Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

Na mm kuna matukio kama mawil matatu hivi dah kila nikikumbuka nacheka[emoji23][emoji23][emoji23]

Mwaka jana 2020 nilipita pale Be Forward posta karibu na ocean road,wakati naendelea na kilichonipeleka pale nilibanwa na haja ndogo baada ya kuuliza wenyeji wangu wakanielekeza chooni..
Nimefika chooni nmekuta mtu kaacha zigo juu hajaflash,dah kwa sababu na mm nlikua na haja nkajaribu kuflash bila mafanikio kwa sababu hapakua na maji,nikaona bora nikojoe nisepe,nmemaliz natoka napishana na mdada flani hivi aisee nlijisikia vibaya mno,nlitamani nimwambie usiingie au huo mzigo si wangu ila sikuweza... nilisikia bonge la sonyo na "kuna watu sio wastaarabu"[emoji23][emoji23][emoji23]basi yule dada nlikua na coincidence nae nikawa naonana nae mara kwa mara mpka kuna siku nilipanda nae mwendokasi na kukaa nae seat moja,nilitamani nmuelezee mzigo haukua wangu ila ndo hivo naanzaje
Aisee
 
Mwaka flani hv nimeenda zangu maeneo kumtembelea sister,siku hyo sister kasafiri nimebaki na anko 2,ilikuwa wikiend nikaenda zangu kucheki mpira narudi zangu mida kama ya saa 5 hv uck,narudi geti limefungwa,namgongea anko nae kalala kinouma nimekaa kama nusu SAA hv nagonga hakuna kufungua,nikaamua kufungua dirisha nipitie hapo,vile vidirisha vya zamani vinakuwa na nondo katikati aisee,so nikapiga hesabu nikaona kupita na nguo haiwezekani so nikavua nguo nikaziingiza ndani nikabaki na chupi 2 nikajua si napita fasta, ile kuanza kupitisha kichwa hakipiti kumbe ni padogo ,kasheshe likaanzia hapo,hangaika wapi, hangaika wapi nikaona jau hili,nikamkumbuka jamaa yangu anakaa mtaa wa pili,ikabidi nitoke pale kwa spidi kali nipo na kichupi 2 nakatiza mtaaan,wikiendi ile mitaa watu wanacjelewa sana kulala so nilikutana na watu wanacheka walijua nimetoka kufumaniwa so nakimbia soo,ile nafika kwa jamaa,jamaa kafungua kunikuta vile anacheka kishenzi,kwa soo lile sikukaa sana ilibidi nirudi home 2
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Nikiwa form 2 kwenye miaka ya 2000 kuendelea..nikiwa kama kijana sharp kabisa kwenye extended family yetu hapa Dar..Mshua akanipa pesa shilingi milioni moja za ujenzi nipeleke moshi kwa bibi yangu mlokole asilimia (100%)Basi laki tano nikaweka mguu wa kushoto tano nyingine mguu wa kulia...
Nikapewa ticket ya Bus moja nakumbuka likiitwa Amazon na fedha taslimu elfu 70 nauli ya kurudi na pesa ya kijikimu na zawadi za njiani kupeleka kwa bibi na simu ndogo ya kufunua aina ya Bird kwa ajili ya mawasiliano.
Nikatoka zangu kinondoni studio mpaka ubungo terminal, bus nikaliona nikaenda kwenye kibanda nikanunua pombe pakti 3 aina ya Tyson nakumbuka walikua wanauza 650 kwa pakti moja nikaipiga pale pale mbili nikapanda nazo kwenye bus...Nilikua nimekaa kwenye siti ya 2 by 2 dirishani ghafla wakapanda wadada wawili na mkaka mmoja ...dada mmoja mweupe mwenye shepu.. yani ni mkubwa kabisa kuliko mimi akaja akakaa akanisalimu wenzake wakakaa siti ya mbele yetu...Sasa mm nina pombe yangu nilikua napenda apande hata msela akae na mm ili niwe huru kukata na kunywa pombe yangu[emoji23]Basi nimejikaza mpaka maili moja kibaha nikasema hapana wakati nafikiria nn cha kufanya wale wa mbele wakampa mwenzao katoni ya castle lager za kopo akatoa moja akafungua akaanza kunywa akaniambia karibu kaka nikachukua kopo ...zikaisha tokaongeza...mara nimetoa kisimu nijifanye kumbeep bibi ilimradi vurugu nikatoa na yale mapomve makali ya viroba nakumbuka tuliwaka sana...To make the long story short nilitakiwa kushuka Kiboriloni nikajikuta niko hoteli moja arusha inaitwa Seven Eleven kama sikosei....niko uchi niko na yule dada[emoji23][emoji23] kumbe nilikata moto simu nimezima sipatikani yule demu kumbe kwenye milioni akadai eti nilinwambia tutumie laki tu zinazobaki tutaenda ngorongoro pakikucha akawa anezihifadhi..kweli kuhesabu nina laki 9[emoji23][emoji23]Nikawasha simu nikapiga kwa bibi nikamwambia nimejikuta asubuhi nyuma ya bus nililotoka nalo dar nimelala na kwenye pesa baba alizonipa imechukuliwa laki moja akapiga vigelegele kanisa lao lina branch arusha akawaelekeza wakaja kunichukua nikapewa shemasi anirudishe Moshi kama shujaaa.....Sijahi muhadithia mtu...yani hapa kwenyewe nlikua naandika nafuta naandika nafuta....kama yule dada yupo humu hata anipM jamaniii[emoji23][emoji23]
Seven /eleven kiwanja changu hicho kila nikiwa arusha
 
