Linapokuja suala la IMANI, Waafrika wanampigania Mungu. Likija suala la Haki zao za msingi, wanamwachia Mungu awapiganie!

Binadamu ni kiumbe mpumbavu sana kwenye maswala ya Imani.

Yani unakuta mtu anatoa sifa kwa kiumbe cha kufikirika, Halafu waliofanya kazi ni binadamu wenzake kama yeye.
 
Wazungu wameshateka akili ya mwafrika kwa kutumia dini. Walitutisha na moto wa milele ili tupokee imani yao. Angalia tunavyojitahidi kujenga makanisa na misikiti imara, wenzetu wapo mbali na technology. Please! Let us wake up!! We need to come out from the cave.
 
sizungumzi suala la uvunjivu wa amani, hapana.

nazungumzia amani ya moyo, utulivu wa nafsi.
Kwani bila dini huwezi kuwa na amani ya moyo?

Kwani bila dini huwezi kuwa na utulivu wa hiyo nafsi?

Wahadzabe, Watindiga, Wasandawe na Bushmen hawana dini, ila wana amani ya moyo huko maporini. Na wana enjoy life kwa furaha huko maporini.

Sasa wewe unahitaji dini ikupe amani ya moyo?
dini inasaidia kudumisha mshikamano kwenye jamii...
Kwanza mataifa yenye dini ndio hayana umoja wala mshikamano.

Na kinacho changia ni utofauti wa kidini na kiimani.
fikiria jambo kama sala; linakufanya uwafikirie wenzako katika namna ya kuwajali, na pia uwe na shukrani kuhusu mafanikio yako.
Huihitaji sala ili uwafikirie wenzako katika namna ya kuwajali.

Kinacho hitajika ni utu na upendo ili kuwajali wengine. Sio sala.
mimi naona ni kitu kizuri...

japo ndio mungu yupo ila dhana ya dini inasaidia.
Hakuna msaada wowote wa dini zaidi ya kuleta utofauti, mabishano na chuki dhidi ya wanajamii.
 
Hili suala hunikera sana. Eti 'ahsante Mungu kwa huyu daktari'.. Bora hata kushukuru wazazi wake waliomlea na kumsomesha.
 
Akili za Yas hizo hohoooo ahouaaa
 
There are more churches and mosques in poor communities because the business of selling false hopes is more profitable than the work of creating solutions.
 
Vita vya Nyerere havikua vya kiimani. Vilikua vita vya Kitaifa, katika uongozi kwenda vitani ni sawa Kwa sabbau ya nafasi Yake, jifunze kuhusu vita vya Daudi na Shauri kwenye Biblia. Lakini mtu wa kawaida kwenda Kuua ni Dhambi
Vita vya kiimani ni nini? Vikoje? Fafanua.
 
Kuna upumbavu wa kuamini mambo ya dini yapo afrika tu. Nenda marekani na uingereza na wao pia dini zinafuatwa sana tu. Tuache kujizarau waafrika
 
Kuna upumbavu wa kuamini mambo ya dini yapo afrika tu. Nenda marekani na uingereza na wao pia dini zinafuatwa sana tu. Tuache kujizarau waafrika
Marekani na Uingereza watu hawategemei dini ziwape mafanikio.

Waafrika ndio wanategemea dini ziwape mafanikio kwa kutafuta miujiza makanisani kila siku.
 
Mungu ndiye Bwana wa mabwana,Mungu wa miungu, Mfalme wa wafalme.Mwanzo na mwisho yeye ndiye Alfa na Omega.

Mwenye uweza wote jemedari mkuu.

NB: Dini ni biashara ila Imani sio biashara. Tunaona biashara ya akina sunguye mwamposa inavyo nawiri Kila kunapokucha. Imani ndo Kila kitu
 
Dini zimewekeza kwenye matumaini feki ya upendo wa mungu wa dhahania ambaye kwenye simulizi zake za dhahania amedhihirisha ni mkatili tu na dikteta uchwara, ahadi hewa za mbingu isiyothibitishika na vitisho vya kuchomwa moto.

Wanauza huu upuuzi kwa watu waoga, wasioweza kufikiri sawasawa na waliokata tamaa.
 
Mkuu, naomba nikuulize..
Hivi nani alisema mungu ni mfalme wa wafalme. Ufalme ni cheo cha kibinadamu. Je, Mungu alingoja binadamu walete dhana ya ufalme Kisha naye ajifanye ndiye mfalme wao?
Pili, Mungu ni bwana wa mabwana gani hasa?
 
Mungu ndiye Bwana wa mabwana,Mungu wa miungu, Mfalme wa wafalme.Mwanzo na mwisho yeye ndiye Alfa na Omega.
Ni wewe tu unahangaika kumsifia na kumwelezea huyo Mungu wako wa kufikirika hapa.

Huyo Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo kwenye uhalisia.
Mwenye uweza wote jemedari mkuu.

NB: Dini ni biashara ila Imani sio biashara. Tunaona biashara ya akina sunguye mwamposa inavyo nawiri Kila kunapokucha. Imani ndo Kila kitu
If faith without work is nothing then faith itself is nothing.
 
Kumpigania Mungu ni sisi dhidi ya sisi, kupigania haki zetu ni sisi dhidi ya dola. Dola yenye jela, polisi, magari ya washawasha, secret detention areas n.k. Lazima uwe makini inapoelekeza vita yako.​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…