Lengo la kuwa na saving ya milioni 20 ifikapo mwaka 2022 mwezi Oktoba

Lengo la kuwa na saving ya milioni 20 ifikapo mwaka 2022 mwezi Oktoba

Mzee Wa Republican

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
1,666
Reaction score
847
Salaam sana wakuu,

Tunamshukuru Muumba wa mbingu na nchi kwa kutufikisha disemba hii 2021 ambapo tunapata nafasi mtawalia ya kutafakari kwa kina malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2021 huku tukijipanga kwa ajili ya mwaka mpya 2022. Binafsi nina lengo la kufanya savings ifike milioni 20 ifikapo mwaka 2022 mwezi Oktoba. Maandalizi kwa ajili ya kufanikisha lengo langu hilo nimeshayaanza kwani mpaka sasa nimeshafungua akaunti ya kufanya savings hiyo. Vile vile kuna kijikazi nakifanya (tofauti na kazi yangu rasmi ya mshahara) kwa hiyo nitakuwa na inflow fulani hivi ambayo kwa miezi tarajiwa mpaka Oktoba 2022 ninaweza kufikia kiwango hicho cha milioni 20.

Lengo kuu la savings hiyo ni kuwezesha ujenzi wa banda langu la kujifichia hapa jijini Dar es Salaam kwani maisha ya upangaji ni magumu na kwa vijana wengi tunajua kuwa wakati wa kutafuta nyumba zetu ni sasa ili kupunguza mzigo wa kodi ya nyumba pale utakapokuwa na familia maana sisi hatuna utegemezi wa kurithi mali za wazazi wetu.

Niko hapa mbele yenu ili nipate uzoefu kwa wale waliowahi kujiwekea malengo ya kufanya savings kwa kipindi fulani cha miezi na hata miaka wanipe uzoefu ni kwa namna gani walifanikiwa kufikia malengo yao sambamba na changamoto walizokutana nazo jambo linaloweza kuwa chachu ya mafanikio sio kwangu tu bali hata kwa wenzangu waliopo katika jukwaa hili kwani changamoto za savings hakuna asiyezijua na isitoshe hakuna mtu asiye na matumizi ya pesa ikiwepo kuruka mitego kadhaa ya maombi ya ndugu, jamaa, marafiki pamoja na watoto wa mjini (hasa wa kike) si mnajua wanavyovutia wakuu ";;;;;;. . . .

Naomba kuwasilisha wakuu . . .
 
kwani changamoto za savings hakuna asiyezijua na isitoshe hakuna mtu asiye na matumizi ya pesa ikiwepo kuruka mitego kadhaa ya maombi ya ndugu, jamaa, marafiki pamoja na watoto wa mjini (hasa wa kike)
#1. Fungua account ya muda maalum benki, Hii account inakuwezesha kuweka tu fedha, na kamwe hairuhusu kutoa fedha hadi muda wa mkataba uishe, kama ni miezi 10 basi hutoweza kutoa hiyo fedha.
 
Hongera na kila la kheri mkuu. Hapo kwa uchache uweke Millioni Mbili kila mwezi.

Kwakua lengo ni kuwa na kwako, kiwanja kipo au ndio unaikusanya upate kiwanja kwanza ndio uanze ujenzi?
 
Una umri gani? Jack Ma alisema katika maisha yako, anza ujuzi au biashara ukiwa 20, 30 hakikisha una ujuzi wa kitosha wa unachokifanya na umeajiri watu. 40 hakikisha ulichoanzisha kina jitegemea bila wewe kuwepo kila siku. 50 hakikisha ulichoanzisha kina kulea.
 
Account itakayokupa riba bora zaidi kwa lengo lako ni kununua vipande vya Liquid Fund ya utt.

Unaiongezea fedha siku yoyote, hata kwa miamala ya simu. Utakapofikia kuzihitaji fedha zako unajaza fomu, within 3 working days unazipata.

Riba ni zaidi kidogo ya 11% per annum. Hupati riba za hivyo benki kwa hali za kawaida.

Watakuja wa kuponda riba hizo na kusema uzifanyie biashara fedha zako - lakini ulivyosema lengo lako ni kusave ili ujenge.
 