Bro wangu ameoa sasa.Alikuwa na demu lake lina msambwanda kinyama.Basi lilivyosikia jamaa anaoa alienda kumfanyia fujo home wote tulikuwepo.Likaanza kubwatuka kuwa jamaa kamla ndogo miaka mingi kwa nini amuoi yeye.Tuliona noma sana.Washua wananiuliza kweli?Nikawaambia mkamuulize bro.Noma sana.
Ungemtetea brother bana... Ukasema anapayuka tu Hana lolote roho inamuuma tu. Sasa kuwaambia wakamuulize broh umepigia jibu mstari... Sijui maza alijisikiaje kusikia baharia anaruka ukuta?

Sent from my GIONEE S11 lite using JamiiForums mobile app
 
Mm 2007 nilikuwa naenda Advance Songea, basi nikatoka kusini hadi dar, Dar nikapanda basi la superfeo kwenda songea, lile basi ilikuwa wakigawa soda ila mukifika maeneo ya Iringa na kwenda mbele, ila mm sikuwa nimewahi kupanda basi ambalo wanagawa soda, sasa ile tunafika mikumi naona njaa kwa mbaaaaali inaninyemelea ile nikipepesa macho nikaona kreti la soda kwa katikati, nikasema isiwe shida sasa kucheki vema siti za jirani zina mabinti wawili wamevalia yunifomu za songea girls basi nikashoboka na kumuuliza mmoja eti dada zile soda kwenye kreti nani anauza?

Yule dada akaniambia haziuzwi mbona watagawa bure tu baadae!!!!! Haki ya mungu niliona fedheha vibaya mno na safari ikawa chungu saanaa hadi tunafika songea mida ya saa mbili na nusu usiku,

Na tangu hapo sikutongoza mwanafunzi wa songea girls Hadi namaliza form six na kurudi zangu kusini,

Pumbavu kabisaaaaaa fedheha ile...
Labda ni wewe ulijishitukia, lakini si fedheha.
 
