Lighter Touch: Ule uvumi ungenoga hivi leo

Lighter Touch: Ule uvumi ungenoga hivi leo

Chadema tu ndio walifurahi, ila nina amini JPM atawafurahisha zaidi! Subiri
Haya ni makosa yanayojirudia. Huwezi kujua nani Chadema nani CCM na nani hayupo miongoni mwao. Unachotakiwa kujua ni kuwa kuna ''ufa''.

Ukianza kusema hawa ni CDM wale ni Uvccm hawa ni Jucuf tayari unaligawa Taifa
Taifa linajengwa na muunganiko wa wote, ukianza kutenga unajenga ufa

Hili ni kosa sijui kwanini watu hawajifunzi.
 
Nakubaliana nawe, naondoa hilo neno ''kila mtu'' kwa kuwa hakuna kigezo wala takwimu. Badala yake natumia ''hali iliyopo''. Swali linabaki pale pale, nini kimebadilika hadi hali ikawa kama ilivyo leo?
Ninakushukuru kwa kuondoa neno KILA MTU.

Hali haijabadilika bali kilichobadilika ni njia/fursa za kufikisha ujumbe. Zamani ilikuwa lazima uwe na Laptop au PC kama unataka kufikisha ujumbe kupitia internet. Leo hii simu ya kiganjani inafanya mambo yote lakini kikubwa zaidi hata gharama yake kwa sasa iko chini.

Kama nilivyosema, zamani kabla ya mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na Instagram haijawa maarufu na kupata watumiaji wengi, watu walikuwa wanategemea forums ambazo zilikuwa na moderators ambao walikuwa wanafuta message hasi kwa jamii. Mfano Jamboforums/Jamiiforums na yahoo forums.

Wewe kama mkongwe hapa umekuwa mtu ambaye unasema taifa limegawanyika hata kabla Rais Magufuli hajaingia madarakani. Nakumbuka ulikuwa unamlaumu sana Rais Kikwete kwa kuligawa taifa halafu leo unahoji kama vile tatizo hili limeanza kwenye awamu ya tano!
 
Haya ni makosa yanayojirudia. Huwezi kujua nani Chadema nani CCM na nani hayupo miongoni mwao. Unachotakiwa kujua ni kuwa kuna ''ufa''.

Ukianza kusema hawa ni CDM wale ni Uvccm hawa ni Jucuf tayari unaligawa Taifa
Taifa linajengwa na muunganiko wa wote, ukianza kutenga unajenga ufa

Hili ni kosa sijui kwanini watu hawajifunzi.
Hakuna muunganiko wa chadema, usitegemee watu wenye akili ya kunguni wakaunganika! Walimtukana kila aina ya tusi kikwete, leo wanamlilia
Chadema sio watu wa kuwa entertain hata kidogo, ni kubana na kuwakanyaga kwa kadri utavyoweza!
Na namuomba mh. Raisi afanye jambo kwa wajinga hawa
 
Hali haijabadilika bali kilichobadilika ni njia/fursa za kufikisha ujumbe. Zamani ilikuwa lazima uwe na Laptop au PC kama unataka kufikisha ujumbe kupitia internet. Leo hii simu ya kiganjani inafanya mambo yote lakini kikubwa zaidi hata gharama yake kwa sasa iko chini.

Kama nilivyosema, zamani kabla ya mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na Instagram haijawa maarufu na kupata watumiaji wengi, watu walikuwa wanategemea forums ambazo zilikuwa na moderators ambao walikuwa wanafuta message hasi kwa jamii. Mfano Jamboforums/Jamiiforums na yahoo forums.

Wewe kama mkongwe hapa umekuwa mtu ambaye unasema taifa limegawanyika hata kabla Rais Magufuli hajaingia madarakani. Nakumbuka ulikuwa unamlaumu sana Rais Kikwete kwa kuligawa taifa halafu leo unahoji kama vile tatizo hili limeanza kwenye awamu ya tano!
Bado sikubaliani nawe kwasababu una hoja mbili. Kwanza, vyama vingi ambayo sasa unaiacha na kuingilia mitandao. Mitandao ipo zaidi ya miaka 20 sasa na awamu zote!

Pili, sijasema kugawanyika kwa taifa kumeanza na awamu hii.
Huko nyuma tuligawanyika hasa baada ya Mkapa kuondoka madarakani. Kukawa na Wanamtandao, Original n.k. Tukaona taifa linagawanyika katika masuala muhimu kama katiba
Tulisema, kugawanyika huko hakukuwa jambo zuri kwani ni mwanzo wa mmomonyoko wa umoja wetu wa kitaifa.

