Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Sasa huyo Halima Mdee amewekwa ndani kwa kosa gani?

Kwani kumkosoa Rais hairuhusiwi nchini kwetu kwa hivi sasa?

Kama yeye ni Rais tuliyempa dhamana ya kuliongoza Taifa letu baada ya kumpigia kura, ni kwa nini vyama vya upinzani na wananchi wengine kwa ujumla wake wakatazwe kabisa kumkosoa Rais hata kama ukosoaji huo ni kwa maslahi ya Taifa?
Unaruhusiwa kumkosoa Rais kwa hoja na ustaarabu sio kwa kejeli na matusi
 
Unaruhusiwa kumkosoa Rais kwa hoja na ustaarabu sio kwa kejeli na matusi
Sasa Halima Mdee kamtukana Rais?

Kwani kusema matamko ya Rais yamegeuzwa sheria ni matusi?

Kwani hatujaona Rais kapiga marufuku vyama vya upinzani visifanye shughuli za kisiasa hadi mwaka 2020, na tumeona naDC,maRC na maRPC wakitekeleza agizo hilo kwa uaminifu mkubwa?
 
Mhaini kesi yake ni kifo au kifungo cha maisha Kuna mpinzani kapata adhabu kama hiyo?

Tufuate sheria,kanuni na taratibu tu hakuna shida
Rais wako kawaambia trafiki wakikuta mtu anaendesha gari kwenye lane ya mwendokasi wachukue gari, waipeleke polisi, watie matairi, wauze, kisha wakatae kwamba wameuza matairi.

Labda ungeanza naye kumwambia atoe masuluhisho yalito ndabi ya sheria

Yeye ni mkuu wa nchi na anachisema kina uzito sana.
 
Kama Kuna vyama vimekubalina na kauli hiyo basi hakuna vyama imara vya siasa
Kauli za Magufuli zinatakiwa kupingwa mahakamani.

Tatizo hatuna wanasheria wanaoweza kudiriki kufanya hili Tanzania.
 
Nchi yetu ilirejea kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, baada ya kuwa kwenye mfumo wa chama kimoja kwa kipindi kirefu baada ya kupata Uhuru wetu toka kwa mkoloni mwaka 1961.

Tuliingia kwenye uchaguzi wa kwanza wa mfumo wa vyama vingi mwaka 1995, na tukaendelea kuingia kwenye uchaguzi mkuu kila baada ya miaka 5.

Lengo kuu la kuwa na mfumo wa vyama vingi ni kwa serikali iliyoko madarakani kupokea mawazo mbadala toka kwa vyama vya upinzani yenye maslahi mapana kwa Taifa letu.

Ingawa katika kipindi chote hicho wapinzani wamekuwa katika mazingira magumu kutokana na nchi kutokuwa na uwanja sawa, kutokana nchi yetu kuendelea kuwa na Katiba ya nchi ya mfumo wa chama kimoja.

Ingawa Katiba hiyo imeendelea kuwekwa viraka ili angalau kukidhi mfumo wa sasa wa mfumo wa vyama vingi, lakini bado mfumo wa utawala wa nchi umeendelea kubaki kama mfumo wa chama kimoja.

Ingawa kwenye utawala wa awamu za 3 na 4 tuliona utawala angalau kwa kiasi fulani ni kama unakubaliana na mfumo wa vyama vingi, hali imekuwa tofauti kwenye utawala wa awamu ya 5, ambao unaonyesha viashiria vingi kuwa unatamani turejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

Nitataja mambo machache yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya 5 ambayo yanaashiria dalili za kuonyesha kuwa serikali ya awamu ya 5 inatamani nchi yetu irejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

1. Mara tu baada ya kuingia madarakani serikali ya awamu ya 5 ikapiga stop matangazo live ya Bunge kwa kisingizio kuwa hizo ni nyakati za kazi, kwa hiyo waTZ wanatakiwa kuwa makazini muda huo.

Hata hivyo imethibitika kuwa sababu hiyo iliyotolewa na watawala siyo ya kweli, kwa kuwa tumeshuhudia matangazo live wakati huo huo wa kazi kwenye ziara za Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapofanya ziara ya sehemu mbalimbali nchini.

Sasa kama kweli sababu ilikuwa watu wasiangalie Bunge live wakati wa kazi mbona wananchi hao hao ni kama wanalazamishwa kumwangalia Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapotoa hotuba zake mbalimbali nchini?

Tumeshuhudia Rais wetu akipiga marufuku mikutano na maandamano yoyote ya kisiasa hadi mwaka 2020. Lakini hata hivyo tumeshuhudia yeye Mwenyekiti wa CCM wa Taifa akifanya shughuli mbalimbali za kisiasa sehemu mbalimbali nchini kwa mwamvuli wa shughuli za kiserikali.

Tumeshuhudia pia maandamano ya wananchi wanaodaiwa wanaridhika sana na uongozi wa Rais Magufuli wanaopendekeza badala ya kuongoza kwa mihula 2 ya miaka 10 kama anavyotakiwa kwa mujibu wa Katiba, badala yake awe Rais wetu wa maisha!

2. Tumeshuhudia Bunge letu lenye wabunge wengi wa CCM, likifanya juhudi kubwa la kuwatimua Bungeni wabunge wengi wa upinzani wenye kutoa hoja nzito za kuibana serikali yetu.

Mfano halisi ni hivi sasa ambapo wabunge Halima Mdee wa Kawe na Esther Bulaya wa Bunda mjini wakifungiwa kutohudhuria vikao vya Bunge hadi mwakani kwa kile kilichodaiwa na wabunge hao wa CCM kuwa wabunge hao waliofungiwa ni watukutu.

Hata hivyo tumeshuhudia baadhi ya wabunge wa CCM ambao wamekuwa wakitumia lugha za maudhi na hadi kuwatukana wabunge wenzao wa upinzani kama vile kuwaita wezi, lakini hatujaona Bunge hilo kuwachukulia hatua wabunge hao, jambo linaloonyesha kuwa kiti cha Spika ambacho kinakaliwa na wabunge wa CCM kinaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa CCM.

3. Tumeshuhudia sehemu mbalimbali nchini hawa wateule wa Rais, hususani maDC na naRC wakiwanyanyasa wawakilishi wa wananchi wa vyama vya upinzani, hususani madiwani, wabunge na mameya kwa kuwaweka ndani pasipo sababu za misingi kwa kile wanachodai kuwa wanazo kisheria saa 'zao' 48 ambazo wanaweza kuzitumia pale wanapojisikia kumweka ndani mkazi yeyote aliyeko kwenye eneo lake ambaye ataona ametoa lugha ya uchochezi au amefanya vitendo vyovyote vyenye kuashiria uvunjifu wa amani wa eneo lake.

Hata hivyo tumeshudia wanaowekwa ndani na hao maDC na maRC ni watu wa upande mmoja pekee ambao ni viongozi wa vyama vya upinzani ambao wanatoa kauli za kuikosoa serikali.

Kama nilivyoeleza awali kuwa lengo la kuwa na mfumo wa vyama vingi nchini ni serikali kupata mawazo mbadala kutoka kwenye vyama vya upinzani yenye lengo la kuliendeleza Taifa letu kimaendeleo, sasa inapotokea serikali iliyoko madarakani haitaki kabisa kupokea mawazo mbadala,badala yake inataka kusikia maneno ya kusifiwa peke yake ni vyema serkali ikaandaa muswada na kuupeleka Bungeni ili nchi hii irejee kwenye mfumo wa chama kimoja ili kuwapunguzia mateso viongozi na vyama vya siasa vya upinzani na wananchi wengine wanaoikosoa serikali ambao kwenye hii serikali ya awamu ya 5 wanahesabika kama wahaini wa nchi hii.
Si kama.....wapinzani wengi wana tabia za kiaini kama sio wahaini.....
 
Jiengezeni kidogo basi, kama umekosa nidhamu ndani ya bunge, unakuwa nayo vipi nje ya bunge? Kuna wakati huwa na pata taabu ni kijiuliza kwa nini baadhi ya hawa jamaa wanastahili kuitwa title ya waheshimiwa. Hivi unakuwaje mheshimiwa kama huwezi hata kujiheshimu?


Na washawasha!
Kwa hiyo kwako wewe Mbunge mwenye heshima ya kuitwa Mheshimiwa ni Mbunge wako wa CCM 'chamatusi' Kibajaj?

Hivi wewe hujui hata lile sakata la kutimuliwa akina Halima Mdee na Esther Bulaya lilitokana na upendeleo wa wazi wa Spika Ndugai?

Kwani wewe hujui kuwa Mbunge Shonza aliwasha mic na kumuita Mnyika mwizi?

Sasa ni kwanini Mnyika alipoomba mwongozo ambapo ni kwa mujibu wa kanuni za Bunge kwa kumwomba Spika kuwa aliyewasha mic na kumuita yeye mwizi, aidha afute kauli yake au authibitishe wizi wake.

Sasa ni kwanini Spika Ndugai alifanya upendeleo wa wazi kwa mbunge mwenzake wa CCM aliyemwita Mnyika mwizi na badala yake akawaamuru Polisi wa Bunge wamtoe Mnyika kama kibaka?

Ni wazi CCM imelewa madaraka na inaamini kuwa itaitawala hii nchi milele.....

Hata hivyo lazima wajikumbushe, wako wapi KANU ya Kenya?

Wako wapi UNIP ya Zambia?

Wako wapi Malawi Congress?

Kitu ambacho CCM wanapaswa waelewe ni kuwa hakuna kitu chochote hapa dunia ni kilichokuwa na mwanzo ambacho hakitakuwa na mwisho....
 
Jiengezeni kidogo basi, kama umekosa nidhamu ndani ya bunge, unakuwa nayo vipi nje ya bunge? Kuna wakati huwa na pata taabu ni kijiuliza kwa nini baadhi ya hawa jamaa wanastahili kuitwa title ya waheshimiwa. Hivi unakuwaje mheshimiwa kama huwezi hata kujiheshimu?


Na washawasha!
Kwa akili zilizo fair kidogo utasema ni wapinzani tu wanaokosa nidhamu bungeniqf ukawaacha akina Shonza, Kibajaji, Msukuma etc ?!
 
Kwenye DS nilipokuwa UDSm niliulizwa: Opposition Parties in Tanzania are dying: Discuss.
 
Katika hii posti yangu uliyo quote nioneshe mahali nilipo andika maneno CCM au CHADEMA, tafadhali.


Na washawasha!


Kwa hiyo kwako wewe Mbunge mwenye heshima ya kuitwa Mheshimiwa ni Mbunge wako wa CCM 'chamatusi' Kibajaj?

Hivi wewe hujui hata lile sakata la kutimuliwa akina Halima Mdee na Esther Bulaya lilitokana na upendeleo wa wazi wa Spika Ndugai?

Kwani wewe hujui kuwa Mbunge Shonza aliwasha mic na kumuita Mnyika mwizi?

Sasa ni kwanini Mnyika alipoomba mwongozo ambapo ni kwa mujibu wa kanuni za Bunge kwa kumwomba Spika kuwa aliyewasha mic na kumuita yeye mwizi, aidha afute kauli yake au authibitishe wizi wake.

Sasa ni kwanini Spika Ndugai alifanya upendeleo wa wazi kwa mbunge mwenzake wa CCM aliyemwita Mnyika mwizi na badala yake akawaamuru Polisi wa Bunge wamtoe Mnyika kama kibaka?

Ni wazi CCM imelewa madaraka na inaamini kuwa itaitawala hii nchi milele.....

Hata hivyo lazima wajikumbushe, wako wapi KANU ya Kenya?

Wako wapi UNIP ya Zambia?

Wako wapi Malawi Congress?

Kitu ambacho CCM wanapaswa waelewe ni kuwa hakuna kitu chochote hapa dunia ni kilichokuwa na mwanzo ambacho hakitakuwa na mwisho....
 
Kwa akili zilizo fair kidogo utasema ni wapinzani tu wanaokosa nidhamu bungeniqf ukawaacha akina Shonza, Kibajaji, Msukuma etc ?!
Tena hiyo list uliyoitaja, kama kweli Spika angekuwa fair, hao ndiyo wangefukuzwa bungeni, lakini badala yake akina Shonza na Kibajaj ambao ndiyo waliosababisha lile tukio la Mnyika kutolewa kama kibaka.......

Badala yake tukamshangaa Spika Ndugai anamsifu Kibajaj, eti wewe ni kiboko umesababisha hadi wabunge wote wa upinzani watoke bungeni?

Halafu Spika huyo huyo eti anawalaumu wabunge wa upinzani, eti ni kwanini walisusia futari ya Waziri Mkuu!

Hivi yeye Spika Ndugai haoni namna anavyofanya jambo la hatari la kuweka mgawanyiko kwenye Bunge letu la vyama vingi?

Mbona maspika wenzake akina Mama Ana Makinda na marehemu Samuel Sitta hawakuongoza Bunge kwa style hiyo?
 
Rais wako kawaambia trafiki wakikuta mtu anaendesha gari kwenye kane ya mwendokasi wachukue gari, waipeleke polisi, watie matairi, wauze, kisha wakatae kwamba wameuza matairi.

Labda ungeanza naye kumwambia atoe masuluhisho yalito ndabi ya sheria

Yeye ni mkuu wa nchi na anachisema kina uzito sana.
Na ndiyo maana Halima Mdee amesema kuwa kauli ya Rais inageuzwa kuwa sheria na watendaji walio chini yake.