Nikiwa form 2 kwenye miaka ya 2000 kuendelea..nikiwa kama kijana sharp kabisa kwenye extended family yetu hapa Dar..Mshua akanipa pesa shilingi milioni moja za ujenzi nipeleke moshi kwa bibi yangu mlokole asilimia (100%)Basi laki tano nikaweka mguu wa kushoto tano nyingine mguu wa kulia...
Nikapewa ticket ya Bus moja nakumbuka likiitwa Amazon na fedha taslimu elfu 70 nauli ya kurudi na pesa ya kijikimu na zawadi za njiani kupeleka kwa bibi na simu ndogo ya kufunua aina ya Bird kwa ajili ya mawasiliano.
Nikatoka zangu kinondoni studio mpaka ubungo terminal, bus nikaliona nikaenda kwenye kibanda nikanunua pombe pakti 3 aina ya Tyson nakumbuka walikua wanauza 650 kwa pakti moja nikaipiga pale pale mbili nikapanda nazo kwenye bus...Nilikua nimekaa kwenye siti ya 2 by 2 dirishani ghafla wakapanda wadada wawili na mkaka mmoja ...dada mmoja mweupe mwenye shepu.. yani ni mkubwa kabisa kuliko mimi akaja akakaa akanisalimu wenzake wakakaa siti ya mbele yetu...Sasa mm nina pombe yangu nilikua napenda apande hata msela akae na mm ili niwe huru kukata na kunywa pombe yangu[emoji23]Basi nimejikaza mpaka maili moja kibaha nikasema hapana wakati nafikiria nn cha kufanya wale wa mbele wakampa mwenzao katoni ya castle lager za kopo akatoa moja akafungua akaanza kunywa akaniambia karibu kaka nikachukua kopo ...zikaisha tokaongeza...mara nimetoa kisimu nijifanye kumbeep bibi ilimradi vurugu nikatoa na yale mapomve makali ya viroba nakumbuka tuliwaka sana...To make the long story short nilitakiwa kushuka Kiboriloni nikajikuta niko hoteli moja arusha inaitwa Seven Eleven kama sikosei....niko uchi niko na yule dada[emoji23][emoji23] kumbe nilikata moto simu nimezima sipatikani yule demu kumbe kwenye milioni akadai eti nilinwambia tutumie laki tu zinazobaki tutaenda ngorongoro pakikucha akawa anezihifadhi..kweli kuhesabu nina laki 9[emoji23][emoji23]Nikawasha simu nikapiga kwa bibi nikamwambia nimejikuta asubuhi nyuma ya bus nililotoka nalo dar nimelala na kwenye pesa baba alizonipa imechukuliwa laki moja akapiga vigelegele kanisa lao lina branch arusha akawaelekeza wakaja kunichukua nikapewa shemasi anirudishe Moshi kama shujaaa.....Sijahi muhadithia mtu...yani hapa kwenyewe nlikua naandika nafuta naandika nafuta....kama yule dada yupo humu hata anipM jamaniii[emoji23][emoji23]
Weee jamaa umenichekesha Sana... Eti Kama shujaaaa.... Laki Tisa ngorongoro

Sent from my GIONEE S11 lite using JamiiForums mobile app
 
siku nimeingia pale cafteria ya coed udom mwafrika asubui tu kwenda kusaka supu...nikaudumiwa fresh tu nikaenda kuweka vitu vyangu mezani nikasema nirudi kunawa....sasa kuna zile ndoo za chuma zinawekwaga maji ya moto me nikaona nikaona kama lile kumbe lile wao wameweka chai bhn ukiitaji unaenda pale unafunguliwa koki unachukua chai...me nikajua ndo lina maji ya kunawa nikaenda nikafungua ili ninawe...asee kelee niliyopigiwa nilpata aibu kubwa sana

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Moja kwa moja niende katika mada.

Leo asubuhi kama kawaida yangu kuna mahali huwa naenda kunywa chai, ni mgahawa wa jamaa yangu mmoja wa karibu, nimekunywa chai, nilipomaliza nikaona kuna funguo juu ya meza, ambazo ninafahamu ni za jamaa yangu(Nimeshazitumia mara kadhaa kukatia kucha kwa maana zina nail cutter), nikatumia katika kukata kucha.

Nilipomaliza kukata kucha nilipigiwa simu, nikasogea pembeni kuzungumza na simu, nikazungumza na simu kwa muda mrefu, hivyo sikuona umuhimu wa kurudi pale tena maana nimemaliza kunywa chai, kumbe wakati huo nimesahau funguo zile nimeziweka mfukoni, nilipofika nyumbani nimeendelea na shughuli zangu bila kuelewa chochote wala kukumbuka, nimekuja kupigiwa simu na binti kuwa kumbe zile funguo zinahitajika, ndio nikakumbuka kujisachi najikuta na funguo kuwa ninazo mfukoni, na kumbe si za jamaa yangu, kumpigia simu anasema si zake kweli, ni za binti anayefanya kazi hapo mgahawani, ni kwamba zimefanana, tukio hili limeniachia fedheha na aibu kubwa maana moja kwa moja nimeonekana kama nilikuwa nina hila mbaya, na hakuna yoyote ninayeweza kumueleza akaniamini, imebaki kuniuma mwenyewe rohoni, maana ningehusishwa na wizi.


