Leo mjanja nimekamatika, naona kama nimetapeliwa Tsh. Milioni 1

Wakala wa benki hawaaminiki, tuwe makini hasa NMB Kuna wakala alipokea pesa kuweka kwenye akaunti ya mteja. Akampa risiti ya kielectroniki mteja kuthibitisha pesa imepokelewa benki. Baada siku kadhaa kwenda kuangalia Salio benki pesa iliyowekwa hakuna. Katika uchunguzi kumbe risiti ilikuwa feki, jina la mwekaji limekosewa, hata tarehe iliyowekwa Hela ni nyingine! LAKINI BADO WANAMLINDA WAKALA WAO. wakati Kuna kesi ya jinai iko wazi dhidi ya wakala. Nmb hawana msaada wowote.
 
Haya mambo ya bank kua na mawakala kama Mitandao ya simu NI upumbavu, bank ibaki kama bank na heshima Yake kama zaman
 
Haya mambo ya bank kua na mawakala kama Mitandao ya simu NI upumbavu, bank ibaki kama bank na heshima Yake kama zaman
 
Hii mambo wangeiondoa tuu ni utapeli
 
Mnawasingizia wakala bure, hata kwenye ATM unaweza kutowa pesa mashine isitowe pesa, ukitowa kadi akiingia mtu mwingine anazikuta pesa zimetoka.

Nilishawahi kuzikuta pesa zimetoka jamaa kaondoka lakini nilimuita aje kuchukuwa pesa zake.
Duuh sasa endapo ungeondoka nazo hizo pesa kosa lingekuwa la nani, bank au mwenye pesa?
 
Kama unaweza kwenda bank unaendaje kutoa million moja kwa wakala duh
 
Mimi ni marufuku kutoa fedha kwa kadi yangu kupitia kwa Wakala.
 
Haya mambo ya bank kua na mawakala kama Mitandao ya simu NI upumbavu, bank ibaki kama bank na heshima Yake kama zaman
Pole kaka, komaa mpaka kieleweke upate fedha yako. Ila mimi siku nakuuliza maswali kwenye uzi huu, nilikuwa nataka kukujenga ujue namna ya kukabiliana nao na ujue possible defense zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…