Lissu aisimamisha Kilimanjaro, Moshi mjini wamsubiri hadi usiku, waimba rais, rais, rais hawataki Lissu awanyamazishe

Ni baba mpumbavu pekee kama stone anayeweza kusifiwa kwa kumnunulia mkewe Iphone X lakini aliacha mwanae akafa kwa kukosa laki moja ya matibabu. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8[1](a) inasema "Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa (wananchi) WATU sio ustawi wa VITU. Asomaye na afahamu.!
 
Hatari sana. Lakini vipi kisheria imekaaje mpaka giza limeingia si kosa?
 
Huyu Mwamba ni kiboko.
Naambiwa Lissu alipaswa kuwa na mkutano Moshi mjini saa tisa mchana, watu wakaanza kumsubiria toka asubuhi uwanjani, kufika saa kumi jioni bado hajafika Moshi mjini(maana msafara wake ulikuwa unasimamishwa njiani na wananchi wakitaka kumuona na kumsikia), joto la mashabiki likawa linazidi kupanda, Polisi ikabidi wafunge barabara za karibu na uwanja ili kupunguza foleni za magari na kupunguza msongamano kukaribia uwanja.
 
Your browser is not able to display this video.

Mimi niliwapa tahadhari toka awali kwamba hizi mnazoziona na kuzishuhudia ni rasha rasha tu, mvua za vuli zinakaribia na kuna watu wanaweza wakabwaga manyanga mapema kwani wakiendelea kukaidi hakutakuwa na namna bali kuvuna walichopanda...bye bye jiwe!
 
Uko sahihi kabisa. Barabara zilifungwa na watu walijaa hadi barabara zote za kuingia uwanjani.
 
Hatari sana. Lakini vipi kisheria imekaaje mpaka giza limeingia si kosa?
Naambiwa ameombwa na polisi waliokuwa wakilinda doria hapo uwanjani afike tu awasalimie na kuwaomba watawanyike ili watu waliokuwa wakimsubiria waridhike na waende majumbani. Nguvu ya polisi isingeweza kuwaondoa kirahisi hao watu walioapa kukesha hapo uwanjani na barabarani mpaka wamuone Lissu na kumsikia.

Naambiwa Umati wa watu tayari ulikuwa umekusanyika uwanjani karibu na barabara ya Moshi-Arusha kiasi cha kuifunga barabara kwa muda.
 
Amini usiamini,
Lissu ana kusudi la Mungu maalumu kwa Tanzania.
Ama ni Zuri au ni baya lakini ni lazima litimie maana limekusudiwa.
Faraja kuuu kwetu na tumaini pekee, .ni kwamba Mungu kwa watoro wake Tanzania amekusudia kutupa mema.
Muuumba tunakusihi hili jema ulilokukusudia kutupa lipitishie kwa mtoto wako TA lissu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…