Katika maisha kuna mambo ambayo yanatukuta kwa bahati mbaya bila sisi kutarajia, hayo mambo huwa yanapelekea aibu na fedheha ambayo haistahili kwa kweli, na hata haielezeki kwa mtu kirahisi.

Kama na wewe una kisa chochote tupe hapa tupate funzo kidogo.
Nilinunua mkanda wa suruali pale kariakoo dar es salaam mida ya usiku usiku huwa wananinginiza ivi kwenye zile henga zao, kwa macho niliuona mzuri sana na strong wa kuvutia kumbe baba ule mkanda ni feki ajabu, umekuja kukatika siku 2 nilikuwa kwenye boti ivi nasafiri kwenda mahali, sasa mule kwenye boti kuna mademu mademu kibao na watu kibao wamekaa kwenye viti na boti inatembea wale mademu wao ndio wamenishtua kaka mkanda wako umekatika nilikuwa nimesimama ivi kwenda huku na kule mle kwenye boti. Yaani niliona aibu aibu aibu fedheha mara elfu1, nikajizoa zoa nikaenda kukaa mahali nikautoa wote tupa baharini., yaani kwa ile aibu ilibidi nijichimbie mahali mule kwenye boti mpaka boti ilipofika niliacha watu wote washuke ndio na mimi nikajikongoja kutoka sikutaka kuonana na mtu yeyote aliyeniona nikipata ile aibu.


Toka siku hiyo pale karikaoo ata kununua chupi naona ntapata feki feki nimejuta sana na nnahasira nao kinyma, tena afadhali huu uzi umekuja ili niwatanabahishe wale walio maeneo ya dar es salaam.
 
We boya sana yani unakata mikucha yako na nail cutter za mtu mwingine magonjwa yote haya.

Mimi ilinikuta miaka kadhaa iliyopita ndio nimeajiriwa kwenye kampuni flani hapa dar.jioni nimekaa na mabosi zangu kupata wine kidogo na kujuana vizuri.tulikua tumeweka simu zetu mezani,bahati mbaya nikachukua simu ya bosi mmoja nikatia mfukoni nikijua ni yangu .mara kidogo jamaa akaanza kuulizi simu yake mimi nimetulia tu nikiamini iliyopo mfukoni ni yangu.

Dah ilivyobipiwa ikaita kwangu halafu hata hawakunipa nafasi ya kujieleza zaidi ya kila mtu kutunza simu yake kwa umakini,nilijisikia fedheha haielezeki
mkuu hii ni balaaa
 
Nilinunua mkanda wa suruali pale kariakoo dar es salaam mida ya usiku usiku huwa wananinginiza ivi kwenye zile henga zao, kwa macho niliuona mzuri sana na strong wa kuvutia kumbe baba ule mkanda ni feki ajabu, umekuja kukatika siku 2 nilikuwa kwenye boti ivi nasafiri kwenda mahali, sasa mule kwenye boti kuna mademu mademu kibao na watu kibao wamekaa kwenye viti na boti inatembea wale mademu wao ndio wamenishtua kaka mkanda wako umekatika nilikuwa nimesimama ivi kwenda huku na kule mle kwenye boti. Yaani niliona aibu aibu aibu fedheha mara elfu1, nikajizoa zoa nikaenda kukaa mahali nikautoa wote tupa baharini., yaani kwa ile aibu ilibidi nijichimbie mahali mule kwenye boti mpaka boti ilipofika niliacha watu wote washuke ndio na mimi nikajikongoja kutoka sikutaka kuonana na mtu yeyote aliyeniona nikipata ile aibu.


