Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

We boya sana yani unakata mikucha yako na nail cutter za mtu mwingine magonjwa yote haya.

Mimi ilinikuta miaka kadhaa iliyopita ndio nimeajiriwa kwenye kampuni flani hapa dar.jioni nimekaa na mabosi zangu kupata wine kidogo na kujuana vizuri.tulikua tumeweka simu zetu mezani,bahati mbaya nikachukua simu ya bosi mmoja nikatia mfukoni nikijua ni yangu .mara kidogo jamaa akaanza kuulizi simu yake mimi nimetulia tu nikiamini iliyopo mfukoni ni yangu.

Dah ilivyobipiwa ikaita kwangu halafu hata hawakunipa nafasi ya kujieleza zaidi ya kila mtu kutunza simu yake kwa umakini,nilijisikia fedheha haielezeki
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119]
 
Kuna siku ndo nimetoka kireport kazini kama siku mbili 3 hivi nmebaki ofisini mwenyewe si nikaachia hewa chafu pale mara paap Boss huyu hapa ofisi inanuka balaa hakika nilipata fedhehea ya kufa mtu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119]
 
ilitokea nimekuja dar kwa ndugu yangu aliepanga chumba maeneo ya uswahilini temeke,nyumba ilikua na vijana na mama mwenye watoto wa kike pale,sasa ilitokea siku moja usiku nimeenda kuoga mida ya usiku nikaona sio mbaya nitoe na haja kubwa kabisa,kumbe nimemaliza kujisaidia na maji nimemwaga yalikua machache,asubuh si ndo akaja mwenye zamu kufagia choo akaukatana nayo,kila akimwagia maji mzigo hausogei mbele ikabid aulize tu ni nan alikua wa mwisho si ndo nikatajwa mm..daaahh ilikua fedhea kwa watoto wa kike wale maana mama alikazia neno 'Alf yule kaka ni mwembamba ila ana mavi magumuuuuu' sikumsalimia mpk namaliza likizo naondoka
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119]
 
Bro wangu ameoa sasa.Alikuwa na demu lake lina msambwanda kinyama.Basi lilivyosikia jamaa anaoa alienda kumfanyia fujo home wote tulikuwepo.Likaanza kubwatuka kuwa jamaa kamla ndogo miaka mingi kwa nini amuoi yeye.Tuliona noma sana.Washua wananiuliza kweli?Nikawaambia mkamuulize bro.Noma sana.
Aisee noma sana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Bora alifukua tope
 
Nakumbuka mwaka 2004 Mimi bishoo kinoma sasa kipindi kile zilikuwa zimetoka jinsi Fulani tulikuwa tunaita mikasi,maana zilikuwa nyeupe mixed mikasi mikasi rangi nyeusi!,sasa bana dukani zilikuwa bei juu kinoma,Mara kuna mshkaji wangu mmoja hivi nilikuwa na rap nae kipindi hicho akaniambia anauza jinsi hiyo mikasi kwa 7000tsh nikaona kama ndoto vile sikuamini ,nikachomoa fasta pesa ya ada ambayo nilikuwa natakiwe nilipe kesho yake nikampa jamaa 7000tsh akaniletea ukali,fasta Mzee mzima nikaingia kuoga kwanza nikatupia vitu vikali na ile jinsi nikaanza kunesa kitaani sikufika hata mbali ni kama mita 200 tu kutoka home mama mmoja alikuwa na wanae kama wa nne hivi wakubwa kimtindo akanisimamisha,nilivyosimama baada ya salamu akaniambia mwanangu samahani Nina wasiwasi na jinsi uliyovaa ni ya mwanangu huwa anaibiwa sana jinsi kwahiyo nikaamua nikimnunulia mpya huwa kuna sehemu naweka alama,kwahiyo kama huamini alama ni Fulani na nimeweka sehemu Fulani tukikuta sio usijali mwanangu nakurudishia jeans yako!
Kwa vile home ilikuwa ni mita 200 tu kutoka pale hao mpaka ghetto nikavua suruali tukakuta ni kweli zile alama zipo,nikamwambia mama Mimi nimeuziwa na MTU Fulani na bahati nzuri ni jirani yake alikuwa anamjua vizuri, Mzee nikaachia jeans kesho yake nikamtokea mshkaji aliyeniuzia kimya kimya ghettoni kwake nikamweleza kisanga jamaa kumbe ndio ilikuwa ndio zake bila hiyana akanipa jinsi nyingine sikuipenda sana lkn nilikuwa sina namna na akanisisitizia hiyo sio ya wizi Mimi nikasepa zangu na urafiki ukaishia hapo
 
Bro wangu ameoa sasa.Alikuwa na demu lake lina msambwanda kinyama.Basi lilivyosikia jamaa anaoa alienda kumfanyia fujo home wote tulikuwepo.Likaanza kubwatuka kuwa jamaa kamla ndogo miaka mingi kwa nini amuoi yeye.Tuliona noma sana.Washua wananiuliza kweli?Nikawaambia mkamuulize bro.Noma sana.
nakuja PM unipe number yake
 
Nikiwa form 2 kwenye miaka ya 2000 kuendelea..nikiwa kama kijana sharp kabisa kwenye extended family yetu hapa Dar..Mshua akanipa pesa shilingi milioni moja za ujenzi nipeleke moshi kwa bibi yangu mlokole asilimia (100%)Basi laki tano nikaweka mguu wa kushoto tano nyingine mguu wa kulia...
Nikapewa ticket ya Bus moja nakumbuka likiitwa Amazon na fedha taslimu elfu 70 nauli ya kurudi na pesa ya kijikimu na zawadi za njiani kupeleka kwa bibi na simu ndogo ya kufunua aina ya Bird kwa ajili ya mawasiliano.
Nikatoka zangu kinondoni studio mpaka ubungo terminal, bus nikaliona nikaenda kwenye kibanda nikanunua pombe pakti 3 aina ya Tyson nakumbuka walikua wanauza 650 kwa pakti moja nikaipiga pale pale mbili nikapanda nazo kwenye bus...Nilikua nimekaa kwenye siti ya 2 by 2 dirishani ghafla wakapanda wadada wawili na mkaka mmoja ...dada mmoja mweupe mwenye shepu.. yani ni mkubwa kabisa kuliko mimi akaja akakaa akanisalimu wenzake wakakaa siti ya mbele yetu...Sasa mm nina pombe yangu nilikua napenda apande hata msela akae na mm ili niwe huru kukata na kunywa pombe yangu[emoji23]Basi nimejikaza mpaka maili moja kibaha nikasema hapana wakati nafikiria nn cha kufanya wale wa mbele wakampa mwenzao katoni ya castle lager za kopo akatoa moja akafungua akaanza kunywa akaniambia karibu kaka nikachukua kopo ...zikaisha tokaongeza...mara nimetoa kisimu nijifanye kumbeep bibi ilimradi vurugu nikatoa na yale mapomve makali ya viroba nakumbuka tuliwaka sana...To make the long story short nilitakiwa kushuka Kiboriloni nikajikuta niko hoteli moja arusha inaitwa Seven Eleven kama sikosei....niko uchi niko na yule dada[emoji23][emoji23] kumbe nilikata moto simu nimezima sipatikani yule demu kumbe kwenye milioni akadai eti nilinwambia tutumie laki tu zinazobaki tutaenda ngorongoro pakikucha akawa anezihifadhi..kweli kuhesabu nina laki 9[emoji23][emoji23]Nikawasha simu nikapiga kwa bibi nikamwambia nimejikuta asubuhi nyuma ya bus nililotoka nalo dar nimelala na kwenye pesa baba alizonipa imechukuliwa laki moja akapiga vigelegele kanisa lao lina branch arusha akawaelekeza wakaja kunichukua nikapewa shemasi anirudishe Moshi kama shujaaa.....Sijahi muhadithia mtu...yani hapa kwenyewe nlikua naandika nafuta naandika nafuta....kama yule dada yupo humu hata anipM jamaniii[emoji23][emoji23]
 
Pole mzee
Niliwahi kwenda migahawa koko maeneo flani ivi nikakuta contena la kunawia mikono wameweka pembeni na nyumba ya mtu alafu mgahawa wenyewe uko mbali kidogo mi niliponawa nikaingia nyumba iliyokuwa jirani nikidhani ndio mgahawa wenyewe kumbe nimeingia kwenye geto la Mmama flani ivi.

Sasa mda naingia alikuwa bize anakula alafu kageukia upande wapili wala hakusikia vishindo mda naingia kwa akili za kitoto nilipogumdua kuwa nimeingia kusipo nikapata akili ya kutoka kimyakimya tena...! Kumbe mda natoka ndani yule mama akashtuka nikajifanya kuchomoka mule ndani kwa haraka ndio akaniitia mwizi..mwizi...mwizi asee nikajifanya kukimbia nikaishia mikononi mwa wanainchi wenye hasira kali aisee sitakaa nisahau kilichonipata yaani kuna watu bongo hii hata ukiwa unatoa maelezo hawayazingatii wao ni kupiga tu na kutafta petroli.... Hadi leo nikikuta mwizi anapigwa huwa napenda kusikiliza maelezo yake kama yanaleta logic....Maana ningechomwa moto na sijawahi kuiba wala kutapeli cha mtu!
 
