Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Na ndiyo maana Halima Mdee amesema kuwa kauli ya Rais inageuzwa kuwa sheria na watendaji walio chini yake.

Cha kushangaza DC Ally Hapi akaamrisha Jeshi la Polisi limkamate, eti kamtukana Rais!
Rais anatakiwa kushukuru watu wanaomtukana wazi, kama kweli kamtukana.

Hilo katika somo la uongozi ni sehemu ya feedback kujua wasichokipenda unaowaongoza ni kipi.

Tanzania hatuwezi kuendelea mpaka tukubali kukosoana kwa lugha kali.

Siku moja kulikuwa na mgogoro mkubwa katika habari kuhusu masuala ya mazingira, mgogoro huu ulihusu kampuni yangu kwani ilihusika katika kutoa fedha zilizofanikisha mradi huu.

CEO wetu akaitisha an online forum kujibu majibu ya wafanyakazi.

Kuna wafanyakazi vijana walikuwa wanapaka mpaka nikaona noma mimi. Yaani kupaka anapaka mtu mwingine, lakini noma naona mimi kwa jinsi walivyokuwa wanapaka kisawasawa. Wengine wakawa kama Twitter activists mpaka na hashtags.

Sasa mimi nikafikiri watakaripiwa au kufukuzwa kazi. Kumbe naona wanaheshimiwa sana kwa kuleta mawazo tofauti katika kampuni!

Nikasema hii ni moja ya sababu wenzetu wanaendelea na sisi hatuendelei.

Mfano mwingine, miaka mingi iliyopita nilivyokuwa nasomea undergraduate, mwalimu wangu wa falsafa nilikuwa namchachafya sana darasani. Nilikuwa namuuliza maswali na kumpinga sana mapaka ikawa kama na dominate darasa. Nilikuwa nimesoma mambo mengi mwenyewe kabla ya darasa na darasani nilikuwa namchallenge sana mpaka wanafunzi wengine wakaniuliza "hivi wewe upinzani wako darasani huwa unaamini unayosema kweli au uzushi tu (mainly atheism). Nikawaambia ni kweli nasimamia hivyo.

Mwisho wa term profesa akanitumia e-mail, akasema nisije kwenye mtihani.

Nikaona hapa nishaharibu Profesa ananifelisha kwa technicality.

Nikamuuliza, kwa vipi nisije kwenye mtihani?

Akasema umeshafaulu kwa kazi yako ya darasani.

Nikauliza nimefaulu vipi? Akasema umepata A+. Yale mahojiano yako ya darasani ni mahojiano ya darasa la masters, si undergraduate. Huna haja ya kuja kwenye mtihani.

Huyu Profesa alikuwa ni conservative, jaji, mtunzi wa vitabu na mwalimu wa chuo kukuu. Mimi ni immigrant mbishi nambishia kila kitu darasani katika namna ambayo Profesa wa kibongo angeona namkosea heshima.

Lakini yeye alithamini sana uwezo wangu wa kujenga hoja. Mpaka akawa ananialika niende kwenye events zao kuongea na ku network na rafiki zake.

Hapo niligundua kwamba wenzetu wanaendelea kwa kuthamini mawazo tofauti.

Na sisi, bila kuthamini mawazo tofauti hatuwezi kuendelea.
 
Mkuu wa Kaya amekazana sana kupandikiza hisia za kwamba kuwa mpinzani Tanzania ni kuwa mhaini. Yaani kwake mtu akiwa Chadema/UKAWA anaonekana si mtanzania kabisa na si mzalendo kwa nchi yako.

Nawashangaa hata wanaoendelea kufanya utafiti kuhusu siasa. Unafanyaje utafiti wa kisiasa wakati shughuli za siasa zimepigwa marufuku?
 
Nchi yetu ilirejea kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, baada ya kuwa kwenye mfumo wa chama kimoja kwa kipindi kirefu baada ya kupata Uhuru wetu toka kwa mkoloni mwaka 1961.

Tuliingia kwenye uchaguzi wa kwanza wa mfumo wa vyama vingi mwaka 1995, na tukaendelea kuingia kwenye uchaguzi mkuu kila baada ya miaka 5.

Lengo kuu la kuwa na mfumo wa vyama vingi ni kwa serikali iliyoko madarakani kupokea mawazo mbadala toka kwa vyama vya upinzani yenye maslahi mapana kwa Taifa letu.

Ingawa katika kipindi chote hicho wapinzani wamekuwa katika mazingira magumu kutokana na nchi kutokuwa na uwanja sawa, kutokana nchi yetu kuendelea kuwa na Katiba ya nchi ya mfumo wa chama kimoja.

