Lissu: Naishi kwenye makazi ya balozi(Ujerumani) kwa sababu maisha yangu hayako salama, nitarejea Ubelgiji

Lissu: Naishi kwenye makazi ya balozi(Ujerumani) kwa sababu maisha yangu hayako salama, nitarejea Ubelgiji

Tundu Lissu akihojiwa na redio Ujerumani DW anasema amepata simu za kutishiwa amani na ameamua kujificha kwenye makazi ya Balozi wa Ujerumani

Anasema maisha yake yako hatarini na anajipanga kuondoka na kurudi Ubeligiji

Tundu ni mwanasheria na very treak man tujihadhari naye sana

=========

LISSU: Niko katika makazi ya balozi wa Ujerumani, Dar es Salaam tangu siku ya Jumatatu.

MWANDISHI: Kulikoni?
LISSU: Naishi kwenye makazi ya balozi kwa sababu maisha yangu hayako salama tangu siku ya Jumamosi iliyopita, napata ujumbe wa kunitishia maisha kwa hiyo niliondoka nyumbani kwangu siku ya Jumapili na siku ya Jumatatu nikaenda ubalozini, nikafatwa na askari polisi wa Tanzania wakiwa kwenye magari mawili, nikakamatwa nikapelekwa kituo cha polisi Central na isingekuwa uwepo wa maafisa wa kibalozi wa Ujerumani siku hiyo pengine nisingerudi nyumbani kwangu.

MWANDISHI(LILIAN MTONO): Unasema kwamba ulianza kupata vitisho siku ya Jumamosi kabla hujahamia kwenye makazi ya balozi, ni vitisho vya aina gani ulivipata na nani hasa alikuwa anakutisha?
LISSU: Siku ya Jumamosi nilipigiwa simu na mtu ambae hakujitambulisha akaniambia kwamba, mheshimiwa maagizo tuliyopewa ni kumalizana na wewe, once and for all na baadae kidogo nikaletewa simu nyingine na mtu mwingine aliniambia hivyo hivyo kwamba mheshimiwa oda ya kukumaliza imetolewa kwa hiyo kama unaweza kujiokoa jiokoe.

MWANDISHI: Kwa hiyo hawa waliokupa taarifa ni wale waliotumwa ama labda ni wasamaria wema?
TUNDU LISSU: Nafikiri kwa jinsi walivyojitambulisha ni wako katika hilo kundi la watu waliotumwa lakini hawakubaliani na mambo haya.

MWANDISHI: Utakuwa hapo hadi lini?
TUNDU LISSU: Nitakuwa hapa mpaka hapo usalama wangu utakapohakikishwa, sipendi kukaa hapa, mimi ni mtu mwenye shughuli nyingi kwa hiyo nataka niondoke hapa haraka iwezekanavyo na bahati mbaya siwezi nikajua itakuwa lini kwa sababu wale wanaopaswa kuhakikisha usalama wangu wanaonekana kama hawataki kujicommit kwamba kama nikitoka nje nitakuwa salama.

MWANDISHI: Kwanini unasema hivyo?
LISSU: Kwa sababu tangu nimekuwa hapa kumekuwa na jitihada za mabalozi wa nchi mbalimbali kuiambia serikali ya Tanzania kwamba haya mambo yanatokea sio masuala sahihi na mpaka sasahivi hizo jitihada hazijafanikiwa bado.

MWANDISHI: Utakapofanikiwa kuondoka, utabakia nchini au utarudi Ubelgiji?
LISSU: Nitaondoka kurudi Ubelgiji kwasababu hali ya usalama sasa hivi sio nzuri hata kidogo, hivi vitisho ni vitu ambavyo lazima nivichukulie kwa uzito mkubwa na wa kipekee.

