Uchaguzi 2020 Lissu hili la Vyama vya Ushirika umedanganywa na sisi umetudanganya

Uchaguzi 2020 Lissu hili la Vyama vya Ushirika umedanganywa na sisi umetudanganya

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
16,054
Reaction score
11,568
Juzi ulivyokuwa mwanza uliongelea kuhusu wakulima wa pamba kukopwa Pamba yao na wanunuzi binafsi wa Pamba. Naona mkuu haukuwepo nchini muda mrefu. Naomba nikusaidie.

1. Msimu wa pamba 2019/2020 hakuna mfanyabiashara aliyenunua Pamba moja kwa moja kwa mkulima, pamba ilinunuliwa na halmashauri za vijiji na hao wamiliki wa vinu vya pamba walienda kununua Pamba kwenye halmashauri za vijiji kwa kulipa taslimu hakuna pamba iliyokopwa na mnunuzi binafsi.

Tatizo lilikuwepo halmashauri ya Bunda ambapo halmashauri nyingi za vijiji ni za chadema na hao viongozi walivyopelekewa fedha badala ya kuwalipa wakulima walizitumia kwa shughuli zingine na kuwakopa wakulima pamba yao kwa kuwadanganya fedha hazijaja.

Serikali ilivyowafuatilia walianza kudai serikali inawafuatilia kwa kuwa wao ni wapinzani, nashukuru takukuru waliingilia kati na walirejesha fedha hili Wenje analijua Ester Bulaya analijua sijui kwanini waliamua kumpotosha muheshimiwa Lissu.

2. Kufujwa kwa mali za NCU, hili JPM kalivalia njuga za kutosha na mali zote za NCU zimerudishwa mikononi mwa ushirika na wapo wafanyabiashara wabishi ambao walidiriki hata kuwapiga risasi maafisa wa serikali waliokuwa wanafuatilia urejeshwaji wa mali za NCU, hivyo anavyosema mali za NCU zimefujwa hapana ziko salama na uongozi wa NCU uko imara.

3. Madai ya Lissu kuwa Pamba inanunuliwa na wana CCM, ni madai ya kijinga tu mnunuzi ambaye ni mwana ccm ni Gachuma naye ana hisa kidogo sana kupitia Bulamba Gingery, hisa nyingi ni za Sumaria Group. Wanunuzi wakubwa wa Pamba ni Bilchard na Gupta group hawana uhusiano wowote na CCM niwafanya biashara huru tu.

Naomba mumwambie Lissu asifikiri yuko Bungeni hivyo anaweza wajibika kisheria kwa uongo wake anaotapanya.
 
Halafu Sera ya mgombea urais kusema ataboresha maisha ya watanzania alafu mwisho wa mkutano anaanza kuwaomba wamchangie hela hao hao anaosema ni masikini wameharibiwa maisha na ccm aache kabisa.

Kama ni masikini wa kutupwa hizo hela wanazokuchangia wanatoa wapi.

Lisu acha upotoshaji
 
Halafu Sera ya mgombea urais kusema ataboresha maisha ya watanzania alafu mwisho wa mkutano anaanza kuwaomba wamchangie hela hao hao anaosema ni masikini wameharibiwa maisha na ccm aache kabisa.

Kama ni masikini wa kutupwa hizo hela wanazokuchangia wanatoa wapi.

Lisu acha upotoshaji
Hili jamaa limetuona hamnazo kabisa, yaani ananiambia nimepigika halafu ananiomba nimchangie saaasa kati yangu na yeye nani kapigika?
 
Halafu Sera ya mgombea urais kusema ataboresha maisha ya watanzania alafu mwisho wa mkutano anaanza kuwaomba wamchangie hela hao hao anaosema ni masikini wameharibiwa maisha na ccm aache kabisa.

Kama ni masikini wa kutupwa hizo hela wanazokuchangia wanatoa wapi.

Lisu acha upotoshaji
Hahahaha LUMUMBA KICHWAN NI MATOPE.

T.LISSU SIO TAJIRI , Angeendesha kampeni bila ilo ,Alijua mtasema " Anapata wapi hela??huyu anafadhiliwa na mabeberu".

Akaamua kua Muombaji msaada ili kuwapoteza maboya kama nyinyi " Mabeberu?? Mbona anaomba msaada?kwann wasimsaidie?"".

KWA LUGHA NYINGINE, KWA KUFANYA IVI, ANAENDELEA KUWAONDOLEA WANANCHI MTAZAMO MLOWAJENGEA WA ET "ANAGADHILIWA", BADALA YAKE SASA, WANANCHI WANAJIKUTA WANAENDELEA KUMUONA LISSU KAMA MTU ANAYEONEWA, KUSINGIZIWA, NDIO MAANA HATA KAMPENI WANAMCHANGIA.

Mabeberu ndio sisi wananchi Tunaochanga[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
 
Kwanini serikali za vijiji vifanye kazi ya kununua pamba ?

Nikupe historia kidogo, wakoloni walivyo anzisha kilimo cha pamba waliletwa makarani wakihindi kutoka india na wanunuzi wa pamba yetu walikuwa makampuni ya uholanzi na uingereza kwa maana ya Mackenzie na Rockefeller, chini ya dalali wao mkubwa Somji and sons na Gupta and Brothers.