Tulipofikia sasa nadhani utakubaliana nami ni hatua mpya. Hii hatua ya kutakiana mabaya kwa pande zote, kuhasimiana katika misiba, matibabu na hali za kibinadamu kama ilivyotokea katika uzushi na uvumi ni mwendelezo lakini hatua ya juu zaidi isiyohitaji microscope kubaini tatizo.

Ndiyo maana nilikuuliza, tumefikaje hapa? Tunaondokaje hapa?
Hoja yangu imejengwa juu ya nini kifanyike turudi katika upendo na umoja wa kitaifa na si uvumi ambao tunajua hauna maana

Tofauti na wengine wanaolaumu uvumi kama tatizo, mimi naona uvumi kama dalili tu ''symptoms' picha kubwa ya uvumi ndilo tatizo na tunapaswa kulijadili wala si kutafuta namna ya kufukia vichwa mchangani mwili nje kwa hoja za vyama vingi au mitandao.
 
Hakuna muunganiko wa chadema, usitegemee watu wenye akili ya kunguni wakaunganika! Walimtukana kila aina ya tusi kikwete, leo wanamlilia
Chadema sio watu wa kuwa entertain hata kidogo, ni kubana na kuwakanyaga kwa kadri utavyoweza!Na namuomba mh. Raisi afanye jambo kwa wajinga hawa
OK! kama hiyo ndiyo njia ya kuliunganisha Taifa, naiwe hivyo!
 
Yote 9 ..kumi playlist ya Msigwa ilinifurahisha

Hauwezii kushindanaaa na wanadamu wenye kinywa
 
Ule uvumi umetufundisha mambo mengi; lakini kubwa ni kuwa mashine ya kuchakatia uzushi ilichakata sana jana.. lakini leo imeshindwa kuendelea. Baada ya Rais wa Watu kutokea leo akiwa na afya njema na kufanya kitu ambacho watu walitakiwa kukidhania kingefanyika (baada ya kufanya uteuzi) basi ule uvumi ulitakiwa ubadilike na kunogeshwa namna hii...

Kwa mfano,

Huyu wa leo siyo Magufuli ni double wake. Si unajua kila Rais ana "double" wake yaani mtu anayefanana naye kwa kila namna. Na huyu double tunaweza kusema alienda akafanyiwa "plastic surgery" huko Cuba na amekuwa akitumika mara kwa mara...

Kwamba, baada ya kuugua alikimbizwa Afrika ya Kusini, ambako alipanda ndege ya mwendo kasi hadi Ujerumani alikofanyiwa matibabu, halafu akapandishwa ndege nyingine ya haraka na kurudi Ikulu Dar ambako alipokelewa kwa njia ya siri kupitia mlango ulioko baharini - akitokea meli ya nyambizi (submarine)..

Kwamba, tukio la leo kwa kweli halikuwa "live" ila lilirekodiwa kabla hajaugua na kuwa limeunganishwa vipande vipande kidigitally. Rais mwenyewe ameendelea mapumzikoni huko pembezoni mwa Milima ya Alps, Uswisi.

Yaani, ukishaamua kutunga uongo usiishie njiani, endelea nao hadi uonekane ni ujinga na watu wachukulie kama ni burudani fulani. Nje ya hapo jambo kubwa la kujifunza ni kuwa Rais Magufuli ule ulinzi labda hautoshi... kuna watu siyo tu wanaweza kuwa wanapanga mabaya, lakini wanayaombea, wanayasubiria, na kila waendapo kulala wanayaotea...

Ila ule uzushi ungenoga kama leo ungeendelea kidogo kuleta mantiki maana nilivyoona anashabikia sambusa na wasaidizi wake kama kuna kuumwa basi labda alipiga chafya tu kubwa watu wakashtuka na "kiwanda cha uvumi" kikaingia kazini.. Yaani, mtu hata kiungulia asipate.. na hakuna aliyefikiria hata ile connection ya suala la DPP uzito wake?

Sasa rais jamani hata chafya asipige. "Tuambiwe haraka alipiga chafya kubwa kiasi gani" , "Ni raisi wetu sote tunataka kujua kwa haraka... "

We unaonaje huu uvumi ungenoga noga vipi leo baada ya Jeuri ya Rais kuonekana leo..?
Ujumbe ni huu tu ama kuna kitu cha ziada umekiweka?
 
Nakubaliana nawe, naondoa hilo neno ''kila mtu'' kwa kuwa hakuna kigezo wala takwimu. Badala yake natumia ''hali iliyopo''. Swali linabaki pale pale, nini kimebadilika hadi hali ikawa kama ilivyo leo?

