Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Mtazamo wako na ulicho kiandika humu kimekuonyesha jinsi ulivyo.
Mm nakushauri tu watu wanapo jadili jambo ww uwe msikilizaji au msomaji tu.
Kwa aina ya uchangiaji huu na muandiko huu watu wanaweza kujua amendika kadada ka kazi kaliko ishia std 3.


Wewe sema kipi si cha kweli? Au unafiki nao ni ibada kwenu?
 
Sipendi kumlaumu Mzee Mwinyi eti kwa sababu ya mengi ya madhara ya rukhsa. Tukumbuke kuwa kipindi cha uongozi wa Mzee Mwinyi tulikuwa tunatoka kwenye itikadi za kijamaa na tunahamia kwenye zile za kibepari, tena kutokana na shinikizo la matajiri.

Kilikuwa ni kipindi very tricky kwa yoyote yule ambaye angekuwa amepewa nafasi ya Mzee Mwinyi, naamini hata Salim Ahmed Salim au mwingine yoyote yule angekumbana na changamoto zilizomkuta Mzee Mwinyi.

Russia ilijikuta ikiongozwa na hisia pamoja na ushawishi wa mabilionea kwa sababu tu katika kipindi cha mpito kutoka ujamaa kuelekea ubepari, waliweza kuibuka warusi wachache wakatumia fursa zilizojitokeza kwa faida yao na ndugu zao.

Mzee Mwinyi alilazimika kufungua fursa za uwekezaji kwa sababu ya uhalisia wa umasikini wa nchi kwa wakati ule.

Na tukumbuke kuwa ubepari wa Marekani na mataifa mengine makubwa wakati unaanza kuota mizizi, na wao pia walikuwa katika kipindi cha kufanya makosa mengi kabla ya kuja kukomaa na kuzielewa vizuri namna mbalimbali za kuendesha ubepari kwa faida ya jamii pana.

Mzee Mwinyi ni binadamu mwenye upungufu wake lakini tuutazame na uhalisia wa wakati ule.
 
Wewe sema kipi si cha kweli? Au unafiki nao ni ibada kwenu?
Niambie kuanzia 1985 mpaka 1995 shule gani inayomilikiwa na kanisa ilichomwa moto na waislam na watoto wa shule hiyo walikufa wangapi?
Mm najua najadiliana na mtu wa aina gani na nilikupa ishauri lakini hujataka kuufata.
Jibu hilo kwanza ili usiwe ww mnafik..
 
Fagio la Chuma aliloanza nalo Mwinyi lilitokana na ukweli huo kuwa alikuta ubadhirifu umeshamiri wakati Nyerere akipiga siasa na kusifiwa kinafiki!.

Nakala; Mag3 JokaKuu
FaizaFoxy

..kuna wachangiaji wanataka zoezi la kukamata wahujumu uchumi la miaka ile lianze upya na kipindi cha redio cha mikingamo kirudi.

..Mwinyi alikuta nchi imegubikwa na matatizo ya uchumi. Alichofanya yeye ni kuchukua hatua za kiuchumi kumaliza matatizo yale.
 
Kutokana na hali ya kisiasa ilivyokuwa ikiendelea tangu kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika, kuna watu walioona kuwa hawaridhishwi na Serikali ya Mwalimu Nyerere, hasa vijana kiasi cha kujasiria hata kuteka ndege ya abiria kwa lengo la kuishinikiza Serikali kufuata matakwa yao. Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania, Boeing 737, ilitekwa mjini Mwanza na vijana watano wa Dar es Salaam.

Baadaye ilikuja kujulikana kuwa majina ya watekaji wale ni Musa Memba (25), Mohamed Ali Abdallah (26) na ndugu yake Abdallah Ali Abdallah (22), Mohamed Tahir Ahmed (21) na Yassin Memba (21). Kiongozi wao alikuwa Musa Memba.

