Linapokuja suala la IMANI, Waafrika wanampigania Mungu. Likija suala la Haki zao za msingi, wanamwachia Mungu awapiganie!

Linapokuja suala la IMANI, Waafrika wanampigania Mungu. Likija suala la Haki zao za msingi, wanamwachia Mungu awapiganie!

Mfano mimi hua nashangaa sana, Daktari anapambana kwa taaluma yake kuokoa maisha ya mtu.

Huyu mtu akipona, yeye na nduguze wanapeleka sadaka kanisani kushukuru, Mchungaji ananunua Range.

Daktari aliyeokoa uhai anaishia kupewa ahsante tu.

Sasa jiulize hapo, kati ya Mungu na Daktari nani aliyeokoa uhai?
Binadamu ni kiumbe mpumbavu sana kwenye maswala ya Imani.

Yani unakuta mtu anatoa sifa kwa kiumbe cha kufikirika, Halafu waliofanya kazi ni binadamu wenzake kama yeye.
 
Wazungu wameshateka akili ya mwafrika kwa kutumia dini. Walitutisha na moto wa milele ili tupokee imani yao. Angalia tunavyojitahidi kujenga makanisa na misikiti imara, wenzetu wapo mbali na technology. Please! Let us wake up!! We need to come out from the cave.
 
sizungumzi suala la uvunjivu wa amani, hapana.

nazungumzia amani ya moyo, utulivu wa nafsi.
Kwani bila dini huwezi kuwa na amani ya moyo?

Kwani bila dini huwezi kuwa na utulivu wa hiyo nafsi?

Wahadzabe, Watindiga, Wasandawe na Bushmen hawana dini, ila wana amani ya moyo huko maporini. Na wana enjoy life kwa furaha huko maporini.

Sasa wewe unahitaji dini ikupe amani ya moyo?
dini inasaidia kudumisha mshikamano kwenye jamii...
Kwanza mataifa yenye dini ndio hayana umoja wala mshikamano.

Na kinacho changia ni utofauti wa kidini na kiimani.
fikiria jambo kama sala; linakufanya uwafikirie wenzako katika namna ya kuwajali, na pia uwe na shukrani kuhusu mafanikio yako.
Huihitaji sala ili uwafikirie wenzako katika namna ya kuwajali.

Kinacho hitajika ni utu na upendo ili kuwajali wengine. Sio sala.
mimi naona ni kitu kizuri...

japo ndio mungu yupo ila dhana ya dini inasaidia.
Hakuna msaada wowote wa dini zaidi ya kuleta utofauti, mabishano na chuki dhidi ya wanajamii.
 
Mfano mimi hua nashangaa sana, Daktari anapambana kwa taaluma yake kuokoa maisha ya mtu.

Huyu mtu akipona, yeye na nduguze wanapeleka sadaka kanisani kushukuru, Mchungaji ananunua Range.

Daktari aliyeokoa uhai anaishia kupewa ahsante tu.

Sasa jiulize hapo, kati ya Mungu na Daktari nani aliyeokoa uhai?
Hili suala hunikera sana. Eti 'ahsante Mungu kwa huyu daktari'.. Bora hata kushukuru wazazi wake waliomlea na kumsomesha.
 
Imani za kidini barani Afrika ni zaidi ya madawa ya kulevya zimeharibu akili na mfumo mzima wa kufikiri wa waafrika.

Linapokuja suala la udini Waafrika wanampigania Mungu kwa nguvu zao zote wakitetea dhana ya kufikirika ambayo hawawezi hata kuithibitisha uwepo wake. Tena unakuta wanaipigania kwa nguvu zote na mabishano makali kabisa.

Lakini huyo Mungu wanaye mpigania miaka nenda rudi hajawahi kuonekana, kujitokeza, kujidhihirisha wala kuwasaidia chochote. Ni watu tu wanabaki kudai, kujifariji na kujipa matumaini uchwara kwamba wanasaidiwa na "Mungu" ilhali kiuhalisia ni wao wenyewe wanahenyeka na kukabiliana na matatizo yao.

Lakini cha kushangaza likija suala la kutetea na kupigania haki zao za msingi katika jamii wanamwachia Mungu awapiganie! Na huyo Mungu hajawahi kuwapigania kwa lolote.

Waafrika maskini wanazidi kuhujumiwa na viongozi wao wa kiserikali, Kodi zao zinaliwa, Haki zao zinaminywa, Mali na rasilimali zao zinaporwa na kutumiwa hovyo hovyo tu.

Halafu watu wanabaki kutulia na kusema tunamwachia Mungu, Mungu atatusaidia, Mungu atatulipia na kutupigania.

Sasa unajiuliza hizo nguvu za kumpigania huyo Mungu wa kufikirika kwenye dini,
Wakizielekeza na kuzitumia kwenye kupigania haki zao za msingi katika jamii zao si wataishi maisha safi kabisa?

Lakini kwa vile wengi wa waafrika wamesha pumbazwa na kuaminishwa utajiri na ufalme wa kufikirika mbinguni wala hawajihangaishi kupigania haki zao za msingi hapa duniani.

Watu wanaishi kwa kujipa matumaini uchwara ya maisha bora ya kufikirika mbinguni. Huku wakizidi kuteseka na umaskini wao, kuhujumiwa na kusulubishwa ipasavyo na viongozi wao wa serikali.

