PakiJinja
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 11,689
- 25,848
Kuna shida gani akilala saa kumi usiku na kuamke saa 4 asubuhi?Tundu Lissu, akihojiwa na kituo Cha online TV kiitwacho Ngasa, alisema huwa anachelewa kuamka asubuhi na kwamba anaweza kuamka saa nne asubuhi au zaidi.
Hivi kama tukiwa na Rais wa aina hii, wa kuamka saa nne saa tano asubuhi, ataongozaje nchi? Maana muda wa kazi yeye ndio bado anavuta shuka akiutwanga usingizi na kuota ndoto za mambo mbali mbali ya kuvutia na ya kutisha.
Atakuwa na mamlaka ya kimaadili kuhimiza Watanzania waamke mapema wakachape kazi?
Tafakari kabla ya kupiga kura.