Cha kushangaza DC Ally Hapi akaamrisha Jeshi la Polisi limkamate, eti kamtukana Rais!
 
Rais wako kawaambia trafiki wakikuta mtu anaendesha gari kwenye kane ya mwendokasi wachukue gari, waipeleke polisi, watie matairi, wauze, kisha wakatae kwamba wameuza matairi.

Labda ungeanza naye kumwambia atoe masuluhisho yalito ndabi ya sheria

Yeye ni mkuu wa nchi na anachisema kina uzito sana.
Only in Tanzania......

Eti Rais anawahimiza Polisi wake wajichiukuliie sheria mkononi!
 
Nchi yetu ilirejea kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, baada ya kuwa kwenye mfumo wa chama kimoja kwa kipindi kirefu baada ya kupata Uhuru wetu toka kwa mkoloni mwaka 1961.

Tuliingia kwenye uchaguzi wa kwanza wa mfumo wa vyama vingi mwaka 1995, na tukaendelea kuingia kwenye uchaguzi mkuu kila baada ya miaka 5.

Lengo kuu la kuwa na mfumo wa vyama vingi ni kwa serikali iliyoko madarakani kupokea mawazo mbadala toka kwa vyama vya upinzani yenye maslahi mapana kwa Taifa letu.

Ingawa katika kipindi chote hicho wapinzani wamekuwa katika mazingira magumu kutokana na nchi kutokuwa na uwanja sawa, kutokana nchi yetu kuendelea kuwa na Katiba ya nchi ya mfumo wa chama kimoja.

Ingawa Katiba hiyo imeendelea kuwekwa viraka ili angalau kukidhi mfumo wa sasa wa mfumo wa vyama vingi, lakini bado mfumo wa utawala wa nchi umeendelea kubaki kama mfumo wa chama kimoja.

Ingawa kwenye utawala wa awamu za 3 na 4 tuliona utawala angalau kwa kiasi fulani ni kama unakubaliana na mfumo wa vyama vingi, hali imekuwa tofauti kwenye utawala wa awamu ya 5, ambao unaonyesha viashiria vingi kuwa unatamani turejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

Nitataja mambo machache yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya 5 ambayo yanaashiria dalili za kuonyesha kuwa serikali ya awamu ya 5 inatamani nchi yetu irejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

1. Mara tu baada ya kuingia madarakani serikali ya awamu ya 5 ikapiga stop matangazo live ya Bunge kwa kisingizio kuwa hizo ni nyakati za kazi, kwa hiyo waTZ wanatakiwa kuwa makazini muda huo.

Hata hivyo imethibitika kuwa sababu hiyo iliyotolewa na watawala siyo ya kweli, kwa kuwa tumeshuhudia matangazo live wakati huo huo wa kazi kwenye ziara za Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapofanya ziara ya sehemu mbalimbali nchini.

Sasa kama kweli sababu ilikuwa watu wasiangalie Bunge live wakati wa kazi mbona wananchi hao hao ni kama wanalazamishwa kumwangalia Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapotoa hotuba zake mbalimbali nchini?

Tumeshuhudia Rais wetu akipiga marufuku mikutano na maandamano yoyote ya kisiasa hadi mwaka 2020. Lakini hata hivyo tumeshuhudia yeye Mwenyekiti wa CCM wa Taifa akifanya shughuli mbalimbali za kisiasa sehemu mbalimbali nchini kwa mwamvuli wa shughuli za kiserikali.

Tumeshuhudia pia maandamano ya wananchi wanaodaiwa wanaridhika sana na uongozi wa Rais Magufuli wanaopendekeza badala ya kuongoza kwa mihula 2 ya miaka 10 kama anavyotakiwa kwa mujibu wa Katiba, badala yake awe Rais wetu wa maisha!

2. Tumeshuhudia Bunge letu lenye wabunge wengi wa CCM, likifanya juhudi kubwa la kuwatimua Bungeni wabunge wengi wa upinzani wenye kutoa hoja nzito za kuibana serikali yetu.

Mfano halisi ni hivi sasa ambapo wabunge Halima Mdee wa Kawe na Esther Bulaya wa Bunda mjini wakifungiwa kutohudhuria vikao vya Bunge hadi mwakani kwa kile kilichodaiwa na wabunge hao wa CCM kuwa wabunge hao waliofungiwa ni watukutu.

Hata hivyo tumeshuhudia baadhi ya wabunge wa CCM ambao wamekuwa wakitumia lugha za maudhi na hadi kuwatukana wabunge wenzao wa upinzani kama vile kuwaita wezi, lakini hatujaona Bunge hilo kuwachukulia hatua wabunge hao, jambo linaloonyesha kuwa kiti cha Spika ambacho kinakaliwa na wabunge wa CCM kinaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa CCM.