Ingawa Katiba hiyo imeendelea kuwekwa viraka ili angalau kukidhi mfumo wa sasa wa mfumo wa vyama vingi, lakini bado mfumo wa utawala wa nchi umeendelea kubaki kama mfumo wa chama kimoja.

Ingawa kwenye utawala wa awamu za 3 na 4 tuliona utawala angalau kwa kiasi fulani ni kama unakubaliana na mfumo wa vyama vingi, hali imekuwa tofauti kwenye utawala wa awamu ya 5, ambao unaonyesha viashiria vingi kuwa unatamani turejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

Nitataja mambo machache yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya 5 ambayo yanaashiria dalili za kuonyesha kuwa serikali ya awamu ya 5 inatamani nchi yetu irejee kwenye mfumo wa chama kimoja.

1. Mara tu baada ya kuingia madarakani serikali ya awamu ya 5 ikapiga stop matangazo live ya Bunge kwa kisingizio kuwa hizo ni nyakati za kazi, kwa hiyo waTZ wanatakiwa kuwa makazini muda huo.

Hata hivyo imethibitika kuwa sababu hiyo iliyotolewa na watawala siyo ya kweli, kwa kuwa tumeshuhudia matangazo live wakati huo huo wa kazi kwenye ziara za Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapofanya ziara ya sehemu mbalimbali nchini.

Sasa kama kweli sababu ilikuwa watu wasiangalie Bunge live wakati wa kazi mbona wananchi hao hao ni kama wanalazamishwa kumwangalia Mwenyekiti wa CCM Taifa kila anapotoa hotuba zake mbalimbali nchini?

Tumeshuhudia Rais wetu akipiga marufuku mikutano na maandamano yoyote ya kisiasa hadi mwaka 2020. Lakini hata hivyo tumeshuhudia yeye Mwenyekiti wa CCM wa Taifa akifanya shughuli mbalimbali za kisiasa sehemu mbalimbali nchini kwa mwamvuli wa shughuli za kiserikali.

Tumeshuhudia pia maandamano ya wananchi wanaodaiwa wanaridhika sana na uongozi wa Rais Magufuli wanaopendekeza badala ya kuongoza kwa mihula 2 ya miaka 10 kama anavyotakiwa kwa mujibu wa Katiba, badala yake awe Rais wetu wa maisha!

2. Tumeshuhudia Bunge letu lenye wabunge wengi wa CCM, likifanya juhudi kubwa la kuwatimua Bungeni wabunge wengi wa upinzani wenye kutoa hoja nzito za kuibana serikali yetu.

Mfano halisi ni hivi sasa ambapo wabunge Halima Mdee wa Kawe na Esther Bulaya wa Bunda mjini wakifungiwa kutohudhuria vikao vya Bunge hadi mwakani kwa kile kilichodaiwa na wabunge hao wa CCM kuwa wabunge hao waliofungiwa ni watukutu.

Hata hivyo tumeshuhudia baadhi ya wabunge wa CCM ambao wamekuwa wakitumia lugha za maudhi na hadi kuwatukana wabunge wenzao wa upinzani kama vile kuwaita wezi, lakini hatujaona Bunge hilo kuwachukulia hatua wabunge hao, jambo linaloonyesha kuwa kiti cha Spika ambacho kinakaliwa na wabunge wa CCM kinaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa CCM.

3. Tumeshuhudia sehemu mbalimbali nchini hawa wateule wa Rais, hususani maDC na naRC wakiwanyanyasa wawakilishi wa wananchi wa vyama vya upinzani, hususani madiwani, wabunge na mameya kwa kuwaweka ndani pasipo sababu za misingi kwa kile wanachodai kuwa wanazo kisheria saa 'zao' 48 ambazo wanaweza kuzitumia pale wanapojisikia kumweka ndani mkazi yeyote aliyeko kwenye eneo lake ambaye ataona ametoa lugha ya uchochezi au amefanya vitendo vyovyote vyenye kuashiria uvunjifu wa amani wa eneo lake.

Hata hivyo tumeshudia wanaowekwa ndani na hao maDC na maRC ni watu wa upande mmoja pekee ambao ni viongozi wa vyama vya upinzani ambao wanatoa kauli za kuikosoa serikali.

