Uchaguzi 2020 Lissu na maadili ya Uchaguzi Mkuu

Uchaguzi 2020 Lissu na maadili ya Uchaguzi Mkuu

Ngamanya Kitangalala

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2012
Posts
501
Reaction score
1,214
Binafsi nimepata wasaa wa kumsikiliza mheshimiwa mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kuna baadhi ya kauli na shutuma zake kwa mawazo yangu nadhani sio sahihi sana

Ukisoma sheria ya Taifa ya uchaguzi sura ya 343,pamoja na mabadiliko yake ya mwaka 2015 ( The National Election Act,Chapter 343, Revised Edition, 2015) kwenye kifungu cha 124A, kuhusu maadili ya uchaguzi (The election code of conduct)

Sheria hiyo, inataka kila chama kitakachoshiriki uchaguzi mkuu wa October 2020, kusaini kanuni za maadili ya uchaguzi, ambapo kwa Chadema kilisaini makubaliano hayo tarehe 27/05/2020 kupitia katibu mkuu wake

Katika kanuni hizo ( Maadili ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka, 2020), kwenye sehemu ya pili, kifungu cha 2, kinaongelea maadili ya vyama vya siasa na wagombea katika kuendesha shughuli za siasa wakati wa kampeni

Ukiendelea kwenye kifungo hicho 2.2 ( h), kanuni inaelekeza wazi kabisa kuwa, kukosoana kati ya vyama na wagombea kunapofanyika, inabidi kujikita katika sera, programu na kazi zao walizofanya, ukosoaji wa vyama vingine au wagombea wengine kwa tuhuma zisizothibitishwa ni lazima uepukwe

Lakini mara kadhaa, mheshimiwa mgombea wa CHADEMA, amekuwa akitoa tuhuma kwa mgombea wa chama kingine, bila hata ya kuwa na uthibitisho wa tuhuma hizo

Binafsi kama mzalendo, napenda kutoa wito kwa wagombea wote kufanya kampeni kwa kutumia lugha ya staha huku wakijikita zaidi kwenye kueleza ilani ya vyama vyao kwa wananchi

Ngamanya Kitangalala Mwaswala
kngamanya@yahoo.com
 
Eti "binafsi kama mzalendo" una uzalendo gani? Kusifia sifia jiwe lenu na serikali yake ya kidhalimu ndo uzalendo?
We ni "liccm" pure tuondolee utopolo wako hapa.
 
Hizo za ununzi wa ndege ujenzi wa bwawa, uwanja wa ndege, isijekuwa kama ya Sigwa aliyeomba msamaha kwa Kinana.

Tuhuma zipi ambazo hazina ukweli ziweke hapa tuzichambue maana nyie ccm mpya saa hv mna kamusi yenu mpya mkiambiwa ukweli maana yake ni matusi
 
Mheshimiwa taja hizo tuhuma ili tuone kama hazina uthibitisho. Najua hamtaki Rais alaumiwe au ashutumiwe lakini kwa sababu ni mgombea basi atatupiwa mawe na hata asingekuwa mgombea pale anapokosea watu wana haki kumlaumu na kumshutumu. Lakini nyinyi mnamfanya Rais ni Mungu mtu ambaye hana makossa.

Kumbuka mzee Wasira aliwahisema CCM hawawezi kumaliza hotuba zao bila kuitaja CHADEMA kwasababu ndie mpinzani wao kama ilivyo shehe au kasisi asivyoweza kumalizia mahubiri yake bila kumtaja shetani.

Ukishaingia kwenye uchaguzi inabidi uwe umekubali kutupiwa mishale na kufukuliwa makaburi. Nyinyi wapambe nyamazeni ngoma ichezwe uwanjani, mbona yeye mwenyewe sijamsikia kulalamika?

Mnachofanya ni kutafuta msaada wa vyombo vya dola kama mlivyozoea, polisi, tume au Msajili wa vyama. Poleni kwa maumivu, ukishajiexpose kwenye mpamabano uwe mpole tu.
 
Kawaida wambea wote wakikosa cha kuzungumza, wanaanza kujadili na kushtaki wengine.
Wakijibiwa wanajiskia rahaaaaa.
Ndio walivyo wagombea wa CDM kazi yao ni kuimba tu taarabu
 
Binafsi nimepata wasaa wa kumsikiliza mheshimiwa mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kuna baadhi ya kauli na shutuma zake kwa mawazo yangu nadhani sio sahihi sana

Ukisoma sheria ya Taifa ya uchaguzi sura ya 343,pamoja na mabadiliko yake ya mwaka 2015 ( The National Election Act,Chapter 343, Revised Edition, 2015) kwenye kifungu cha 124A, kuhusu maadili ya uchaguzi (The election code of conduct)

Sheria hiyo, inataka kila chama kitakachoshiriki uchaguzi mkuu wa October 2020, kusaini kanuni za maadili ya uchaguzi, ambapo kwa Chadema kilisaini makubaliano hayo tarehe 27/05/2020 kupitia katibu mkuu wake

Katika kanuni hizo ( Maadili ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka, 2020), kwenye sehemu ya pili, kifungu cha 2, kinaongelea maadili ya vyama vya siasa na wagombea katika kuendesha shughuli za siasa wakati wa kampeni

Ukiendelea kwenye kifungo hicho 2.2 ( h), kanuni inaelekeza wazi kabisa kuwa, kukosoana kati ya vyama na wagombea kunapofanyika, inabidi kujikita katika sera, programu na kazi zao walizofanya, ukosoaji wa vyama vingine au wagombea wengine kwa tuhuma zisizothibitishwa ni lazima uepukwe

Lakini mara kadhaa, mheshimiwa mgombea wa CHADEMA, amekuwa akitoa tuhuma kwa mgombea wa chama kingine, bila hata ya kuwa na uthibitisho wa tuhuma hizo

Binafsi kama mzalendo, napenda kutoa wito kwa wagombea wote kufanya kampeni kwa kutumia lugha ya staha huku wakijikita zaidi kwenye kueleza ilani ya vyama vyao kwa wananchi

Ngamanya Kitangalala Mwaswala
kngamanya@yahoo.com
Kuengua wagombea kwa wiki tatu Sasa bila sababu, bila kutolea maamuzi rufaa ndo kanunui ipi?
 
Nakupongeza kwa andiko zuri. Werevu tu Ndio watakuelewa wengine watakushambulia maana ukweli huuma na maumivu yake hayaishi kwa haraka.
 
Back
Top Bottom