haina uhusiano wowote na Uwezo Mkubwa wa Kufikiri,Natarajia na natambua uwezekano wa kuwepo kwa matusi ya kutosha kupitia yeye na washirika wenye kiwango kama chake n.k
Haijalishi !