Lindi: Ally Chinga mkazi wa kata ya Msinjaili, amefungiwa ndani na kupuliziwa dawa ya Mbu kwa tuhuma za Wizi

Lindi: Ally Chinga mkazi wa kata ya Msinjaili, amefungiwa ndani na kupuliziwa dawa ya Mbu kwa tuhuma za Wizi

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Screenshot_20211228-202028.png

Kijana mmoja aliefahamika kwa jina la Ally Chinga mkazi wa kata ya Msinjaili manispaa ya Lindi amefungiwa ndani na kupuliziwa dawa ya Mbu baada ya kupigwa na mtu aliyemtuhumu kuiba betri ya gari leo Disemba 28, 2021.

Imeelezwa kuwa, Mtuhumiwa huyo ambaye ni kondakta, alipewa gari hiyo kwenda kujaza mafuta na dereva wake Mussa Mshamu na baadae ndipo ikasemekana aliiba betri hiyo jambo ambalo mtuhumiwa huyo amelikana.

Mjumbe wa mtaa huo Bi. Rehema Omary amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa, dereva huyo sio mara yake ya kwanza kufanya hivyo jambo ambalo limekuwa kero mtaani hapo huku akikemea vikali matukio ya kujichukulia sheria mkononi.

Chanzo: Mashujaa FM
 
Sasa Dawa ya mbu imepuliziwa room au kapuliziwa mtu?

Hamna case hapo.
 
Kama alofanya vile ni mtu mzima mwenye Akili zake timamu,
Basi atakua hajamsingizia, uyo dogo kaiba kweli au kushiriki huo wizi.

aliyofanyiwa Ni sawa TU Tena alitakiwa achomwe Moto kabisa apotee DUNIANI.

Mahakama na polisi vimekua sio tishio Tena kwa wezi.
 
Story ya upande mmoja Hii[emoji848]

Sema Tatizo sikU hizi kumeibuka wimbi kubwa la ndugu wanafamilia wa wezi kuja mitandaoni kuwatetea vijana wao wanaposhughulikiwa kwa kutafuta huruma ya jamii.

Ndo maana,
Tunataka Katiba mpya itamke wazi kua ndugu wa wezi nao wachukuliwe hatua kwa kufeli kwao katika malezi na kufuga wezi.

WIZI KILA SIKU TUSHACHOKA SISI[emoji3525]
 
Amepata madhara yoyote baada ya kupuliziwa hiyo dawa? , pole yake
Nyie ndo mnaofuga wezi sasa,

wezi (hasa Hawa wa sio vifaa vya magari) wa kuchomwa moto kabisa.

Wanaiba Gari wanaiacha Kama skeleton[emoji3525]
 
Sasa si kweli ameiba we upewe gari kwenda sheli irudi bila betri kwamba limeibiwajwe biwajwe.
 
Hao wamama wangekuwa wazaramo wangemsuta mpaka angekufa..wazaramo hawapigi mwizi wanamsuta mpaka anakufa kwa amani kabisa
 
"huku akikemea vikali matukio ya kujichukulia sheria mkononi''.

HIVI WEZI WAO WANATUMIA SHERIA GANI KUHALALISHA WIZI WAO?


KAMA MTU ANAJICHUKULIA SHERIA MKONONI KUIBA VYA WENGINE, KWA NINI WENGINE WASIJICHUKULIE SHERIA MKONONI KUMUADHIBU?
 
Back
Top Bottom