Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

"I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Wazanzibar wanataka kufanya majaribio/Utafiti ili waone nini matokeo yake. Wanatak kutenganisha mabehewa mawili katika treni iliyo kwenye mwendo, nia na madhumuni wajue kipi kitaendelea na safari kati ya kichwa cha treni chenye mabehewa(Tanganyika) na mabehewa mawili(Zanzibar) yaliyochomolewa wakati treni inatembea.
 
Wala hujakosea huo mtihani wa 0+++=? nisingeuweza ila weye ulosoma sana.

Kati yetu sisi na wewe nani asojua haki zake maana unachozungumzia sio madai ya haki ya Wazanzibar pale inapostahili. Kama wewe kweli unaijua haki yako kwa nini usimuulize kiongozi wako Dr.Shein, Bilal Maalim Seif na wengineo ambao wananufaika na Muungano? hayo maandamano kwa nini yasielekee Ikulu kwa Dr,Shein mtake kupata majibu lakini mnaandamana kwa kuitazam Bara ambayo haipo huko. haya wee nambie kitu chochote ambacho bara inanufaika kutoka Zanzibar maanake twende kwa maelezo binafsi kusema kweli sielewi bara tunanufaika nini na muungano zaidi ya kuisoma Historia ya nchi hizi. Kwa fikra zako unafikiri hawa watu wanalipwa na Wazanzibar au unataka nasi tunaze kuuliza hawa watu tunaowalipa mabillionni wakati sii Wabara inakuwaje?.

Binafsi mkuu wangu napenda sana muungano uvunjike hata kesho maana sababu hasa ya muungano ilitokana na Zanzibar kuwa nchi ya Kikomunist. Ukomunist haupo tena kina Abraham babu wameisha kufa, hao walobakia kina Nassor Moyo na Salim hawana tena nguvu ya kurudisha Ukomunist kwanza hakuna mtu anaupenda hivyo sioni sababu ya kuendelea kuuliza Muungano.

Kifupi haki yetu haitokani na Muungano wala hakuna jambo lolote ambalo Muungano huu unatuongezea zaidi ya kuwafadhili nyie kama protectorate alipewa Sultan na waingereza. lakini waulize wazanzibar watasema Muingereza alikuwa mbaya sana wakati Sultan mwenyewe alitaka kuwa protected against Portuguese na makoloni mengineyo. Ni akili mbovu kutoelewa maana hasa kwa Wazanzibar wahamiaji ambao wamepoteza uraia huko walikotoka sasa wanatafuta nchi na makazi mapya kwa kudai Uhuru wa Sultan ulopinduliwa.

Huwezi kumnyofoa Mzanzibar kwa kabila hata kidogo isipokuwa kwa mahamiaji ambao wote wana historia ya kukimbia makwao toka hao WaOman, Washiraz, Wabarush, Wanyamwezi hadi Wangazija wote wampewa hifadhi sasa mnataka kuifanya nchi hiyo kama Wayahudi - Mna akili sana nyie!

Sisi tunaelewa matatizo yetu wala hayahusiani na kabila, jinsia wala rangi wa tu isipokuwa uongozi wa CCM ambao nyie wasomi mlipiga kura na kuchagua serikali ya mseto ambayo viongozi wake wote ni Wazanzibar bado hamtaki wakati wenzenu wanakula nchi. Na kibaya zaidi kila kiongozi wenu anapoiba huko anakuja jenga bara pengine hili mngelitazama zaidi kuliko kudai nchi wakati hao viongozi wenu wamefungua biashara na account zao bara. Nimekumaliza mkuu kaa pembeni acha wenye kuelewa maana wazungumze.
 
Let Zanzibar go!! Asante Mzee Mwanakijiji kwa darasa lako, let them decide their destiny kuliko wanavyotuandama wakati uamuzi uko mikononi mwao! Let them go. Waliamua kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa kujitangazia kuwa wao ni nchi ndani ya nchi na hakuna aliyewauliza, Walivunja katiba ya JMT ya kumpa Rais wa Zanzibar uamiri jeshi mwingine badala ya Rais wa JMT hakuna aliyewauliza!! Sasa kipi kinawashinda kuanzisha mchakato kwenye bunge lao wakaondoka? Ushauri wa Mzee Mwanakijiji ni mzuri sana kwa hatima ya Wazanzibar. Ninaunga mkono ili wachukue hata waondoke! tena ikiwezekana july 1 , 2012
 
na waende wakapewe misaada na ndugu zao wa Oman!lkn for sure watatukumbuka na ukalimu wetu!!

kupewa misaada na waoman kwani kunatatizo gani? na sifikirii kama kuna mzenji hata mmoja atakae kukumbukeni kwa
jema isipokua kwa ujambazi na kutuzalilisha.
 

