Licha ya Tanzania kuwa na ndege 11, Rais Samia anatumia ndege za abiria

Licha ya Tanzania kuwa na ndege 11, Rais Samia anatumia ndege za abiria

Ze Bulldozer

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2020
Posts
1,070
Reaction score
568
Rais Hakainde Hichilema kutoka Zambia na Rais Samia Suluhu Hassan kutoka Tanzania ndio marais pekee kutoka Africa wanaokwenda ng'ambo kwa kutumia ndege za abiria|Umma.

Rais Samia Suluhu wa Tanzania pamoja na kuwa na ndege mpya 11 zikiwemo zenye uwezo wa kuruka moja kwa moja kwa zaidi ya masaa 20 angani bado ameendelea kutumia Usafiri wa abiria|umma.

Wakati tukimngonjea pale JNIA akitokea Glasgow Scotland alikokwenda kutuwakilisha kwenye mkutano wa 26 wa Kujadili kuhusu mabadiliko ya tabianchii ( COP26 ) unaoendelea hadi trh 12|11|2021 tulidhani angeshuka pengine na lile Boing 787-800 letu.

Maajabu ya kutia moyo ni kwamba Rais wetu akiwa na Ujumbe wake wa watu wachache alishuka kwenye ndege ya abiri mali ya sherika la ndege la Emirates (Emirates Airline).

Ujumbe Wangu nataka Watanzania tuelewe mama huyu hayupo kufanya Starehe yeyote, Mama huyu yuko kuwapambania Wananchi wake tu ndio maana hataki makuu anaacha ndege mpya 11 zimepaki anakwenda kurukia Emirates wakati huo huo wenzake wanakwenda na ndege zao binafsi,

Mfano, Rais Samia Suluhu katika Safaris ile ya New York kwenye UNGA Rais mwenzake toka Africa -Angola alitumia Jumla ya TZS 9.5BL licha ya nchi yake kuwa na deni kubwa kiasi cha kutaka kufilisiwa na China,Huyu ndio Samia Suluhu Rais Mzalendo wa kweli tuliyepewa na Mungu wetu,

<<< Uzalendo ni huu angalia >>>


 
Mkuu umeongea ukweli kuhusu nia na malengo mazuri aliyonayo raisi wetu kwa sisi wananchi wake. Ila ngoja lile genge la yule muhutu wa rwanda lije lichafue uzi wako.
 
Rais Hakainde Hichilema kutoka Zambia na Rais Samia Suluhu Hassan kutoka Tanzania ndio marais pekee kutoka Africa wanaokwenda ng'ambo kwa kutumia ndege za abiria|Umm...
Daaah,

Ila huyu mama kuna kitu ndani yake, Unaweza kuacha Boing limepaki ukarukie Emirates na wapiganaji, Kweli huu ndio Uzalendo
 
Hii nayo ni sifa ya kipekee!!!![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sisi kamaTaifa hatuwezi kuendelea kupiganiwa na mtu mmoja huku tukiwa tuna nguvu za kujipigania wenyewe, kupitia uwezeshwaji mdogo tu kutoka seriaklini na pia kutoka kwa mabenki yetu ya ndani, kupunguza riba zaidi na masharti ya mikopo.

Pia tuna hamu kubwa ya kuona ile Rasimu yetu ya Katiba, ikipitishwa na kuwa Katiba kamili, kuliko huko kupiganiwa kwa kupitia misaada na mikopo yenye masharti magumu kutoka kwa Mabeberu.
 
Je! Rais wetu SSH alikwenda huko ughaibuni na Mzee wetu, the First Gentleman?

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
Hili swali nimekua nikijiuliza sana kwamba,marais wakike ni ubinafsi ama ni kitu gani mbona hatumwoni huyu baba kwenye mishemishe za mheshimiwa,ili khali marais wa kiume tuliona wakati mwingine wakiongozana na wake zao.
 
Back
Top Bottom