Kama nilivyoeleza awali kuwa lengo la kuwa na mfumo wa vyama vingi nchini ni serikali kupata mawazo mbadala kutoka kwenye vyama vya upinzani yenye lengo la kuliendeleza Taifa letu kimaendeleo, sasa inapotokea serikali iliyoko madarakani haitaki kabisa kupokea mawazo mbadala,badala yake inataka kusikia maneno ya kusifiwa peke yake ni vyema serkali ikaandaa muswada na kuupeleka Bungeni ili nchi hii irejee kwenye mfumo wa chama kimoja ili kuwapunguzia mateso viongozi na vyama vya siasa vya upinzani na wananchi wengine wanaoikosoa serikali ambao kwenye hii serikali ya awamu ya 5 wanahesabika kama wahaini wa nchi hii.

Aya ya kwanza tu inaonyesha hujui historia ya nchi yetu.Chama kimoja hakikuanza 1961,uliza ujue ndipo uandike.Humu jukwaani kuna watu kila wanachosoma wanaamini kuwa ndicho.Tuandike tunachokijua.
 
Rais anatakiwa kushukuru watu wanaomtukana wazi, kama kweli kamtukana.

Hilo katika somo la uongozi ni sehemu ya feedback kujua wasichokipenda unaowaongoza ni kipi.

Tanzania hatuwezi kuendelea mpaka tukubali kukosoana kwa lugha kali.

Siku moja kulikuwa na mgogoro mkubwa katika habari kuhusu masuala ya mazingira, mgogoro huu ulihusu kampuni yangu kwani ilihusika katika kutoa fedha zilizofanikisha mradi huu.

CEO wetu akaitisha an online forum kujibu majibu ya wafanyakazi.

Kuna wafanyakazi vijana walikuwa wanapaka mpaka nikaona noma mimi. Yaani kupaka anapaka mtu mwingine, lakini noma naona mimi kwa jinsi walivyokuwa wanapaka kisawasawa. Wengine wakawa kama Twitter activists mpaka na hashtags.

Sasa mimi nikafikiri watakaripiwa au kufukuzwa kazi. Kumbe naona wanaheshimiwa sana kwa kuleta mawazo tofauti katika kampuni!

Nikasema hii ni moja ya sababu wenzetu wanaendelea na sisi hatuendelei.

Mfano mwingine, miaka mingi iliyopita nilivyokuwa nasomea undergraduate, mwalimu wangu wa falsafa nilikuwa namchachafya sana darasani. Nilikuwa namuuliza maswali na kumpinga sana mapaka ikawa kama na dominate darasa. Nilikuwa nimesoma mambo mengi mwenyewe kabla ya darasa na darasani nilikuwa namchallenge sana mpaka wanafunzi wengine wakaniuliza "hivi wewe upinzani wako darasani huwa unaamini unayosema kweli au uzushi tu (mainly atheism). Nikawaambia ni kweli nasimamia hivyo.

Mwisho wa term profesa akanitumia e-mail, akasema nisije kwenye mtihani.

Nikaona hapa nishaharibu Profesa ananifelisha kwa technicality.

Nikamuuliza, kwa vipi nisije kwenye mtihani?

Akasema umeshafaulu kwa kazi yako ya darasani.

Nikauliza nimefaulu vipi? Akasema umepata A+. Yale mahojiano yako ya darasani ni mahojiano ya darasa la masters, si undergraduate. Huna haja ya kuja kwenye mtihani.

Huyu Profesa alikuwa ni conservative, jaji, mtunzi wa vitabu na mwalimu wa chuo kukuu. Mimi ni immigrant mbishi nambishia kila kitu darasani katika namna ambayo Profesa wa kibongo angeona namkosea heshima.

Lakini yeye alithamini sana uwezo wangu wa kujenga hoja. Mpaka akawa ananialika niende kwenye events zao kuongea na ku network na rafiki zake.

Hapo niligundua kwamba wenzetu wanaendelea kwa kuthamini mawazo tofauti.

Na sisi, bila kuthamini mawazo tofauti hatuwezi kuendelea.
You are very right.....

Kiongozi bora ni yule hachukii kukosolewa ili ajirekebishe pale alipokosea, kwa kuwa yeye as Human being hawezi kuwa 100%
 
You are very right.....

Kiongozi bora ni yule hachukii kukosolewa ili ajirekebishe pale alipokosea, kwa kuwa yeye as Human being hawezi kuwa 100%
Huyu wetu anasema hapangiwi na hakuchukua fomu na mtu.
 
Aya ya kwanza tu inaonyesha hujui historia ya nchi yetu.Chama kimoja hakikuanza 1961,uliza ujue ndipo uandike.Humu jukwaani kuna watu kila wanachosoma wanaamini kuwa ndicho.Tuandike tunachokijua.
Nimekwambia tulirejea kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

Nafahamu pia kuwa nchi yetu ilikuwa kwenye mfumo wa vyama vingi kwa kipindi kifupi baada ya nchi yetu kupata Uhuru wake mwaka 1961.

Baadaye nchi ikaingia kwenye mfumo wa chama kimoja.

Na baadaye ndiyo tukarejea tena kwenye mfumo wa vyama vingi nwaka 1992.
 
Sasa kama Rais kukosolewa inaruhusiwa, ni kwanini DC wa Kinondoni amewaamrisha Polisi wamkamate Halima Mdee na wamweke korokoroni kwa yale aliyoyaita masaa 'yake' 48?

Ndiyo tunapata jibu kuwa serikali hii ya awamu ya 5 inachotaka ni kusifiwa peke yake, haitaki hata kidogo kukosolewa, kwa hiyo kwa mazingira hayo badala ya kuendelea kuwanyanyasa wananchi wote wanaoikosia, ni bora wapeleke miswada bungeni wa kuirejesha nchi hii kwenye mfumo wa chama kimoja ili wananchi tujue moja

Je ungependa kuwa na binti wa aina ya Halima Mdee kwa tabia.mwenendo na lugha? ana uwezo mkubwa wa akili na kujenga hoja.Ana tatizo kubwa la kuudhibiti ulimi wake.Waingereza wana msemo muhimu sana kwa Halima Mdee na watu wa aina yake,unasema"What matters is not what you say but how you say it".

Ukiwa timamu kimalezi unajua namna ya kusema na waliokuzidi umri na unapaswa kujua unasema wapi.Siyo kila mahali ni bungeni.
 
Hivi wakoloni wangemminya Nyerere kama wanavyominywa wenye mtazamo tofauti na watawala wa sasa tungepata uhuru? Tungekuwa na kumbukumbu zipi za Nyerere? nakumbuka Nyerer alikuwa na maneno makali kuliko ya Mdee au Lissu. Akiwahutubia wananchi aliwataja wakoloni kuwa ni makupe, mabeberu, mapepari, wanyonyaji wakubwa. Akasema mmetupuuza na kutunyonya vya kutosha sasa tunataka tuwe huru. Pamoja na kwamba wakoloni walikuwa na dola lakini walimpa Nyerere uhuru wa kuhutubia na kufanya siasa na matunda yake tulipata hotuba zake nyingi na vitabu vyake vingi kabisa. Leo watu wanaogopa hata kuandika vitabu vya riwaya, mashairi, n.k.

Nakumbuka enzi za Nyerere kulikuwa na riwaya, mashairi na vitabu vya kiuanaharakati vingi tu hadi kwenye utawala wa Mkapa. Lakini leo kila mtu yuko kimyaaaaaaaaa! Anakufa na maarifa yake kichwani kwa hofu ya utawala uliopo. Ngoja tuone mwisho wake.
 
Nimekwambia tulirejea kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

Nafahamu pia kuwa nchi yetu ilikuwa kwenye mfumo wa vyama vingi kwa kipindi kifupi baada ya nchi yetu kupata Uhuru wake mwaka 1961.

Baadaye nchi ikaingia kwenye mfumo wa chama kimoja.

Na baadaye ndiyo tukarejea tena kwenye mfumo wa vyama vingi nwaka 1992.

Waambie baada ya uhuru vyama vingi viliondolewa lini? vimerejeshwa 1992 sawa baada ya kuwa chini ya Chama kimoja kwa muda gani?
 
Hiyu wetu anasema hapangiwi na hakuchukua fomu na mtu.
Kwanza yale maneno ya kusema kuwa hakuna mtu aliyenituma kwenda kuchukua fomu ya Urais kwa hiyo hakuna mtanzania yeyote anayepaswa kunielekeza la kufanya, ni maneno ya dharau kubwa kwa wapiga kura wake, kwa kuwa anajua siyo yeye mwenyewe aliyejipeleka Ikulu, Bali kwa kura za watanzania.

Sasa tusubiri 2020 kwa hizo tambo zake tuone kama kura yake moja na ya mama Jesca kama ndizo zitakazomrejesha Ikulu!
 
Je ungependa kuwa na binti wa aina ya Halima Mdee kwa tabia.mwenendo na lugha? ana uwezo mkubwa wa akili na kujenga hoja.Ana tatizo kubwa la kuudhibiti ulimi wake.Waingereza wana msemo muhimu sana kwa Halima Mdee na watu wa aina yake,unasema"What matters is not what you say but how you say it".

Ukiwa timamu kimalezi unajua namna ya kusema na waliokuzidi umri na unapaswa kujua unasema wapi.Siyo kila mahali ni bungeni.
Tumemsikia DCwa Kinondoni akisema kuwa aliamuru Polisi wamkamate Halima Mdee kwa kuwa amemtukana Rais.

Sasa nikuulize wewe Halima Mdee kusema Rais anaichukulia kauli yake kuwa sheria, hapo tusi liko wapi?
 
Kwanza yale maneno ya kusema kuwa hakuna mtu aliyenituma kwenda kuchukua fomu ya Urais kwa hiyo hakuna mtanzania yeyote anayepaswa kunielekeza la kufanya, ni maneno ya dharau kubwa kwa wapiga kura wake, kwa kuwa anajua siyo yeye mwenyewe aliyejipeleka Ikulu, Bali kwa kura za watanzania.

Sasa tusubiri 2020 kwa hizo tambo zake tuone kama kura yake moja na ya mama Jesca kama ndizo zitakazomrejesha Ikulu!
Yule kwajinsi anavyompeleka Mama Jesca puta nina shaka hata kama kura ya Mama Jesca aliipata.

Wewe huoni hata kwenye kampeni tu Mama Jesca aligoma mpaka wazee wakamshawishi sana kwamba haileti picha nzuri Baba azunguke kwenye kampeni bila mama?

Na hivi kura ilivyo siri Mama wa watu anaweza kuwa kampigia Lowassa au hata Rungwe au kuharibu tu kura ilinafsi isimsute kwa kumpigia kura gubegube huyu anayemjua vizuri sana kwa vituko vyake vya mpaka ndani ya nyumba.
 
Aya ya kwanza tu inaonyesha hujui historia ya nchi yetu.Chama kimoja hakikuanza 1961,uliza ujue ndipo uandike.Humu jukwaani kuna watu kila wanachosoma wanaamini kuwa ndicho.Tuandike tunachokijua.

anaweza kuwa kakosea hapo vipi hayo mengine?
 
Yule kwajinsi anavyompeleka Mama Jesca puta nina shaka hata kama kura ya Mama Jesca aliipata.

Wewe huoni hata kwenye kampeni tu Mama Jesca aligoma mpaka wazee wakamshawishi sana kwamba haileti picha nzuri Baba azunguke kwenye kampeni bila mama?

Na hivi kura ilivyo siri Mama wa watu anaweza kuwa kampigia Lowassa au hata Rungwe au kuharibu tu kura ilinafsi isimsute kwa kumpigia kura gubegube huyu anayemjua vizuri sana kwa vituko vyake vya mpaka ndani ya nyumba.

Msitafute matusi ya bure ili mseme unaona wanapendelea wa kumshtaki.Kuna mama niliyedhani anastahili heshima kubwa,wakati wa kampeni alikamatwa sehemu zinazostahili kuguswa na baba mwenye nyumba tu,tena chumbani.Sijasikia chochote kulaani kitendo hiki.JPM akisemwa hovyo mnaona sawa na mnamtaka avumilie kuna mtu akiguswa tu mnatamani maandamano yaruhusiwe.Poleni.
 
Msitafute matusi ya bure ili mseme unaona wanapendelea wa kumshtaki.Kuna mama niliyedhani anastahili heshima kubwa,wakati wa kampeni alikamatwa sehemu zinazostahili kuguswa na baba mwenye nyumba tu,tena chumbani.Sijasikia chochote kulaani kitendo hiki.JPM akisemwa hovyo mnaona sawa na mnamtaka avumilie kuna mtu akiguswa tu mnatamani maandamano yaruhusiwe.Poleni.
Unaposema "msitafute" unakikusudia kikundi gani?

Mimi sifungamani na namba yoyote, ni "singularity" kama kugawanya kwa ziro.

Huyo Mama nisiyemjua wala hata kumtaja unamhusishaje na mimi mpaka ukaniwekee habari zake kwenye nukuu ya bandiko langu?

Watu tunamsema ovyo Mungu, nini JPM huyo gubegube ambaye hata Kiswahili hajui?

Uhuru wa wananchi kuwasema vibaya viongozi ni sehemu muhimu ya jamii kuendelea.

Hakuna namna ya kulikwepa hili.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
usisome juu tu huu mjadala huru sio shule
.

Mjadala ni zaidi ya shule ya darasani.Ni mahali sahihi pa kujifunzia maisha halisi ya mtaani.Huku hakuna "copy and paste".Ukianzisha uzi hakiki kwa uhakika unachoandika,ukikosea sarufi si kosa kubwa japo utawapotosha wanaojifunza lugha lakini ukipotosha mada unawapoteza kabisa watoto wa kizazi cha "copy and paste".

Nilisoma makala nzima mkuu.
 
Back
Top Bottom