Nonda, umetoka usingizini au? Uhalali au uharam au 'whatever' juu ya Muungano huu mmeshasema ktk mikutano yenu na JUMIKI, kilichopo hapa ni: LET ZANZIBARI GO!
 
prof. Idrissa Kikula amewajaza wazanzibar pale chuo cha ardhi, amepelekwa UDOM nako admistration wamejaa wazenji, kila sehemu yenye bosi mzenji basi ujue kuna harufu ya uzenji, aaaaagh!! let them go to take our positions, LET THEM GOO!
 
Kwanini bara tusiwe na referendum yetu kuhusu Muungano??
 
Inasikitisha kuona kuwa sasa tumefikia hapa, tena mara nyingi tu! Tukumbuke kwamba sasa hivi kuna wale ambao wanachekelea mdahalo huu, wanajua fika kuwa tumefika wanapotaka tufike.

Nitasisitiza kuwa muungano wowote ule ambao uko nje na matakwa ya mabepari na watwana wa magharibi(kama wapo) basi ni karaha kwao. Ni mtazamo wangu.


Muungano lazima uudumishwe.
 
 
haya mbona unayaandika hapa tu huwezi weka muhadhara ukawaambia watu haya ??? unakimbilia JF na Magazetini tu !!!

Mbona waliokuwemo katika system tokea kuundwa Huo Muungano , wengine wahai wanasema vyengine???

Unafikri ana ubavu huo?
 
Unafikri ana ubavu huo?

kweli unafikiri kuna yeyote anayeweza kujadiliana na mimi kwa hao jamaa? zaidi itakuwa ni yale yale tu "ooh wewe Mkristu huelewi!". Hakuna size yangu kule. Siyo kwenye hili aisee.
 
Tuliwapenda sana kwa miaka 46 lakini naona hawapendeki! potelea mbali, hakuna anayekataa kuwapatia talaka wanayoitaka!!! Wanachotakiwa kufanya ni kuomba talaka yao, waende! Let them go. Tumechoka na kelele zao kila siku.
 
Nonda, umetoka usingizini au? Uhalali au uharam au 'whatever' juu ya Muungano huu mmeshasema ktk mikutano yenu na JUMIKI, kilichopo hapa ni: LET ZANZIBARI GO!
Zinedine
Bado nimelala..niko kwenye ndoto kuwa niko katika mikutano yetu na JUMIKI.:confused2:


Mkuu kama umesoma mchango wangu na kuelewa nimefanya masahihisho kidogo juu ya matumizi ya majina Tanzania na bara katika mchango wa Pasco.

Unasema:Kilichopo hapa ni :Let ZANZIBARI GO!

Why don't we let Zanzibar go?

Haiwezekani baada ya gazabu, hasira tulizonazo kuwaambia "pack and go!"

I would rather have the courage to say "GO!"

Kwa sababu gani hatu"opt" hii option? Hakuna mwenye uwezo/ujasiri katika viongozi,wabunge ,watendaji wa Tanganyika wa kusema" Zanzibar go!"

Nani ametoka usingizini? Zinadine au Nonda?

Kwa bahati mbaya Mijadala ya sasa imeanza/imeanzishwa juu ya dhana kuwa UAMSHO(waislamu wa Zanzibar) wamechoma makanisa. This was a false start kwa mijadala hii. Tumeingia mtego wa Magamba.
 
Nonda, mkuu ebu tazama picha hiyo hapo juu kisha utuambie kama kweli hao ni Magamba?.. Hawa ni wananchi wenye hasira na wenye kuitaka haki yao kwa nini nasi tusiwasikilize ikiwa tunawasikia watu wa Palestine au Burma..

Maadam tunawapa muda tosha ifikapo July mosi 2014 wawe tayari wameisha fanya maamuzi ya kura za maoni basi hatuna sababu ya kuendelea kulonga. Kazi kwao, badala ya kuandamana walivamie bunge lao kesho na kuomba kupiga kura za maoni kama walivyofanya mwaka 2010.

Viongozi wa serikali ya mseto kutoka CUF na CCM Zanzibar (baraza la Mapinduzi) wapeni wananchi wenu haki yao ya msingi, tena kama ikiwezekana nasi bara tuandamane kuwaunga mkono Wazanzibar ili wapewe ruksa ya haki yao kudai kuondoka ktk Muungano ifikapo July 1 2014.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…