Kilichobadilika ni uwepo wa mitandao ya kijamii na upatikanaji mrahisi wa simu janja [ aka mitambo ya kuzalisha na kueneza ujinga na ujuha].
 
Ule uvumi umetufundisha mambo mengi; lakini kubwa ni kuwa mashine ya kuchakatia uzushi ilichakata sana jana.. lakini leo imeshindwa kuendelea. Baada ya Rais wa Watu kutokea leo akiwa na afya njema na kufanya kitu ambacho watu walitakiwa kukidhania kingefanyika (baada ya kufanya uteuzi) basi ule uvumi ulitakiwa ubadilike na kunogeshwa namna hii...

Kwa mfano,

Huyu wa leo siyo Magufuli ni double wake. Si unajua kila Rais ana "double" wake yaani mtu anayefanana naye kwa kila namna. Na huyu double tunaweza kusema alienda akafanyiwa "plastic surgery" huko Cuba na amekuwa akitumika mara kwa mara...

Kwamba, baada ya kuugua alikimbizwa Afrika ya Kusini, ambako alipanda ndege ya mwendo kasi hadi Ujerumani alikofanyiwa matibabu, halafu akapandishwa ndege nyingine ya haraka na kurudi Ikulu Dar ambako alipokelewa kwa njia ya siri kupitia mlango ulioko baharini - akitokea meli ya nyambizi (submarine)..

Kwamba, tukio la leo kwa kweli halikuwa "live" ila lilirekodiwa kabla hajaugua na kuwa limeunganishwa vipande vipande kidigitally. Rais mwenyewe ameendelea mapumzikoni huko pembezoni mwa Milima ya Alps, Uswisi.

Yaani, ukishaamua kutunga uongo usiishie njiani, endelea nao hadi uonekane ni ujinga na watu wachukulie kama ni burudani fulani. Nje ya hapo jambo kubwa la kujifunza ni kuwa Rais Magufuli ule ulinzi labda hautoshi... kuna watu siyo tu wanaweza kuwa wanapanga mabaya, lakini wanayaombea, wanayasubiria, na kila waendapo kulala wanayaotea...

Ila ule uzushi ungenoga kama leo ungeendelea kidogo kuleta mantiki maana nilivyoona anashabikia sambusa na wasaidizi wake kama kuna kuumwa basi labda alipiga chafya tu kubwa watu wakashtuka na "kiwanda cha uvumi" kikaingia kazini.. Yaani, mtu hata kiungulia asipate.. na hakuna aliyefikiria hata ile connection ya suala la DPP uzito wake?

Sasa rais jamani hata chafya asipige. "Tuambiwe haraka alipiga chafya kubwa kiasi gani" , "Ni raisi wetu sote tunataka kujua kwa haraka... "

We unaonaje huu uvumi ungenoga noga vipi leo baada ya Jeuri ya Rais kuonekana leo..?

Si ajabu ndege hiyo yenye kasi ya ajabu iliyompeleka kote huko, imetoka kwa wazee wa Gamboshi.
 
Tulipolazimishwa/kukubali kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi bila kujiandaa kama taifa, wenye uelewa wa masuala ya saikolojia walijua kitatokea nini?

Siasa za vyama vingi kwenye nchi ambazo zilikuwa na mfumo wa kijamaa zimezalisha taifa lililogawanyika katika pande mbili. Hakuna political meeting point ambayo inabeba hoja za pande mbili.

Mtu anayedhani Taifa limegawanyika katika utawala wa awamu ya tano atakuwa haijui vizuri Tanzania na siasa zake.

Hoja ya kusema tuwe na national dialogue ni ndoto za mchana katika mazingira yaliyozaa taifa linaloitwa Tanzania!

mkuu


nisingeweza kumjibu vizuri na kwa ustaarabu kama hivi

ningemtukana tu
 
Mkuu katika hili bila kumung'unya maneno wajinga ni kurugenzi ya mawasiliano kushindwa kutoa taarifa sahihi kwa wakati na kuruhusu tetesi kuzaa uhasama na njozi mbaya.
Kwani tokea juzi wangejibu kiaina yote haya yangetokea?
Kurugenzi isafishwe na kuwekwa wenye utaalamu sio wanaofanyakazi kama idara ya Polepole.

kwanini haumlaumu mzushi?
 
