Lindi: Mtumishi wa LATRA amtishia sime dereva wa lori ili ampe leseni

Lindi: Mtumishi wa LATRA amtishia sime dereva wa lori ili ampe leseni

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191


Emmanuel Manase, Mtumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (LATRA) alimtolea sime dereva wa lori akimtaka ampe leseni yake.

Tukio hilo limeonekana kuwa na ugomvi mkubwa na baadae mtumishi huyo aliamuru dereva aandikiwe faini ya Tsh. 500,000 ili kumkomoa.

Umoja wa Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) wamelaani tukio hilo kwa kuwa kama asingekuwa afisa wa polisi katika tukio lile wanasema yangetokea madhara makubwa.
 
Hii ndiyo inaitwa kufanya kazi kwa mazoea, inaonekana hizo tabia keshazoea huyo
Hivi vitu ndiyo unakutana na mtu ambaye ameshapiga cha Arusha, na kiunoni ana mguu wa kuku anakufumua ubongo na hicho kisime chako. Mwenzio ataishia kifungo cha maisha (maana kusaini kifo nayo mtihani) wewe umeshatangulizwa motoni huko.

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
 
Huyo dereva anatakiwa akafungue kesi ya kutishiwa maisha hiyo ni haki yake kabisa kama alishikiwa sime.

Latra ni nani had aombe leseni yeye amekua polisi? Mi nisingetoa halafu ningemtandika kinyama kunishikia sime ni kunitishia kuniua ni lazima nijihami, kwanza hana mamlaka ya kunikagua leseni.
 
Askari wa trafiki hapo wameonesha busara ya hali ya juu ila huyo jamaa wa LATRA sjui ni ushamba au
panga la nini tena hapo, angempiga nalo si angejitafutia balaa au ndiyo kutaka kujionesha shujaa?

Ova
 
Back
Top Bottom