Tetesi: Lema kutimkia CCM

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kupokelewa muda wowote tangu sasa, maandalizi yote muhimu yamekamilika. Maombi yake ya kujiunga CCM yalipokelewa muda mrefu sana tu, ni taratibu za kichama tu ndio zilikuwa zikisubiriwa zikamilike na apokelewe rasmi. Ataambatana na viongozi waandamizi wenzie kadhaa kutoka kanda ya kaskazini na kuna moja kutoka kanda ya Nyasa, na wengine wawili ni wa chama kingine tofauti na Chadema. Mnyetishaji alidokeza.

Kilichochochea uamuzi huo ni mgawanyiko ndani ya Chadema, inayochochewa na viongozi wakuu kutokubaliana katika baadhi ya mambo ya ndani ya chama, hususani nafasi ya uenyekiti wa chama Taifa, maridhiano na CCM, rushwa, upendeleo na matumizi mabaya ya fedha kwenye chaguzi za kanda, wabunge 19 wa COVID-19, na mgombea urais kupitia Chadema 2025. Baada ya kutathmini hali hiyo ya mvutano na kuona kwamba haitakuwa na mwisho mwema, Lema alianza kujiweka pembeni na baadaye akajitenga kabisa na shughuli za chama pamoja na uongozi wa juu Chadema. Ndipo sasa baada ya kutafakari kwa kina, uamuzi wa kujiunga CCM ukaibuka na kupewa kipaumbele na umuhimu wa kipekee, na akaamua kuchukua hatua.

Mnyetishaji alidokeza na kuendelea kueleza kwamba, ndipo Kamanda Lema akaamua kuandika barua kupitia mwandamizi mmoja wa CCM taifa, na kwa kupitia tawi la CCM la karibu aliloko Lema, alimshauri awasilishe maombi yake huko, kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria za chama kupokea wanachama wapya. Kwa ahadi kwamba mwandamizi huyo atapushi jambo lake na kumuandalia mapokezi ya heshima ndugu Lema kwa platform ya kitaifa kupitia tawi hilo.

Muda utaongea zaidi, Lema atalamba dume CCM kama wengine au atalamba garasa?
 
Kwani CCM bila yeye haisongi mbelee? Kama ni kweli atakaribishwa vyemaa
 
Kwani tangu Kalisit na Milya na Nasari watimkie ccm Nini kimebadilika dogo!

Ndio kwanza mpina anasema Ikulu imetoa vibali vya sukari kifisadi

Wazabuni wa serekali wakiwemo wa Tanroad hawajalipwa tangu January
 
Maombi yake ya kujiunga CCM yalipokelewa muda mrefu sana tu, ni taratibu za kichama tu ndio zilikuwa zikisubiriwa zikamilike na apokelewe rasmi. Hapa sisi wasomi tuliokuwa huru kiakili ndio tunapata shaka. Lema aombe kujiunga usiku basi alfajiri mapema angalipokelewa tena kwa media zote kuwa live.
 
Kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa ujenzi !
Aluta continua πŸ™„πŸ‘
 
Hivi Bananga yupo CCM?
 
Huu uzi umenifanya nimkumbuke Lizaboni kipindi cha miaka ya 2010's.
 
Lema yupi?

Huyu Michael lema wa hapa pasua?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…