MWANDISHI: Bado unajiona utasimama tena kwenye kinyang'anyiro kijacho cha Urais na utaendelea na harakati zako za kisiasa?
LISSU: Tuombe Mungu atupe uzima tujue miaka inayokuja itatuweka vipi lakini nachoweza kusema waziwazi ni kwamba harakati ni maisha yangu.
Kaa tu hata miezi kadhaa pumzika
 
Mwanzoni mliongea hup upumbavu lakini mwishowe ukaenda Dodoma na Bashite na akina cyprian Musiba mkaenda kumpiga risasi na sasa katoa tahadhari lazima watu wawe makini na yeye binafsi ajihami

Hakuna kitu kibaya kama kuongea vitu usivyokua na uhakika navyo.

Siku utakapokuja kuujua ukweli unaweza kujikimbia kwa aibu na kujiona ulivyo mtu wa ajabuajabu sana hapa duniani
 
Ametafuta justification ya kuhalalisha kuishi Brussels. Nani ahangaike na Lissu wakati huu ambapo hana madhara. Labda ndani ya CHADEMA huenda anatishia uenyekiti wa mtu ambapo ni sawa na uhaini.
Kwani kurudi Ubelgiji ni jinai? hana sababu za kujustify kwenda ubelgiji, anaenda kwa ajili ya check up ya afya,lakini pia kama alivyo sema anakwenda kwa ajili ya usalama wake.

Kabla ya kupigwa risasi alilalamika na kutoa taarifa Polisi kuhusu hali ya usalama wake, hakuna aliye jali, mwisho wake ikawa nini? akapigwa risasi 16.
Jukumu la kwanza la kuhakikisha usalama wako ni lako mwenyewe kabla ya serikali kukuhakikishia usalama
 
Huruma ipi? Wananchi wa wapi unawasemea? Hukuna mwananchi mpumbavu kama wewe
Ww nshakuzoea kuona post zako ukimtetea huyo mume wako, cha msingi mngefanya kuandamana tuu kama mlivosema
 
Ww nshakuzoea kuona post zako ukimtetea huyo mume wako, cha msingi mngefanya kuandamana tuu kama mlivosema
Mme wako cyprian Musiba bado anakuvutisha Bangi? Maandamano tarehe 2 lakini wewe tarehe 1 siku moja kabla ukawakamata viongozi wa ACT na chadema huku ukitembeza vitisho kibao, maandamano yapi pasipo viongozi wala uhamasishaji? Huoni kuwa wewe na Polisiccm ndiyo waoga?
 
unajaza upumbavu humu lazima ukimewe ukizingatia na wewe ni mjamzito unaandika chochote kutokana na hali yako
Huo ujauzito umenipa wewe au baba yako mzazi?? Sindano yenye dawa imekuingia nywiii sasa tulia upone.
Kama unaona mm ni mpumbavu usijibu post zangu nilizozijaza humu. Ukizijibu basi nitaamini na ww pia dishi limeyumba.
By the way, maneno yako hayatanikatisha tamaa mm kupost hoja zangu humu.
 
Hujui mambo mengi kwa upeo wa juu. Uongo unathibitishwa, haukataliwi tu. Ungesema basi hakupigiwa hizo simu!
Nadhani hata wewe upo Kwenye group la kinder' thinkers.Inaingia akilini mwako eti wauaji wametumwa kukuua halafu wanakuambia eti wametumwa kumalizana na wewe safari hi kwa hiyo kimbia tusikuue.
 
Mme wako cyprian Musiba bado anakuvutisha Bangi? Maandamano tarehe 2 lakini wewe tarehe 1 siku moja kabla ukawakamata viongozi wa ACT na chadema huku ukitembeza vitisho kibao, maandamano yapi pasipo viongozi wala uhamasishaji? Huoni kuwa wewe na Polisiccm ndiyo waoga?
Sasa kwann hukuandamana kisa viongoz wako kukamatwa.? Au ndio mpaka mume wako awepo ndio upate nguvu za kuandamana
 
Mara ya kwanza aliposema anataka kushambuliwa mlikuja na maneno ya kibwege kama haya matokeo yake akina cyprian Musiba wakatekeleza shambulio
Kwa hiyo hata kama akishambuliwa na majambazi pia bado mtasema ni njama za CCM. Hivi wote walioshambuliwa na risasi hapa duniani ni njama za CCM??
Naamini wangekua ni askari wa Tanzania ndio wamehusika basi asingepona, risasi moja tu ingemtosha kuondoa uhai wake.
 