3. Tumeshuhudia sehemu mbalimbali nchini hawa wateule wa Rais, hususani maDC na naRC wakiwanyanyasa wawakilishi wa wananchi wa vyama vya upinzani, hususani madiwani, wabunge na mameya kwa kuwaweka ndani pasipo sababu za misingi kwa kile wanachodai kuwa wanazo kisheria saa 'zao' 48 ambazo wanaweza kuzitumia pale wanapojisikia kumweka ndani mkazi yeyote aliyeko kwenye eneo lake ambaye ataona ametoa lugha ya uchochezi au amefanya vitendo vyovyote vyenye kuashiria uvunjifu wa amani wa eneo lake.

Hata hivyo tumeshudia wanaowekwa ndani na hao maDC na maRC ni watu wa upande mmoja pekee ambao ni viongozi wa vyama vya upinzani ambao wanatoa kauli za kuikosoa serikali.

Kama nilivyoeleza awali kuwa lengo la kuwa na mfumo wa vyama vingi nchini ni serikali kupata mawazo mbadala kutoka kwenye vyama vya upinzani yenye lengo la kuliendeleza Taifa letu kimaendeleo, sasa inapotokea serikali iliyoko madarakani haitaki kabisa kupokea mawazo mbadala,badala yake inataka kusikia maneno ya kusifiwa peke yake ni vyema serkali ikaandaa muswada na kuupeleka Bungeni ili nchi hii irejee kwenye mfumo wa chama kimoja ili kuwapunguzia mateso viongozi na vyama vya siasa vya upinzani na wananchi wengine wanaoikosoa serikali ambao kwenye hii serikali ya awamu ya 5 wanahesabika kama wahaini wa nchi hii.
Hivi unaweza kusema eti Halima na Esther walifungiwa kwa kutoa hoja nzito Bungeni,hebu tuletee hapa hizo hoja nzito walizotoa hadi kupelekea kufukuzwa Bungeni ni zipi kama siyo mizuka ya kusukumwa na bangi hatimaye kufanya matendo yasiyostahili. DC au RC atamuweka ndani yeyote yule atakayehatarisha amani ndani ya eneo lake bila kujali anatoka mrengo upi,na woote wanaohatarisha amani ni hao vichaa wanaojiita makamanda wasio na mafunzo ya kijeshi..!!!
 
Sasa sijui hivyo viwanda vitajengwa wakati gani, wakati kila siku serikali ya awamu hii priority no 1 kwao ni kudeal na wapinzani!
Kwani uliambiwa serikali inajenga viwanda au inaweka mazingira bora ya ujenzi wa viwanda?
 
We
Tatizo watanzania wengi hawajielewi, pamoja na matatizo yote haya yanayosababishwa na serikali ya ccm bado huendelea kuichagua! Siku bunge letu likiwa na idadi kubwa ya wabunge wa upinzani ndio itakuwa mwisho wa maringo na majivuno ya watawala wa ccm! Hawa wachache kina Esta na Halima wanawapanikisha kina Job kiasi hiki, wangekuwa wengi hakika tungeheshimiana! Wameshatuona wa tz mazoba!

Eti wanasema mataifa mengine ikiwemo na Kenya wanamuomba Baba J akawe rais wao! Huyo hapo Kenya hawezi kuongoza hata kwa wiki 2, wakenya wanajiamini, sio waoga, sio wanafiki na wengi wao wameelimika vya kutosha! yeye hapendi kuongoza watu wa aina hiyo.
Wewe usiye muoga chukua hatua,mbona unaishia humu JF na kelele nyiingii
 
Hivi unaweza kusema eti Halima na Esther walifungiwa kwa kutoa hoja nzito Bungeni,hebu tuletee hapa hizo hoja nzito walizotoa hadi kupelekea kufukuzwa Bungeni ni zipi kama siyo mizuka ya kusukumwa na bangi hatimaye kufanya matendo yasiyostahili. DC au RC atamuweka ndani yeyote yule atakayehatarisha amani ndani ya eneo lake bila kujali anatoka mrengo upi,na woote wanaohatarisha amani ni hao vichaa wanaojiita makamanda wasio na mafunzo ya kijeshi..!!!
Hebu tuwe wakweli hivi ni nani kati ya Halima Mdee na Esther Bulaya wa Chadema na Kibajaj na Msukuma wa CCM wanaoonekana hawa ndiyo wanaopata lile jani?
 
Back
Top Bottom