Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

mkuu ni sawa sawa kumlinganisha didier drogba na didier kavumbagu. mwl nyerere alikuwa alikuwa wakimataifa na mpaka leo anaheshima kubwa sana ndani na nje ya nchi, mpaka mzee mugabe anaandika kitabu kumuhusu. ukisikiliza hotuba za mwl nyerere utaona jinsi alivyo kuwa na upeo mkubwa. sasa wanasahau mwl aliichukua nchi ilikuwa katika hali gani katika nyanja zote hata wataalam alikuwa nao wachache sana akafanya juhudi za kusomesha.

wakati anajaribu kuiweka nchi kwenye mstari kuna ibuka vita na uganda lakini bado mzee wa watu hakushindwa wala kukata tamaa na ikumbukwe alikuwa na maadui wengi wa ndani na nje.
Nilishauri mwanzo kabisa vijana wa miaka ya 90 wangekuwa wasomaji wangejifunza mengi kwenye huu uzi.

Hamna mtu anayemfananisha Nyerere na Mwinyi kila mtu katawala kivyake.

Unasema Nyerere alijaribu kuiweka nchi kwenye mstari vikaibuka vita vya Uganda siyo?

Nyerere kachukuwa nchi mwaka 1960 vita vya Uganda vimetokea mwaka 1978.

Hiyo miaka 18 alikuwa anafanyaje kwenye utawala wake?
 
Nilishauri mwanzo kabisa vijana wa miaka ya 90 wangekuwa wasomaji wangejifunza mengi kwenye huu uzi.

Hamna mtu anayemfananisha Nyerere na Mwinyi kila mtu katawala kivyake.

Unasema Nyerere alijaribu kuiweka nchi kwenye mstari vikaibuka vita vya Uganda siyo?

Nyerere kachukuwa nchi mwaka 1960 vita vya Uganda vimetokea mwaka 1978.

Hiyo miaka 18 alikuwa anafanyaje kwenye utawala wake?
kwahiyo miaka 18 unaona ni mingi sana. kumbuka anaachiwa nchi alikuwa hana wataalamu wakutosha mfano wahandisi madaktari hata upande wa kiusalama bado wataalam hakuwanao wakutosha.

na ujue waliokuwa wanamezea mate rasilimali za taifa hili walikuwa ni wengi ndani na nje ya nchi, ila mwl nyerere kwa hekima kubwa sana alihakikisha rasilimali ya taifa hili itawanufaisha wa tz na hakuwa na haraka nayo.
 
kwahiyo miaka 18 unaona ni mingi sana. kumbuka anaachiwa nchi alikuwa hana wataalamu wakutosha mfano wahandisi madaktari hata upande wa kiusalama bado wataalam hakuwanao wakutosha.

na ujue waliokuwa wanamezea mate rasilimali za taifa hili walikuwa ni wengi ndani na nje ya nchi, ila mwl nyerere kwa hekima kubwa sana alihakikisha rasilimali ya taifa hili itawanufaisha wa tz na hakuwa na haraka nayo.
Nyerere kapewa nchi na wakoloni nchi ipo vizuri.

Vita vya vya miezi minane ndiyo viliifanya Tanzania kuwa masikini?

Unajua kama Tanzania walilipwa?
 
Hao vijana wa wakati ule wanatoka maneo tofauti nadhani siyo vyema kuangalia majina yao na kuwajadili kama Waislam maana hata wanajeshi waliyota kumpindua Mwalimu Nyerere walikuwa na majina ya Kikristo lakini tuwajadili kama Watanzania siyo dini zao.

Takupa hiki kisa cha watekaji ndege kiduchu.

Baada ya maagano na ndugu, jamaa na marafiki, abiria walipanda katika ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania iliyokuwa na jina la Kilimanjaro, Boeing 737, kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, Ijumaa ya Februari 26, 1982, saa 11 jioni.Uwanja wa ndege wa Mwanza ulikuwa na sifa mbaya kwa sababu haukuwa na usalama kiasi kwamba baadhi ya marubani walikuwa wakiutaja kama ‘kituo cha basi.’Makundi yaliyokuwa uwanjani hapo yalikuwa ya kawaida kama ya siku zote kwa wasafiri wa kwenda Dar es Salaam. Wasafiri wengi walikuwa ni Wahindi, Waarabu na Waafrika wachache. Ingawa mambo yote yalionekana kuwa ya kawaida, jambo dogo liliifanya safari hiyo isiwe ya kawaida.