Kama utakuwa na muda takupa dondoo kiduchu.
Mkuu hujasoma mambo ya coast sharing yaliyotambulishwa na nchi zilizoendelea kupitia imf.... Kabla ya hapo kila kitu kilikuwa chini ya serkal kuu
 
Wakati Mzee mwinyi anapokea nchi uchumi ulikuwa unasoma negative hali ya maisha ya watanzania ilikuwa mbaya sana watanzania walikuwa wanavaa viraka naona taratibu tunarudi enzi za nyerere kwenye huu utawala
 
Mwinyi aliporomoshaje nchi?, kwani alikuta nchi ina nini hasa.

Afadhali umenena. Alichokikuta ni umasikini uliokithiri na watu kufika hadi kuvaa nguo zilizoshonwa kwa kutumia mifuko ya mchele na unga (enzi zile vyakula vikiletwa kwenye mifuko ya kitambaa kigumu)
 
Arabuni ni pamoja ghuba ya uajemi, ukingo wa magharibi pmj na mashariki ya Kati
Mzee mwinyi alijipatia toto la kiarabu safari zikawa hazikatiki huko alimaanusura ndoa yake na siti ivunjike kama si busara za mama Maria nyerere

Uko finyu sana.
 
Complexity ya biashara ya nchi ilikuwa ngumu, hasa kwa wakati Mwinyi. Alichofanya si haba, mapungufu yapo ila faida nazo si haba, kwa sasa sukari tu tunalia..... wakati huo kila bidhaa ilikuwa adimu! Ombeni sana yasiwakute enyi dotcom,
 
usibishe kitu usichokijua, sio wote ni wanazi wa vyama kama wewe
Wapi nimebisha mie nimeuliza tu! Wewe umesema Mzee Mwinyi kajengewa nyumba kubwa ya bilioni 9 ipo nyuma ya Sea Cliff.

Nikauliza ili kupata kujua mbona nyuma ya Sea Cliff kuna bahari.

images-7.jpeg


Hiyo barabara ndiyo yakuingilia Sea Cliff mkuu.

2016-05-09-20-19-38--1708143328.jpeg

Mkuu ukiingia Sea Cliff ndiyo pako hivi huko nyuma kuna bahari ni Peninsula.

Labda tufahamishe huyo nyumba ya Mzee Mwinyi ipo kwa sehemu gani mkuu wangu.

Nakala: FaizaFoxy
 
Pig
Wapi nimebisha mie nimeuliza tu! Wewe umesema Mzee Mwinyi kajengewa nyumba kubwa ya bilioni 9 ipo nyuma ya Sea Cliff.

Nikauliza ili kupata kujua mbona nyuma ya Sea Cliff kuna bahari.

View attachment 346019

Hiyo barabara ndiyo yakuingilia Sea Cliff mkuu.

View attachment 346020
Mkuu ukiingia Sea Cliff ndiyo pako hivi huko nyuma kuna bahari ni Peninsula.

Labda tufahamishe huyo nyumba ya Mzee Mwinyi ipo kwa sehemu gani mkuu wangu.

Nakala: FaizaFoxy
Piga picha inayoonyesha lilipo jiko na store utanielewa Kama huamini nenda ukajionee
 
Kwa ufupi tu Nyerere alitinyanga Mwinyi akaweka sawa,Mkapa akaharibu tena JK akarekebisha sasa sijui awamu hii wasije kumpa tabu tu Membe au January Makamba.
 
Pig
Piga picha inayoonyesha lilipo jiko na store utanielewa Kama huamini nenda ukajionee
Mkuu wewe mwenyewe umesema hiyo nyumba ipo nyuma ya Sea Cliff nimekuwekea picha tumeona Sea Cliff ipo baharini tena Peninsula.

Sasa hivi unasema ipo karibu na jiko la Sea Cliff na Store daaah!!

Mkuu hivi unajua maana ya Peninsula?
 
Back
Top Bottom