Nimejaribu kuvaa viatu vyake vimenibanaHii ni Kali kuliko zoteee[emoji23][emoji23][emoji23] ,pole sana kamanda ,nimecheka sanaaa
Mkuu chukua hiiKuna rafiki yangu wa kike (Sio Girlfriend) aliweka whtsp status ya rafiki yake mwanamke aliyevaa kimini na wkt hana ushepu, sasa mimi nikaichukua ile nikaituma ktk group la jamaa wa ofisini kulikuwa na mada kuhusu mavazi ya wanawake huku mie nikimtolea mfano huyo mdada pasipo kufahamu kuwa ni mke wa staff mwenzetu na yeye yupo ktk group. Mara paap naona washikaji wananitumia sms inbox kuwa kaka unaharibu, umepatwa na nn mbona unatolea mfano mke wa Flani amekukosea nini au umelewa upo vyombo hapo ulipo? Kumbe masikini ya Mungu mimi sikuwa nafahamu, jamaa naye akaja inbox akaniambia "Ahsante kaka nashukuru sana". Nilijisikia vibaya kila nikijaribu kum-please kuwa sikuwa najua jamaa hapokei simu wala hajibu sms, na kipindi kile whatsapp haikuwa na feature ya kudelete sms kama ilivyo sasa. Sitakuja sahau aisee hilo jambo..
Mwaka flani hv nimeenda zangu maeneo kumtembelea sister,siku hyo sister kasafiri nimebaki na anko 2,ilikuwa wikiend nikaenda zangu kucheki mpira narudi zangu mida kama ya saa 5 hv uck,narudi geti limefungwa,namgongea anko nae kalala kinouma nimekaa kama nusu SAA hv nagonga hakuna kufungua,nikaamua kufungua dirisha nipitie hapo,vile vidirisha vya zamani vinakuwa na nondo katikati aisee,so nikapiga hesabu nikaona kupita na nguo haiwezekani so nikavua nguo nikaziingiza ndani nikabaki na chupi 2 nikajua si napita fasta,
Ile kuanza kupitisha kichwa hakipiti kumbe ni padogo ,kasheshe likaanzia hapo,hangaika wapi, hangaika wapi nikaona jau hili,nikamkumbuka jamaa yangu anakaa mtaa wa pili,ikabidi nitoke pale kwa spidi kali nipo na kichupi 2 nakatiza mtaaan,wikiendi ile mitaa watu wanacjelewa sana kulala so nilikutana na watu wanacheka walijua nimetoka kufumaniwa so nakimbia soo,ile nafika kwa jamaa,jamaa kafungua kunikuta vile anacheka kishenzi,kwa soo lile sikukaa sana ilibidi nirudi home 2
Hahahahaaaaaa jamaa umenichekesha kinoma.Niliwahi kushikwa tumbo la kuharisha ukweni
Ilikuwa hivi:
Kuna binti nkikuwaga namnyandua enzi hizo na alikuwaga ananisaidia mambo mengi sana miaka hiyo maana nilikuwa na maisha magumu kiaina
Sasa mahusiano yetu yakafikia binti kutaka akanitambulishe kwao ilikuwa wilaya tofauti.
Siku ikafika mwanaume huyo mpaka ukweni nafika naandaliwa msosi tukaanza kula
Kosa kubwa walilofanya kunipa maji ya kunywa yaliyowekwa water guard (enzi hizo ilikuwa dawa maarufu ya kuweka kwenye maji ya kunywa) sasa hiyo kitu huwa sipatani nayo nilipokunywa tu hayo maji nikasikia tumbo linaunguruma kama nimemeza chura wa bwawani!
Kilichofuata ni maumivu makali ya tumbo yakiambatana na kichefuchefu cha makalio(kubanwa kunya)
Nilijizuia nikashindwa kabisa ikabidi nimuombe binti anielekeze chooni ikabidi kustop kula nikanawa mikono haraka bahati nzuri sebureni tulikuwa tumeachwa watatu tu ndo tunakula nilikuwa mimi, binti na kidogo chao cha kiume hivyo tulitoka na binti ili anipeleke chooni ilikuwa choo cha uani.
Ile tunatoka nje ya nyumba kufika kule uani ambako ndiko kuna choo na vyumba vingine vya wapangaji tukakuta mama mkwe amekaa na wanawake wengine kama wanne nahisi ni wapangaji halafu walikuwepo na mabinti wengine mashemeji kama watatu yaani mbaya zaidi wamekaa pale pale karibu na mlango wa kuingia chooni wanasukana hapo na kupiga umbea waliponiona walijikausha nikapita kuingia chooni huku binti akibaki nao hapo nje ile nafunga mlango wa chooni tu nilisikia vicheko vya kisirisiri kwa nje nikajipa moyo kwamba ntavumilia tu hii aibu maana ishatokea
Mbaya zaidi ile nachuchumaa tu chooni niliharisha kinoma kiasi kwamba yalikuwa kama yanamwagika maji huku zinasikika sauti za mripuko kama radi nilijaribu kujibana nizuie hizo sauti za kujamba lakini zikawa kama ndo naongeza wakati huo huko nje nasikia vicheko vya wazi wazi kabisa iliniuma sana nilitamani nitokee juu ya paa nipotee kabisa eneo lile lakn haikuwezekana.
Nilimaliza kujisaidia naanza kujisafisha kulikuwa na maji kidogo kwenye ndoo yakaisha nikajaribu kufungulia bomba maji hayatoki nahisi yalikuwa yamekatika halafu hapo sijamwaga maji kwenye sinki la choo kinyesi kimejaa na kutapakaa kwenye sinki ikabidi nijitoe aibu nivae tu nitoke nikamuite binti pembeni nimwambie maji chooni hakuna ikiwezekana anisaidie kwenda kumwaga maji kabla hawajastukia lakn cha ajabu ile natoka tu nawakuta wale wadada wamekaa ila mamkwe na mchumba wangu sikuwakuta nahisi walikuwa ndani ikabidi nizame ndani huku nyuma bado nasikia vicheko watu wanacheka mpaka wanaanguka chini!
Nafika ndani namkuta yule dogo bado anakula nikamuuliza dadake yuko wapi akasema ameenda dukani mama mkwe naye sikumuona nahisi alijifungia chumbani kwa aibu!
Nikarudi pale uani ili nijitoe ufahamu niwaombe wanisaidie maji lakn kabla sijafanya hivyo namuona binti mmoja kati ya wale mashemeji zangu anatokea mule chooni na ndoo mkononi akapitiliza ndani akachota maji na kurudi chooni akaanza kusafisha chooni!
Ile kitendo ilinifanya nijiskie aibu ambayo sijawahi kuona!!!!
Kufupisha story nilijikuta nje ya geti ambako nilimuona mchumba wangu anarudi na kibahasha cha dawa mkononi akanipa eti alienda duka la dawa kuninunulia vidonge vya kuzuia kuharisha nilivimeza pale pale mlangoni nikaondoka sikutaka tena kurudi ndani maana sio kwa aibu ile.
LLBUnasoma nini?
Nawe ushamba ulikuzidi,tabia za kikeKuna rafiki yangu wa kike (Sio Girlfriend) aliweka whtsp status ya rafiki yake mwanamke aliyevaa kimini na wkt hana ushepu, sasa mimi nikaichukua ile nikaituma ktk group la jamaa wa ofisini kulikuwa na mada kuhusu mavazi ya wanawake huku mie nikimtolea mfano huyo mdada pasipo kufahamu kuwa ni mke wa staff mwenzetu na yeye yupo ktk group. Mara paap naona washikaji wananitumia sms inbox kuwa kaka unaharibu, umepatwa na nn mbona unatolea mfano mke wa Flani amekukosea nini au umelewa upo vyombo hapo ulipo? Kumbe masikini ya Mungu mimi sikuwa nafahamu, jamaa naye akaja inbox akaniambia "Ahsante kaka nashukuru sana". Nilijisikia vibaya kila nikijaribu kum-please kuwa sikuwa najua jamaa hapokei simu wala hajibu sms, na kipindi kile whatsapp haikuwa na feature ya kudelete sms kama ilivyo sasa. Sitakuja sahau aisee hilo jambo..
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]dah mkuu pole sana,nadhani mimi ningefariki siku hiyo hiyo,unajua watu walichokuwa wanakuwazia hakikuwa kizuri .Sitasahau nikiwa Mpanda soko Kubwa, chizi wa Kike akanikomalia huku ananifuata kwa nyuma kuwa wewe Bwana wangu. Mbona unajifanya hunijuinsasa wakati huwa unanilala.
Aiseee, sijawahi fedheheka kama siku ile. Simjui yule Dada kwa kuwa mimi mweupe ndio akanikomalia kwa maana nasikia vichaa huwa hawaendani na watu weupe.
😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂Nikiwa chuo iringa nakaa mbali afu chuo kipo town
So lazma ntumie usafiri . Siku moja nikiwa nimevaa suluari modo Ime tight hatari,
Nikapanda zang bajaji , nmeshuka nikapiga hatua mbili hv nakuta Kila mtu Kama ananiangalia hiv , afu Kama upepo unaingia ndan HV ,
Kucheki suluari imetatuka kweny msamba ,
Asee ilibidi nipand bajaj nyingn fasta kurudi gheto,,
Hahaa SAUT moja....Nyamalango-maduka9...we wapi
Waliona wameajiri kibaka[emoji1787][emoji1787]We boya sana yani unakata mikucha yako na nail cutter za mtu mwingine magonjwa yote haya.
