Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Huko hakuna hayo yalioko nikuwa wakubwa wa kiccm hawataki kusikia madai ya katiba mpya na ndicho alichokamatiwa yeye hayo mengine nikunogeshana tu hapo lumumba ili kuaminishwa hayo.



Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app

Kumbuka utetezi wa Sabaya kwenye kesi yake...ikitokea madai ya Sabaya akiwa kiongozi wa umma hapo tutawalaumu Lumumba....?
 
Huu mchezo umekaa kimkakati sana.

Bado naamini jamaa atatoka.

Kuna watu wanabeba credit for now. ! Tukisahau atarudi mtaani soon.
 
Take a note from this post/thread, hukumu hii kuna kitu inataka kuhalalisha. Watamfunga Mbowe!
Then baadaye Sabaya will be pardoned!
Sidhani. Hakuna kesi ya maana dhidi yake. Ungeniambia nibashiri probability ya Mbowe kufungwa, ningesema ni chini ya 5%. Mimi naamini wanataka kum manage tu ili wenye nchi watawale bila "kelele" za wapinzani. Makesi tu hayo yatachukua muda.

Well, hii nchi haiishi vituko. Ngoja tusubiri.
 
Shenzi kabisa haki ipo wapi hapo, mtu alikuwa anapokea maelezo kutoka juu una muhukumu vipi? Kwa hiyo JPM angekuwa hai angehukumiwa?
Anapokea maelekezo kutoka juu kwa Mungu? Hakuna aliye juu ya sheria.wewe unaambiwa ukachukuwe fedha za watu kwanguvu unaenda kama mbumbumbu .haya si alisema makamu wa Rais na Mama samia walikua wanajua wako wapi sasa mbona wasimsaidie? Huyo bwanamdogo ni ulimbukeni wake na tamaa ya mali za harakaharaka vimemponza.
 
Utaambiwa hata kwa Sabaya busara ilitamalaki ndio maana akapigwa 30yrs baadala ya 90yrs au kunyongwa mpaka kufa.... utaambiwa mwenye uwezo wa kusema una hatia au huna ni mahakama si vinginevyo, ukitaka kuipinga mahakama kata rufaa...

Uliona pale kwenye "uamuzi ni wao?"

Uamuzi si lazima uwe wa haki au siyo?

Sisi tunasubiri kama wao wanavyosubiri kila mmoja akiwa entitled to one's opinion au vipi?

Kuna taabu hapo?
 
Wanajukwaa poleni kwa kumbukumbu ya kifo cha muasisi wa Taifa letu,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Bila shaka baada ya Hukumu ya Lengai Ole Sabaya kuhairishwa tarehe 1/10/2021 ilipangwa kwamba itatolewa leo. Hivyo tuelekeze masikio yetu katika viunga vya mahakama.

=======

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili leo Ijumaa Oktoba 15, 2021 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kusikiliza hukumu ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha.

Hakimu mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Amalia Mushi aliahirisha hukumu hiyo Oktoba Mosi, 2021 baada ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo, kutokamilisha kuandika hukumu hiyo.

Agosti 24 mwaka huu, Sabaya na wenzake Sylvester Nyegu na Daniel Mbura walikamilisha kujitetea mahakamani hapo baada ya Jamhuri kukamilisha mashahidi 11 na vielelezo vinane.

Sabaya alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Juni 4, mwaka huu baada ya kukamatwa Mei 27 wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi

UPDATE: MAHAKAMA YAMKUTA NA HATIA OLE SABAYA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imemkuta na hatia Lengai Ole Sabaya na wenzake katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mahakama ilimpatia nafasi Ole Sabaya ajitetee(Shufaa) kwanini asipewe adhabu kali naye aliiomba Mahakama imuonee huruma kwani si yeye bali alikuwa anatekeleza amri ya mamlaka ya uteuzi, pia ameomba mahakama imuonee huruma kwani ana mchumba anayetegemea kufunga naye ndoa na mahari ameshalipa.

UPDATE: SABAYA NA WENZAKE MIAKA 30 JELA

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wamehukumia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

WASIFU WA OLE SABAYA

Lengai Ole Sabaya amezaliwa 26/12/1986 mkoani Arusha. Amesoma Shahada ya Sayansi katika Elimu Chuo Kikuu cha Mtakatifu John Dodoma (St. John University).

Ole Sabaya aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Mkoa wa Arusha na pia aliwahi kushika wadhifa wa Udiwani katika kata ya Sambasha Wilaya ya Arusha Mjini mwaka 2015.

Ole Sabaya aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro tarehe 28 Julai 2018 ya aliyekuwa Rais wa Tanzania awamu ya tano, Hayati John Pombe Magufuli.

Sabaya alitenguliwa nafasi hiyo ya ukuu wa Wilaya ya Hai tarehe 13 Mei 2021 na Rais Samia Suluhu Hassan ili kupisha uchunguzi wa makosa yaliyokuwa yakimkabili ikiwemo unyang’anyi wa kutumia silaha. Tarehe 15 Oktoba 2021 Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Arusha imemhukumu Sabaya na wenzake kifungo cha miaka 30 jela.
Makengeza is next!
 
Wote mnaofurahia msiombe siku moja ukaenda mahakamani na ujua kabisa ukweli huna kosa ila ukaenda na maji ...

Duniani hakuna mahakama ni upumbavu mtupu hakuna cha mahakama wala nini ni ujinga + ujinga ...

Sibirini ya Mbowe ndio mtajua hamjui
Kama hutendi uovu, na haupendi uovu Hilo halita kukuta labda ubambikiwe kama aliyebambikiwa ugaidi.
 
Back
Top Bottom