Tatizo kubwa sio mfumo wa vyama vingi, bali ni chama tawala kulazimisha kuwepo madarakani bila ridhaa ya wengi. Inaonekana chama tawala kulikubali kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi bila chenyewe kuwa tayari kwa hilo. Matokeo yake wananchi wengi wamesharidhia hali hiyo, huku chama tawala kikilazimisha kubaki chenyewe au madarakani kwa njia ya kunajisi box la kura. Hali hiyo inachangia mvutano na mgawanyiko usio wa lazima hasa anapotokea rais asiyeheshimu kutofautiana kimitazamo.
Wengi wanatafuta sababu zisizotoa jawabu. Vyama vingi vilikuwepo miongo dahari

Rais Mkapa kuna wakati alikerwa sana na vyama vingi.
Aliwajibu kwa hoja na mantiki.Aliwapiga kwa hoja na kuanzia hapo wakawa kimya.

Rais Kikwete, tofauti na Mkapa yeye alionekana kutojali sana wapinzani wanasema nini.

Viongozi hao walikuwa katika zama za mitandao na vyama vingi.

Nakumbuka hotuba ya Mw Nyerere pale Jangwani wakati akina Mrema wakiwa juu kisiasa.

Mwl aliona tatizo linaloweza kutokana na mgawanyiko wa mambo madogo ya siasa.
Mwl alijua kuna umuhimu wa watu kutofautiana kimitazamo bila kuhasimiana
Hilo litawezekana watu wakiridhiana bila chuki au vinyongo

Pengine kuna kitu sielewi au ninakiona ''upside down''.Uvumi sioni kama ni hoja

Ninachokiona ni picha ya uvumi huo, na kujiuliza kwanini uvumi umepewa nafasi kiasi hiki?

Kwanini haya yanatokea? Nini tofauti na nini kifanyike?Je, hizi si dalili njema za Taifa?
Kama siyo tumefikaje hapa Watanzania wenye upendo hata ''kushabikia'' uvumi na mabaya?

Hivi tukiondoa mitandao, tukafuta vyama vingi, tutawezaje kufuta ''hizi roho za kutakiana mabaya'' Kumbuka hizi ni ''intrinsic'', hujitokeza tu zenyewe, hatuna uwezo nazo

Kuna mzee hapa Kicheba alitueleza,mgonjwa wa akili akiongeza msikilize, utapata kitu

Hawa mashabiki na wazua uvumi wadharauliwe , lakini pia kuna kujitazama kupitia uvumi na uzushi wao iwapo kuna cha kujifunza , kama hakuna, tuwadharau

Tukiwaacha kama ''wagonjwa'' kwa hoja za vyama vingi na mitandao hatujitendei haki!

Tutakuwa tunalaumu jinsi wanavyosambaza uvumi wao(mitandao) kwa itakadi zao(vyama vingi) na kuacha hoja ya '' nini msukumo ulio nyuma ' hadi wanafikia kuzusha uvumi na uongo wa mabaya! tusiyoyataka wala kuyaombea!
 
Hakuna muunganiko wa chadema, usitegemee watu wenye akili ya kunguni wakaunganika! Walimtukana kila aina ya tusi kikwete, leo wanamlilia
Chadema sio watu wa kuwa entertain hata kidogo, ni kubana na kuwakanyaga kwa kadri utavyoweza!
Na namuomba mh. Raisi afanye jambo kwa wajinga hawa

Uko too emotional mpaka unakosa hoja ya msingi zaidi ya kuja na mitazamo ya kujipendekeza ili utoke kimaisha. Kikwete hakutukanwa bali aliambiwa ukweli wake, na hata sasa hakuna anayemlilia, bali anapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa ili kumnanga Magufuli. Kila siku rais anasifiwa hasafiri kama sehemu ya kujibu tuhuma za awali kuwa JK alikuwa anasafiri sana. Hii vita yenye double standard ya ufisadi ni kilio cha upinzani. Uwepo wa katiba mpya ni jambo lililopata msukumo sana kutoka hao cdm.

Ni hivi usimuombe rais afanye kitu kuhusu cdm, bali muagize achukue hatua yoyote atakayo dhidi ya cdm, kwani ni hujuma ipi hajafanya kuhusu cdm useme hivi sasa ndio atakuwa amefanya jambo jipya? Ana mwaka wa nne huu, katumia madaraka yake awezavyo kuwafanyia kila hujuma na bado cdm ipo, mshauri aifute kabisa ili uridhike. Maoni ya kujipendekeza kwa umri ulio nao yatakupa maisha ya kiwango fulani, ila cdm ikifa kipi kitapeleka tena familia yako chooni?
 
Back
Top Bottom