Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

Life Experience: Jambo gani liliwahi kukutia aibu katika maisha?

Same as me
Nakushauri ukimaliza jitahidi uende law school mapema masharti yanaenda kuwa magumu mbeleni wameanza na kupandisha ada wanahamia kwenye mtihani ndio uwe admitted wataongeza jingine ili iwe ngumu kusoma usiogope kwamba watu wanafeli first sit

Kwenye sheria jitahidi kujichanganya na hasa mawakili wazoefu hata kama bado haujawa wakili utapata njia

Muzahula yupo?
Katabalo vipi?
Sr ngonyani yuko hapo?
Je Jiniazi masoud yupo?
Wanangu kina Mwita, kawiche, mwasi mbegu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23], Luhigo yupo?
Lutechura yupo?
Je mnoko sunga?[emoji23][emoji23][emoji23]
Kamwiche ,mbegu,luhigo na lutechura ndo sjawai waskia Ila wengine wapo...
Mi Sheria nmesoma tu sabu Ila ilkua so chaguo langu nliapply coz course nyingne zlikua full na nliapply awamu ya tatu baada ya kupata boom 100%nlivyofika nilikaziwa kubadili ko nkaamua tu kukaza,natamani tu nmalize.
mazngira ya home hayaruhusu kuendelea Cha mno after chuo Ni kujtafta tu kitaa iktokea nmepata pakujishikiza kupitia nlichosomea fresh Ila sitegemei kabsa
 
Kamwiche ,mbegu,luhigo na lutechura ndo sjawai waskia Ila wengine wapo...
Mi Sheria nmesoma tu sabu Ila ilkua so chaguo langu nliapply coz course nyingne zlikua full na nliapply awamu ya tatu baada ya kupata boom 100%nlivyofika nilikaziwa kubadili ko nkaamua tu kukaza,natamani tu nmalize.
mazngira ya home hayaruhusu kuendelea Cha mno after chuo Ni kujtafta tu kitaa iktokea nmepata pakujishikiza kupitia nlichosomea fresh Ila sitegemei kabsa

Komaaa
Kuna pesa unataka kuiacha
 
Dah kuna siku gari ya mshua ilikodiwa kwenda Njombe... Ilibeba wanakwaya wanaenda kwenye harusi ya mwenzao. Sasa kufika kule wakawa kanisani wanasherehekea...mimi nipk ndani ya gari nimelala daaaaaaaaaaah!!!! NILIJAAMBAAA KWANGUVU KAMA MARA 3 AFU KWA UHURU NIKIJUA NIPO PEKEANGU NDANI.... baada ya dakika mbili hivi nikashituka kuangalia hivi kuna mmama kakaa pembeni daaaaaaaah!!!!!!
[emoji28][emoji28][emoji119]
 
Niliwahi kujamba mbele za wanafunzi wangu, nikiwa mbele ya wanafunzi wananisikiliza kwa umakini wa hali ya juu sasa hapo kijambo kikaja cha kimyakimya ..duh kumbe ilikuwaa inanuka hatari...niliona wengine walijuwa mimi halafu wingine wakamsingizia dogo flani ambae anajambagajamba ovyo duh nilijisikiaa ovyo kwelii....
aisee
 
Nikiwa chuo iringa nakaa mbali afu chuo kipo town
So lazma ntumie usafiri . Siku moja nikiwa nimevaa suluari modo Ime tight hatari,
Nikapanda zang bajaji , nmeshuka nikapiga hatua mbili hv nakuta Kila mtu Kama ananiangalia hiv , afu Kama upepo unaingia ndan HV ,
Kucheki suluari imetatuka kweny msamba ,

Asee ilibidi nipand bajaj nyingn fasta kurudi gheto,,
😂😂😂😂
 
Kuna siku ndio nimetoka kureport kazini kama siku mbili 3 hivi nmebaki ofisini mwenyewe si nikaachia hewa chafu pale mara paap Boss huyu hapa ofisi inanuka balaa, hakika nilipata fedhehea ya kufa mtu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Hii huwa inawakuta wengi sana
 
Daaah umenikumbusha mbali sana mkuu, Nilitongozaga demu mtandaoni baada ya kumuona akiwa anapost picha mara kwa mara akila bata na alionekana mzuri balaa kama unavyowaona akina Beyonce vile, yaani ukiona picha yake utafikiri hajazaliwa ni kama malaika kashushwa vile nikamfuata Inbox baada ya kuzoeana sana nikamtongoza akakubali kwa vile nilikuwa mkoani kikazi na yeye alikuwa Dar, ikabidi tukakubaliana nimtumie nauli aje niliko akakubali nikamtumia.