Ndege ya Kilimanjaro ilipaa angani kutoka uwanjani hapo saa 11.20 jioni ya siku hiyo kwa kile kilichotazamiwa kuwa ni safari ya dakika 90 - maili 500, kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam.Lakini ikageuka kuwa safari ya juma zima - maili 9,500 - na kwa wakati mwingi abiria wa ndege wakisafiri ‘chini ya mtutu wa bunduki’ kabla ya kuwasili Dar es Salaam.Dakika tano tu baada ya ndege kupaa angani, vijana wanne walisimama ghafla kwa wakati mmoja. Mmoja wao alijipenyeza ghafla katika chumba cha rubani, halafu akaelekeza ‘bastola’ yake kwenye kichwa cha mmoja wa marubani wa ndege hiyo, Kapteni Deo Mazula, na kumtaka awapeleke kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi.

Wakati huo huo, watekaji nyara wengine, huku wakipunga ‘bastola’ zilizotengenezwa kwa vigogo vya miti na ‘mabomu’ ya kutupwa kwa mkono, waliwatangazia abiria kuwa wao ni viongozi wa ‘Vijana wa Harakati za Mapinduzi Tanzania’ na kwamba shabaha yao ni “kuhakikisha kuwa Rais Julius Nyerere anajiuzulu.”Wakati hayo yakitokea, Rais wa Tanzania waliyemtaka ajiuzulu, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa Ikulu mjini Dar es Salaam akijiandaa kurudi nyumbani baada ya kupokea risala kutoka kwa Chipukizi nchini waliomwahidi kuwa “Tutaendelea kuwa watiifu, wakakamavu na wenye bidii kwa kuwa tunafahamu mchango wetu unahitajika sana katika ujenzi wa nchi.”

Mpaka wakati anaondoka kwenda nyumbani kwake, Msasani, akiwa amefurahishwa na risala aliyosomewa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chipukizi, Frank Uhahula (15) wa darasa la saba katika Sule ya Mingi ya Tumbi, Kibaha katika mkoa wa Pwani, Mwalimu Nyerere hakuwa amejua kilichotokea upande mwingine wa nchi -Mwanza.Watekaji nyara hao waliwaamuru abiria wote wakae kimya kwenye viti vyao na kufumba macho yao na, kwa sababu ambazo hazikujulikana lakini za kustaajabisha, waliwalazimisha watumishi kuzima viyoyozi vya ndege. Wakati hali ya hewa katika ndege hiyo ilipoanza kuwa nzito na kukaribia kutovumilika tena, ndege hiyo ilitua mjini Nairobi kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta.

Lakini katika kipindi cha dakika kadhaa baadaye, Rais Nyerere alipewa taarifa za kutekwa kwa ndege hiyo na kuambiwa kwamba tayari ilishatua Nairobi, Kenya. Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, John Samuel Malecela, ambaye aliteuliwa rasmi kushughulikia utekaji huo, alitumwa kwenda Nairobi kushughulikia tatizo hilo. Mwalimu Nyerere alitaka kuwa na hakika kwamba Serikali ya Kenya haingeruhusu ndege hiyo iondoke Nairobi.Wakati huo huo polisi wa Kenya wakifunga uwanja wa Ndege wa Kenyatta, na wanajeshi walisambazwa uwanjani hapo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Robert Ouko, alikuwa uwanjani hapo akitokea Addis Ababa, Ethiopia, wakati ndege ya Tanzania ilipotua.Alipopewa habari za yaliyotokea, Dk Ouko hakusita, alikwenda kwenye chumba cha kuongozea ndege kujaribu kushughulikia jambo hilo.

Hii habari ndefu nadhani tawachosha tunaendelea muda mwingine.
Nimeacha kwenda kulala kwa kusoma hii taarifa

sasa je nini kilichotokea bbada ya hapo?
Je hawa vijana walikuwa na uhusiano wowote na akina McGhee waliotaka kumpindua Juliasi au hizi zilikuwa 2 different incidents?
 
Kisiasa, Uongozi wa Mwinyi ulifanikiwa katika mambo makuu mawili; kufunguliwa kwa milango ya demokrasia na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Dhana ya demokrasia, japo haikutumika katika chaguzi za kipindi chake, lakini angalau miaka miwili kabla ya kuondoka madarakani nchi ilifungua mlango wa demokrasia ambapo siasa za vyama vingi zilianza wakati yeye akiwa madarakani.Kwa pamoja na Uhuru wa Vyombo vya habari, nchi ikajenga mazingira mapya kutoka yale ya utawala usiokosolewa kuja utawala uliokosolewa hadharani. Kwa mara ya kwanza ikashuhudiwa demokrasia ya Rais kuchorwa na kusemwa vibaya.

Vijana wa Chuo Kukuu cha Dar es Salaam wao walifikia hatua mbaya zaidi pale walipoifuja demokrasia hiyo kwa kuchora picha za matusi dhidi ya Rais Ali Hassan. Kama tutakavyoona katika kipengele cha elimu, Mwinyi alileta nafuu kubwa ya maisha ya Wanataaluma Chuoni hapo.

Japo wanataaluma walianza kuonesha mfano mbaya wa matumizi ya uhuru wa kujieleza ambao haukuwepo enzi za Nyerere lakini bado Mwinyi hakufunga mlango wa demokrasia.

Kwa mara kwanza tangu miaka ya 1960, Watanzania wakaanza kushuhudia majukwaa ya upinzani dhidi ya Chama tawala na serikali. Ukizungumzia mwanzo wa mageuzi ya kisiasa basi lazima utayakuta ndani ya kipindi cha Mwinyi.

Kama kuna eneo lililoung’arisha mapema utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi basi lilikuwa ni lile la Uchumi. Mwinyi aliaswa na wataalamu wa uchumi kuwa aachane kabisa na fikra zilizoshindwa na Mwalimu Nyerere kama alitaka kufanikiwa katika eneo hili.
Ahsante malim...kwa kuweka bayana kuhusu mafanikio ya mwinyi hasa kuhusu uhuru wa vyombo vya habari
 
Nimeacha kwenda kulala kwa kusoma hii taarifa

sasa je nini kilichotokea bbada ya hapo?
Je hawa vijana walikuwa na uhusiano wowote na akina McGhee waliotaka kumpindua Juliasi au hizi zilikuwa 2 different incidents?
Akizungumza kupitia katika redio ya ndege hiyo, mmoja wa watekaji wa ndege hiyo alijitambulisha kwa jina la Luteni Wami, ofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.Alisema kuwa ni lazima Rais Nyerere ajiuzulu vinginevyo ndege hiyo italipuliwa. Dk Ouko alijaribu kujadiliana na mtekaji huyo, lakini alijibiwa: “Tayari nimeshaua abiria watatu na nitaendelea kuwaua wengine zaidi.”

Dk Ouko alistushwa na kauli hiyo. Ilimbidi amsihi mtekaji huyo akimwambia, “Usiendelee kuua zaidi.” Lakini ukweli wa mambo ni kwamba hakuna mauaji yoyote yaliyokuwa yametokea mpaka wakati huo.Kupitia mawasiliano yao ya redio ya upepo, mtekaji huyo alimwambia Waziri Ouko hivi: “Sasa namuua huyu rubani.” Rubani mwingine aliyekuwa akisaidiana na Kepteni Deo Mazula ni Oscar Mwamwaja (kuna vyombo vingine vya habari vya Ulaya vilimtaja kwa jina la Mwangala Jotham).

Lakini Dk Ouko akamjibu kwa kumwambia kuwa huo utakuwa ujinga kwa sababu “…rubani huyo atahitajika kuirusha ndege hiyo kwenda kwingineko.” Mtekaji huyo akajibu: “N’naweza kuendesha ndege hii mwenyewe. Mimi ni luteni wa anga.”Watekaji hao walitaka ndege hiyo ijazwe mafuta kwa ajili ya safari ya kwenda Saudi Arabia. Akiwa hana lingine la kufanya, Waziri Ouko alikubaliana na matakwa hayo.Wakati huo huo katika mji wa Dar es Salaam, kumbukumbu za kijeshi zilianza kuchunguzwa kutafuta jina la Luteni Wami. Jina hilo halikupatikana popote. Wala hakukuwa na cheo chochote cha uluteni wa anga katika jeshi la Tanzania.

Nikipata wasaa takumalizia...
 
sio sukari na mchele tu mpaka dawa ya mbu ilikuwa hanasa ele dawa ya mbu ya coil ulikuwa unaikata vipande vipande na kuiuza kwa wale unaowafahamu ole wako mgambo au Jkt wa kipindi hicho wakukamate utaomba ardhi ipasuke ili uingie mzima mzima kwa jinsi utakavyopata mkong'oto wa kufa mtu
Hahaaaaaaahaaaaa..mkuu unanchekesha sana..ingawa ilikuwa hali ngumu kipindi hiko
 
Ahsante malim...kwa kuweka bayana kuhusu mafanikio ya mwinyi hasa kuhusu uhuru wa vyombo vya habari
Inaposemwa mfumo wa vyama vingi ulirudi tena mwaka 1992, huenda vijana wadogo wanashindwa kuelewa. Ni kwamba Vyama vingi vilikuwepo hadi mwanzoni mwa miaka ya uhuru lakini Serikali ya Nyerere ikavifutilia mbali.

Serikali ya Mwinyi ndiyo iliyorudisha tena mfumo huo hata kama ni kwa shinikizo la Mataifa ya Magharibi. Karibu vyama vyote vikubwa vya Siasa vya Upinzani vilianza shughuli zao katika kipindi cha Mwinyi.

Mwinyi aliondoka madarakani mwaka 1995, miaka mitatu baada ya Mfumo wa Vyama vingi kuanza. Alikuwa ni baba wa mageuzi ya kisiasa, na baba wa Uhuru wa Vyombo vya habari.
 
Wengine wazazi wetu walifungwa kwa kudhaniwa kuhujumu uchumi eti wamekutwa na vyakula kutoka nje ya nchi!
Bro...kuna mzee mmoja nilikutana nae kule njombe ndani kuna kijiji.kinaitwa kidugala yeye alisema alikuwa tajiri sana nyakati hizo ilipofika suala la uhujumu uchumi lilimuathiri sana kwani ilimlazimu kuendesha matrekta na gari lake kwwnda kuyatupa mashambani ukiachilia kuwa alivimiliki kihalali nchi hii imetoka mbali
 
Hahaaaaaaahaaaaa..mkuu unanchekesha sana..ingawa ilikuwa hali ngumu kipindi hiko
Unakumbuka hii kitu.

IMG_55621849287152.jpeg

Na hii hapa! Hahahahaha
IMG_56189663508464.jpeg
 
Nimeacha kwenda kulala kwa kusoma hii taarifa

sasa je nini kilichotokea bbada ya hapo?
Je hawa vijana walikuwa na uhusiano wowote na akina McGhee waliotaka kumpindua Juliasi au hizi zilikuwa 2 different incidents?
Two different incidents.
 
Anafanya vema sana kwenye afya yake (angalau kwa muonekano wa nje)! Namuona akigonga miaka 100 kirahisi kabisa akiwa bado anatembea bila msaada wowote! Analo la kutufunza ni kwa vipi ameweza kutunza afya yake kwa kiasi hicho (pamoja na kuwa bigamist?)
Braza...hapo kuna kitu mzee inabidi atufundishe inshallah..sasa tatizo.waandishi wa habari hawana la msingi la kumhoji huyu mzee zaidi ya kuuuliza kwa nini unaitwa mzee ruksa...mwaka jana huyu mzee tumetembea naye kilometa nyingi kwwny matembezi ya hisani yaliyoandaliwa na rotary yaan ana nguvu kubwa ametembea kwa spidi ile ile km nyingi sana...vijana wanakula chips walichemka wakati miaka yao ni kuzaliwa 95.
 
Kabla ya Mzee watu wali choka vijana walifanya majaribio mara 2 ya kuteka ndege ya ATC na mara moja walifanikiwa kuipeleka UK...na kudai Serikali iondoke imeshindwa..ilikua moja ya aibu kuu kwa Mwalimu. Kwani habari ile na ya mateka wale ilitangazwa dunia nzima na wote wali sypathisize na watekaji...kwani hali ilikua mbaya TZ..
Mkuu tafadhali iongezee nyama hio habari nipate kuifahamu vizuri..
 
