Leo nafanya interview Ubalozi wa Marekani kwa ajili ya viza

Leo nafanya interview Ubalozi wa Marekani kwa ajili ya viza

All the best Bro
Usijali hivi vibwengo vinavyotapatapa, sijui utumwa sijui kuna hela bongo wakati venyewe ukiviangalia ni choka mbaya mbovu... kutwa kushinda humu JF...
Na kuna kimoja kinaoneka ni kizee `kweli kipo humuJF toka 19kweusi kina wanga kwenye kila siredi...
Vita mbele, ushawaacha wala vumbi....
Watu wamejikatia tamaa wanatakakuwakatisha tamaa na wenzao,maisha popote.
 
Moja ya kinachofurahisha Jf ni ukianzisha uzi kuhusu nchi yoyote na wachangiaji watajidai wako huko huko hata kama wengi sio kweli.

Utasikia, karibu sana huku Marekani. Mara mwingine atasema, kwa kweli kwa sisi tunaoishi hapa Landani Uingereza hilo suala tunalikubali. Na hata wapo watakaokwambia huko Bongo mnateseka sana, karibuni huku falme za kiarabu.
Mkuu hapa JF kuna watu wa kila aina,wapo waliopo Bongo na wapo waliopo nje ya Bongo,kwa Dunia ya leo ni rahisi sana kwenda nchi yeyote ile na kutafuta riziki,

So,mtu akikwambia sijui yupo nchi fulani usichukulie kua ni jambo kubwa sana,ni kawaida tu,

Karibu hapa kwa Malkia tukomae na box.
 
Salamu wakuu,

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu, nikihangaikia suala la kutoka huku nchini kwetu kwenda Marekani, hatimaye leo ndio siku yenyewe ya kujua mbivu na mbichi. Nitakuwa ubalozini kwa ajili ya visa interview saa tatu na dakika 45 asubuhi hii.

Namuomba sana Mwenyezi Mungu anifanikishe katika jambo hili, niombeni pia rafiki zangu, nitaleta mrejesho.

Wasalaam.
Ishi na watu vizuri VISA haina interview
 
Unadhani wote ambao huwa wanaokoswa huwa hawamshawishi consular officer? wakati mwingine jitahida haizidi kudra Mkuu, ndio maana namuomba Mungu.
Mkuu umetumia gharama kiasi gani Hadi hapo ulipofika? Kwenye interview uliulizwa maswali gani? Na Ni visa ipo umepata.? Kama vip tusaidie njia ulizopita na sisi wengine wenye Nia tujue pa kuanzia ...
 
Mkuu umetumia gharama kiasi gani Hadi hapo ulipofika? Kwenye interview uliulizwa maswali gani? Na Ni visa ipo umepata.? Kama vip tusaidie njia ulizopita na sisi wengine wenye Nia tujue pa kuanzia ...
Mkuu OllaChuga Oc, ahsante kwa swali.

  • Visa niliyopata ni F1 - student Visa.
  • Hii ina gharama kubwa kuliko B1 na B2 ( Tourist & Business Visa).
Jumla ya gharama zote ni ngumu ku analyse
Maana si rahisi kukumbuka gharama ndogo ndogo kama, stationery, usafiri wa hapa na pale, kuandaa documents, internet nk.

Lakini gharama kubwa ambazo ni rahisi kuwa noted ni,

  • Application fee dollars 300 (kwa vyuo vitano nilivyoomba)
  • Visa Fee - Tsh 384000
  • Sevis Fee - Tsh 873000
  • Visa Insurance - 696000
  • WES - Dollars 220
  • English Proficiency Test ( Duolingo) - Dollar 45.

Maswali.

  • Kwanini ukasome USA sio Tanzania au nchi nyingine?
  • Nani atakulipia gharama za masomo na kwanini akulipie wewe na sio mwingine?
  • Sponsor wako anajishughulisha na nini?
  • Umekijuaje hicho chuo?.
  • Unatuhakikishiaje kuwa utarudi baada ya masomo?
  • Ni course gani ulizojisajili kwa ajili ya Program uliyoomba?

Baada ya hapo, YOUR VISA HAVE BEEN APPROVED.

Unapewa card ya rangi ya kijani hivi, yenye namba (namba imezungushiwa star [emoji93] nyekundu, karatasi ya kulipia visa insurance, (hapo hapo ndani kama una cash)

Cash points ni dirisha namba 4, (karibu na sehemu ya kukaa watoto).
 
Mkuu hapa JF kuna watu wa kila aina,wapo waliopo Bongo na wapo waliopo nje ya Bongo,kwa Dunia ya leo ni rahisi sana kwenda nchi yeyote ile na kutafuta riziki,

So,mtu akikwambia sijui yupo nchi fulani usichukulie kua ni jambo kubwa sana,ni kawaida tu,

Karibu hapa kwa Malkia tukomae na box.
Uko positive sana Mkuu.
 
Watu wamejikatia tamaa wanatakakuwakatisha tamaa na wenzao,maisha popote.
Yaani kuna jamaa alianza kuniambia mambo ambayo hadi sasa hivi najiuliza kama hiyo roho anayo mtu anayekujua vizuri anakuua kabisa.

Nilichojifunza tu ni kuwa sitakuwa naweka masuala binafsi mtandaoni, ni kukaribisha roho za kishetani tu maishani.

Niliweka ili tu niweze kupata usaidizi na ushauri kutoka kwa wajuzi wa mambo, ili kupata insight ya kupambana,ila matokeo yake mtu anakuandikia.

