Lissu Anaungwa Mkono na Watu Wababaishaji wasio na Ushawishi wala kukubalika kwa Jamii


Kwa nini mambo ya ndani ya nani anaongoza CHADEMA yanakusumbua sana wakati wewe si mwanachama wa CHADEMA?
 
Kwa nini mambo ya ndani ya nani anaongoza CHADEMA yanakusumbua sana wakati wewe si mwanachama wa CHADEMA?
Hayanisumbui hata kidogo.lakini ni lazima ufahamu kuwa mimi ni mlipa kodi ambayo inatumika pia kuilipa CHADEMA Ruzuku
 
funua maandiko, uone yesu aliungwa mkono na watu wa aina gani, then uje kulinganisha na mashudu uloandika hapa.

mpenda haki yeyote, huungwa mkono na wengi, bila kujali ni watu wa aina gani.
 
Kwani Mbowe amekuwa anakuwa madarakani kwa kupigiwa kura au kulazimisha kwa nguvu? Si amekuwa anachaguliwa na wana CHADEMA wenyewe kuendelea kuwa Mwenyekiti wao?
Kwa hiyo unataka Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti?
 
Sawa,, wewe humuungi mkono, kwan una akili, una ushawishi?
 
Hapa umeandika ukweli mtupu aiseee, nimeshangaa kuona Sativa mtukanaji wa kule X katoa hela ya Mheshimiwa Lissu kuchukulia form ?
 
Ya Tundu lisu yanakuhusu nini wewe *bwa
 
Hayanisumbui hata kidogo.lakini ni lazima ufahamu kuwa mimi ni mlipa kodi ambayo inatumika pia kuilipa CHADEMA Ruzuku
Wewe kuwa mlipa kodi hakukupi haki yoyote ya kuingilia mambo ya ndani ya uchaguzi wa CHADEMA.

Zaidi, wewe mwana CCM tukikuona unamshabikia kiongozi fulani wa CHADEMA tunapata shaka na huyo kiongozi na kuona labda CCM mmemnunua ndiyo maana mna m promote.
 
Kama CCM mnajiamini iga muone😂
 
Tangia lini Mwamba akanunuliwa?
 
Kitendo cha wewe mwenye upeo wa 'kihayawani' kudai ya kuwa hafai hii inamaana ya kwamba anafaa sana.
 
Hatuna cha kuiga maana sisi ni chama kiongozi Barani Afrika na Dunia kwote kwa ujumla wake
Ndo maana mnaishia kutoa fomu ya mgombea mmoja tu kwenye chama chenu ruhusu mchuano muone mtakachoambulia mnajiita chama cha Mapinduzi ila mnaogopa kufanya hayo mapinduzi🤯
 
Ndo maana mnaishia kutoa fomu ya mgombea mmoja tu kwenye chama chenu ruhusu mchuano muone mtakachoambulia mnajiita chama cha Mapinduzi ila mnaogopa kufanya hayo mapinduzi🤯
Mchuano na nani? Wenye chama ndio tumeamua kuwa Fomu ya Urais ni Moja tu kwa ajili yake Mama yetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.hii ni baada ya kufanya kazi kubwa sana ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi iliyoleta tabasamu na matumaini makubwa kwa mamilioni ya watanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…