Katika maswala ya "Imani" binadamu ni kiumbe mpumbavu sana. Badala ya kujipigania yeye mwenyewe, Anapigania dhana ya kufikirika iitwayo Mungu ambayo kiuhalisia hata haijawahi kuwepo na haipo kujidhihirisha yenyewe.

No amount of prayers, faith, hope and grace can solve your problems in life for you.

No matter how strong you shout or scream the name of God in what you call praying, Your life will be miserable if you don't think, reason, plan and take productive actions to solve your own problems in life.

During those darkest moments in life when it feels like God has abandoned you, Remember that God was never with you in the first place. Because he doesn't exist in reality. He exists only in your head and in your imaginations.

The same God who has disappointed uncountable people in the world, Keep disappointing many people daily including you.

Any country waiting for God to come and help them will forever remain poor economically, medically, academically, technologically until such mental slavery religious faith is totally abolished.

Any person waiting for God to come and solve his or her problems in life will forever remain poor financially, Until such mental slavery religious faith is totally abolished.

In the jungle of life salvation is largely on your hands. No God, spiritual power or ritual can solve your problems.

If you are born into a poor financial foundation and you keep waiting for God to come and help you, You will suffer financially and die miserably.

Poverty strikes hard when laziness and ignorance is combined with prayers.

Take this bitter truth and let it sink deep in your mind.

I'm out.
Akili za Yas hizo hohoooo ahouaaa
 
Wazungu wameshateka akili ya mwafrika kwa kutumia dini. Walitutisha na moto wa milele ili tupokee imani yao. Angalia tunavyojitahidi kujenga makanisa na misikiti imara, wenzetu wapo mbali na technology. Please! Let us wake up!! We need to come out from the cave.
There are more churches and mosques in poor communities because the business of selling false hopes is more profitable than the work of creating solutions.
 
Vita vya Nyerere havikua vya kiimani. Vilikua vita vya Kitaifa, katika uongozi kwenda vitani ni sawa Kwa sabbau ya nafasi Yake, jifunze kuhusu vita vya Daudi na Shauri kwenye Biblia. Lakini mtu wa kawaida kwenda Kuua ni Dhambi
Vita vya kiimani ni nini? Vikoje? Fafanua.
 
Kuna upumbavu wa kuamini mambo ya dini yapo afrika tu. Nenda marekani na uingereza na wao pia dini zinafuatwa sana tu. Tuache kujizarau waafrika
 
Kuna upumbavu wa kuamini mambo ya dini yapo afrika tu. Nenda marekani na uingereza na wao pia dini zinafuatwa sana tu. Tuache kujizarau waafrika
Marekani na Uingereza watu hawategemei dini ziwape mafanikio.

Waafrika ndio wanategemea dini ziwape mafanikio kwa kutafuta miujiza makanisani kila siku.
 
Mungu ndiye Bwana wa mabwana,Mungu wa miungu, Mfalme wa wafalme.Mwanzo na mwisho yeye ndiye Alfa na Omega.

Mwenye uweza wote jemedari mkuu.

NB: Dini ni biashara ila Imani sio biashara. Tunaona biashara ya akina sunguye mwamposa inavyo nawiri Kila kunapokucha. Imani ndo Kila kitu
 
Dini zimewekeza kwenye matumaini feki ya upendo wa mungu wa dhahania ambaye kwenye simulizi zake za dhahania amedhihirisha ni mkatili tu na dikteta uchwara, ahadi hewa za mbingu isiyothibitishika na vitisho vya kuchomwa moto.

Wanauza huu upuuzi kwa watu waoga, wasioweza kufikiri sawasawa na waliokata tamaa.
 
Mungu ndiye Bwana wa mabwana,Mungu wa miungu, Mfalme wa wafalme.Mwanzo na mwisho yeye ndiye Alfa na Omega.

Mwenye uweza wote jemedari mkuu.

NB: Dini ni biashara ila Imani sio biashara. Tunaona biashara ya akina sunguye mwamposa inavyo nawiri Kila kunapokucha. Imani ndo Kila kitu
Mkuu, naomba nikuulize..
Hivi nani alisema mungu ni mfalme wa wafalme. Ufalme ni cheo cha kibinadamu. Je, Mungu alingoja binadamu walete dhana ya ufalme Kisha naye ajifanye ndiye mfalme wao?
Pili, Mungu ni bwana wa mabwana gani hasa?
 
Mungu ndiye Bwana wa mabwana,Mungu wa miungu, Mfalme wa wafalme.Mwanzo na mwisho yeye ndiye Alfa na Omega.
Ni wewe tu unahangaika kumsifia na kumwelezea huyo Mungu wako wa kufikirika hapa.

Huyo Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo kwenye uhalisia.
Mwenye uweza wote jemedari mkuu.

NB: Dini ni biashara ila Imani sio biashara. Tunaona biashara ya akina sunguye mwamposa inavyo nawiri Kila kunapokucha. Imani ndo Kila kitu
If faith without work is nothing then faith itself is nothing.
 
Kumpigania Mungu ni sisi dhidi ya sisi, kupigania haki zetu ni sisi dhidi ya dola. Dola yenye jela, polisi, magari ya washawasha, secret detention areas n.k. Lazima uwe makini inapoelekeza vita yako.​
 
Back
Top Bottom