Licha ya maongezi ya kwenye simu baina ya Rais Uhuru na Magufuli, upimaji lazima ubaki pale pale

Licha ya maongezi ya kwenye simu baina ya Rais Uhuru na Magufuli, upimaji lazima ubaki pale pale

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Kwanza naanza kwa kutanguliza shukrani kwa Watanzania kukubali kuiga Wakenya kwenye zoezi la kupima kila dereva anayeingia, hiyo sasa imewezesha sote tuongee lugha moja, pima huko na sisi tupime huku, hapo tunakua na uhakika wa usalama wa kiafya kwa watu wetu.

Ingewagharimu sana kama mngeendelea kuruhusu Wakenya walioathirika kuingia huko na kujiachia full bata. Ninachokifahamu ni kwamba madereva wote ukanda huu wanaambukizana kwa kasi maana wengi hulala kwenye magesti uchwara kwa vitanda ambavyo malazi hufuliwa hata mara moja kwa wiki, na huingia wakiwa walevi bila kujali nani kalala humo jana, hivyo lazima tutegemee mamia ya madereva kuathirika.

Kile ambacho labda kifanyike, wataalam wa nchi zote mbili washirikiane na kukubaliana aina gani ya mashini zitumike, kila anayekuja anapimwa, huku zoezi likishuhudiwa na wataalam wa pande zote, ila wa Tanzania akigunduliwa ana kirusi, anapokezwa kwenye mamlaka husika kimya kimya maana hao bado wanahangaika kuweka siri na kuendelea kuaminisha umma kwamba hamna tena corona kwao, hivyo kelele zote hizi zinatokana na hili la Kenya kutaja idadi ya madereva wa Tanzania walioathirika.

Sasa ili kupunguza makelele, upande wao ibaki siri, wawe wanataja kama nilivyoona juzi wakifanya, walitumia maneno kama "raia wa nchi ambayo haitatajwa kwa sasa", ila kwa upande wetu watajwe kabisa idadi yao wangapi waliogunduliwa.
Hapo nina uhakika tutaendana vizuri sana tena tutaongea lugha moja na kuendelea kuitana pumba za "undugu".
 
"Kukubali kuiga wakenya kwenye zoezi la kupima"...

Unaweza kuthibitisha tumewaiga
 
Eti tumewaiga daah aisee wakenya hadi kupima corona mnasingizia tumewaiga

Je na sie tuwaige kuwapakazia madereva wenu corona? Maana mtz akija kenya vipimo vinaonyesha anayo ila mkenya aliyekaa tz kwa wiki kadhaa kipimo kinaonyesha hana corona
 
Hii issue itakuwa resolved tu,pale wakakubaliana kuwa na one stop centre ya kupima pale mipakani,kila upande unakuwa na wawakulishi na wanapima kwa pamoja
 
Hii issue itakuwa resolved tu,pale wakakubaliana kuwa na one stop centre ya kupima pale mipakani,kila upande unakuwa na wawakulishi na wanapima kwa pamoja
Maafisa kutoka GOK-MOH wamekuwa wakifanya hilo hapo OSBP tangu mwanzoni na hadi sasa hivi bado wanaendelea na shughuli yenyewe.
 
Eti tumewaiga daah aisee wakenya hadi kupima corona mnasingizia tumewaiga

Je na sie tuwaige kuwapakazia madereva wenu corona? Maana mtz akija kenya vipimo vinaonyesha anayo ila mkenya aliyekaa tz kwa wiki kadhaa kipimo kinaonyesha hana corona
FALSE! Madereva wa Kenya watokao TZ pia wanapatikana na Corona. Of the 214 tests done at the border, around 180 were TZians, around 30 Kenyans and the rest other nationalities. Itabidi muache kukurupuka tuu.

Halafu pia ni kweli mmetuiga kwani awali mlisitisha kufanya covid19 tests kwa wananchi na pia Madereva, ila sasa lisilo na budi hubidi.
 
Maafisa kutoka GOK-MOH wamekuwa wakifanya hilo hapo OSBP tangu mwanzoni na hadi sasa hivi bado wanaendelea na shughuli yenyewe.
Hivi kwanini Uhuru aliamua kuomba msamaha?, Mimi ninadhani kitendo cha Tanzania kuzuia malori ya Kenya kuingia Tanzania kingesaidia zaidi kupunguza maambukizi huko Kenya, vipi tena Uhuru anataka hayo malori yaruhusiwe kuja Tanzania?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu tuone kama mtaendelea na kamchezo kenu ka kuitaja taja Tanzania kwenye habari zenu za idadi ya maambukizi ya kila siku. Mkome kufikiri ni wajanja nyie nyanag'au.
Aisee, kwahivyo mnaona aibu kutangaziwa waliopatikana +ve? Kisa nini, mbona nchini Kenya wizara ya afya huwa inatutangazia kila siku? Haya basi, jana jioni wageni 182 wamerejeshwa Tanzania baada ya kupatina kwamba wana virusi vya Corona. Kenya sends back 182 foreigners with virus to Tanzania
 
FALSE! Madereva wa Kenya watokao TZ pia wanapatikana na Corona. Of the 214 tests done at the border, around 180 were TZians, around 30 Kenyans and the rest other nationalities. Itabidi muache kukurupuka tuu.

Halafu pia ni kweli mmetuiga kwani awali mlisitisha kufanya covid19 tests kwa wananchi na pia Madereva, ila sasa lisilo na budi hubidi.
Iweje rais wenu aliomba msamaha ili malori yenu yaendelee kuja Tanzania?
 
Mpaka ufungwe jamani mbaka kieleweke wakilia sana tunawauzia Unga sio mahindi hela si wanazo sasa... Naona mmepewa $ Billioni 1 nyengine na WB sio?...
Hahaha ndoto za alinacha 😂. Hakutatokea siku Kenya kununua UNGA kutoka nje ya nchi. TZ, UG au kwengineko. Halafu ujue kwamba Kenya ukosefu wa chakula/nafaka sio jinsi mlivyokaririshwa. Isitoshe, nyinyi wenyewe(wakulima) ndio mtaumia mkitelekeza soko la Kenya.
 
Hii issue itakuwa resolved tu,pale wakakubaliana kuwa na one stop centre ya kupima pale mipakani,kila upande unakuwa na wawakulishi na wanapima kwa pamoja

Ndicho nimekisema kama umesoma nilichoandika, timu iundwe moja ya wataalam pande zote mbili, wakubaliane mashini ipi ya kutumia. Sema kwa Tanzania kwa vile mnataka siri, kila akigunduliwa Mtanzania inapigwa kimya anarejeshwa kwao.
 
Ndicho nimekisema kama umesoma nilichoandika, timu iundwe moja ya wataalam pande zote mbili, wakubaliane mashini ipi ya kutumia. Sema kwa Tanzania kwa vile mnataka siri, kila akigunduliwa Mtanzania inapigwa kimya anarejeshwa kwao.
Njia rahisi ya kuondoa hizi longolongo ni kama ile aliyopendekeza mkuu wa mkoa wa Tanga, kwamba hakuna kuruhusu malori ya Tanzania wa Kenya, ninashanga Uhuru Kenyatta anaomba msamaha ili malori yaruhusiwe, hii ni dalili kwamba Kenya haiwezi kuishi bila Tanzania, wakati ninyi mnasisitiza kupima, sisi tunasisitiza kufunga kabisa mipaka, tuone nani ni kidume kati ya Kenya na Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msamaha aliouomba ni upi? Unayo evidence ama ni kukurupuka kama kawaida? Mbona bado mpaka UMEFUNGWA? Mbona bado madereva wanaotoka kwenu wamepanga foleni ndefu kungoja kupimwa? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahaha, Uhuru alipiga simu haraka sana kuomba msamaha, Magufuli ametoa maelekezo, yakitekelezwa ndio mtaruhusiwa kupitisha malori yenu. Ninyi hamna ubavu wa kupambana na Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie ndio mnaokurupuka kutwa matakoni mwa watanzania. Kila day mnaibuka na habari za madereva wa kitz .Mmelazimisha lockdown weee mmeshindwa wakati huo huo huko kwenu hamna lockdown bali usaniitl mtupu

Bwahahahaha so dunia nzima au afrika nzima kenya ndio ilikua inapima corona pekee mpaka tz tuwaige aiseee bora corona haikuanzia kenya mkaanza kujimwambafai tumewaiga kuumwa
FALSE! Madereva wa Kenya watokao TZ pia wanapatikana na Corona. Of the 214 tests done at the border, around 180 were TZians, around 30 Kenyans and the rest other nationalities. Itabidi muache kukurupuka tuu.

Halafu pia ni kweli mmetuiga kwani awali mlisitisha kufanya covid19 tests kwa wananchi na pia Madereva, ila sasa lisilo na budi hubidi.
 
Wana maneno mengi vitendo haba. Kila day Tanzania inawagaragaza vibaya. Hadi covid wakenya wakataka iwe yao na misaada yote iishie kwao
Hahahaha, Uhuru alipiga simu haraka sana kuomba msamaha, Magufuli ametoa maelekezo, yakitekelezwa ndio mtaruhusiwa kupitisha malori yenu. Ninyi hamna ubavu wa kupambana na Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom