Pre GE2025 Lissu anaipa ushindi CCM mapema sana

Pre GE2025 Lissu anaipa ushindi CCM mapema sana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tume huru tunayo au unazungumzia ipi mkuu?
Kwa hiyo Tume hii inayoshuhudi uenguaji na mauaji ya Wagombea wa Upinzani kila mara kwako ni sawa?? Sasa Mh Lissu alichosema hawako na hawatakuwa tayari kuwapeleka Vijana au Watoto wa Kitanzania kwenye uchaguzi utakaosimamiwa na tume zile zile wakauawe. Mauaji ya kila mara wakati wa uchaguzi sasa basi.
 
Shida ya Africa sio tume huru wala chaguzi huru bali kupata mifumo itakayo badili akili za waafrika waweze kuona fursa tele zinazowazunguka ili watatue shida zao.
Mambo ya uchaguzi ni matumizi mabaya tu ya fedha zetu
Wewe ni katika wachache wenye akili. Uongozi unapimwa hata kwako wewe binafsi. Uwezo wako, fikra yako, socialization, Lakini hata humu kwenye group unakuta mtu ni mbaguzi Lupita kiasi, matusi kupita kiasi, unaweza ukajifunza kuwa tuna watu wa namna gani ktk nchi. Watu hawa ndio tunategemea wounded dola, wakawe watumishi ktk ngazi tofauti, tutegemee Mimi kama sio umasikini. Wizi kwa Watanzania imekuwa ni biological trait. Mtu anajiibia hata yeye m wenyewe.
Uwongo ndio fashion, unadanganya mpaka mkeo, pesa umehonga ukiulizawa Majibu yake ni wewe jua imeisha tu, ukivyokula vilitokana na nini. Duu ni shida
Ila Sisi tuna utamaduni tofauti Lisu ajue, hatuwezi kuwa kama Kenya au Congo Lisu anakolinganisha. Afanye siasa kwa kuangalia utamaduni wa mtanzania. Akifanya siasa kama Kenya au Congo lazima afeli, Sisi ni watu wa Amani, ukitaja taja tu Congo au Kenya au Somalia inatosha Watanzania kukutosa hata kama ni masikini, Sisi kwetu cha muhimu ni Amani.
 
Mama je wote Wana CCM wanamkubali?
Hawezi kupendwa na wote lakini anaonesha kuwahitaji wote,anajipambanua kwa wote,wanadini,wanasiasa wenzie,wanamichezo,wasanii,mitaani mabonanza,mpaka chini ubalozini na hivyo vyote hakuna kiongozi wa upinzani aliyezuiliwa kuvifanya,viwe na umuhimu visiwe na umuhimu ila vinavuta watu upande wake! Na siasa kabla ya uchaguzi ni watu,mengine ni baada ya uchaguzi.

I'm signing out!
 
Hakuna tume huru duniani inayoweza kutenda haki,tume bora lazima iwe haiko huru.LAZIMA IDHITIWE TENA IDHITIWE HASWA NA SHERIA,ili isiwe huru kufanya lolote lililo kinyume na haki,maana ikiwa huru itakuwa imepewa haki ya kufanya vyovyote na isifanywe lolote maana iko huru kisheria!
Iabda hoja kwa mtazamo wangu iwe namna iyo tume inavopatikana!

..uko upande mzuri kwasababu unazungumzia HAKI.

..pia umeweka msisitizo kuhusu namna Tume Huru inavyopatikana.
 
Ni kweli ccm wana hela nyingi,wana miradi,wana wafadhili na zingine wanaweza kuwa wanajichotea kwa sababu wako jikoni.lakini hii bado haijawapa kiburi cha kuacha kubembeleza na kushawishi watu wawaunge mkono.

Hata chadema wanapokea ruzuku,
Hata chadema wana wafadhili.

Je,lisu hanufaiki na hizo fedha?
Je ni kosa chama kutumia fedha zake kuwalipa watu wenye ushawishi kujiongezea watu na umaarufu?

Mi nafikiri chadema na wao wanatakiwa kubadilika,kutenga fungu la wasanii kwenye kila idara,wasanii,vyombo vya habari kote huko watu wako kazini,wanatafuta riziki na sio machawa kama tunavowaita!

Ni kweli ajira ni tatizo ndio maana hata lisu ni msomi ila aliamua kujiajiri kwenye siasa na imemlipa sana leo ana maisha mazuri kupitia hizi hizi siasa.
Sasa kama viongozi wa chadema waliopita wangegomea chaguzi yeye na kina msigwa,heche,sugu,mdee,mbowe na wengine walionufaika tungewajua Leo kupitia siasa?

Chadema inatakiwa kubadilika,ccm wanatumia nyenzo zote walizonazo,wanaonesha hata kidogo walichoahidi na kutimiza au kuanza,wana ahidi kikubwa,wanajichanganya na wananchi na wanapiga hadi magoti kwa wananchi inapofikia swala la kuomba kura.

Nikupe tu mfano kwenye mji niliopo,ccm iliungana na serikali bega lwa bega kuhamasisha watu kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.na hakukuwa na mwanachadema hata mmoja alieyehasisha watu kujiandikisha,hata lisu hakufanya hivyo.
Je,unahisi hao watu walijiandijisha ccm watakubali kuwapoteza kirahisi?

Chadema iache siasa za matamko na mtusi,ishuke chini kwa wananchi.
Hakuna kura za huruma,kura zinatafutwa.
CCM wanachofanya kuhamasisha umma kushiriki katika michakato ya chaguzi si kwa ajili ya kupenda sana watu washiriki, bali ni katika kuhalalisha wizi wa kura wanaoufanya.

Kuna kituo mwaka 2020, kura za urais zilizidi mara mbili zaidi ya idadi ya wakazi wote wa huo mtaa.
Wapigakura halali kwenye daftari ni 130, lakini idadi ya kura za mgombea wa CCM ni 322.
 
Subira the princess Jipe muda uone kama huta muona ndugai akimpigia kampeni samia, ccm inapofikia wakati wa maslahi ya chama na kukilinda chama wako makini kuliko vyama vyote nchini,hawana uadui wa kudumu,na huo ndio ukamavu wa kisiasa,jipe muda utamuoana ndugai!
Ukiwa "kigogo" ndani ya CCM halafu ukaenda kinyume nao, basi yatakukuta kama yaliyowahi kuwakuta wakina Kolimba, Abdu Jumbe, Mangula.
Unaweza kuKolimbwa.
Unaweza kubambikiwa kodi ya mabilioni kwenye biashara zako.
Unaweza kusingiziwa mambo mengi sana.
Tumeyaona.

CCM inapokuja kwenye swala la kulinda maslahi yao, wapo tayari kuwa zaidi ya shetani, na hilo ndilo linalowaogopesha watu wenye hoja za msingi huko CCM.
 
Kwanza,kwenye chama chake tu kuna watu zaidi ya 40% hawamkubali,hiyo imethibitika kwenye uchaguzi mkuu wa chama,hata kama atapambana kuwarudisha, hutawarudisha wote.wengine atakua nao ila hawatakua upande wake abadani,na huo ndio ukweli akubali ukatae!

Hoja ya kugomea uchaguzi na kutangaza kuzuia uchaguzi mapema hivi ni dalili ya uoga na kukubali kushindwa mapema sana,yani umetupa taulo hata kabla hujaingia ulingoni.maana kama hoja ni katiba na tume tu inabidi utuambie kwanza wakati ulipokua mbunge ulitangazwa mshindi kupitia katiba na tume za namna gani?

Je kama tume zilikua hazitendi haki,je na wewe ulipokua mbunge ubunge uliupata kinyume na haki? Tambua kuwa sibezi hitaji la katiba na tume bora yenye kujisimamia.ila kususia uchaguzi kwa hoja hiyo ni kichaka cheupe sana ikiwa viongozi wengi tu ukiwemo wewe mwenyewe ulitangazwa mshindi na tume hizo hizo tunazozilalamikia.

Vijana wengi saizi ni ccm tena CCM haswa,kwanini vijana wengi wanakua CCM,kwa sababu wanajionea ukiwa CCM kuna chochote kitu unapata,japo hili hutakubaliana nalo ila haitabadilisha ukweli.vijana saizi wanataka hela,na wanaelewa vyama vyote vina hela.wanaona vijana wenzao waliopo CCM wanavyopata hela na fursa,sasa yeye aendelee kufanya siasa za kuchangisha wanachama bila kuwaeleza fungu la ruzuku lime limefanya kazi gani! Ujinga una mwisho(sisemi kwa ubaya bali hoja).

Siasa ni watu na CCM inatafuta watu usiku na mchana,majumbani,makanisani,misikitini,michezoni.popote palipo na watu CCM ipo na ina watu wake hapo.na yote inayofanya CCM hakuna chama kinazuiliwa kufanya.nyinyi endeleeni kujifungia ofisini mkitoka mnatangaza migomo na kuwatukana wahamasishaji na washawishi wa ccm kuwa ni machawa.haya! Machawa hao hao wanasepa na kijiji! Mkija kushtuka kuwa mliokuwa mkiwabeza na kuwakashifu kumbe wana umuhimu, kumekucha!

Lingine niwambie CHADEMA kuwa wasiishi wakati uliopita,maana katika wakati huu wapenzi wao wengi iliokuwa nao chaguzi mbili mpaka tatu zilizopita,wengi wao wamevujwa mioyo sana na mienendo ya viongozi wao wa juu tatika hizo chaguzi,na ukweli wengi wamejiunga au wamehamia ccm na wengine kuchukia na kuachana kabisa na siasa.

Na kosa lingine analofanya mwenyekiti mpya CHADEMA ni kutangaza hadharani hahitaji muungano na chama kingine.anaamini yeye ndio yeye na anaweza peke yake,wakati hata ccm wanapambana kuungwa mkono na vyama vingine yeye anagoma.yaani unafanya siasa halafu hutaki watu wakuunge mkono.
CCM ukiona hawamtaki mtu ujue huyo mtu hawaungi mkono na amegoma kubadilika au kushawishika.

Na katika hili CCM wameweza sana,wamewekeza sana katika watu,wapo karibu sana na watu,kutoka ngazi ya taifa hadi ubalozi wa nyumba kumi,na inawalipa!

Huu ndio ukweli japo ni mchungu.

Sisi CHADEMA tuendelee kujifungia ofisini, tukitoka tunaita waandishi wa habari,tunakashifu vyama,viongozi wa nchi,wa dini,wa taasisi,wasanii na wote wanaoiunga mkono CCM kana kwamba wanachofanya ni ni kosa kikatiba.,

Tuendelee kutafuta kuhurumiwa huku tunatangaza migomo na fujo kisha tunaomba michango mwisho tunagawana posho za ruzuku, tupanda V8 zetu nyumbani kutulia na familia zetu tukiendelea kufuatilia maoni ya wanachama wetu mitandaoni.wakati ccm wako mtaa kwa mtaa nyumba kwa nyumba wakihamasisha watu kujiandikisha na kuwaunga mkono!

Na hakika wanawapata! Maana

Siasa ni sanaa na sanaa ni kazi! Naona wengi wapo kazini kushawishi,wachache wanatia huruma kukashifu na kutukana(timing mbovu kabisa).

Muda ambao unatakiwa kuji-brand unampaisha mshindani kwa kumtajataja kila ulipo.

Mgonjwa hakatai dawa, akikataa dawa ujue hali ni mbaya!

Mida!
Bila mabadiliko ya sheria na kanuni za uchaguzi Tume ya uchaguzi imeshaipa CCM ushindi hata kabla kupigwa kura.
 
Back
Top Bottom