Toka siku hiyo pale karikaoo ata kununua chupi naona ntapata feki feki nimejuta sana na nnahasira nao kinyma, tena afadhali huu uzi umekuja ili niwatanabahishe wale walio maeneo ya dar es salaam.
Hapa inamaana baada ya mkanda kukatika suruali ilidondoka ama ulikatika tu
 
Kuna demu mtaani alikuwa wa kishua na huwa hana shobo na mtu wala hasilimii kenge yoyote pale mtaani.Masela wakawa wanamuongelea vibaya sasa siku moja mama yake alikunywa sumu kwa wivu wa mapenzi (baba yake ambae anafanya kazi UN) nashangaa bonge la usiku akaja mbio kuniomba nimpe maziwa(tulikuwa tunafuga ng’ombe) ikabidi familia nzima iamke ili kujua nani huyo anataka maziwa usiku wa manane? mimi kwa uninja wangu nikaenda mbio kwenda kumkamua ng'ombe wetu nikampa kama nusu jagi akabeba huku anakimbia kuelekea kwao huku analia.Nikaona haitoshi kuna dokta mwenye ki dispensary pale jirani na,home nikamcheck akapokea simu kwa sababu alikuwa mchizi wangu sana,ikabidi nimuelezee kilichotokea si akaamka tukaenda kumchukua yule mama na kumtundikia ma dripu.Yule mama baada ya siku 3 akawa na nafuu kumbe lile tendo lilinipa marks kubwa kwa yule demu so mtaa mzima akawa ananisalimu na kuongea na mimi tu(upande wa wavulana).
Siku moja moja sina lile wala hili akashika simu yangu aina ya L6 motorola ili asave namba yake kumbe alinipenda sana the way nilivyojitoa kwa mama yake.Daaa ile anaandika number akakuta namba yake imaseviwa NGEDERE MAPOZI daaa nashangaa ananiuliza hii nini kumbe una namba yangu alafu umenisave jina la ajabu.? Kwa kweli niliona aibu sana siku ile nilikosa cha kusema isitoshe alianza kunipenda na alikuwa anakuja home niliishiwa nguvu asijue kuwa lile jina na namba nililisave,zamani kabla ya tukio la mama yake kula sumu.
WANA WALISHAANZA KUNIPA RESPECT KWA KUWA KARIBU NA YULE MTOTO WA KISHUA.Daaaaa
ungemwambia tu simu umenunua kwa mtu mtaani na namba hukujua Kama ipo kwenye hiyo simu

Na wewe ungejifanya kumuuliza ni yako hiyo namba? Hapo angekuelewa
 
Mwaka flani hv nimeenda zangu maeneo kumtembelea sister,siku hyo sister kasafiri nimebaki na anko 2,ilikuwa wikiend nikaenda zangu kucheki mpira narudi zangu mida kama ya saa 5 hv uck,narudi geti limefungwa,namgongea anko nae kalala kinouma nimekaa kama nusu SAA hv nagonga hakuna kufungua,nikaamua kufungua dirisha nipitie hapo,vile vidirisha vya zamani vinakuwa na nondo katikati aisee,so nikapiga hesabu nikaona kupita na nguo haiwezekani so nikavua nguo nikaziingiza ndani nikabaki na chupi 2 nikajua si napita fasta, ile kuanza kupitisha kichwa hakipiti kumbe ni padogo ,kasheshe likaanzia hapo,hangaika wapi, hangaika wapi nikaona jau hili,nikamkumbuka jamaa yangu anakaa mtaa wa pili,ikabidi nitoke pale kwa spidi kali nipo na kichupi 2 nakatiza mtaaan,wikiendi ile mitaa watu wanacjelewa sana kulala so nilikutana na watu wanacheka walijua nimetoka kufumaniwa so nakimbia soo,ile nafika kwa jamaa,jamaa kafungua kunikuta vile anacheka kishenzi,kwa soo lile sikukaa sana ilibidi nirudi home 2
[emoji23][emoji23][emoji23]..Mama.e
 