Kilindi nipo chuo nilikuwa naingia masomo ya jioni baada ya job, sasa kutokana na ule uchovu wa kazi mara nyingi kipindi cha lecture siku nyingine nasinzia kutokana na uchovu
Siku moja buana tecture anaendelea na kumetulia tuli mm na kale kausingizi si nikaachia Ushuzi tena ule wa puuuuuu.....[emoji23] i.
Ile nashtuka tu darasa lote wanacheka balaa aisee usingizi uliishia palepale na ile aibu sitokuja kuisahau na kibaya zaidi pembeni nilikuwa nimekaa na demu wangu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1487][emoji1487]
 
Siku moja mama mkwe aliniomba kiasi fulani cha hela mida kama saa sita mchana basi bila kusubiri nikaingia kwenye menu ya mobilebanking nikamtumia, kama sekunde tano nikaona sms ya exim sikutaka hata kusoma nikaacha simu getini kwa mlinzi mana hatuingii na simu kazini kutokana na sensitivity ya process inayofanyika humo ndani. saa kumi jion natoka nakuta missedcalls kibao plus sms "mwanangu ninashida na hiyo pesa nitumie then nitakurudishia!". Nikashangaa hela si nimeshatuma tangia mchana!? Ile kucheki ile sms ya exim kumbe muamala ulifeli,,,, Sikuwahi kufedheheka kama nilivyofedheheka ile siku kwa kuonekana mnyimi japo sikuambiwa hivyo.

Hivi kuna mama mkwe analipaga deni?
 
Mimi na mke wangu tulienda kusalimia kwao(ukweni) sasa tukarudi nyumbani nikaona bora niwajurishe kuwa tumefika salama daaaa nikajikuta nimetype haraka haraka na kisimu changu cha tochi kuwa "TUNASHUKURU TUMEFI.LA SALAMA" Then nisend faster kwa mama mkwe aisee alienistua mke wangu kwa sababu ya upekuzi (u spy) wake inbox
 
Nikiwa form 2 kwenye miaka ya 2000 kuendelea..nikiwa kama kijana sharp kabisa kwenye extended family yetu hapa Dar..Mshua akanipa pesa shilingi milioni moja za ujenzi nipeleke moshi kwa bibi yangu mlokole asilimia (100%)Basi laki tano nikaweka mguu wa kushoto tano nyingine mguu wa kulia...
Nikapewa ticket ya Bus moja nakumbuka likiitwa Amazon na fedha taslimu elfu 70 nauli ya kurudi na pesa ya kijikimu na zawadi za njiani kupeleka kwa bibi na simu ndogo ya kufunua aina ya Bird kwa ajili ya mawasiliano.
Nikatoka zangu kinondoni studio mpaka ubungo terminal, bus nikaliona nikaenda kwenye kibanda nikanunua pombe pakti 3 aina ya Tyson nakumbuka walikua wanauza 650 kwa pakti moja nikaipiga pale pale mbili nikapanda nazo kwenye bus...Nilikua nimekaa kwenye siti ya 2 by 2 dirishani ghafla wakapanda wadada wawili na mkaka mmoja ...dada mmoja mweupe mwenye shepu.. yani ni mkubwa kabisa kuliko mimi akaja akakaa akanisalimu wenzake wakakaa siti ya mbele yetu...Sasa mm nina pombe yangu nilikua napenda apande hata msela akae na mm ili niwe huru kukata na kunywa pombe yangu[emoji23]Basi nimejikaza mpaka maili moja kibaha nikasema hapana wakati nafikiria nn cha kufanya wale wa mbele wakampa mwenzao katoni ya castle lager za kopo akatoa moja akafungua akaanza kunywa akaniambia karibu kaka nikachukua kopo ...zikaisha tokaongeza...mara nimetoa kisimu nijifanye kumbeep bibi ilimradi vurugu nikatoa na yale mapomve makali ya viroba nakumbuka tuliwaka sana...To make the long story short nilitakiwa kushuka Kiboriloni nikajikuta niko hoteli moja arusha inaitwa Seven Eleven kama sikosei....niko uchi niko na yule dada[emoji23][emoji23] kumbe nilikata moto simu nimezima sipatikani yule demu kumbe kwenye milioni akadai eti nilinwambia tutumie laki tu zinazobaki tutaenda ngorongoro pakikucha akawa anezihifadhi..kweli kuhesabu nina laki 9[emoji23][emoji23]Nikawasha simu nikapiga kwa bibi nikamwambia nimejikuta asubuhi nyuma ya bus nililotoka nalo dar nimelala na kwenye pesa baba alizonipa imechukuliwa laki moja akapiga vigelegele kanisa lao lina branch arusha akawaelekeza wakaja kunichukua nikapewa shemasi anirudishe Moshi kama shujaaa.....Sijahi muhadithia mtu...yani hapa kwenyewe nlikua naandika nafuta naandika nafuta....kama yule dada yupo humu hata anipM jamaniii[emoji23][emoji23]
Hahahahaa we mse.nge unakismati kichizi[emoji23][emoji4][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Iyo kitu naomba isije nitokea kwa kwel
Moja kwa moja niende katika mada.
Leo asubuhi kama kawaida yangu kuna mahali huwa naenda kunywa chai, ni mgahawa wa jamaa yangu mmoja wa karibu, nimekunywa chai, nilipomaliza nikaona kuna funguo juu ya meza, ambazo ninafahamu ni za jamaa yangu(Nimeshazitumia mara kadhaa kukatia kucha kwa maana zina nail cutter), nikatumia katika kukata kucha.
Nilipomaliza kukata kucha nilipigiwa simu, nikasogea pembeni kuzungumza na simu, nikazungumza na simu kwa muda mrefu, hivyo sikuona umuhimu wa kurudi pale tena maana nimemaliza kunywa chai, kumbe wakati huo nimesahau funguo zile nimeziweka mfukoni, nilipofika nyumbani nimeendelea na shughuli zangu bila kuelewa chochote wala kukumbuka, nimekuja kupigiwa simu na binti kuwa kumbe zile funguo zinahitajika, ndio nikakumbuka kujisachi najikuta na funguo kuwa ninazo mfukoni, na kumbe si za jamaa yangu, kumpigia simu anasema si zake kweli, ni za binti anayefanya kazi hapo mgahawani, ni kwamba zimefanana, tukio hili limeniachia fedheha na aibu kubwa maana moja kwa moja nimeonekana kama nilikuwa nina hila mbaya, na hakuna yoyote ninayeweza kumueleza akaniamini, imebaki kuniuma mwenyewe rohoni, maana ningehusishwa na wizi.
Katika maisha kuna mambo ambayo yanatukuta kwa bahati mbaya bila sisi kutarajia, hayo mambo huwa yanapelekea aibu na fedheha ambayo haistahili kwa kweli, na hata haielezeki kwa mtu kirahisi.
Kama na wewe una kisa chochote tupe hapa tupate funzo kidogo.
 
We boya sana yani unakata mikucha yako na nail cutter za mtu mwingine magonjwa yote haya.

Mimi ilinikuta miaka kadhaa iliyopita ndio nimeajiriwa kwenye kampuni flani hapa dar.jioni nimekaa na mabosi zangu kupata wine kidogo na kujuana vizuri.tulikua tumeweka simu zetu mezani,bahati mbaya nikachukua simu ya bosi mmoja nikatia mfukoni nikijua ni yangu .mara kidogo jamaa akaanza kuulizi simu yake mimi nimetulia tu nikiamini iliyopo mfukoni ni yangu.

Dah ilivyobipiwa ikaita kwangu halafu hata hawakunipa nafasi ya kujieleza zaidi ya kila mtu kutunza simu yake kwa umakini,nilijisikia fedheha haielezeki
Hili nalo tukio aiseee. Pole
 
ilitokea nimekuja dar kwa ndugu yangu aliepanga chumba maeneo ya uswahilini temeke,nyumba ilikua na vijana na mama mwenye watoto wa kike pale,sasa ilitokea siku moja usiku nimeenda kuoga mida ya usiku nikaona sio mbaya nitoe na haja kubwa kabisa,kumbe nimemaliza kujisaidia na maji nimemwaga yalikua machache,asubuh si ndo akaja mwenye zamu kufagia choo akaukatana nayo,kila akimwagia maji mzigo hausogei mbele ikabid aulize tu ni nan alikua wa mwisho si ndo nikatajwa mm..daaahh ilikua fedhea kwa watoto wa kike wale maana mama alikazia neno 'Alf yule kaka ni mwembamba ila ana mavi magumuuuuu' sikumsalimia mpk namaliza likizo naondoka
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom