Leo nafanya interview Ubalozi wa Marekani kwa ajili ya viza

Leo nafanya interview Ubalozi wa Marekani kwa ajili ya viza

Huu uzi unaonyesha jinsi gani watanzania ni wanafiki na wenye roho mbaya, yaani mtu hata humjui lakini unaanza kuonyesha chuki za wazi kisa safari ya hapo marekani?
Mtu aliyefanikiwa kukuzidi hutakiwi kumponda bali unatakiwa kujifunza kutoka kwake.

Ndio maana watanzania wengi ni masikini sababu ya chuki na roho mbaya.
Hivyo vitu viko ndani kabisa ya DNA za watanzania wengi.
Mkuu uzuri nimewapuuza, wengi wameanza kufuta comments maana sijawazingati, ila nimepata kitu cha kujifunza maishani.

A Fish with his mouth closed never gets caught.
 
Mm Nina lottery yangu imbayo inanidirect interview JANUARY .ulivyopata ujuui tu umenitia nguvu mno...nawezaje kwenda kwenye interview bila ya kuwa na consent ya mzazi mmoja juu ya watoto kuruhusu kuondoka bila yeye kujua
Mungu akutimizie mahitaji yote mkuu, nakuombea
 
All the best Bro
Usijali hivi vibwengo vinavyotapatapa, sijui utumwa sijui kuna hela bongo wakati venyewe ukiviangalia ni choka mbaya mbovu... kutwa kushinda humu JF...
Na kuna kimoja kinaoneka ni kizee `kweli kipo humuJF toka 19kweusi kina wanga kwenye kila siredi...
Vita mbele, ushawaacha wala vumbi....
Ahsante kiongozi, tuombeane mema tu kaka
 
Kwanza mi nikupongeze kwa hatua uliyofikia na Mungu azidi kukuongoza na kukupa hitaji la moyo wako. Kingine achana na hao roho nyeusi na mbaya wapo kwa ajili ya kukatisha watu tamaa na kutopenda wengine wapige hatua. Kila la kheri Mkuu.
Ahsante ndugu yangu [emoji120]
 
Kama wewe ni Pro-Russia usijionyeshe hivyo katika interview
Salamu wakuu,

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu, nikihangaikia suala la kutoka huku nchini kwetu kwenda Marekani, hatimaye leo ndio siku yenyewe ya kujua mbivu na mbichi. Nitakuwa ubalozini kwa ajili ya visa interview saa tatu na dakika 45 asubuhi hii.

Namuomba sana Mwenyezi Mungu anifanikishe katika jambo hili, niombeni pia rafiki zangu, nitaleta mrejesho.

Wasalaam.
 
Mkuu OllaChuga Oc, ahsante kwa swali.

  • Visa niliyopata ni F1 - student Visa.
  • Hii ina gharama kubwa kuliko B1 na B2 ( Tourist & Business Visa).
Jumla ya gharama zote ni ngumu ku analyse
Maana si rahisi kukumbuka gharama ndogo ndogo kama, stationery, usafiri wa hapa na pale, kuandaa documents, internet nk.

Lakini gharama kubwa ambazo ni rahisi kuwa noted ni,

  • Application fee dollars 300 (kwa vyuo vitano nilivyoomba)
  • Visa Fee - Tsh 384000
  • Sevis Fee - Tsh 873000
  • Visa Insurance - 696000
  • WES - Dollars 220
  • English Proficiency Test ( Duolingo) - Dollar 45.

Maswali.

  • Kwanini ukasome USA sio Tanzania au nchi nyingine?
  • Nani atakulipia gharama za masomo na kwanini akulipie wewe na sio mwingine?
  • Sponsor wako anajishughulisha na nini?
  • Umekijuaje hicho chuo?.
  • Unatuhakikishiaje kuwa utarudi baada ya masomo?
  • Ni course gani ulizojisajili kwa ajili ya Program uliyoomba?

Baada ya hapo, YOUR VISA HAVE BEEN APPROVED.

Unapewa card ya rangi ya kijani hivi, yenye namba (namba imezungushiwa star [emoji93] nyekundu, karatasi ya kulipia visa insurance, (hapo hapo ndani kama una cash)

Cash points ni dirisha namba 4, (karibu na sehemu ya kukaa watoto).

Kila la kheri mkuu

Mungu akufanikishe upate na chaka la kazi huko huko...
 
Huyo huyo ndio kaa approve mkuu,anapenda kuwa window 3, black sura nzuri kiasi nyembamba, mwembamba pia, kama mnyarwanda hivi, namshukuru Mungu.

Window 2 alikuwa, Mzungu wa kiume, mrefu, mwenye upara mtu wa makamo.

Window 1, nilifanya fingerprint, kuna mdada mswahili,mnene kiasi, maji ya kunde,na ku submit passport na Ds 160 printed page, na picha moja yenye white background.

Window 4, nikalipia cash ( Visa Insurance) karibu na screen mwisho wa ukumbi, (Sehemu ya watoto).

Mzee baba hongera sana! Karibu USA! Wamarekani wakikuamini basi ndo imeisha hiyo. Vipi hawaja kuuliza kuhusu familia? Kama umeoa au lah?
 
Salamu wakuu,

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu, nikihangaikia suala la kutoka huku nchini kwetu kwenda Marekani, hatimaye leo ndio siku yenyewe ya kujua mbivu na mbichi. Nitakuwa ubalozini kwa ajili ya visa interview saa tatu na dakika 45 asubuhi hii.

Namuomba sana Mwenyezi Mungu anifanikishe katika jambo hili, niombeni pia rafiki zangu, nitaleta mrejesho.

Wasalaam.
Unaenda kufanya nini US mwaya? Ili nikiwa nakuombea na hilo lengo nilijumulishe kwenye maombi
 
Back
Top Bottom