Vina uhusiano gani na ushetani wenu wa kutaka kumuua?
Hahaha aliyetaka kumuua labda dereva wake aliyemficha asije akatoa Siri polisi ya kilichoendelea siku ya tukio..wangeumbuka wengi mno... nahisi..na yeye anajua..kwanini anakimbia kimbia hataki kwenda polisi kuhojiwa na dereva wake Kama kweli haya Mambo hawajayafanya wait wenyewe ndani ya chama chao
 
Kwa hiyo hata kama akishambuliwa na majambazi pia bado mtasema ni njama za CCM. Hivi wote walioshambuliwa na risasi hapa duniani ni njama za CCM??
Naamini wangekua ni askari wa Tanzania ndio wamehusika basi asingepona, risasi moja tu ingemtosha kuondoa uhai wake.
Hahaha eti askari shupavu wa jeshi au polisi wa Tanzania kapiga risasi 16 hazijammaliza...hayo Ni mazingaombwe basi si bure
 
Huu upumbavu ndiyo umeikosesha CCM kura mpaka NECCCM Tumeccm wakurugenziccm na Polisiccm wakaamua kuubaka kuunajisi kuulawiti uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani maana hakuna Mtanzania mwenye Akili timamu anaweza kuipa kura yake CCM kutokana na kusheheni watu wapumbavu kama wewe
Chadema walipata kura ngapi jomba...kulingana na mahesabu yenu...hahahahah ujinga wa kiwango Cha matope
 
Unakumbuka baada ya alitekua mjumbe wa Tume ya Katiba Mpya Dr. Sengondo Mvungi kuua kinyama na watu walioitwa majambazi zoezi zima lilivurugika na wajumbe wote waliokua wamebaki hai walijawa na hofu mpaka Leo ndio wamejisalimisha na kuungana na wapinga katiba mpya.
Wajumbe waliokua wametumia mbilioni ya fedha za watanzania leo wanasema kwa wazi kabisa kuwa hawako tayari kuona katiba mpya inapatikana Tanzania mana itakwamisha maendeleo.

Jiulize kitu gani kimewatia hofu wajumbe waliobaki hai? Je, huoni kuwa mauaji ya kinyama ya Dr. Sengondo ndiyo yaliyowatia hofu ? Huoni kuwa waliofanya njama za kijambazi kumuua Dr.Sengondo bado wapo na ndio waliojenga mazingira ya kuwatia hofu akina Kabudi ,Polepole, na Wengineo ?

Ni MTU mwenye Roho ya kimungu Pekee asiyeogopa kifo lakini wengine wote wanaogopa kifo!!

Shetani kwa muda Mrefu ameutawala ulimwengu kwa sababu alikua ameshikilia funguo za Mauti . Mauti ndiyo tishio kwa watu.
Wakristo na waislam wanaamnini katika ufufuo siku ya kiyama. Imani hiyo ndiyo raraja kuu ya kuondoa hofu ya kifo mana wanaoua hawana mamlaka ya kuwapeleka marehemu popote baada ya kifo.
Yaani akisha muua binadam mwenzake kazi inakua imeishia hapo hana la kufanya tena kwenye nafsi ya marehemu.

Mpaka sasa jambo baya kabisa kumtendea binadamu ni kuua mana kila mmoja anatamani kuishi !!
Wanaoshabikia kuuawa kwa wengine bila hatia ni wale wanaofanya kazi za kumwakilisha shetani duniani japo kila siku tunasafiri kuelekea siku ya kufa. Kila mnapofurahiya siku kuongezeka lakini mfurahiye pia siku kupungua kwenye zile siku zilizopangwa na Mungu.
 
Back
Top Bottom