Lile fupa lililowashinda marais wanaume 4, rais mwanamke 1 aligegeda kama mlenda!. Miswada 3 ya ukombozi mpya wa taifa letu yatua bungeni asubuhi hii

Pale msomi anapoamua kua chawa na kusifia kitabu kwa picha ya jalada, acha tuendelee kutazama hiyo futuhi itaishia wapi, kwa sababu kama kuna kuna kitu sitawahi kukiamini basi ni serikali na watu wake wote hasa wale waigizaji wa isidingo walio jazana mle mjengoni
 
Kisome kitabu chote kabla ya kusifia.
 
Unaishi kwa matazamio na ndoto,hongera.
 
Ccm sija wahi kuwaamini mileld.
Rais anaweza kuwa na nia njema lakini wassidizi wake waka leta ushenzi kama ule wa bunge la katiba.
Wabunge walio pelekewa huo mswada wenyewe hawana legitimacy ya kukaa huko bungeni.
Uliwahi kuona haramu ikiwa halali?
Usitegemee miujiza kwa wabunge wezi wa kura walioko bungeni. Never
 
Bro are you being sarcastic ama!
Bunge ni kijiwe cha stori hamna kitu hapo..
Ni maumivu mtarajie
Mwenye kigoda yupo anatalii to the fullest karibu na kule mitulinga inarushwa kumwanganiza mwanadamu.
 
Nimeisoma hiyo miswada, SSH hayuko serious na mabadiliko. Hakuna tume huru ambayo mwenyekiti na makamu wake ni wateule wa rais ambaye ni mgombea kwenye uchaguzi huohuo.

Hakuna uchaguzi huru unaosimamiwa na wakurugenzi wa halmashauri wanaoteuliwa na Rais ambaye ni mgombea kwenye uchaguzi huohuo, tena watu hao ni makada wa chama cha rais.

Ni afadhali angeacha tu mambo yawe kama yalivyo kuliko kuwafanya watu kama vile ni wapumbavu.

Anyway, 2025 anakwenda kupumzika na kulea wajukuu, tusipoteze muda na hizi sarakasi zake. Tumngoje huyo ajaye.
 
Wewe Si wa kuaminiwa,

Mkataba Ule haramu ulipovuja ulianza hivi hivi,

Mara HGA zitakuwa wazi na kurekebishwa, saiz umeanza kusifia na hujaona kilicho ndani.

Nikikwita " Advanced Chawa" ntakuwa sijakosea.
 
Ntarudi kucomment content zake zikiwa hadharani.
 
Aisee kutumia neno kugegeda imenifanya nicheke…. Yani Rais ana ugegeda muswada hahahha refer maana ya kugegeda kwa hapa Jf?
We jamaa umesifia hadi umetoka nje ya mstari na hujui contents
 
Aisee kutumia neno kugegeda imenifanya nicheke…. Yani Rais ana ugegeda muswada hahahha refer maana ya kugegeda kwa hapa Jf?
We jamaa umesifia hadi umetoka nje ya mstari na hujui contents
Mzee kawa chawa nae yuko kwenye ligi ya kutafuta uteuzi na kina Lucas Mwashabwa. Najaribu kuvuta picha jinsi maza anagegeda daah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…