Dah,wakati uzi huu unaletwa sikuwa online kwakwel
Nina visa vyangu viwili na kingine ni cha mwanafunzi mwenzangu
Kisa no 1
Miaka kadhaa ya nyuma nikiwa form one huko vijijini basi kulikuwepo na utaratbu kila terminal na annual walikuwa wanasoma top ten na wale kumi wa kutoka mwisho basi siku hyo ilikuwa ijumaa tukifunga kwenda likizo ya mwezi disemba siku hyo nilkuwepo period na kipindi hiko tulikuwa tunavaa matambala hata pedi nilkuwa sizijui basi mida ya sa nane tukaa skuli balaza mawaidha yakaendelea mara nasikia damu zinatiririka mithili ya maji yaani nasikia sehemu nilyokaa kama imejaa hivi najiuliza niombe ruhusa kabla sijajifikiria vizuri nasikia wanaanza kusoma majina ya top ten mara jina langu linaitwa ,wa kwanza darasani ni fulani(sasa inabidi ninyanyuke niende kupewa mkono na meza kuu na kupewa zawadi)aseee!nildata pale chini kwa sekunde kadhaa,theni nkasimama ,nilihisi damu zinachuruzika hadi miguuni(but haikuwa hivo ni hisia tu) bahati nzuri sketi ilikuwa nyeusi afu ndefu basi nkapata akili nkavua sweta nkajifunga kiunoni ikabid niende mbele kuchukua zawadi(unapoenda mbele wanafunzi unawapa mgongo )japo sijui sikugundulika lakini niliona aibu sana yaani kama wiki nzima nilkuwa nikifikiria hicho kitu

Kisa no 2
Hii ni miaka ya hivi karibuni,kawaida mimi pombe nakunywa,lakini ni zile za kureflesh na ni mara chache mno na mara nyingi huwa nakunywa wine na konyagi ikitokea basi bwana siku hyo nimejisikia kunywa nimeenda glossary nkaulizia wine hakuna,konyagi hakuna nkaambiwa imebaki k,vant tu sijawahi kunywa kivant ila uwa nasikia wanaisifia basi nkasema wacha nichukue kivant ndogo maana sina namna,nkabeba zangu nkaenda home nkanywa but naona radha yake siyo nzuri nkajikaza nkanywa nilivomaliza nkaenda kulala,nimelala usingizi mzuri mara kama naota hivi nasikia mme wangu ananiamsha anasema umekuwaje????aseee kumbe natapika mashuka yote na blanket yashakula matapishi fasta usingizini(ikumbukwe sijawahi tapika tangu nakunywa pombe)haraka niliamka nkaenda chooni tapika wee mpaka nyongo aseeee siku hiyo niliona aibu yaani kutapika kisa pombee??na mme wangu yeye hata hanywiii,naichukia k,vant

Kisa 3
Tukiwa form four miaka hyo wavulana kwa wasichana ilikuwa mida ya sa saba jua kali kipindi cha hesabu darasani kilikuwa kinaendelea,ikumbukwe hii mida ni mida ambayo wanafunzi wengi wanakuwa wamelala basi kuna binti mmoja alikuwa amekaa sehemu ambayo ni katikati ya darasa kama kawaida akauchapa usingizi wake kwenye dawati,mda kidogo akaanza kuota na kukojoa akakojoa mkojo unatiririka kwenye sakafu,hyo nayo ilikuwa aibu kwake hata sisi wasichana tuliona aibu but ni mambo ya kawaida

Nilivokoswa na aibu ambayo nilishaiona mbele yako
2016 nilkuwa natoka gongo la mboto naenda job,kumbe nilvotoka nkabeba mkoba mwingine wa jana ambao ulikuwa na hela nkauacha,tumefika sokota nakumbuka nimebeba mkoba hauna nauli dah nkaona hapa ni hatari,nkimuona konda ni wale micharuko akili akanijia kwamba itabid nimwambie hela yake namtumia m pesa kwani nashukia njiani,nkaanza kuwaza ntakavodhalilishwa nkasema eeh Mungu wangu sijafanya makusudi,huwezi amini konda alinipita wala hakuniuliza nauli nami nkasema hii ndo inaitwa miujiza
But all in all aibu zinakuja vyovote kikubwa ni kuzipotezea
 
Back
Top Bottom