Account itakayokupa riba bora zaidi kwa lengo lako ni kununua vipande vya Liquid Fund ya utt.

Unaiongezea fedha siku yoyote, hata kwa miamala ya simu. Utakapofikia kuzihitaji fedha zako unajaza fomu, within 3 working days unazipata.

Riba ni zaidi kidogo ya 11% per annum. Hupati riba za hivyo benki kwa hali za kawaida.

Watakuja wa kuponda riba hizo na kusema uzifanyie biashara fedha zako - lakini ulivyosema lengo lako ni kusave ili ujenge.

Elimu ya uwekezaji inahitajika sana. Wengi wetu hatuelewi kabisa mambo ya hisa, hati fungati, mambo ya UTT ndio kabisaaaa.

Natamani mitaala ingeboreshwa haya mambo na ujasiriamali (ijikite kwenye finance) yakapigwa hata kwa utangulizi tu.
 
Natamani nikushauri lakini naona maoni ya watu wengi yanafanana na hisia nanmalengo yako... kila lakheri.....
 
  • Thanks
Reactions: Cyn
Hii na mimi nitaifaut , wa mkoan inakuwaje sasa.
Account itakayokupa riba bora zaidi kwa lengo lako ni kununua vipande vya Liquid Fund ya utt.

Unaiongezea fedha siku yoyote, hata kwa miamala ya simu. Utakapofikia kuzihitaji fedha zako unajaza fomu, within 3 working days unazipata.

Riba ni zaidi kidogo ya 11% per annum. Hupati riba za hivyo benki kwa hali za kawaida.

Watakuja wa kuponda riba hizo na kusema uzifanyie biashara fedha zako - lakini ulivyosema lengo lako ni kusave ili ujenge.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Account itakayokupa riba bora zaidi kwa lengo lako ni kununua vipande vya Liquid Fund ya utt.

Unaiongezea fedha siku yoyote, hata kwa miamala ya simu. Utakapofikia kuzihitaji fedha zako unajaza fomu, within 3 working days unazipata.

Riba ni zaidi kidogo ya 11% per annum. Hupati riba za hivyo benki kwa hali za kawaida.

Watakuja wa kuponda riba hizo na kusema uzifanyie biashara fedha zako - lakini ulivyosema lengo lako ni kusave ili ujenge.
📌
 
Account itakayokupa riba bora zaidi kwa lengo lako ni kununua vipande vya Liquid Fund ya utt.

Unaiongezea fedha siku yoyote, hata kwa miamala ya simu. Utakapofikia kuzihitaji fedha zako unajaza fomu, within 3 working days unazipata.

Riba ni zaidi kidogo ya 11% per annum. Hupati riba za hivyo benki kwa hali za kawaida.

Watakuja wa kuponda riba hizo na kusema uzifanyie biashara fedha zako - lakini ulivyosema lengo lako ni kusave ili ujenge.
Hii riba nzuri kabisa....ebu nielekeze wapi naweza pata taarifa zaidi
 
Weka standing order kukata milioni 1 kila mwezi kwenye mshahara
Na hio side business kila mwezi chukua 1m peleka benki
Kwa mwaka 24M hiooo

Acha ama punguza anasa
Inawezekana
 
Usiangaike kufanya saving. Kama una kiwanja anza kununua materials kama matofali, nondo, simenti na mchanga. Unaweza kuweka site au kuviweka kwa jirani ya site. Pia ukiweza kuanza uanze tu.

Mimi nina nyumba kadhaa na sehemu tofauti tofauti na sikuwahi kuanza kujenga nikiwa na milioni 10. Hata nikiwa na milioni mbili tu nachora ramani nalianzisha na baada ya muda zinaisha na nawapangisha raia zinazalisha naanza nyingine.

Kama una laki tano hapo kanunue tofali leo peleka site,nakuhakikishia mwezi Disemba utakuwa mbali zaidi ya hiyo milioni 24 unayotaka kusevu. Tofauti na hapo huwezi kukusanya hiyo hela labda ukope

Fanya nilivyokuelekeza utanishukuru baadae. Achana na savings
 
Back
Top Bottom