Mimi ilinikuta miaka kadhaa iliyopita ndio nimeajiriwa kwenye kampuni flani hapa Dar. Jioni nimekaa na mabosi zangu kupata wine kidogo na kujuana vizuri, tulikuwa tumeweka simu zetu mezani, bahati mbaya nikachukua simu ya bosi mmoja nikatia mfukoni nikijua ni yangu. Mara kidogo jamaa akaanza kuulizia simu yake mimi nimetulia tu nikiamini iliyopo mfukoni ni yangu.
Dah ilivyobipiwa ikaita kwangu halafu hata hawakunipa nafasi ya kujieleza zaidi ya kila mtu kutunza simu yake kwa umakini, nilijisikia fedheha haielezeki.
Dah, hii ngumu sana hapo lazima ulionekana mwizi / una nia ovuWe boya sana yani unakata mikucha yako na nail cutter za mtu mwingine magonjwa yote haya.
Mimi ilinikuta miaka kadhaa iliyopita ndio nimeajiriwa kwenye kampuni flani hapa Dar. Jioni nimekaa na mabosi zangu kupata wine kidogo na kujuana vizuri, tulikuwa tumeweka simu zetu mezani, bahati mbaya nikachukua simu ya bosi mmoja nikatia mfukoni nikijua ni yangu. Mara kidogo jamaa akaanza kuulizia simu yake mimi nimetulia tu nikiamini iliyopo mfukoni ni yangu.
Dah ilivyobipiwa ikaita kwangu halafu hata hawakunipa nafasi ya kujieleza zaidi ya kila mtu kutunza simu yake kwa umakini, nilijisikia fedheha haielezeki.
Shukuru Mungu upo hai kaka na labda hiyo mitaa sio ya matukio sana, tungeshakusahauNiliwahi kwenda migahawa koko maeneo flani hivi nikakuta contena la kunawia mikono wameweka pembeni na nyumba ya mtu halafu mgahawa wenyewe uko mbali kidogo, mimi niliponawa nikaingia nyumba iliyokuwa jirani nikidhani ndio mgahawa wenyewe kumbe nimeingia kwenye geto la Mmama flani hivi.
Sasa muda naingia alikuwa bize anakula halafu kageukia upande wa pili wala hakusikia vishindo muda naingia kwa akili za kitoto nilipogundua kuwa nimeingia kusipo nikapata akili ya kutoka kimyakimya tena...! Kumbe muda natoka ndani yule mama akashtuka nikajifanya kuchomoka mule ndani kwa haraka ndio akaniitia mwizi..mwizi...mwizi asee nikajifanya kukimbia nikaishia mikononi mwa wananchi wenye hasira kali aisee sitakaa nisahau kilichonipata yaani kuna watu bongo hii hata ukiwa unatoa maelezo hawayazingatii wao ni kupiga tu na kutafuta petroli....
Hadi leo nikikuta mwizi anapigwa huwa napenda kusikiliza maelezo yake kama yanaleta logic....Maana ningechomwa moto na sijawahi kuiba wala kutapeli cha mtu!
Ni kweli alikuwa na roho mbaya au ulikuwa unamkandia tu?Mimi nilikuwa namsema mshikaji kwamba ana roho mbaya kumbe yupo hapo kwenye group, daah nilijisikia vibaya kishenzi
Sidhani kama kutokujua ku scan ni aibu sema ulijishtukia tu, hii ilinikuta pia kigamboni pale kivukoni na zile kadi zao ila mi niliuliza na hakuna aliyenishangaaFedheha nnazozipataga mimi ni ndogo ndogo kwenye matumizi ya vyombo vya mzungu.
Kuna mabomba ufunguaji wake mrahisi ila kama hujui hangaika sana afu anakuja mtu tu anakufungulia kirahisi[emoji23]
Siku ya kwanza kupanda mwendokasi sijui kuscan ticket aibu tupu
Siku ya kwanza kutumia lift[emoji3] nk
Yani vitu vya aina hio ndo aibu nnazopataga
Bro code 101 Never trust a fart.[emoji23] [emoji23] Pole mkuu.
Mwenzio nilikuwa naendesha kikao. Tumbo limebana hatari. Nikaamua nitoe kaushuzi ka kimyakimya kurekebisha hali.
Lahaulah! Ilitoka harufu ambayo sijawahi kuinusa maisha yangu yote na ofisi nzima hakuna aliyevumilia kukaa hata mimi mwenyewe.
Aisee, nilitamani nisirudi tena kwenye kikao. Lakini mimi ndo kiongozi pale kazini. Nilirudi tu.
Aibu!
Nipe story pmBro code 101 Never trust a fart.