Mtoa Taarifa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2024
- 213
- 671
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa amezikumbusha Taasisi na mashirika yote ya Serikali yaliyopo kote nchini Tanzania ambayo yanahudumia watu zaidi ya 100, kutekeleza bila shuruti agizo lake la kuitangaza Disemba 31, 2024 kuwa siku ya mwisho kwa matumizi ya Mkaa na Kuni kwenye shughuli za Mapishi.
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa ametoa kauli hiyo mapema Leo Jumanne Disemba 31, 2024 wakati akihutubia wananchi kwenye Tamasha la Azimio la Kizimkazi 2024, linalofanyika kwa mara ya pili Ruangwa Mkoani Lindi ikiwa ni mara baada ya kuzinduliwa kwake mapema mwaka huu na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kizimkazi Visiwani Zanzibar.
Waziri Mkuu amezitaja taasisi zinazohusika na agizo hilo kuwa ni pamoja na Taasisi zote zenye kuhudumia watu zaidi ya mia moja ikiwemo Majeshi mbalimbali, Shule za bweni za Binafsi na za serikali, Magereza pamoja na Wazabuni wanaopika vyakula vya zaidi ya watu 100.
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa ametoa kauli hiyo mapema Leo Jumanne Disemba 31, 2024 wakati akihutubia wananchi kwenye Tamasha la Azimio la Kizimkazi 2024, linalofanyika kwa mara ya pili Ruangwa Mkoani Lindi ikiwa ni mara baada ya kuzinduliwa kwake mapema mwaka huu na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kizimkazi Visiwani Zanzibar.
Waziri Mkuu amezitaja taasisi zinazohusika na agizo hilo kuwa ni pamoja na Taasisi zote zenye kuhudumia watu zaidi ya mia moja ikiwemo Majeshi mbalimbali, Shule za bweni za Binafsi na za serikali, Magereza pamoja na Wazabuni wanaopika vyakula vya zaidi ya watu 100.