Marehemu Paul Bomani alivyounda NCU alibadilisha ununuzi wa Pamba kutoka kwa madalali wa kihindi hadi kuwa chini ya uongozi wa vijiji na ushirika wao wa NCU, badae yalivyokuja mambo ya ubinafsishaji mambo yakabadilika. Na sasa tumerudi kwenye utaratibu wa vijiji kusimamia uchumi wa vijiji vyao wao wenyewe na sio kutumia madalali wanyonyaji.
 
nikupe historia kidogo, wakoloni walivyo anzisha kilimo cha pamba waliletwa makarani wakihindi kutoka india na wanunuzi wa pamba yetu walikuwa makampuni ya uholanzi na uingereza kwa maana ya Mackenzie na Rockefeller, chini ya dalali wao mkubwa Somji and sons na Gupta and Brothers.

Marehemu Paul Bomani alivyounda NCU alibadilisha ununuzi wa Pamba kutoka kwa madalali wa kihindi hadi kuwa chini ya uongozi wa vijiji na ushirika wao wa NCU, badae yalivyokuja mambo ya ubinafsishaji mambo yakabadilika. Na sasa tumerudi kwenye utaratibu wa vijiji kusimamia uchumi wa vijiji vyao wao wenyewe na sio kutumia madalali wanyonyaji.
Kwani vyama vya ushirika ni Mali ya vijiji ?

Narudia swali langu kwanini vijiji vinunue pamba?
 
Halafu Sera ya mgombea urais kusema ataboresha maisha ya watanzania alafu mwisho wa mkutano anaanza kuwaomba wamchangie hela hao hao anaosema ni masikini wameharibiwa maisha na ccm aache kabisa.

Kama ni masikini wa kutupwa hizo hela wanazokuchangia wanatoa wapi.

Lisu acha upotoshaji
Ukaona ukaanzishe na uzi kabisa!Yaani mataga mnahaha sana!Umecomment halafu ukaona hako kacomment kanafaa kuwa uzi,ukahamisha hivyo hivyo!Mmeishiwa ya kuandika kiasi hiki?Mko desperate sana!Haya ndio madhara ya kufanya siasa wenyewe kwa miaka mitano!
 
Tundu Lissu huwa haongei pasipokuwa dhulma ngojeni ashuke na kwenye Koroshow
Mimi najua mkulima wa Pamba ameanza kuibiwa na CCM tokea enzi na enzi na Vyama vya Ushirika vimefilisiwa na CCM angalao awamu ya nne Makampuni binafsi yaliianza kufungua ginneri zakusindikia pamba

Lissu huwa hapayuki kama mgombea wa Wasanii
 
Hili jamaa limetuona hamnazo kabisa, yaani ananiambia nimepigika halafu ananiomba nimchangie saaasa kati yangu na yeye nani kapigika?
Mchangie tu mkuu, huenda atashinda na tutakula bata.
 
Pamba inanunuliwa na wanaccm full stop hapo..... Ccm wameua viwanda Mwanza full stop. Wakulima wa Pamba wanakopwa badala ya papo kwa papo full stop.

Sasa we msukule wa lumumba unabisha nini
Aliyewakopa wakulima pamba yao ni Ester Bulaya na wapambe wake uzuri wameshamstukia hapati tena ubunge na watendaji wake wa vijiji washatimuliwa, kiwanda gani kilichokufa?

Kwa taarifa yako viwanda vyote vya mwanza vinafanyakazi chini ya JPM, anaongelea mambo ya kikwete. Halafu huyu jamaa kujadili biashara za watu akome, eti alipewa tenda mtoto wa dada yake, yaani kila kitu mtoto wa dada yake, hivi huyo dada yake jpm anawatoto wangapi kila mtu mtoto wa dada yake. Hata kipindi cha JK kila jengo jipya mjini la Rizwan. hawa jamaa sijui watoto wa Ibilisi? waongo kweli.
 
Bora hashimu rungwe na sera yake ya chakula maana anaamini kama mtu una njaa huwez fanya kazi vizuri na huwez kuwa na maarifa kwakuwa tayari huna afya yeye anasema atahakikisha kilimo kinakuwa namba moja.CHAUMA anasera nzuri ila ndo hawez pata na hawez kutete sera zake maana jana usiku nimesilikza sana
 
nikupe historia kidogo, wakoloni walivyo anzisha kilimo cha pamba waliletwa makarani wakihindi kutoka india na wanunuzi wa pamba yetu walikuwa makampuni ya uholanzi na uingereza kwa maana ya Mackenzie na Rockefeller, chini ya dalali wao mkubwa Somji and sons na Gupta and Brothers.

Marehemu Paul Bomani alivyounda NCU alibadilisha ununuzi wa Pamba kutoka kwa madalali wa kihindi hadi kuwa chini ya uongozi wa vijiji na ushirika wao wa NCU, badae yalivyokuja mambo ya ubinafsishaji mambo yakabadilika. Na sasa tumerudi kwenye utaratibu wa vijiji kusimamia uchumi wa vijiji vyao wao wenyewe na sio kutumia madalali wanyonyaji.
Hawa nyumbu hata uwaelimishe vipi watapinga tuu, waache na huyo mbwatukaji aendelee kuwapotosha wakati wakulima wa pamba wanaujua ukweli.
 
Madai ya Lissu kuwa Pamba inanunuliwa na wana CCM, ni madai ya kijinga tu mnunuzi ambaye ni mwana ccm ni Gachuma naye ana hisa kidogo sana kupitia Bulamba Gingery, hisa nyingi ni za Sumaria Group. Wanunuzi wakubwa wa Pamba ni Bilchard na Gupta group hawana uhusiano wowote na CCM niwafanya biashara huru tu.
Wacha upumbavu wako mwamba! Unaijua ginnery ya Nsagali wewe? Inanunua makalio ya shangazi yako? Unamfahamu Simon Kisenha na ginnery zake pale Maswa na Malampaka? Vipi kuhusu Kigwangala? Wote hao ni wanaccm wacha ujinga kabisa!
 
Back
Top Bottom