  • UNAENDA UTUMWANI UNAONA SIFA.
  • UTAKUFA NJAA HUKO
  • UTARUDI NA MAKOBAZI HUTAFANIKIWA
  • UTARUDI KAMA ULIVYOKWENDA.
  • UNATUANDIKIA MAREKANI UNADHANI NI MBINGUNI.
  • UNATAKA SIFA, NK.
  • CHUKUA MIFAGIO YA KUZOLEA MAVI YA WAZUNGU.

Ina discourage sana, anyway tuishi.
 
Ukitaka kumpatia mzungu akupe viza yake ki rahisi,wwe cheza na documents tu, angalia ni documents gani wanazitaka kwa ajili ya safari yako kwenye web zao zinakuwepo! Mtalii ana documents zake, mfanyabiashara pia na Wanafunzi nao kuna aina ya documents zao za kiwanafunzi! Sababu ya safari yako ndiyo itakuelekeza ni documents gani ukusanye!!
Point[emoji1666]
 
Mzee baba kwanza hongera kwa uthubutu! Sema umeenda muda mbaya sana! Pale kuna consolar mmoja tu dirishani ambaye ni mdada black america. Ana roho mbaya sijawahi pata kuona yaani sijui kama utatoboa. Kulikuwa na mama wa kizungu pale sema karudi kwao yule ndo alikuwa poa sana wengi walikuwa wanapewa tu Visa. Ila yule dada wa kimatumbi ana roho ya mwendazake! Walah ukipata wewe kidume. Ukuje utuletee mrejesho hapa.
Huyo huyo ndio kaa approve mkuu,anapenda kuwa window 3, black sura nzuri kiasi nyembamba, mwembamba pia, kama mnyarwanda hivi, namshukuru Mungu.

Window 2 alikuwa, Mzungu wa kiume, mrefu, mwenye upara mtu wa makamo.

Window 1, nilifanya fingerprint, kuna mdada mswahili,mnene kiasi, maji ya kunde,na ku submit passport na Ds 160 printed page, na picha moja yenye white background.

Window 4, nikalipia cash ( Visa Insurance) karibu na screen mwisho wa ukumbi, (Sehemu ya kukaa na kucheza watoto).
 
Yaani kuna jamaa alianza kuniambia mambo ambayo hadi sasa hivi najiuliza kama hiyo roho anayo mtu anayekujua vizuri anakuua kabisa.

Nilichojifunza tu ni kuwa sitakuwa naweka masuala binafsi mtandaoni, ni kukaribisha roho za kishetani tu maishani.

Niliweka ili tu niweze kupata usaidizi na ushauri kutoka kwa wajuzi wa mambo, ili kupata insight ya kupambana,ila matokeo yake mtu anakuandikia.

  • UNAENDA UTUMWANI UNAONA SIFA.
  • UTAKUFA NJAA HUKO
  • UTARUDI NA MAKOBAZI HUTAFANIKIWA
  • UTARUDI KAMA ULIVYOKWENDA.
  • UNATUANDIKIA MAREKANI UNADHANI NI MBINGUNI.
  • UNATAKA SIFA, NK.
  • CHUKUA MIFAGIO YA KUZOLEA MAVI YA WAZUNGU.

Ina discourage sana, anyway tuishi.
Kwanza mi nikupongeze kwa hatua uliyofikia na Mungu azidi kukuongoza na kukupa hitaji la moyo wako. Kingine achana na hao roho nyeusi na mbaya wapo kwa ajili ya kukatisha watu tamaa na kutopenda wengine wapige hatua. Kila la kheri Mkuu.
 
Kila la kheri mkuu usisikilize negative comments, chukua zile positive tu alafu zifanyie kazi. Simamia lengo kuu linalokupeleka USA, kuwa na nidhamu katika mambo yote (socially, economically n.k). Pia usisahau ulipotoka, iogope kesho yako na mshirikishe Mungu katika mambo yako.
Ahsante kwa ushauri bora kabisa, Mungu akubariki sana.
 
Kila la kheri mkuu usisikilize negative comments, chukua zile positive tu alafu zifanyie kazi. Simamia lengo kuu linalokupeleka USA, kuwa na nidhamu katika mambo yote (socially, economically n.k). Pia usisahau ulipotoka, iogope kesho yako na mshirikishe Mungu katika mambo yako.
Siwazingatii mkuu, nashukuru sana.
 
Salamu wakuu,

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu, nikihangaikia suala la kutoka huku nchini kwetu kwenda Marekani, hatimaye leo ndio siku yenyewe ya kujua mbivu na mbichi. Nitakuwa ubalozini kwa ajili ya visa interview saa tatu na dakika 45 asubuhi hii.

Namuomba sana Mwenyezi Mungu anifanikishe katika jambo hili, niombeni pia rafiki zangu, nitaleta mrejesho.

Wasalaam.
Hongera Sana chief Mungu azidi kukupigania
 
Allah akujaalie kheri,



Jf kuna wachawi wengi makonkodi,

Rana yao kuona umeleta uzi wa kuomba msaada,halafu wao wanajivisha ngozi ya kondoo na Kufariji/pole nyingi za kinafiki.
Jana nimeamini humu ndani kuna watu wa ajabu mno, jambo la kuomba visa na kupata ni jambo la kawaida kabisa, me sio wa kwanza kupata wala sitakuwa wa mwisho.
Me kupata sitaziba ridhiki aliyoandikiwa mja kwa namna yoyote ile, ila jana nimeshangaa watu wananitolea hadi MATUSI na maneno ya LAANA,sijui kosa ni nini?
 
Back
Top Bottom