Kuruhusu kitimoto kuuzwa hadi karibu na misikitiki bila ya kubagua imani za watu
 
Ritz, naona na wewe umeamua kuandika historia mpya ya Tanzania baada ya uhuru kama yule kakayo naye alipoamua kuandika historia mpya ya Tanganyika kabla ya uhuru ha ha haa? Yeye anadai pororjo anazoandika alisimuliwa barazani na wazee wake wa Gerezani, je wewe nani alikusimulia hizi porojo unazowapa vijana?

Kama kawaida naona vijana wako nao badala ya barazani wamehamia JF kusikiliza porojo zako wanameza tu bila kuhoji. Nakutakia kila la kheri kwani hata humu limbukeni wapo kibao wamejaa tele.
 
Hao vijana wa wakati ule wanatoka maneo tofauti nadhani siyo vyema kuangalia majina yao na kuwajadili kama Waislam maana hata wanajeshi waliyota kumpindua Mwalimu Nyerere walikuwa na majina ya Kikristo lakini tuwajadili kama Watanzania siyo dini zao.

Takupa hiki kisa cha watekaji ndege kiduchu.

Baada ya maagano na ndugu, jamaa na marafiki, abiria walipanda katika ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania iliyokuwa na jina la Kilimanjaro, Boeing 737, kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, Ijumaa ya Februari 26, 1982, saa 11 jioni.Uwanja wa ndege wa Mwanza ulikuwa na sifa mbaya kwa sababu haukuwa na usalama kiasi kwamba baadhi ya marubani walikuwa wakiutaja kama ‘kituo cha basi.’Makundi yaliyokuwa uwanjani hapo yalikuwa ya kawaida kama ya siku zote kwa wasafiri wa kwenda Dar es Salaam. Wasafiri wengi walikuwa ni Wahindi, Waarabu na Waafrika wachache. Ingawa mambo yote yalionekana kuwa ya kawaida, jambo dogo liliifanya safari hiyo isiwe ya kawaida.

Ndege ya Kilimanjaro ilipaa angani kutoka uwanjani hapo saa 11.20 jioni ya siku hiyo kwa kile kilichotazamiwa kuwa ni safari ya dakika 90 - maili 500, kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam.Lakini ikageuka kuwa safari ya juma zima - maili 9,500 - na kwa wakati mwingi abiria wa ndege wakisafiri ‘chini ya mtutu wa bunduki’ kabla ya kuwasili Dar es Salaam.Dakika tano tu baada ya ndege kupaa angani, vijana wanne walisimama ghafla kwa wakati mmoja. Mmoja wao alijipenyeza ghafla katika chumba cha rubani, halafu akaelekeza ‘bastola’ yake kwenye kichwa cha mmoja wa marubani wa ndege hiyo, Kapteni Deo Mazula, na kumtaka awapeleke kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi.

Wakati huo huo, watekaji nyara wengine, huku wakipunga ‘bastola’ zilizotengenezwa kwa vigogo vya miti na ‘mabomu’ ya kutupwa kwa mkono, waliwatangazia abiria kuwa wao ni viongozi wa ‘Vijana wa Harakati za Mapinduzi Tanzania’ na kwamba shabaha yao ni “kuhakikisha kuwa Rais Julius Nyerere anajiuzulu.”Wakati hayo yakitokea, Rais wa Tanzania waliyemtaka ajiuzulu, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa Ikulu mjini Dar es Salaam akijiandaa kurudi nyumbani baada ya kupokea risala kutoka kwa Chipukizi nchini waliomwahidi kuwa “Tutaendelea kuwa watiifu, wakakamavu na wenye bidii kwa kuwa tunafahamu mchango wetu unahitajika sana katika ujenzi wa nchi.”

Mpaka wakati anaondoka kwenda nyumbani kwake, Msasani, akiwa amefurahishwa na risala aliyosomewa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chipukizi, Frank Uhahula (15) wa darasa la saba katika Sule ya Mingi ya Tumbi, Kibaha katika mkoa wa Pwani, Mwalimu Nyerere hakuwa amejua kilichotokea upande mwingine wa nchi -Mwanza.Watekaji nyara hao waliwaamuru abiria wote wakae kimya kwenye viti vyao na kufumba macho yao na, kwa sababu ambazo hazikujulikana lakini za kustaajabisha, waliwalazimisha watumishi kuzima viyoyozi vya ndege. Wakati hali ya hewa katika ndege hiyo ilipoanza kuwa nzito na kukaribia kutovumilika tena, ndege hiyo ilitua mjini Nairobi kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta.

Lakini katika kipindi cha dakika kadhaa baadaye, Rais Nyerere alipewa taarifa za kutekwa kwa ndege hiyo na kuambiwa kwamba tayari ilishatua Nairobi, Kenya. Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, John Samuel Malecela, ambaye aliteuliwa rasmi kushughulikia utekaji huo, alitumwa kwenda Nairobi kushughulikia tatizo hilo. Mwalimu Nyerere alitaka kuwa na hakika kwamba Serikali ya Kenya haingeruhusu ndege hiyo iondoke Nairobi.Wakati huo huo polisi wa Kenya wakifunga uwanja wa Ndege wa Kenyatta, na wanajeshi walisambazwa uwanjani hapo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Robert Ouko, alikuwa uwanjani hapo akitokea Addis Ababa, Ethiopia, wakati ndege ya Tanzania ilipotua.Alipopewa habari za yaliyotokea, Dk Ouko hakusita, alikwenda kwenye chumba cha kuongozea ndege kujaribu kushughulikia jambo hilo.

Hii habari ndefu nadhani tawachosha tunaendelea muda mwingine.
Mkuu tafadhari endelea
 
Hao vijana wa wakati ule wanatoka maneo tofauti nadhani siyo vyema kuangalia majina yao na kuwajadili kama Waislam maana hata wanajeshi waliyota kumpindua Mwalimu Nyerere walikuwa na majina ya Kikristo lakini tuwajadili kama Watanzania siyo dini zao.

Takupa hiki kisa cha watekaji ndege kiduchu.

Baada ya maagano na ndugu, jamaa na marafiki, abiria walipanda katika ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania iliyokuwa na jina la Kilimanjaro, Boeing 737, kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, Ijumaa ya Februari 26, 1982, saa 11 jioni.Uwanja wa ndege wa Mwanza ulikuwa na sifa mbaya kwa sababu haukuwa na usalama kiasi kwamba baadhi ya marubani walikuwa wakiutaja kama ‘kituo cha basi.’Makundi yaliyokuwa uwanjani hapo yalikuwa ya kawaida kama ya siku zote kwa wasafiri wa kwenda Dar es Salaam. Wasafiri wengi walikuwa ni Wahindi, Waarabu na Waafrika wachache. Ingawa mambo yote yalionekana kuwa ya kawaida, jambo dogo liliifanya safari hiyo isiwe ya kawaida.

Ndege ya Kilimanjaro ilipaa angani kutoka uwanjani hapo saa 11.20 jioni ya siku hiyo kwa kile kilichotazamiwa kuwa ni safari ya dakika 90 - maili 500, kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam.Lakini ikageuka kuwa safari ya juma zima - maili 9,500 - na kwa wakati mwingi abiria wa ndege wakisafiri ‘chini ya mtutu wa bunduki’ kabla ya kuwasili Dar es Salaam.Dakika tano tu baada ya ndege kupaa angani, vijana wanne walisimama ghafla kwa wakati mmoja. Mmoja wao alijipenyeza ghafla katika chumba cha rubani, halafu akaelekeza ‘bastola’ yake kwenye kichwa cha mmoja wa marubani wa ndege hiyo, Kapteni Deo Mazula, na kumtaka awapeleke kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi.

Wakati huo huo, watekaji nyara wengine, huku wakipunga ‘bastola’ zilizotengenezwa kwa vigogo vya miti na ‘mabomu’ ya kutupwa kwa mkono, waliwatangazia abiria kuwa wao ni viongozi wa ‘Vijana wa Harakati za Mapinduzi Tanzania’ na kwamba shabaha yao ni “kuhakikisha kuwa Rais Julius Nyerere anajiuzulu.”Wakati hayo yakitokea, Rais wa Tanzania waliyemtaka ajiuzulu, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa Ikulu mjini Dar es Salaam akijiandaa kurudi nyumbani baada ya kupokea risala kutoka kwa Chipukizi nchini waliomwahidi kuwa “Tutaendelea kuwa watiifu, wakakamavu na wenye bidii kwa kuwa tunafahamu mchango wetu unahitajika sana katika ujenzi wa nchi.”

Mpaka wakati anaondoka kwenda nyumbani kwake, Msasani, akiwa amefurahishwa na risala aliyosomewa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chipukizi, Frank Uhahula (15) wa darasa la saba katika Sule ya Mingi ya Tumbi, Kibaha katika mkoa wa Pwani, Mwalimu Nyerere hakuwa amejua kilichotokea upande mwingine wa nchi -Mwanza.Watekaji nyara hao waliwaamuru abiria wote wakae kimya kwenye viti vyao na kufumba macho yao na, kwa sababu ambazo hazikujulikana lakini za kustaajabisha, waliwalazimisha watumishi kuzima viyoyozi vya ndege. Wakati hali ya hewa katika ndege hiyo ilipoanza kuwa nzito na kukaribia kutovumilika tena, ndege hiyo ilitua mjini Nairobi kwenye Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta.

Lakini katika kipindi cha dakika kadhaa baadaye, Rais Nyerere alipewa taarifa za kutekwa kwa ndege hiyo na kuambiwa kwamba tayari ilishatua Nairobi, Kenya. Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, John Samuel Malecela, ambaye aliteuliwa rasmi kushughulikia utekaji huo, alitumwa kwenda Nairobi kushughulikia tatizo hilo. Mwalimu Nyerere alitaka kuwa na hakika kwamba Serikali ya Kenya haingeruhusu ndege hiyo iondoke Nairobi.Wakati huo huo polisi wa Kenya wakifunga uwanja wa Ndege wa Kenyatta, na wanajeshi walisambazwa uwanjani hapo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Robert Ouko, alikuwa uwanjani hapo akitokea Addis Ababa, Ethiopia, wakati ndege ya Tanzania ilipotua.Alipopewa habari za yaliyotokea, Dk Ouko hakusita, alikwenda kwenye chumba cha kuongozea ndege kujaribu kushughulikia jambo hilo.

Hii habari ndefu nadhani tawachosha tunaendelea muda mwingine.

Baki na hadithi yako ya kwenye gazeti la RAI miaka hio.
 
Kisiasa, Uongozi wa Mwinyi ulifanikiwa katika mambo makuu mawili; kufunguliwa kwa milango ya demokrasia na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Dhana ya demokrasia, japo haikutumika katika chaguzi za kipindi chake, lakini angalau miaka miwili kabla ya kuondoka madarakani nchi ilifungua mlango wa demokrasia ambapo siasa za vyama vingi zilianza wakati yeye akiwa madarakani.Kwa pamoja na Uhuru wa Vyombo vya habari, nchi ikajenga mazingira mapya kutoka yale ya utawala usiokosolewa kuja utawala uliokosolewa hadharani. Kwa mara ya kwanza ikashuhudiwa demokrasia ya Rais kuchorwa na kusemwa vibaya.

Vijana wa Chuo Kukuu cha Dar es Salaam wao walifikia hatua mbaya zaidi pale walipoifuja demokrasia hiyo kwa kuchora picha za matusi dhidi ya Rais Ali Hassan. Kama tutakavyoona katika kipengele cha elimu, Mwinyi alileta nafuu kubwa ya maisha ya Wanataaluma Chuoni hapo.

Japo wanataaluma walianza kuonesha mfano mbaya wa matumizi ya uhuru wa kujieleza ambao haukuwepo enzi za Nyerere lakini bado Mwinyi hakufunga mlango wa demokrasia.

Kwa mara kwanza tangu miaka ya 1960, Watanzania wakaanza kushuhudia majukwaa ya upinzani dhidi ya Chama tawala na serikali. Ukizungumzia mwanzo wa mageuzi ya kisiasa basi lazima utayakuta ndani ya kipindi cha Mwinyi.

Kama kuna eneo lililoung’arisha mapema utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi basi lilikuwa ni lile la Uchumi. Mwinyi aliaswa na wataalamu wa uchumi kuwa aachane kabisa na fikra zilizoshindwa na Mwalimu Nyerere kama alitaka kufanikiwa katika eneo hili.


Unafiki ni nguzo kuu ya kuwa mwanachama wa CCM.

Je, hayo yote uliyoyataja kwa kumsifia Mzee Ruksa ambayo yanaenziwa na kupiganiwa na wanasisiemu wa leo wanaotamani kumtafuna yeyote anayeikosoa serikali?

Yote uliyoyataja ni ya kweli na ndiyo msingi wa utu na maisha bora kwa kila binadam lakini awamu hii ya tano inayaacha kwa kasi ya ajabu .
 
Back
Top Bottom