Pre GE2025 Lissu awasili Mlimani City akiwa ndani ya gari yake aliyopigwa nayo risasi Dodoma na watu wasiojulikana, tena ikiwa bado na matundu yake ya risasi

Pre GE2025 Lissu awasili Mlimani City akiwa ndani ya gari yake aliyopigwa nayo risasi Dodoma na watu wasiojulikana, tena ikiwa bado na matundu yake ya risasi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mgombea wa Uenyekiti CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, amewasili Mlimani City akiwa ndani ya gari alilopigiwa risasi na watu wasiojulikana mjiji Dodoma mwaka 2017 likiwa bado na alama za risasi katika ubavu wa kushoto ambao alikaa wakati akishambuliwa, ambapo leo Januari 21, 2025 unafanyika uchaguzi wa kuwapata viongozi wa juu wa chama hicho.

Soma, Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA nafasi ya Mwenyekiti & Makamu Mwenyekiti 2025: Ni Mbowe au Lissu?

Lissu amewasili katika viwanja vya ukumbi huo saa 10:15 asubuhi, akiwa ndani ya gari jeusi la Land Cruiser lenye namba za usajili T216 DHH. Kitendo cha Lissu kuingia Mlimani City akiwa ndani ya gari aliyopigwa nayo risasi, tena ikiwa bado na matundu ya risasi, kumeibua hamasa kubwa kutoka kwa wafuasi wake.

Snapinst.app_474652697_8997444453696272_8782384701939738942_n_1080.jpg

Kupata matukio ya nyuma kuhusu watu wasiyojulikana ingia hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Ila siasa bwana!!!

Labda nikose kitu cha kufanya kabisa yaani hata kulala kuwe tena siyo kitu cha muhimu ndiyo na mimi nitasema sasa ngoja nikasukume gari la mwanasiasa kuonyesha mahaba kwamba namkubali sana.
 
Anatafuta kura za huruma kama ambavyo alifanya akigombea umakamu mwenyekiti

Anasaka kura za huruma wakati hana huruma na mwenyekiti wake Mbowe anamponda anaponda hadi Chadema na kukivua nguo na kukichafua kionekane rushwa tupu

Hana huruma kuchafua image ya chama halafu yeye anataka huruma za wapiga kura
Hayuko sahihi

Image ya chama ndio kila kitu
 
Anatafuta kura za huruma kama ambavyo alifanya akigombea umakamu mwenyekiti

Anasaka kura za huruma wakati hana huruma na mwenyekiti wake Mbowe anamponda anaponda hadi Chadema na kukivua nguo na kukichafua kionekane rushwa tupu

Hana huruma kuchafua image ya chama halafu yeye anataka huruma za wapiga kura
Hayuko sahihi

Image ya chama ndio kila kitu
Ana qualify
 
Huyu ndiye atanifanya niendelee kuwa Chadema ama lah

Haya yote, ni siku hii hii ya leo kati ya hayo mawili, moja litakuwa chaguo langu, na wala stajutia kwa lolote kama ambavyo nimekuwa sijutii kuwa Chadema kipindi kirefu kilichopita,

Chadema inapojinadi kuwa chama cha Demokrasia basi ni mhimu itofautiane na vyama vyote maana huko kote kuna kusiginwa wazi wazi kwa katiba zao pia katiba ya nchi

Ni vyema Mbowe akalielewa hili
 
Ila siasa bwana!!!

Labda nikose kitu cha kufanya kabisa yaani hata kulala kuwe tena siyo kitu cha muhimu ndiyo na mimi nitasema sasa ngoja nikasukume gari la mwanasiasa kuonyesha mahaba kwamba namkubali sana.
Kama unaweza kuwa na mahaba na mpira wa miguu, hata siasa vivyo hivyo
 
Back
Top Bottom