Siku ya kuja Alifika muda kama saa8 unusu nikiwa bado niko kazini na kwa vile rafiki zangu nilishawaonesha picha za yule mdada na kwa kweli na wao wakaona nimeopoa lulu, ikabidi nimtume dereva na gari la ofisi akampokee ampeleke hoteli akale then nikamuelekeze pa kumuacha.... nikiwa nimetulia muda wote nachart nae nikaona text kutoka kwa dereva " mzee demu gani huyu umeleta, njoo umpeleke mwenyewe hotelini mimi siwezi kuongozana nae" nikajua jamaa anatania maana ni mtu wa utani..

Alivorudi akawa anacheka sana anawahadithia rafiki zangu nikiwemo nikajua anatania hasa nikirudi kuangalia zile picha hata rafiki zangu hawakuamini muda wa kazi ulipoisha marafiki zangu wakanifuata kwenda kumuona shemeji yao. Sitaki kuamini nilichokiona kule, picha ni zake kweli lakini sio uhalisia wake kabisa jamaa wakaniacha bhna hawakutaka hata kukaa na mimi halafu sijui ex wangu alijuaje niko pale si akaja aliongea maneno yaliyofanya ile siku ikawa mgumu sana kwangu.

Kesho yake nikampa nauli arudi, yule demu hata sikupiga aisee, nilipoingia ilikuwa ni kila mtu akawa ananidiscuss mimi kwa kilichotokea usiku wa jana yake.

Hawa madada msiwaamini kwa picha za mitandaoni, wakiwa nyuma ya camera za iphone ni tofauti na uhalisia wao.

Mtandaoni binafsi sitongozi tena
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Juzi kati hapo nlikua naangalia Porn kwenye site nikasahau kufunga page baadae nikaingia kwenye check point jengo moja wakati wa ukaguzi nikatoa simu kumbe nmefungua Chrome data ipo on video ina play mlinzi alikua mwanamke , nliona aibu, mbaya zaidi njemba ilikua inapeleka moto kwa mtandao haramu
The fvcck
 
Sitasahau nikiwa Mpanda soko Kubwa, chizi wa Kike akanikomalia huku ananifuata kwa nyuma kuwa wewe Bwana wangu. Mbona unajifanya hunijuinsasa wakati huwa unanilala.

Aiseee, sijawahi fedheheka kama siku ile. Simjui yule Dada kwa kuwa mimi mweupe ndio akanikomalia kwa maana nasikia vichaa huwa hawaendani na watu weupe.
Ahaa soko kubwa sehem gani mzee mnarani au stendi ya bajaji
 
Miaka hiyoo nilipokuwa bado bwana mdogo ndio naanza kupendapenda vischana alikuwepo sista du fulani mzuri kiasi chake, nikaanza kumtamani. Shida sasa ikawa kwenye kumtongoza, kila nilipojaribu kumkabili mojakwamoja moyo ukawa unasita nikaona isiwe tabu nikachana karatasi kwenye daftari nikamuandikia barua kisha mimi mwenyewe nikamfuata na kumpa halafu haraka nikatoweka kabla hajaisoma, siku ileile nikaanza kupokea taarifa kwa vijana wenzangu waliokuwa wananihathia kuhusu ile barua huku wananicheka, kumbe yule demu baada ya kuisoma akaamua kumpelekea kila mtu pale mtaani kuwaonesha kuwa namtaka na yeye hanitaki, Dah basi ilikuwa ngumu hata kutoka nyumbani kwa aibu, na kwabahati mbaya barua ile ikafikishwa na nyumbani hapo sasa nikawa nikitoka nyumbani asubuhi sirudi mpaka usiku tena kwa kujifichaficha washkaji wasinone, mtaa niliuona mchungu zaidi ya wiki.
Ungemuandikia meseji Kama ya yule mzee,You need to grow up
 
Back
Top Bottom