Leo ni miaka 20 tangu kufariki kwa Rais Mobutu Seseseko Kukungedu Wanzabanga wa Zaire ya Zamani(Congo DRC)

Leo ni miaka 20 tangu kufariki kwa Rais Mobutu Seseseko Kukungedu Wanzabanga wa Zaire ya Zamani(Congo DRC)

Hasira hii ni baada ya kuroroka shule akiwa anafanya O- levels na kwenda kwa girlfriend. Ilikuwa shule ya RC adhabu yake iliamuriwa aende jeshini baada ya mitihani ndiyo ukawa mwanzo wa kuchukia dini
Duuu
 
Habari zenu familia ya JF. Wadau mtakumbuka bara hili liliwahi kutawaliwa na viongozi wadhalimu na Madikteta wa hatari. Zaire ama Congo DRC iliwahi kutawaliwa na Mobutu seseseko 1965 hadi 17/05/1997. Alipinduliwa na Laurence kabila kwa msaada wa Banyamulenge wa Rwanda nyuma ya Kagame. Huyu bwana alikuwa anajiita pia kukungedu wa Zabanga, maana yake jogoo katikati ya majogoo. Alipora madini ya Zaire(Congo) kwa kuweka fedha za nchi kwenye akaunti yake binafisi. Alikuwa hanywi wala kuoga maji ya Congo DRC. Kulikuwa na ndege ya kuleta maji yake kila wiki kutoka Paris ufaransa. Alipinduliwa akiwa mgonjwa wa kansa na wakati vuguvugu la mapinduzi likianza alikuwa yupo ufaransa matibabuni. Alijaribu kurejea nyumani kuzima uasi lakini jeshi lake lilikuwa dhaifu sana Mbele ya Banyamulenge wa Rwanda. Baada ya muda wa takribani miezi minane ya uasi kuanzia mash mwa nchi majeshi yalifika Kinshasa huko Magharibi na kutwaa dola. Alikufa akiwa tajiri mkubwa sana. Alikufa tarehe 07/09/1997 huko Morocco na alizikwa Rabat mji mkuu wa Morocco na watu 15 tu wa familia yake baada ya serkali ya kabila kukutaa mwili wake kurejeshwa Congo kutokana na kuchukiwa sana na Wazaire/Wakongomani.
Hilo jina lake,kama hujapiga supu na chapati mbili lazima ushikwe na kizunguzungu ukimaliza kulitamka...
 
Tulio zaliwa miaka ya 90 na ushee
tunafuatilia tu kuijua Historia yake vzr

Wakongwe heshima kwenu [emoji120] [emoji120] [emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
Mobutu alipenda sana kuvaa kofia makoti, kutumia fenicha na vifaa vingi vilivyotengenezwa kwa ngozi ya chui na alijitanabaisha kuwa na roho ya chui (Leopard spirit) kwa namna alivyoogopwa na kuwadhibiti vilivyo wapinzani wake wa kisiasa, baada ya kuondolewa madarakani na Laurent Kabila, Wakongomani walimpa heshima Kabila na kumpa hadhi iitwayo IKIBINDA NKOY yaani muuaji wa chui.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wachina wamejenga reli ya Uhuru mwaka 1972 (dar to k/mposhi) kwa gharama ya dola za marekani 300 Milioni na wakati mwaka 1980 Mobutu alikuwa na fedha uswiss aluzoibia Zaire thamani ya dola billioni 5 ,maana yake angeweza kujenga reli za tazara 17. Mwafrika aliyeibia nchi yake sana halafu familia take haijapata chochote huko uswiss na hats DRC ya Leo wakifuatilia hiyo pesa mikwara mingi hadi wamechoka. Ni funzo viongozi kuiba mapesa na kuyaweka huko familia zao huambulia zero after their death. Nyerere ,Kaunda na Mobutu waliunda Mulungushi club kujadili ukombozi Wa Africa miaka ya early 70's halafu kila issue wakijadili Mobutu anaipatia siri walizoongea wafaransa Mwalimu akaona ujinga club ikafa .Fikiria na utajiri wote huo kazikwa na watu sita tu baada ya kifo chake kilichosababishwa na cancer ya prostate . Halafu ajabu miaka miwili kabla ya kifo chake alijigamba kuwa anamshukuru Mungu kwa sababu tangy azaliwe alikuwa hajaugua kiasi cha kulazwa hospitali. Alipougua hakupona. Mobutu alikuwa na vituko sana huwezi kuvimaliza labda utunge kitabu. Ila wazaire ,Leo DRC wanasema maisha chini ya Mobutu yalikuwa bora kuliko baada yake,maana uvamizi Wa baada take kuna instability na insecurity ya kutisha .aliwafukarisha ila walipata usingizi Leo vyote hawana. Hicho ndio kitendawili cha maisha Africa. Bara lenye rasilmali kuliko mabara yote ila maskini kuliko yote. Hivi sisi tutajikomboa lini? MUNGU ATUJALIE IKO SIKU. OBAMA ALISEMA AFRICA DOES NOT NEED STRONG MEN, BUT IT NEEDS STRONG INSTITUTIONS. (TAASISI IMARA SI VONGOZI IMARA ) TUTAJIENDELEZA SIO KUENDELEZWA. nimepitia tu nikachangia .wajuzi zaidi watiririke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wakati nilidhani wa Zaire walikuwa ama wajinga ama wazembe kuwa na kiongozi ka Mobutu !! Mhh nilidanganyika!!

Tanzania tuombe Mungu atunusuru na viashiria, najifunza kuwa hata ujerumani walifanya uchaguzi tena wa kidemocrasy kumpata Adolf Hitler aliyekuja kuwafanya mbaya

Cairo's
Hitler alishindwa uchaguzi

Samsung S8
 
Sky Eclat thanks kwa Maelezo yako kuhusu huyu mshenzi..Mobutu..Kiukweli huwa nikiangalie ile ya clip ya pale Patrice Lumumba alivyokamatwa na wale askari wa Mobutu na kufungwa kamba mikono nyuma huko analazimishwa kula karatasi ya speech au hotuba yake ya mwisho huku Mobutu akiaangalia kwa dharau kabla hajasafirishwa kwenda jimbo la kati la Kasai kisha kuuwawa inasikitisha sana.
Naipata wapi mkuu hiyo clip,tafadhali kama hutojali share na wengine tujue.

sent from my Infinix S2 Pro using JamiiForums mobile app
 
candidat mobiso mobutu
Alimkamata hayati Fránco Luambo Màkiadi kipindi hiko anajifanya kumkosoa kwenye nyimbo zake akamtia jela akamwambia atumie akili yake kutafuta kitu kitakachomfurahisha ili amwachie huru ndipo Frànco akamtungia hiki kibao kumfagilia,alifurahi mno akamtoa na kwenda kumfanyia Frànco party ikulu kisha kumwachia huru.

sent from my Infinix S2 Pro using JamiiForums mobile app
 
......
. Halafu ajabu miaka miwili kabla ya kifo chake alijigamba kuwa anamshukuru Mungu kwa sababu tangy azaliwe alikuwa hajaugua kiasi cha kulazwa hospitali. Alipougua hakupona. Mobutu alikuwa na vituko sana huwezi kuvimaliza labda utunge kitabu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hata Nyerere, miaka miwili kabla ya kifo chake, katika sherehe ya kuadhimisha miaka 75 ya kuzaliwa, alisema ana afya nzuri sana na kwamba ANA UHAKIKA ataishi kumuona rais wa awamu ya nne! Naye pia alipougua hakupona. Mungu hadhihakiwi!
 
Back
Top Bottom